Ukweli ni kwamba huwezi kumlazimisha mtu asiyetaka kuja kwenye mkutano. Hata umpe usafiri, kama hataki, hataki.
Vilevile, mikutano ya CCM imekuwa ikihudhuriwa na maelfu ya wananchi. Sasa kama basi moja linabeba watu 65, je, utahitaji mabasi mangapi kuwasomba maelfu ya watu? Hilo haliwezekani...
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesalimiana na maelfu ya Wananchi wa Rungwe, Mkoani Mbeya, waliofurika barabarani kumlaki katika Mkutano wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu leo, Septemba 05, 2025
🌿 Mbeya – Uyole
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan,
amepokelewa kwa shangwe na nyomi kubwa la wananchi wa Jimbo la Uyole, waliojitokeza barabarani kumlaki kwa furaha kubwa wakati wa Mikutano ya Kampeni za Uchaguzi...
Maelfu ya Wananchi wa Wilaya ya Rungwe, Mkoani Mbeya, wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu, uliohudhuriwa na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 05, 2025...
Wingi wa wananchi kwenye mikutano ya kampeni ni ushahidi kuwa sera na maendeleo ya CCM yanagusa maisha ya watu moja kwa moja. Demokrasia inatoa nafasi kila mtu achague, sisi tumechagua maendeleo. 💚💛
#Haijapatakutokea
#Kurayakwanzakwasamia
Jengo la Mama na Mtoto – Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (Meta)
Jengo hili ni miongoni mwa majengo ya kisasa yaliyotekelezwa katika hospitali 7 za kanda nchini.
Ni ushahidi wa dhamira ya dhati ya Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha mama na mtoto wanapata huduma...
Kasumulu – Mbeya
Kituo cha Pamoja cha Forodha kilichojengwa katika mpaka wa Tanzania na Malawi ni matunda ya utekelezaji wa Sera ya Diplomasia ya Uchumi.
Mradi huu umelenga kuimarisha mwingiliano wa watu, kukuza biashara na kudumisha mshikamano wa ujirani mwema kati ya mataifa haya mawili...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.