Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Hii ngoma imekuwa ndefu sana nipeni fursa kuweka SUMMARY,

  • Wenye busara wamemshauri Zitto pamoja na nia yake nzuri ya kutaka kuwa rais aendelee kusoma alama za nyakati ili wakati ukifika aingie ulingoni akiwa na nafasi nzuri kushinda/ kuchaguliwa na chama chake
  • Pro CCM members wamefurahia sana uamuzi huu wa Zitto, hii imewapa mashaka makubwa sana Pro CDM members kwamba kwa nini akina Ritz, Topical, Geniusbrain nk wamfurahie Zitto katika nia yake ya kugombea against chama chao? Kuna ujumbe mzito sana behind this scene...
  • Wengine wameegemea kwenye age ain't nothing but a number kwamba ujana au uzee sio ishu sana kwani kuna vijana tumewaona ni wahuni kama Adam Malima na pia kuna wazee wengine hawana busara kama Wassira. Cha muhimu ni kuwa na sifa na uwezo wa kukabiliana na matatizo yaliyopo hapa nchini na sio changamoto kwa kuwa changamoto hata zisipotatuliwa hakuna wa kulaumiwa but matatizo kama ajira kwa vijana na umaskini lazima yamalizwe na rais ajaye, Na Zitto amesema anayajua vizuri sana
Nilitegemea baada ya summary itafuatia Recommendation na Conclusion! Nimetafuta recommendation na conclusion nimevikosa.
 
Zitto anafaa walau kuanzia 2025 atakuwa amepikwa na kukomaa vizuri.Kwa hivi sasa ni nafasi ya Dr Slaa.Dr Slaa kwa sasa hana mbadala ndani ya CDM.Ni kujilisha upepo kudhani kuna mtu mwingine atapitishwa kugombea Urais zaidi ya Dr wa ukweli walau kwa sasa.CDM ina vijana wengi na hakika huko Mbeleni kina Zitto na Mnyika na wengine ni hazina kubwa ya chama

kisha zeeka halafu tumemchoka cdm tuna utaratibu wetu mtu akigombea mara moja akishindwa basi aende akalime tu. Zitto hakika anafaa. Slaa kisha zeeka nchi ikiongozwa na mzee itaenda kizee slaa hafai tena bw.ege
 
Pandikizi la CCM hili tunalijua, kamwe wana CDM musikubali. Toka awe mjumbe tume ya madini hana tofauti na akina Chiligati. Hata hiyo 2025 kutakuwa na watu bora katika CDM kuliko Zitto.
 
Nilitegemea baada ya summary itafuatia Recommendation na Conclusion! Nimetafuta recommendation na conclusion nimevikosa.
Tatizo ningeweka Conclusion watu watatoka povu humu na kudai nimewasemea...

Namshauri mleta uzi aweke conclusion halafu ngoma iende kwenye ARCHIVE maana imezidi urefu
 
kisha zeeka halafu tumemchoka cdm tuna utaratibu wetu mtu akigombea mara moja akishindwa basi aende akalime tu. Zitto hakika anafaa. Slaa kisha zeeka nchi ikiongozwa na mzee itaenda kizee slaa hafai tena bw.ege

Your comments show you are stupid!
 
Zito umeweka mbele maslai yako umesahau chama, kitu hata kama ni kizuri vp kisipo kuja kwa wakati ni kibaya ndugu yangu! Kwa nini usingesubiri tumalize ya arumeru ndio utoe hilo jibu la makala ya huyo mwanazuoni huoni kwa hayo mawazo yako umetudhihirishia kuwa hatuko pamoja kama chama, mawazo ya chama yako arumeru kwa sasa ila kasoro wee peke yako, busara ingetumika bwana zito. Nimelipenda jibu la makala kwa mwanazuoni ila co muda wake
 
Zitto go ahead, umeweka wazi katika makala yako, utafuata taratibu za kichama na si vinginevyo kwa mimi sioni tatizo.
Bigup na dream zako you never know! una full support yetu!
 
WAKUU.
tusipotoshane hapa.
slaa sio mgombea urais wa chadema 2015 isipokuwa alikuwa mgombea 2010. yeye mwenyewe alitamka hadharani kuwa alikuwa hautaki urais lakini alilazimishwa. sasa kama kuna mtu amejitokeza kuutaka urais mimi nadhani anapaswa kuungwa mkono sana mana huwezi ivaa nguo nusiyoipenda ukaenda nayo safari. slaa alifanywa chambo na mbowe na sasa mnataka kumlazimisha kuwa yeye ndiye mgombea urais wa chadema.
shame on you.

