Mail inatafutwa, uhai wa Mtu utafidiwa vipi? Isitoshe hao Askari walifanya mauaji hata baada ya uharibifu huo kutokea kwa kupiga risasi Raia Majumbani mwao, nafikiri kama ingetokea mmoja ya Ndugu zako kuuawa usingeandika utumbo huu..
Nafikiri hawa Walimu ni wa kuwasamehe tu, ni ugumu wa Maisha ndiyo unaosababisha waombe hiyo kazi ya kusimamia ili angalau wajikimu..
Mimi nawafahamu baadhi ya Walimu ambao ni Wapinzani wa haya yanayoendelea, lakini hawana namna, na baadhi yao ndiyo wametoa siri kuwa waliambiwa watiki karatasi...
Kuna Jamaa katoa ushuhuda, amesema kwenye kituo alichchokua anasimamia, mpaka saa nane mchana Wapiga kura walikuwa hawazidi 40, licha ya jitihada mbalimbali walizofanya wana Fisiem, ikiwemo kufuata Watu hadi Majumbani..
Baadae lilitoka agizo kwamba watiki hizo karatasi za kupigia kura ili...
Wewe huna tofauti na Mchawi, hata kama Mtu ni muovu kiasi gani, hasitahili kufanyiwa haya, ingekuwa amekamatwa na kufunguliwa Mashitaka kama ana kesi ya kujibu, ila cha kuleta faraja kwangu ni kuwa hakuna Mtu atakayeishi milele.
Kwa hiyo wewe umekuwa msemaji wetu? Utafiti gani uliofanywa mpaka uje na Matokeo hayo? Ulishawahi hata kujua idadi ya Watu waliopo kwenye eneo husika na idadi ya Wahudhuriaji?
Kwani kichwa cha habari cha Uzi wako si umemrejelea Mh. Polepole? Sasa kwa nini maelezo yako yasiendane na kichwa cha habari? Hata ufanyaje huwezi aminisha Watu kwamba kipindi cha Magufuli kilikuwa cha hovyo kuliko kipindi hiki na vingine kabla..
Ukiwa ni mnufaika wa uozo unaoendelea katika Serikali hii huwezi kuona mapungufu na utaendelea kumpinga kila anayekosoa, ulitakiwa uje na hoja kuonesha anachoongea Mh. Polepole hakina ukweli.
Na ndiyo maana niliandika hapo juu kuwa, huenda hukumsikiliza au kama ulimsikiliza basi hukumuelewa...
Inawezekana hajamsikiliza vizuri Polepole, maana mimi sikusikia sehemu ambapo amesema kwamba mambo ya maendeleo ya Nchi yaliharibiwa na CCM mtandao kipindi cha Magufuli, ameeleza namna CCM mtandao walivyokuwa wakitumia mbinu mbalimbali kuhujumu Serikali ya awamu ya tano,.
Inaonekana huyu...
Bandari ni sehemu muhimu kwa usalama wa Nchi, unapowapa Wageni kusimamia sehemu nyeti kama hiyo ni hatari kwa usalama wa nchi, kusema kwamba mapato ya Bandari yameongezeka sioni uhalisia na wala Uchumi wetu haujafunguka kama unavyodai, ndiyo maana Deni la Taifa limeongezeka karibu mara mbili ya...
Hivi unafuatilia kweli jinsi mambo yanavyoenda au upo kishabiki zaidi? Angalia Rasilimali zetu jinsi zinavyobufaisha Watu wachache hasa wageni, sehemu muhimu kama Bandali unawapaje wageni ili waendeshe?
Leo hii sekta ya Madini wanufaika wakubwa ni wageni ukiacha huyu Rostam Aziz ambaye naye...
Inategemea alikuwa anatoa ushauri upi? Huenda manufaa yalionekana, Watu wanazungumza kwa sababu wanaona mambo yanaharibika siku hadi siku huku Mstaafu akiwa karibu na Serikali.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.