Ni kweli ila tambua binadamu tunatofautiana, mimi natamani niwe na roho mbaya, nisiyejali wala kuthamini wengine ila nimeshindwa.
Naomba kama kuna mahala unaweza kubadilisha nafsi ya hofu ya mungu na kuwa na roho mbaya nipeleke au nipe notes nipitie niweze kubadilisha nafsi hii.
Naomba unipatie kozi fupi ya kuwa na roho mbaya na ya ukatili, nisiyejali wala kujua ya wengine kwa ufupi nifunze kuwa kama wao kwa kuwa naamini mimi sijajiumba ila naitaji kubadilika niwe zaidi yao.
Moja ya makosa ninayoyajutia ni hayo lakini changamoto kubwa ya kazi yangu ni ukionekana unajambo unafanya litakalokutoa kwenye utegemezi utaamishwa ili kukuvuruga usiweze kusimamia mambo yako.
Ni kweli ni kawaida ila kwangu nimekuja kujua makazini roho nzuri haina nafasi, ni bora kumfunza mwanao roho mbaya ili akapambane na walimwengu kuliko kumfunza utu , ukarimu na upendo kwa imani kuwa utakupeleka peponi.
Moja ya majuto ya nafsi yangu juu ya mkasa wangu ni kuwa tusiwafundishe watoto utu na ukalimu bali tuwajaze kutojali na roho ya ukatili na ushirikina juu, nafahamu kwa kuwa yote yamenitokea.
Ukiwa na roho ya ubinadamu utapendwa na watu unaowapa huduma lakini si wale unaofanyanao kazi.
shida kubwa sana ni kwamba chuki si za eneo la kazi bali ni jamii fulani au kabila fulani ambao wanaamini kwamba taasisi ni haki yao na wako wengi hivyo kokote uendako utawakuta.
Habari zenu watanzania wenzangu popote mlipo, mimi nikiwa member hai wa forum napenda kutoa ushuhuda wa manyanyaso kazini yalivyopelekea kuangukia kwenye ugonjwa sugu wa figo.
Mimi ni mfanyakazi wa taasisi fulani serikalini, nimeajiliwa 2007, katika kupata kwangu ajila sikuwahi kufikilia kwamba...
Kinachoumiza watu wengi sio kusemwa kuhusu maisha, wengi tunaumizwa na matendo ya wazi kuhusu mazaifu yako wewe mwenyewe ukisikia,mioyo inatofautiana.
Mfano: Unakuta mtu labda muonekano wako au vile ulivyo unaonekana Huna mvuto kwa wengine kwa kulitambua hilo unaamua kuwa unafanya mambo yako...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.