Whether you like or not our Candidate in 2015 will be Dr Slaa.Nenda kawaeleze na wanaCCM wenzako hivyo.Kamwe CDM haitawekwa rehani kwa vibaraka wa CCM
 
Pandikizi la CCM hili tunalijua, kamwe wana CDM musikubali. Toka awe mjumbe tume ya madini hana tofauti na akina Chiligati. Hata hiyo 2025 kutakuwa na watu bora katika CDM kuliko Zitto.

Leo founder wa chama amekuwa pandikizi la CCM? Pandikizi wa ccm ni slaa anayekipeleka chama kuwa cha kimaeneo na watu wa mrengo fulani.ZItto,Mbowe hawa wapo neutral na wanaweza kupeperusha bendera ya CDM sio SLAa mropokaji. Ikulu inahitaji mtualiye balanced
 
Leo founder wa chama amekuwa pandikizi la CCM? Pandikizi wa ccm ni slaa anayekipeleka chama kuwa cha kimaeneo na watu wa mrengo fulani.ZItto,Mbowe hawa wapo neutral na wanaweza kupeperusha bendera ya CDM sio SLAa mropokaji. Ikulu inahitaji mtualiye balanced

Stupid at his work!
 
Japokuwa umri si hoja, nina wasiwasi sana sana na busara za mtu yeyote anayetaka kuwa raisi wa nchi katika umri wa miaka 35, na hata kutaka katiba ya nchi kubadilishwa ili kukidhi kiu yake hiyo. Sioni tofauti na busara za kijana wa miaka 15 anayetaka kuwa na gari yake mwenyewe, katika mazingira ya sheria isiyomruhusu kuendesha gari hadi awe na umri wa miaka 18.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Nimeshindwa kuelewa inakuwaje baadhi ya watu wanashindwa kusoma makala na kisha ndiyo wachangie?Inakuwaje waje wengine waibuke na kutaka au kuonyesha dalili za kuzima mjadala kwa visingizio kibao kuhusu chaguzi ndogo zinazoendelea? binafsi mimi nina-discourage majungu na fitina katika kipindi hiki cha chaguzi ndogo ila nashindwa kuelewa tumefikiaje hatua ya kumzuia mtu asiweke sawa upotoshaji uliofanywa na mtu kwenye makala.

Kama Zitto angekaa kimya na mjadala ukaendelea kwa jinsi ambavyo watu walikuwa wameanza kuupotosha kwa vyovyote vile ungekuwa na madhara.Watu wangesubiri hadi tarehe 2 Aprili huku wengine wakiendelea kuamini ndivyo sivyo.je ndiyo tulikuwa tunataka iwe hivyo?kwa maslahi ya nani?Halafu sijui tunapata wapi moral authority ya kuchagulia watu kitu cha kusema?Wengine wamedhani linalojadiliwa ni umri tu wa Urais,makala iliyoandikwa iko wazi.

Kuna Mwingine ameibuka na kuanza kushambulia kuhusu siasa za Alliance.Mwingine alitunga jina "BENZITTO" alliance kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe.Labda pengine kwa kuonyesha msimamo wangu,kama Zitto atagombea nafasi hiyo ndani ya chama na chama kikamteu kwa kuzingatia muafaka ndani ya chama NITAMUUNGA MKONO.Hata makala hii NIMEIUNGA MKONO.Tatizo tumezoea kuwa na wanasiasa wanafiki na wanaofanya hila kwenye siasa.sijui ni nani alisema kuweka msiamo wako wazi ili watu wakujue na wakupime bila kuathiri utangamano ndani ya chama ni tatizo?

Nina uhakika makala hii iliyoandikwa na Zitto,kwenye jina lake angekuwa ameandikwa mwingine mjadala ungekuwa tofauti.pia niweke wazi sina Alliance yoyote ndani ya chama,na hata hivyo ninashangaa sana watu wanaoharamisha siasa za Alliance.Tangu lini siasa za Alliance zikawa haramu?Nilishawahi kusema tena,siasa za alliance haziepukiki.

