Haha uongo mkuu..nakupa mfano mdogo Kuna zahanati nilikua nafanya ya private C.O tulikua tunalipwa 13k kwa shift lakini Dentist dogo mmoja mdogo tu alikua akilipwa kwa kichwa kwenye elfu 10 yeye anakata elfu 3 na kwa siku alikua ana ng'oa zaidi ya watu 20 bado alikua anazipa meno Kuna hela...
Iko hivi Kama unataka sifa mtaani Soma C.O Ila utakua na Maisha Duni maana ajira mkasi kwa Sasa.
Ila Kama unataka mafanikio bila jasho chukua Macho,Radiology na Meno hizo ndo kozi ambazo hazina wataalamu wa kutosha mtaani na ukiajiriwa na serikali Basi hukai kijijini Kamwe na pia hata private...
Dah mdogo samahani Ila nakushauri hivi kwa sababu Mimi nimepita huko C.O...futa Anza upya itoe kabisa hiyo pharmacy maana Kama umeweka juu ya optemetry Ina maana kipaumbele chako no pharmacy kabla ya hiyo hivyo utapelekwa pharmacy.
Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
Kwa kuanzia tu semista ya kwanza una masomo 8...module zingine ingie Google utaletewa ..hapa nilipo mtandao shida zinafeli kuaupload humu
Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
Maksi zako za Hali ya juu unapata Muhimbili bila tabu..narudia Tena achana na pharmacy kwa hapo komaa na Radiology, Optemetry na Meno achana pia na C.O utajipotezea muda.
Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
Achana na pharmacy Kama huna hela ya kujiajiri Kasome Radiology..ukishindwa Kasome macho au meno...maksi zako zipi?
Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
Chuo Cha serikali kinachotoa hiyo kozi ni kimoja pekee nacho ni Muhimbili na kwa private Bugando japo Ada yake 2M na Muhimbili Ina range 70k+ kwa morning na 1.5M kwa evening...Bugando hawajaweka kwa mfumo wa Nacte ukitaka kuomba ingia moja kwa moja kwenye website yao na Muhimbili hivyo hivyo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.