Oct 29-30 chama kimepitia changamoto. Mpaka sasa kipo kwenye changamoto ya yanayojiri baada ya tukio lile.
Poleni sana Watanzania waliopeteza ndugu, jamaa na marafiki kwenye kumbukumbu ile isiyopendeza.
Jeshi la wananchi kazi yake ni kuilinda nchi na hatari kutoka nje, ukiwaona wametapakaa kabla hujakabiliana nao jiulize kuna hatari gani isiyo ya kihalifu wa kiraia ya kuruhusu uwepo wao. Tanzania sio kisiwa.
Viongozi, wanachama na raia wapenzi na wapiga kura kwa ccm wengi walishakuwepo na sasa hawapo ila wameiacha ccm madarakani ikiendelea kuaminiwa kuongoza.
Kuamini kuwa CCM ina mpasuko ni kete muhimu sana kwa upinzani kutoka CCM. Imefanya kazi tangu enzi za Mrema na itafanya kazi hata leo sababu wafuasi wa upinzani na viongozi wa upinzani wakati wote wana malengo, mategemeo, matendo tofauti na maneno yanayofanana ili kuwafikirisha wao ni kitu kimoja.
CHADEMA si tishio kwenye nafasi ya uraisi. Kumpitisha au kutompitisha Daktari Samia kuipeperusha bendera ya chama cha mapinduzi haina uhusiano na wanachofanya CHADEMA.
Soma Katiba ya nchi yako kuelewa majukumu ya Jeshi la nchi yako.
Unaonekana ni mtu unayependa nadharia au mambo ya kufikirika. Kupiga kura against CCM ni haki yako kama ilivyo haki ya watakao ipigia kura 2025.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.