Mimi si mwanachadema na wala sina chama lakini kwa hilo nakuunga mkono. Msigwa kasema mengi ambayo ukweli wake wanaujua wanachadema na viongoxi wenzake lakini kwa uzito wa hizo shutuma ingekuwa jambo la kingwana kwa Mbowe kukaa pembeni na kupisha uongozi mwingine na ikiwezekana uchunguzi...
Hawa ni Marais wastaafu ambao walikuwa wawili na sasa kabaki moja Kikwete na wenza wa Mwinyi, Makamu wa rais mstaafu mmoja Dr. Ghalib Bilal, mawaziri wakuu wastaafu walikuwa saba baada ya Lowasa wamebaki sita lakini tunagharimia mwenza wake Lowasa.. Walio hai ni Salim A. Salim, Msuya, Warioba...
Katika bunge hili hakuna mwingine kama Luhaga Mpina. Kuna wakati huwa najiuliza hivi huyu ni mbunge wa CCM kweli!
Sent from my Infinix X689F using JamiiForums mobile app
Waingereza walimenzi na kumtunuku nishani ya MBE yaani Member of the British Empire. Viongozi (watawala) wetu wanapenda sifa kukosolewa kwao ni uchochezi. Wao ni miungu watu hawakosei.
Sent from my Infinix X689F using JamiiForums mobile app
Inasikitisha sana kwa kiongozi wa nchi alieapa kuihifadhi na kulinda katiba akitoa kauli za kuidharau. Ni sawa na askofu kuidharau biblia au sheikh kuidharau Koran tukufu. Haishangazi kuona nchi inaendeshwa bila ya kufuata katiba.
Yaani jinsi gani tutaweka na kuondoa uongozi, jinsi gani uongozi utawajibika kwa raia, kwani, na namna maslahi ya Kila mtu yatalindwa ndani ya nchi yetu.
Sasa haya yanahitaji utuelimishe nini!? Mama anataka kutulazimisha aendelee kutuongoza bila ridhaa yetu. Anazingumzia wananchi kuburuzwa haoni...
Kusema katiba mpya isiandikwe kabla ya elimu kutolewa ni sawa na kusema mwanafunzi alielimishwe kabla ya kujua kusoma. Nyere alipodai uhuru watanganyika wangapi walikuwa wanajua hata maana ya uhuru wenyewe?
Sent from my Infinix X689F using JamiiForums mobile app
Ni kiinimacho hawataki lawama. Kilingana mkataba wa DTW wao watakuwa na mamlaka ya mwisho ya kumtangaza mshindi. TPA ni kipaza sauti tu.
Sent from my Infinix X689F using JamiiForums mobile app
Kwani hujui kwamba hela ya budget inapangiwa na rais. Kama JPM aliweza kujenga uwanja wa ndege bila idhini ya bunge sembuse festival.
Sent from my Infinix X689F using JamiiForums mobile app
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.