Magazetini
Nimemsikiliza LOWASSA, LIPUMBA, MBATIA, hata MAALIM SEIF, hakuna hata mmoja aliyewataka vijana kuingia barabarani! wote wanaombea AMANI ya Tanzania, sasa hili la kuwaambia vijana wavunje AMANI, January amelitoa wapi? Mbona CCM mnakuwa hivi?
Sasa kama ZEC iligundua kulikuwa na madudu yaliyosababisha mshindwe vibaya huko Zenji, mlipaswa kuwaunga mkono ili kufanikisha hili lengo lenu, nashangaa mnawakataa tena! Kweli CCM imefitinika!
Alichofanya seif ni kukusanya matokeo na kutangaza, bila kujitaja kama ameshinda au la!
Sasa kama amechukua matokeo yaliyobandikwa na watendaji wa ZEC, na CCM ilikuwa na mawakala wake mle, shida iko wapi?
January Makamba aliyetutajia idadi na ya majimbo ambayo CCM imeshinda, pamoja na kututajia tarehe ya kuapishwa kwa MAGUFULI, je, yeye hakuvunja sheria, Watu wa CCM mmelogwa nini?
CCM itajuta kumfahamu LOWASSA, nimemuona January Makamba anajitoa ufahamu eti anasema kuwa ya ZNZ hayatuhusu, bila kufahamu kuwa, kama kulikuwa na "wapiga kura hewa", "vitambulisho feki" basi na matokeo ya huku yameathirika!
Sasa kama ZEC wanasema kuwa hali ya uchaguzi haikuwa shwari, kwanini...
Moja ya sababu ya kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar ni kuwepo kwa raia ambao walipiga kura bila ya kuwa na vitambulisho.
Je watu hao hawakumpigia Magufuli au Lowassa? Lubuva ana uthibitisho gani mpaka anatuhakikishia kuwa kufutwa kwa uchaguzi wa zanzibar hakujaathiri huku bara?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.