Hata chama changu kilifanya alliance na NCCR-Mageuzi mwaka 1995.Mwaka 2000 Chadema hakikusimamisha mgombea urais kwa kuwa kilifanya alliance na CUF na mwaka 2005 chama kilisimamisha mgombea urais halikadhalika mwaka 2010.Kama kijana ninayeelewa vyema nadharia za siasa na kwa vitendo napata shida kuona baadhi ya watu wenye akili timamu wanataka kuharamisha siasa za Alliance.

Kenya mwaka 2002,siasa za Alliance ndizo zilizoiondoa brutal party (KANU) madarakani. Raila Amolo Odinga alimuunga mkono Mwai Emilio Kibaki wa chama cha DP.Pale Uhuru Park Raila alimu-endorse Kibaki kwa kusimamia "Kibaki Tosha".Muungano wa NAARC ulifanikiwa kukipoteza chama tawala cha KANU katika ramani ya siasa za Kenya.
Uchaguzi wa juzi hapo Congo DRC,Mgombea wa Upinzani nusura amuangushe the Incumbent Joseph Kabila baada ya kufanya alliance na wagombea wengine.Tshisekedi aliiungwa mkono hadi naJean pierre Bemba akiwa The Hague

Tusiharamishe vitu bila kufuat principle za siasa kwa kusukumwa na utashi binafsi na matamanio ya upotoshaji tu.Sasa wanaosema kuhusu kuunga mkono hoja ya kutanua wigo wa ugombea urais,wanaopinga hawaji na logic yoyote kisiasa,kisheria wala kiuchumi.Mwandishi na mwanafalsafa Nguli Jenerali Ulimwengu aliandika kuhusu hili kwenye makala yake nadhani ni the East African Standard wiki 2 zilizopita.Nilifurahi jinsi alivyojadili hili ndani ya mantiki na kujenga hoja nzito ya kiunafalsafa.Hakuna mtu aliyemuhusisha na alliance,pia mwandishi mahiri na msomi aliyebobea Comrade Ayoub Rioba ameandika makala kuhusu hili na akaitendea haki taaluma yake na kufafanua kwa weledi kuhusu hili jambo.Hakuna aliyemuhusisha na Alliance.Ninachoona hapa ni hofu zaidi kuliko logic.

Jamii forums(Where we dare to talk openly) ni jukwaa la hoja ndani ya mantiki na inajulikana hivyo.Pia,tusikubali kuyumbishwa na upotoshaji wa watu wachache kwa maslahi yao tu.

Vijana msikubali/tusikubali kutumika kama daraja kwa baadhi ya wanasiasa.kuna baadhi ya wanasiasa wana-take advantage ya matatizo ya vijana hasa ajira n.k. mmewasikia CCM wakigombea hoja ya ukosefu wa ajira upande mmoja ukitoa takwimu na upande mwingine ukitoa tuhuma.Aliyeituhumu serikali alikuwa waziri mkuu na alikuwa na uwezo wa kulisiammia hilo angalao angetoa data kwamba alilisimamia hapa hadi pale serikali ikashindwa.kumbe mwenzetu tunaweza kumhoji ilikuwaje akasimamia mradi wa shule za kati huku akijua sera hiyo inakuja kutuzalishia failures ambao leo hii ndiyo wako mtaaani na kulifikisha taifa katika alarming stage.(bomu linalokaribia kulipuka)Upande mwingine wa CCM hawakuonyesha jitihada zozote zaidi ya kutoa takwimu na kumshambulia kada wao aliyejiuzulu uwaziri mkuu bila kutoa suluhisho au kuainisha mkakati madhubuti wa kupamabana na tataizo hilo. Hii inaonyesha ni jinsi gani wanasiasa hawa walivyozoea kutumia mataizo ya vijana kujipatia political mileage

Tusikubali kucheka na wale waliochangia taifa hili kufikia hapa,tufanye kazi na tuungane na wale wanaotekeleza kwa vittendo yale wanayosema.Vijana tusikubali sasa kuamuliwa hatima yetu kwa kigezo tu cha umri ati mtu akishafikisha umri wa miaka 40 tayari ana hekima na busara.Katika mikataba yote ya ufisadi hakuna katibu mkuu yoyote wa wizara ambaye alikuwa below 40,wote walikuwa juu ya miaka 40. Hizi ndizo buasara tunazosimamia?

