nina ombi kwako mheshimiwa mtema,naomba hii budget yao ya kitapeli ipitishwe kila mkoa kutapokuwa na maadamano na ichambuliwe ili wananchi wa chini especially vijijini waone utapeli wa seriakali yao. hatuna uwezo wa kufanya lolote kwa maana ya kuikataa kwa kura kwa maana wako wengi bungeni lakini tutachoweza kukifanya ni kwenda straight kwa wananchi na kuwa expose jinsi walivyo.
Dr. Slaa itisha maandamano tupinge usanii, jamaa wameshajisahau wanadhani enzi za TANU
8. Mheshimiwa Spika, Bajeti ya mwaka 2011/12 itazingatia
vipaumbele vifuatavyo:
i) Umeme;
ii) Maji;
iii) Miundombinu ya usafiri na usafirishaji (reli, bandari,
barabara, viwanja vya ndege, Mkongo wa Taifa);
iv) Kilimo na umwagiliaji; na
v) Kupanua ajira kwa sekta binafsi na ya umma.
Wakati wa faini za 20,000 mbona chenge alipigwa 700,000? Jee si kosa la barabarani?
Kwanza nilishitushwa na kujibu budget kwa Zitto kwa muda mfupi kiasi hichi... pili nikasema hawa watu si wana nafasi jumatatu. Mwisho kumbe kweli ameleta mazagazaga.
Zitto mbunge wangu ninayekuamini sana acha papara... budget ya serikali imeandaliwa na watu wengi... it is possible to get fault on it... lakini be sure... kwamba wenzako waliangalia mengi zaidi. yako... so be carefully...huna uwezo hata ungekuwa kipanga wa namna gani kuzidi vichwa wa wataalamu wengi... that is it... angali sasa tunajadili budget yako ya uongo na sio ya Mkulo.
Wakuu, pendekezo la Zitto Kabwe la kutumia asilimia 4 ya "Skills Development Levy " iliyokuwa inaingia serikali kuu kusomesha vijana wetu limetekelezwa kwenye bajeti ya mwaka 2011/2012.
Nanukuu
"79. Mheshimiwa Spika, napendekeza kufanya marekebisho kwenye sheria ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, SURA 82 kama ifuatavyo:
Kufanya marekebisho katika mgawanyo wa mapato yatokanayo na tozo ya kuendeleza ufundi stadi (Skills Development Levy) ya asilimia 6 ili asilimia 4 zipelekwe kwenye Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, na asilimia 2 zipelekwe Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Vocational Education and Training Authority - "VETA"). Lengo la hatua hii ni kuongeza fedha za mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu.
Hatua hii katika Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi haitarajiwi kupunguza wala kuongeza mapato ya Serikali."
1. Nadhani Zitto anajua kuwa nishati hapa Tanzania hujengwa kutokana na misaada na mikopo kutoka nje.Hata TANESCO hutafuta funds na mikopo kutoka nje ya serikali kwa ajili ya miradi mbalimbali,mfano ule wa kusambaza umeme kilomita 667 toka Iringa mpaka shinyanga ambao umekuwa funded na European Investment Bank,shs bilioni 150...je ulikuwa kwenye bajeti yoyote?
2.Kulipa deni la taifa ni moja kati ya matumizi ya maendeleo,ina facilitate uwezo wa kupata mikopo.
3. Kuhusu posho, ni wajibu wetu watanzania, hasa wafanyakazi wa serikali kuamua au kujitolea kutokuzipokea au kuomba kupunguziwa kwa asilimia hamsini..... hapatakalika!
4. Jumatano nakuchallenge Zitto, usome bajeti itakayoonyesha vyanzo mbadala vya kodi na makato ya matumizi, ili elimu iwe bure!...cos you promised this in your campaigns na ilani ya CDM, kama haita-include free education huo utakuwa ni uhuni tu! Ninayo video ya Mnyika akielezea what you will do in your first year kwenye utawala kama mngepata ridhaa.
inatakiwa awajibishwe bunge ni mahala patakatifu, mkulo alikusudia kuwapotosha wananchi kupitia chombo tukufu akisaidiana na wanamagamba kutuuzia mbuzi kwenye gunia