Bouncer
Mkuu naona leo umeonja sana,
mimi nina ombi moja tu kwako
Hebu yasome maneno yako kwa sauti huku ukiwa unayarikodi, halafu uyasikilize, ukisha uniambie kama unaamini mwenyewe kama ni maneno ya maana
Wakuria wenu watakuja znz kulima tu
Kulingana na mikata ya kimataifa nchi inahaki ya kudai ardhi yake, ndio maana Slovakia wakavunja mkataba na Check, Scot,and walipewa uhuru kuvunja mkataba na England. Ingekuwa Yes vote imepasi basi scotland wangedai ardhi yao officially
Sasa na znz ikiwa huru itaweza kudai ardhi zake officially
Job K
CMM wameshalipima joto letu, wanajuwa fika kwamaba watz hatuwezi kufanya chochote, kwahivo wanajuwa kwamba uamuzi wao ndio uamuzi bora kwa raia wote
nngu007,
hizo ni kasumba zilizowekwa kichwani kwako na CCM ili kuweza kukutawala kiuaini zaidi.
Fukwe za Mrima alikodishwa Mjerumani na serikali halali ya znz. Ikiwa wewe umesomeshwa kurikiri zaidi ya hapo endelea tu siku utakayoanza kulipia kodi ya kuishi dar ndio utakajuwa uweli wa mambo.
Gor,
Mkuu ninakupa ahadi ukivunjika muungano, Tanganyika itakuwa landlocked country overnight, maudhi na dhuluma zote zinazofanyiwa znz na tanganyika zitajilipa. Tupo tayari kwa hilo na haturudi nyuma.
Freeland,
wewe unaonekana umesoma kweli,
ninakuhakikishia, na uiweke barua hii, siku ukivunjika muungano, patishaka UN kuhusu mipaka. na hakuna mtanganyika anayethubu kusema neno kwasababu nyaraka za ukodishaji wa coastal areas ya mrima kwa mjerumani zipo.
angalia patashika hiyo, mtwara...
Mkuu,
Ukiristo makanisani, Uislamu misikiti, hayo ndio mawazo halisi ya ccm.
Usidanganywe na kuona zinga la sanamu la yesu katika ofisi ya pinda kule dodoma, kile ni kitega uchumi tu. na wale usidanywe na kuona misahafu katik ameza za waziri same deals
ccm wanaangalia masilahi yao binafsi...
Mkuu,
Tukurudisha nyuma zaidi hautoipenda wewe, maana itabidi sisi wazanzibari tukutawaleni tena nyinyi watanganyika, itakuwa si jambo zuri kwenu au vipi
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.