Zitto kuweka hadaharani msimamo wake hakuna tatizo lolote.Mbona wenzetu huko magharibi tunakoiga demokrasia wanaweka misimamo yao mapema?Seneta Barack Obama aliweka nia yake hadharani mwaka 2004,ndiyo 4 years before General Election.Iweje leo hili suala liwe tatizo?au huwa tunaangalia majina ya watu?hebu tujenge hoja ndani ya mantikiVijana tusikubali kuwa daraja,tusikubali kufanywa door mart.

Tatizo kubwa ninaloliona hapa ni kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi bila kuaandaa watu kifikra.Lazima tuapambane na hii status quo haramu.Vijana tujisimamie,tujenge taifa lenye kuzingatia merits na siyo hisani.Tusitumie kigezo cha dini,kabila wala rangi na tusitumie kigezo cha umri bali tuzingatie uwezo wa kufikia kule kwenye change,not only change but Radical change/reforms.

Sasa hili ndilo lengo la Youths patriotic movement(YPM) iliyozuiwa katika usajili kwa ghiliba za wanasiasa wachache wenye hofu na matamanio mfu tu.We are an assemblage of young Tanzanins whose primary aim is to change the course of governance, not from the sidelines this time, but from inside the system. We plan to build a membership of, at least, 20 million people -from every tribe and religion - who will participate in educating Tanzanins about the need to destroy the existing order that is fast running our country out of existence and instituting a new order that will birth equity, fairness, justice and development for all. We will be partisan becausepolitics is too serious a business to leave for the politicians alone.


We will participate fully in the politics of this country. Our army of 20 million people will organize themselves, pick intelligent, courageous, transparent and detribalized candidates for all positions in the 2015 elections and run their campaigns from ground up. There is no age limit, but leadership of the movement will be restricted to young people alone.We are tired of just becoming critics. Aluta Continua isn't one of our favorite quotes. We won't continue with the struggle. WE SIMPLY WILL END THE STRUGGLE by ending the grip of the corrupt in our polity. We owe our generation the duty of saving this country, building it to become a force to be respected in the world, and passing down to our children a nation they can be proud of.
 
Mkuu Ben inaonekana post yako ni nzuri lakini haisomeki vyema nimefika katikati nikashindwa kuendelea naona kama kiwi ya macho vile. Ifanyie uhariri kidogo. Kwa kuwa ni ndefu basi ongeza font ili tuisome vizuri.
 
Badala ya vyombo vya habari kuzidi kuanika hila zinazotaka kufanywa na wajanja kupokonya haki ya CDM kule Arumeru,leo magazeti yote yalikuwa yakitangaza nia ya mtu mmoja aliyetangaza rasmi nia yake ya kugombea urais 2015.Wito wangu kwa wanaCDM wote endeleeni kuungana katika kipindi hiki kigumu cha kufa na kupona kule Arumeru.Msikubali myumbishwe na yeyote.Nimepata taarifa mgombea wetu kule Arumeru amehuzunishwa sana na haya mambo ya kutangaza nia za urais leo.Ninampa moyo mgombea wetu huyo kwamba asiwe na hofu yeyote kwa sababu viongozi wote wenye nia ya kweli wako pamoja naye.Wanachama ondoeni hofu chama kiko imara kabisa na Arumeru tutashinda.Kutangaza kugombea urais si hoja bali hoja ni kuaminiwa na wenzako kwamba wewe ni mwenzao.Nani asiyejua hata msaliti Shibuda alitangaza nia ya kugombea urais 2010? Kwa hiyo wanachama wasishangae huenda Shibuda naye akatangaza nia yake kuomba kugombea urais kupitia CDM wiki ijayo.
 
Ndugu zangu. Naomba msome makala nzima kabla ya kuchangia. Msichangie kwa kusoma kichwa cha habari tu. Hii ni makala nimeandika kama majibu kwa makala ya mwanazuoni mmoja kuhusu umri wa Urais.

Nimesema wazi, kuutaka Urais na kuupata ni mambo mawili tofauti. Kwanza lazima chama changu kiniteue. Kama chama kikiona bado lazima nikubaliane na chama. Kama chama kikiona kuna mwanachama mwingine ana uwezo zaidi yangu lazima nimwunge mkono huyo. Hata kama chama kikiniteua lakini wananchi lazima wakubali. Kwa hiyo unaweza kuutaka Urais lakini usiupate!

Pili nimejibu hoja za ubaguzi, hatari na matabaka za mwanazuoni huyo. Ni vizuri MoD akachukua makala hiyo na kuiweka juu kabisa ili watu wachangie jambo walilolisoma.

Miye nitaweka makala hiyo kwenye blog yangu zittokabwe.com

kuna Kaushauri labda naweza kukutupilia kidogo..
kwanza ujue mimi nafurahi na kuunga mkono matamshi, michango na vuguvugu la wabunge wetu hasa Vijana wa vyama vyote vinavyoliunda Bunge, Kumbuka Mhe Sita aliwahi kusema vijana wabunge hukesha kwenye maktaba za Bunge wakikokotoa taarifa na kujenga semi zenye hoja na mashiko wanapowakilisha maada au wanapouliza maswali.. na Hutoa Changamoto chanya kwa serikali. Na Kumbuka Mhe Zitto ulijichotea umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi yako. kuna kitu kina nituma niwaze kwamba kipindi kile ulikuwa wewe kama wewe Zito ukitegemea hazina ya mawazo na utashi wako. Lakini Zito wa Leo umebadilika sana, sizuiliki kuwaza pia kwamba umezungukwa na mamluki wapambe ambao inawezekana kula yao inategemea na uhai wako, na wapambe hao mara zote ni ndio mzee, na ushauri wao daima umekuwa ukikuzuzua, ukikulimbuka. sidhani kama una muda wa kusoma na kuelewa utitiri wa vyombo vya habari ambavyo kila kukicha kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakikuandika, kwa maana hiyo mara zote lazima utegemee taarifa za marafiki na "feedback" zako. Nadhani hupewi taarifa sahihi kutoka kwa wapambe hawa. mara baada ya uchaguzi ulikumbwa na wingu baya la kuchukiwa sana na wale waliokupenda, na unakumbuka mama mmoja alipiga magoti ndani ya Ndege alipowaona mabosi wa chama chako akiwalilia wakung’oe kwenye chama haraka ila nadhani mabosi wale walimjibu vizuri kwa hakma ingawa hawakutarajiwa kupatwa na ugeni ule ndani ya chombo cha usafiri.

Najua wewe ni mwoga sana inapotokea kitu physical atack, ndio maana mara zote kwenye mikiki ya chama hutokei anyway hakuna mwenye nafasi ya kukuhukumu kwa hilo kwa sababu sisi binaadam wote tuna degree tofauti za woga. lakini una uwezo wa kushawishi ambao ni kitu kizuri kwenye medani ya siasa. SASA niseme kwa uwazi tu kwamba UMEKOSA WASHAURI WAZURI. na ukiendelea na tabia hii utajikuta unatokomea gizani kwenye pori la wasiojulikana tena kwa aibu.
Hoja yako uliyolimwa na mwana zuoni ambaye unajua ni si wa chama chako, unatutumuka this way kumjibu sidhani kam ni dhana yenye mantiki.. mwanasiasa gani aliyekomaa yuko hivi. ina maana kila post ikiandikwa kuhusu wewe lazima uijibu?, zito kanya karimjee..."utajibu", zito kaiba kuku .. "Utajibu" zito kampiga flan.. ujibu, utajibu mangapi.. si kujibu kunako leta maana but why now, why soon.. Yaani huna moyo wa kusikiliza neno na kulihifadhi.. Unashindwa hata na Lowassa, kasemwa mangapi na hawa "mboga za CHAMA" .. mwaka mzima ila jamaa yuko kimya na ilipotengwa CC ya chama chake akajimimina vilivyo, sasa wewe hata hujui wapi useme nini kiongozi gani Jukwaa hili na majukwa mengine yote ya mitandaoni ni majukwaaa huria. Yanatiwa mikono na raia wa aina mbalimbali, watoto kwa wakubwa.. seuze ni mwanafunzi tu wa chekechea aliyeleta hoja ile umejitutumua this way kumnanga kwa majibu. Wewe kiongozi wa wapi usiyejua kwamba kuna vikao halali ndani ya Chama ambavyo unaweza kuweka vuguvugu lako. Upwayukaji wa namna hii mapema kiasi hiki unanipa shaka sana. Si bure unaweza kuwa na kasoro. Wagonjwa wengi walioathirika na propaganda za kisiasa si rahisi wakakiri kwamba hapo kuna tatizo. Usikariri siaza za kizayuni na za nje wala historia. Jamii ya Tanzania ni tofauti sana na jamii za Nchi nyingine Duniani. Nakushauri Pata washauri makini, linda sana Kinywa chaweza ponza kichwa. .. Kama una maarifa utaelewa usipoelewa hayanihusu.. if you lost who cares.. na akina muddy mdogo (mtoi) watalost vilevile..
 
USHAURI WA BURE KWA BWANA ZITTO

Nimesoma vizuri sana makala yako uliyomjibu huyu mwandishi ambaye hukupenda kumtaja japokuwa anaonekana kabisa, kwa hoja zako, kutokuwa na imani na vijana katika utawala wa sasa. Mh. Zitto umejipambanua vizuri kabisa namna ulivyo, mafanikio yako na muonekano wako katika jamii. Aidha, umejaribu kuonyesha ni namna gani umekuwa ukijijenga kupitia wasomi na watu mbalimbali kama ulivyowaorodhesha. Hata hivyo nafikiri hukumaanisha kuwa DR. Lwaitama ni mtaalam wa lugha bali ni mtaalam wa Falsafa.

Mh. Zitto, mimi ni kijana wa rika lako na ninayevutiwa sana na mwenendo wako kisiasa. Nimekufahamu kitambo sana tangu harakati zako za kisiasa pale chuo kikuu Dar es salaam. Ni jambo lisilopingika kwamba kwa sasa wewe ni very hot kisiasa hasa unapokuwa unapanda majukwaani. Kipindi fulani ulianza kupungua umaarufu wako na minong'ono ilikuwa imeshaanza kueenea kwa wananchi kuwa wewe si yule waliyemtumainia. Labda niseme hivi; katika maandiko (siyo ya Mungu) tunasoma, watu wanatabia ya kuchoka/kukichoka kitu hata kama ni kizuri. Hata amani walionayo watu wanaweza kuichoka. Kadhalika, hiki ndo kinachojitokeza kwa chama kilichoko madarakani sasa. Mh. Zitto, jahazi ulilopanda sasa ni CDM ambalo wananchi waliowengi, watoto, vijana, makamo na hata wazee wanaona ni jahazi lililo imara na litawafikisha kule wanakokutarajia. Jahazi hili linakubalika machoni, mioyoni na hata masikioni mwa watu.

Ukitumia moyo wako huu wa uzalendo wa kuendelea kukijenga chama hiki ambacho kwa sasa kinapendwa na watu walio wengi, ukashirikiana vizuri na viongozi wandamizi waliopo, nyota yako haitazimika kamwe. Kwa sasa itakuwa ni mapema mno bwana Zitto kugombea uraisi. Kitu nilichokifurahia kwako ni kwamba you are thinking on bigger things. Nina uhakika kama utaendelea hivi na ukavumilia kidogo, utaongoza nchi hii tena kwa ridhaa ya wananchi walio wengi na si kama kwa viongozi wetu wa sasa. I think Dr. Slaa deserves to be our next presedent. Let it be, you will be blessed.
 
Badala ya vyombo vya habari kuzidi kuanika hila zinazotaka kufanywa na wajanja kupokonya haki ya CDM kule Arumeru,leo magazeti yote yalikuwa yakitangaza nia ya mtu mmoja aliyetangaza rasmi nia yake ya kugombea urais 2015.Wito wangu kwa wanaCDM wote endeleeni kuungana katika kipindi hiki kigumu cha kufa na kupona kule Arumeru.Msikubali myumbishwe na yeyote.Nimepata taarifa mgombea wetu kule Arumeru amehuzunishwa sana na haya mambo ya kutangaza nia za urais leo.Ninampa moyo mgombea wetu huyo kwamba asiwe na hofu yeyote kwa sababu viongozi wote wenye nia ya kweli wako pamoja naye.Wanachama ondoeni hofu chama kiko imara kabisa na Arumeru tutashinda.Kutangaza kugombea urais si hoja bali hoja ni kuaminiwa na wenzako kwamba wewe ni mwenzao.Nani asiyejua hata msaliti Shibuda alitangaza nia ya kugombea urais 2010? Kwa hiyo wanachama wasishangae huenda Shibuda naye akatangaza nia yake kuomba kugombea urais kupitia CDM wiki ijayo.

Kama kweli hali hii imemuathiri kisaikolojia mgombea wenu kule Arumeru Iam very dissappointed with Zitto
 
it is true bro,if u have a will,u have achieved half of your success.Be patient,the time will tell who is to do what.it is very early to anounce the tournament...got me?
 
Mungu akubariki kwa kumwonyesha nia kamanda
kuna Kaushauri labda naweza kukutupilia kidogo..
kwanza ujue mimi nafurahi na kuunga mkono matamshi, michango na vuguvugu la wabunge wetu hasa Vijana wa vyama vyote vinavyoliunda Bunge, Kumbuka Mhe Sita aliwahi kusema vijana wabunge hukesha kwenye maktaba za Bunge wakikokotoa taarifa na kujenga semi zenye hoja na mashiko wanapowakilisha maada au wanapouliza maswali.. na Hutoa Changamoto chanya kwa serikali. Na Kumbuka Mhe Zitto ulijichotea umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi yako. kuna kitu kina nituma niwaze kwamba kipindi kile ulikuwa wewe kama wewe Zito ukitegemea hazina ya mawazo na utashi wako. Lakini Zito wa Leo umebadilika sana, sizuiliki kuwaza pia kwamba umezungukwa na mamluki wapambe ambao inawezekana kula yao inategemea na uhai wako, na wapambe hao mara zote ni ndio mzee, na ushauri wao daima umekuwa ukikuzuzua, ukikulimbuka. sidhani kama una muda wa kusoma na kuelewa utitiri wa vyombo vya habari ambavyo kila kukicha kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakikuandika, kwa maana hiyo mara zote lazima utegemee taarifa za marafiki na "feedback" zako. Nadhani hupewi taarifa sahihi kutoka kwa wapambe hawa. mara baada ya uchaguzi ulikumbwa na wingu baya la kuchukiwa sana na wale waliokupenda, na unakumbuka mama mmoja alipiga magoti ndani ya Ndege alipowaona mabosi wa chama chako akiwalilia wakung'oe kwenye chama haraka ila nadhani mabosi wale walimjibu vizuri kwa hakma ingawa hawakutarajiwa kupatwa na ugeni ule ndani ya chombo cha usafiri.

Najua wewe ni mwoga sana inapotokea kitu physical atack, ndio maana mara zote kwenye mikiki ya chama hutokei anyway hakuna mwenye nafasi ya kukuhukumu kwa hilo kwa sababu sisi binaadam wote tuna degree tofauti za woga. lakini una uwezo wa kushawishi ambao ni kitu kizuri kwenye medani ya siasa. SASA niseme kwa uwazi tu kwamba UMEKOSA WASHAURI WAZURI. na ukiendelea na tabia hii utajikuta unatokomea gizani kwenye pori la wasiojulikana tena kwa aibu.
Hoja yako uliyolimwa na mwana zuoni ambaye unajua ni si wa chama chako, unatutumuka this way kumjibu sidhani kam ni dhana yenye mantiki.. mwanasiasa gani aliyekomaa yuko hivi. ina maana kila post ikiandikwa kuhusu wewe lazima uijibu?, zito kanya karimjee..."utajibu", zito kaiba kuku .. "Utajibu" zito kampiga flan.. ujibu, utajibu mangapi.. si kujibu kunako leta maana but why now, why soon.. Yaani huna moyo wa kusikiliza neno na kulihifadhi.. Unashindwa hata na Lowassa, kasemwa mangapi na hawa "mboga za CHAMA" .. mwaka mzima ila jamaa yuko kimya na ilipotengwa CC ya chama chake akajimimina vilivyo, sasa wewe hata hujui wapi useme nini kiongozi gani Jukwaa hili na majukwa mengine yote ya mitandaoni ni majukwaaa huria. Yanatiwa mikono na raia wa aina mbalimbali, watoto kwa wakubwa.. seuze ni mwanafunzi tu wa chekechea aliyeleta hoja ile umejitutumua this way kumnanga kwa majibu. Wewe kiongozi wa wapi usiyejua kwamba kuna vikao halali ndani ya Chama ambavyo unaweza kuweka vuguvugu lako. Upwayukaji wa namna hii mapema kiasi hiki unanipa shaka sana. Si bure unaweza kuwa na kasoro. Wagonjwa wengi walioathirika na propaganda za kisiasa si rahisi wakakiri kwamba hapo kuna tatizo. Usikariri siaza za kizayuni na za nje wala historia. Jamii ya Tanzania ni tofauti sana na jamii za Nchi nyingine Duniani. Nakushauri Pata washauri makini, linda sana Kinywa chaweza ponza kichwa. .. Kama una maarifa utaelewa usipoelewa hayanihusu.. if you lost who cares.. na akina muddy mdogo (mtoi) watalost vilevile..
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom