Zitto Kabwe: "UKs Aid is reparation for colonial exploits"

Status
Not open for further replies.
Viongozi wanaotumia ukoloni kama kisingizio cha umaskini wetu ni wa kuwaogopa kama ukoma. Wengi wao hutumia excuse hiyo kutowajibika kwa wananchi, huku wakijilimbikizia mali ya umma, na hali ikiwa mbaya, hukimbilia huko huko kwa hao wakoloni ambako wameshajinunulia majumba ya kifahari, na kujiwekea akiba za mamilioni ya dollar. Zitto has to be very careful na kauli yake hii, kwani ni rahisi sana kuzidi kubomoa kuliko kujenga.

Makombo ya mezani unaita reparation? Mbona wanafurahi wenyewe.

Viongozi kama Zitto wanaoendekeza kutafuta majibu rahisi kama ukoloni kwa maswali magumu kama "kwa nini sisi masikini?", au hata kujivika kilemba cha ukoka kwamba wanaweza kuongelea "reparation" inavyotakiwa tu.

Kuna proponents wa reparation wa kweli wanatokea kwenye Garveyite families huko wanajua reparation ni ninii wakimsikia anai debase na kuilinganisha na vimsaada anavyotoa Muingereza kwa hiyari yake wanaweza kutaka kumtundika mtini.

Utasemaje msaada unaotolewa baada ya watu kuridhika na bajeti zao, kubakisha crumbs on the table ngoja tuwatupie waafrika wana njaa hawa ndio ziwe reparation?

Lakini wa kuogopwa zaidi ya hawa wanaotaka kupanda mgongo wa common least denominator ya Watanzania karibu wote (kuchukia dhuluma tuliyofanyiwa wakati wa ukoloni, ambayo ni ya kweli) ni wale viongozi wanaoendeleza ukoloni wa mtu mweusi dhidi ya mtu mweusi, mtanzania dhidi ya mtanzania.

Kama utawala wa CCM vile.

Kwa sababu, hata tukisema tusihesabu mabaya yote, CCM wangetupa elimu tu, utawala wa CCM ungehakikisha mtoto wa Kigoma anapata elimu bora, labda tusingekuwa na kina Zitto leo.


Wakuu, haswa Kiranga, hiyo notion ya reparation viongozi wetu wa kiafrika ndivyo wanaitafsiri. Ebu som hapa chini"

"The perception of the reparation issue is fundamentally different for Africans than for African Americans..............In particular, the African reparation movement concentrates on debt forgiveness rather than the educational and social reforms sought in the United States........."

Hawa viongozi wanachukulia hilo suala kwa kutaka kusamehewa madeni wakati Garveyism inachukulia suala la reparation katika mtazamo huu:
......."whatsoever things common to man that man has done, man can do".Therefore Africa can become as glorious and profoundly advanced in the scientific and technological realm as any, when Africans will it to be....."

Lakini viongozi kwa kuchukulia suala la reparation katika kupata msaada na misamaha ya madeni, mwisho wa siku mambo yanakua hivi:

".......... some commentators contend that the West is not at all responsible for the conditions of Africa.They contend that “many of the African colonies progressed very rapidly during colonial rule, much more so than the independent countries in the same area.”............ “Difficulties of servicing these debts do not reflect external exploitation or unfavourable terms of trade. They are the result of wasteful use of the capital supplied, or inappropriate monetary and fiscal policies........”

Kuna article moja ya zamani kidogo, 2002, inaitwa The African Holocaust: Should Europe Pay Reparations to Africa for Colonialism and Slavery?, imeandikwa na Ryna Michael Spitzer na kuchapishwa katika Vanderbilt Jolurnal of Transnational Law, volume 35. Jamaa kaongelea masuala mengi sana ambayo nadhani pia Zitto (kama hajawahi kuisoma hiyo article) itamsaidia
 
Naamini kabisa kama wao waliweza sisi pia tunaweza kama tutawezeshwa kwa Policies ambazo zitawajenga kwanza wananchi wake na sio kutegemea wageni iwe kwa misaada au uwekezaji..Kuna matajiri wengi sana Dar nimewaona mimi enzi zetu wakiwa na vibanda (kiosk)vya kuuza urembo wa wanawake, kimbo na sabuni mitaani leo ni mabillionea, Kina Bakhresa walianza kama washona viatu leo mabillionea tena tajiri kuliko mashirika ya wazungu wengi tu..Kwa nini taifa liwe tegemezi kwa wazungu ikiwa tunaweza kabisa kuanza toka ndani..

sababu na misingi ni UNAFIKI wa Mwafrika!... tunauzana wenyewe kwa kupewa Unyapala.. viongozi wetu wote ni manyapala na ukielewa hilo sidhani kama utaona taabu kuelewa kwa nini sisi maskini.. How can we have Gold yetu ndani ya ardhi yetu waje watu wachimbe watuachie ruzuku ya 3% na tunadai hii inatosha tena kubwa sana ukilinganisha na....Hivi Amerika miaka ya 1700 walipogundua dhahabu waliwaita kina nani kwenda kuichimba?

Viongozi wetu wenyewe akili zao zinawaza katika kuomba misaada na wawekezaji nje tu. Juzi mmemsikia Kikwete kwa mara ya kwanza akijaribu kujibu kwanini Tanzania ni masikini wakati ipo endowed na abundant natural resources; akasema kwamba kwa sababu hatuna wawekezaji, na wawekezaji walio kwenye kichwa chake ni kina Paul Jones and the like. Hawezi kuwaza kwamba hata kina Mengi, Bakhresa et al. nao wanaweza kuwa wawekezaji kama kipaumbele kikiwepo.

Pia juu ya suala la "Hivi Amerika miaka ya 1700 walipogundua dhahabu waliwaita kina nani kwenda kuichimba?" linaingia katika mentality ya viongozi wetu (juu ya uwekezaji) na pia suala la Balkanisation nalo linachukua nafasi kwani linafanya mataifa kama Tanzania kuendelea kuwa tegemezi kwa westerners.
 
yap na ndio maana huwa nawauliza watu hivi hawa wazungu walipogundua dhahabu na mafuta huko kwao walimwita nani kuja kuchimba? Si walichimba wenyewe, tena wakati huo hawana uwezo, nyenzo wala usafiri kama tulonao leo ktk masoko... Sasa kwa nini sisi tunataka Utajiri wa haraka sana kwa kufanya Umalaya ili tuwe kama wao ama tupewe ranks kulinganisha na wao?.

Hawa watu wote wanaopongeza Ukolonimambo leo hawana tofauti na malaya ambaye anafikiri akiuza mwili wake atatoka ktk umaskini na kupata utajiri haraka sana...Na hakuna kitu kibaya zaidi kama kufanya umalaya kwa shida, hapo ndipo utalishwa hata unga na kuwa kijiwe((addicted)..sio tu hutakuwa tajiri bali utafupisha hata maisha yako. Hizo HongKong, SouthAfrka na kadhalika walitumiwa tu kama malaya wa Cuba Club.. Yes ukiwaona mitaani wana magari ya nguvu na nyumba Masaki lakini nyuma ya pazia, wanawake hawa hulala na hata mbwa kuwafurahisha mabwana zao... Mtanisamehe kutumia lugha mbaya, lakini my message ni kwamba hatuna sababu ya kujifananisha na Hongkong wala South Afrika..We are who we are!..

Ni wakati watanzania tunatakiwa kuipenda nchi yetu, tufikirie sisi tunaweza vipi kuijenga nchi yetu maana haiwezekani misaada hii kutusaidia ikiwa inatulazimu kuwa malaya or to be Down low!..tukilaani ushoga kumbe!..
.

Mkuu uwa nakubaliana sana na mambo unayoyachambua. Umenena vyema hapo juu.

Lakini suala la sisi kama nchi kujifananisha na mataifa mengi kwa masuala fulani haliepukiki katika kujifunza. Mfano, tunaweza kujiuliza kwamba kwanini tiger economies ambazo almost zilikua katika kiwango sawa cha uchumi na Tanzania miaka ya 1960, lakini sasa wapo mbali? Au kwanini mataifa yaliyokua pia yametawaliwa kama Marekani, viongozi wake hawalalami katika kuomba misaada kutoka kwa watawala wao wa zamani?!


Hoja yako ya mwisho ndiyo ya msingi. Lakini napo pia tutajiuliza kwa vipi? Ukichukulia viongozi wetu (haswa kiongozi mkuu) ni mendicants? Mimi nadhani jibu suluhisho sahihi ni katika kuweka misingi ya kupata viongozi ambao wenye kuamini katika self-reliance. Kiongozi ambae anaweza kusema hataki msaada wowote kutoka nchi za maghabiri hata masharti yawe laini kama mlenda.

Hapo napo kuna changamoto; kwani kwa hali ya sasa sijaona kiongozi ambae anaweza kusema hayo maneno.
Labda watu kama wewe mkuu ukijotokeza naweza kuanza kupata imani ya kwamba taifa litaondoka katika mendicancy!
 

Money given in aid by the people of the United Kingdom to Tanzania is reparationfor colonial exploits states Tanzanian M.P. Zitto Kabwe.

The "country was built by colonial exploitation. Whether your born or not. We can as well survive without youraid, take it" he says.

Zitto Kabwe is a member of the Tanzanian Parliament (CHADEMA), representingKigoma North and is Shadow Finance Minister and Chairperson for Tanzania'sPublic Investments Committee. He is therefore a man that shapes governmentpolicy in Tanzania.

In times of unprecedented recession in the UK, I am sure that most would indeed like to stop aid to a country whose policy makers display these kind of sentiments when you scratch the surface!

Pole Sana Tanzania!

Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
@Chomachomp your country was built by colonial exploitation. Whether your born or not. We can as well survive without your aid, take it.

Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe11 Jan11 Jan@Chomachompyour case is genuine totally but don't link to aid Tanzania gets from UK. Your country's aid is reparation for colonial exploits




--------
Zitto's response to this thread:



Evidence Mr. Kabwe?

Quote from Zitto:

Ndugu zangu. Nadhani ni hekima kujua Jambo kwa kina kabla ya kuanza kulitolea maneno na hukumu.
Ninaomba kueleza kifupi sana nini kilitokea huko twitter


Mh. Zitto, nadhani ni hekima zaidi ukiwa na ufahamu kwamba wewe ni mmoja wa viongozi wetu muhimu sana wa kizazi hiki, katika nyakati hizi muhimu. Kwahiyo kila unapotoa tamko, watanzania wanakusikiliza, wote - wale wenye nia njema na nia mbaya na wewe. Ni muhimu ukalijua hilo ili kama ikibidi kukwepa kutoa kauli au misimamo yako pale pasipo na ulazima basi ufanye hivyo. Lakini endapo kuna umuhimu wa kutoa msimamo au kauli yako, kama hiyo mada, ambayo sasa tumeelewa baada ya ufafanuzi wako, jaribu kutafuta jukwaa ambalo utakuwa na nafasi ya kujieleza ili watu wakuelewe, na wasipinde mambo. Kwa mtazamo wangu, tweeter sio sehemu nzuri ya kufanikisha hilo.
 
yap na ndio maana huwa nawauliza watu hivi hawa wazungu walipogundua dhahabu na mafuta huko kwao walimwita nani kuja kuchimba? Si walichimba wenyewe, tena wakati huo hawana uwezo, nyenzo wala usafiri kama tulonao leo ktk masoko... Sasa kwa nini sisi tunataka Utajiri wa haraka sana kwa kufanya Umalaya ili tuwe kama wao ama tupewe ranks kulinganisha na wao?.

Hawa watu wote wanaopongeza Ukolonimambo leo hawana tofauti na malaya ambaye anafikiri akiuza mwili wake atatoka ktk umaskini na kupata utajiri haraka sana...Na hakuna kitu kibaya zaidi kama kufanya umalaya kwa shida, hapo ndipo utalishwa hata unga na kuwa kijiwe((addicted)..sio tu hutakuwa tajiri bali utafupisha hata maisha yako. Hizo HongKong, SouthAfrka na kadhalika walitumiwa tu kama malaya wa Cuba Club.. Yes ukiwaona mitaani wana magari ya nguvu na nyumba Masaki lakini nyuma ya pazia, wanawake hawa hulala na hata mbwa kuwafurahisha mabwana zao... Mtanisamehe kutumia lugha mbaya, lakini my message ni kwamba hatuna sababu ya kujifananisha na Hongkong wala South Afrika..We are who we are!..

Ni wakati watanzania tunatakiwa kuipenda nchi yetu, tufikirie sisi tunaweza vipi kuijenga nchi yetu maana haiwezekani misaada hii kutusaidia ikiwa inatulazimu kuwa malaya or to be Down low!..tukilaani ushoga kumbe!...

Upo sahihi. Ebu tazama wajasiriamali wenye mafanikio Afrika kama ni Dongate (Nigeria) ambae ni the richest black person in the world, Motsepe, (South Africa), Mohamed Ibrahim (Sudan) etc, hawa wote wakitaka kuingia Marekani au UK kwa pamoja, au mmoja mmoja ili kuwekeza kwa msuli mkubwa wataruhusiwa kweli? Sidhani. Watakuruhusu tu ununue shares zao kwenye masoko ya hisa, ingawa hata hayo ambayo wanatuhubiria umuhimu wake in an economy, ukiwaambia wasajili makampuni yao basi na huku kwenye visoko vyetu hivi vya hisa ili na sisi tufaidi na utajiri wao, wanagoma. Ebu tazama jinsi gani yule mtu kutoka Dubai mwenye shares kadhaa citigroup, wamarekani walisema sana hilo, lakini wakatulizwa kwa sababu mwisho wa siku, ana pump hela into the US economy; ebu tazama UK, hata kwenye umiliki wa timu za mpira, ikiwa ni mtu toka nje, ni malalamiko matupu.
 
Ndugu Mukandara,

Hoja yako kuhusiana na maada hii ni ya msingi kabisa. Kama alivyoeleza Ndugu Soby, Tanganyika ilikuwa Mandated Territory. Hii inamaanisha Jamii ya Kimataifa (wakati huo League of Nations) iliipa Uingereza madaraka ya kisheria ya kuindesha Tanganyika kwa niaba yake hadi hapo Watanganyika wagelikuwa tayari kujitawala wenyewe.

Kwa hiyo, kama mtoa hoja hiyo alivyosisitiza, Waingereza walikuwa wakiripoti huko huko kwenye League of Nations, kuhusu maswala yote ya Tanganyika. Kadhalika, hii inaeleza kwa nini wakati wa kudai uhuru (kumradhi kwa wale wanaopendelea neno 'kupigania' uhuru) Mwalimu Nyerere alikwenda makao makuu ya League of Nations huko Marekani badala ya kwenda Uingereza kwa shughuli hiyo.

Swali sasa ni ilikuwaje miaka 50 baada ya kujitawala tunajikuta katika hali hii? Kwa miaka hii 50 taifa letu limekuwa likiishi (na linaendelea kuishi) kwa misaada kutoka mataifa ya nje wakati mataifa mengine ya Kiafrika kama vile Botswana na Mauritius yamefanikiwa kuinua hali za maisha ya raia wake; na muhimu zaidi, hayatembezi mabakuli yakiomba kutoka Stockholm hadi Pyongyng. Siyo hiyo tu bali Tanzania ina rasilimali nyingi mno kiasi kwamba ikitumia rasilimali hizo vizuri, inaweza kujitegemea katika kipindi kifupi cha miaka 10. Ilikuwaje?!

Je, Waingereza wangelikuwa wanapenda kujibu maada hii si wangelisema: 'Ehe! Nyie vipi, hamuoni pesa ambazo tumekuwa tukiwapeni kusapoti bajeti na miundo mibinu yenu, kwa miaka hiyo yote, ni zaidi ya reparation mnayo zungumzia hivi sasa?'; na pengine wangeliongeza: 'Hivi inakuwaje mnalaumu kunguru kwa kushuka nchini mwenu na kudonoa mzoga kabla ya kulaumu mazingira yaliyo sababisha mzoga kuwepo katika nafasi ya kwanza. Hamjui kuwa bila mzoga kuwepo, kunguru hashuki? Come on be fair! Sisi Waingereza tunaongoza nchi yetu kulingana na maslahi ya taifa letu, na siyo yenu, na wala sisi siyo Mother Tereza au charity organisation ya namna fulani. Sisi ni taifa, linalowajibika kwa mlipa kodi wa nchi hii na ambaye ni chanzo cha fedha ambazo tumekuwa tukikupeni miaka nenda-rudi. Hivi mlizitumiaje hela hizo? Mliendeleza a luta continua tu kwa gharama ya maendeleo ya taifa lenu au vipi? Tafadhali, msitulaumu kwa matumizi mabaya au udokozi wa fedha za misaada tuliyokupeni' wangelimaliza hoja yao.

Ninakili lkwamba kwa sababu za kidiplomasia na maslahi-tajwa, Waingereza wasingeliweza kusema hiivi bayana. Wao wanafahamu vizuri zaidi namna ya kudili na watawala mafisadi wa mataifa changa; mafisadi wanaotumia nyadhifa zao kujilimbikizia mali kwa gharama ya mnyonge. La zaidi, wanafahamu fika kwamba viongozi mafisadi wa Kiafrika hupenda sana kufanya yale wafadhili wanayopenda kwa imani kwamba, kwa kufanya hivi, wafadhili hawatawabana warejeshe kwa wananchi utajiri waliopata visivyo halali (na bila kujirudia walioupata kwa kutumia nyadhifa zao). Isitoshe, wanafahamu fika kuwa hiki ndicho chanzo cha siasa nchini Tanzania kuwa ni biashara kubwa na ya aina yake na wala siyo art, kama inavyopashwa kuwa. Kadhalika wanafahamu kuwa mali nyingi viongozi mafisadi waliyonayo, mara nyingi, huificha huko kwao.

Lakini mbali ya ufisadi, sababu nyingine zilizotufikisha hapa tulipo zinafahamika kwa wana JF, hakika. Je, hatukuelewa tangu mwanzo kwamba services sector iki exert pressure kwenye sekta ya kuzalisha tungeliweza kuwa na matatizo kama haya? Je, tulitumia muda mwingi kupambana na adui wetu, kinadharia, badala ya kutumia muda huo kujenga uchumi wenye nguvu kama njia pekee ya kupambana na ubeberu?

Ni kwa kiasi gani tulitazama mbele? Mathlan, hatukujua kwamba miundo mbinu tuliyoirithi wakati wa ukolloni, wakati idadi ya Watanzania ikiwa ndogo, isingelistahimili idadi kubwa ya watu inayoongezeka kila mwaka huko siku za mbeleni? Tulijiandaa vipi katika hilo? Je, hatukujua kwamba sisi kama wakulima wa pamba, wakubwa wakibuni synthetic, pamba yetu isingelikuwa na soko na kwa hiyo kuathiri uchumi wetu? Tuilidhani kama hali hii ingelitokea (kama ilivyotokea) pamba yetu tungeliifanyaje? Tuile?

Na teknolojia je? Hatukuelewa kwamba dunia inayotawaliwa na mifumo ya biashara na uzalishaji wa bidhaa ikivumbua vitu vipya kama Inernet, mathlan, itaua kwa kiasi kikubwa huduma za posta na watu wengu kupoteza ajira zao? Tulijiandaaje, kwa vitu vya namna hii kama taifa? Kwa maana wakubwa kule kwao, hawawezi kusitisha kukua kwa teknolojia yao kwa kuyafikiria mataifa ya wakulima na wafanyakazi kama yetu. Wajibu huo ni wa mataifa yetu na viongozi wake.

Na hili suala la Afrika kuzalisha isichotumia, na kutumia isichokizalisha, tulilishughulikiaje kama taifa? Maana kiongozi wa kitaifa kuwashauri wananchi ni nini cha kupanda na lini, peke yake hili halimalizi tatizo hili sugu. Na hili suala la rushwa tulidhani tutalimalizaje? Kuwapiga viboko watoao na kupokea rushwa ili waende waonyeshe wake zao? Je, tulipofanya hivyo kwa nini basi hatukufanikiwa kumaliza tatizo hili sugu?

Je, wazungu katika mataifa ya Magharibi ambapo kupigwa viboko mtu ni mwiko, mbona hawana rushwa kama sisi? New Zealand, Denmark, Norway, Iceland n.k kati ya mataifa yanayoongoza kutokuwa na rushwa, walifanikiwaje kutokuwa na wala rushwa katika jamii zao wakati kuwapiga watu viboko ni mwiko kwao?

Je, inawezekana waliopigwa viboko baadaye wakawapiga wengine mapanga; wanaopigwa mapanga kuwapiga wengine mashoka; wanaopigwa mashoka kuwapiga wenzao tindikali, na vitu kama hivyo? Ni kwa nini Wazungu hawapendi kuwapiga viboko raia wake na sisi tuifanye kama sera ya siasa? Kwa nini tunatofautiana katika mambo kama haya? Je, values za Wazungu; ambazo ndio msingi wa mataifa yao yalipojengwa; ndilo jambo mojawapo lililowafanya Wazungu wasonge mbele kijamii na kiuchumi kuliko sisi?

Vyuo vikuu ni ni chem-chem ya fikra mpya kwa taifa lolote; je, tunawatumia kiasi gani wataalamu wetu vijana katika kuushauri uongozi wa kisiasa katika maswala ya namna hii? Ukoloni unaweza kuwa umechangia kwa kiasi fulani katika hali yetu, kama watoa hoja wengine walivyoonyesha, lakini pengine ni vyema tutahadhari tusije kuwa watumwa wa historia yetu. Tukifikia hali hiyo, tunaweza kudhurika maradufu.

'Many people...want to punish you for speaking the truth, for being correct, for being you. Never apologise for being correct, or for being years ahead of your time. If you are right and you know it, speak your mind. Speak your mind even if you are a minority one. The truth is still the truth'-Mohandas Gandhi

All said ukweli utabakia kwamba hii misaada wanayoitoa ni aibu yao wenyewe kama reparation...Can't fool me! huwezi nambia Muingereza ana huruma saaana kutusaidia sisi wakati anatumia - When we were rulers they were better off! Hizi ndio story nazisikia sana kuhusu Oman na Zanzibar ati Zanzibar ilikuwa imeendelea sana chini ya Sultan na wajinga wanaamini wanataka kuvunja muungano bora warudi kwa Sultan. Hii misaada yote anayoahidi ni aibu ya kukoloni watu ati huruma!.

Siwezi kumsemea Zitto lakini size yake kuwaambia They can stick that shit in their ashakum!...huwezi kumsaidia mtu na matusi juu ukitegemea sisi tutakaa kimya kama tulivyotukanwa na Israel..
 
Pamoja na ukweli kwamba UK was built in that way, we should not be fooled by politicians who use it as an excuse to justify their poor perfomance. Mkoloni aliondoka miaka 50 iliyopita, mbona hakuna kikubwa cha maana kilichofanyika? Kikubwa tulichofanya ni kuvuruga hata yale mazuri yaliyofanywa na wakoloni. Angalia shule alizoacha mkoloni uone hali yake ya sasa ikilinganishwa na mwaka 60, angalia hospitali, angalia barabara ovyo ovyo. Bado tunamlalamikia mwingereza?? Ukiangalia misaada iliyopata Tanzania toka kwa Uingereza, na nini kimefanyika na misaada hiyo unaweza kuonesha ni nini kimefanyika?

Si siri kuwa mkoloni alikuwa mwizi, lakini viongozi wetu wa sasa ni worse kuliko mkoloni, hawana haki ya kumlaumu mwingereza.

Nawaonea huruma sana wale wanaojidanganya eti ukoloni uliisha miaka hamsini iliyopita. Hawana tofauti na wale waliojidanganya na Obamamania na kuamini kuwa Baraka kumrithi Bush basi ubeberu wa marekani umekwisha....

Hili la kujidanganya eti kuna mazuri yaliyoachwa na mkoloni sishangai sana maana hata kule Zanzibar wapo wanaoendelea kuimba wimbo wa neema za enzi ya Sultan na Waingereza, na hapa Tanganyika bado tunawashabikia viongozi walewale katika ujana wao walicharazwa viboko na Nyerere kwa kuthubutu kuropoka eti heri ya ukoloni kuliko uhuru....

Uzalendo wa kisasa unashangaza sana maana yaelekea kuna wanaoijiita wakombozi wako tayari kukumbatia wanaodhalilisha utu na utaifa wao mradi tu wanawasaidia katika vita yao ya kuondoa uhalali wa CCM madarakani.....
 
Quote from Zitto:



Mh. Zitto, nadhani ni hekima zaidi ukiwa na ufahamu kwamba wewe ni mmoja wa viongozi wetu muhimu sana wa kizazi hiki, katika nyakati hizi muhimu. Kwahiyo kila unapotoa tamko, watanzania wanakusikiliza, wote - wale wenye nia njema na nia mbaya na wewe. Ni muhimu ukalijua hilo ili kama ikibidi kukwepa kutoa kauli au misimamo yako pale pasipo na ulazima basi ufanye hivyo. Lakini endapo kuna umuhimu wa kutoa msimamo au kauli yako, kama hiyo mada, ambayo sasa tumeelewa baada ya ufafanuzi wako, jaribu kutafuta jukwaa ambalo utakuwa na nafasi ya kujieleza ili watu wakuelewe, na wasipinde mambo. Kwa mtazamo wangu, tweeter sio sehemu nzuri ya kufanikisha hilo.

Kaka hudhani kuwa ushauri wako ni sawa na kumwambia Zitto ajitahidi awe kama "wanasiasa wetu" - Average politicians ambao wanasema yale tu wanayodhani yanatakiwa kusemwa na sio kuongea yale wanayoamini yanapaswa kusemwa hata kama yanahatarisha maslahi yao kisiasa?
 

Money given in aid by the people of the United Kingdom to Tanzania is reparationfor colonial exploits states Tanzanian M.P. Zitto Kabwe.

The "country was built by colonial exploitation. Whether your born or not. We can as well survive without youraid, take it” he says.

Zitto Kabwe is a member of the Tanzanian Parliament (CHADEMA), representingKigoma North and is Shadow Finance Minister and Chairperson for Tanzania’sPublic Investments Committee. He is therefore a man that shapes governmentpolicy in Tanzania.

In times of unprecedented recession in the UK, I am sure that most would indeed like to stop aid to a country whose policy makers display these kind of sentiments when you scratch the surface!

Pole Sana Tanzania!

Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
@Chomachomp your country was built by colonial exploitation. Whether your born or not. We can as well survive without your aid, take it.

Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe11 Jan11 Jan@Chomachompyour case is genuine totally but don't link to aid Tanzania gets from UK. Your country's aid is reparation for colonial exploits




--------
Zitto's response to this thread:



Evidence Mr. Kabwe?

Actually, this was Zitton original response.

13[SUP]th[/SUP] January 2012 Ndugu zangu. Nadhani ni hekima kujua Jambo kwa kina kabla ya kuanza kulitolea maneno na hukumu. Ninaomba kuelewa kifupi sana nini kilitokea huko twitter.
Kuna mama anaitwa Sarah. Mwingereza ambaye pamoja na mume wake waligombana na Benjamin Mengi kuhusu mashamba yanayoitwa sasa Silverdale Farms.
Ugomvi huu ulikuwa mkubwa na kuripotiwa mpaka katika Bunge la Uingereza. Huyu mama sasa hivi ameufanya Ugomvi ule binafsi na wa kibiashara kati yake na kina Mengi kuwa ni Ugomvi dhidi ya Watanzania wote. Amekuwa akiandika makala mbalimbali za kuichafua Tanzania. Amekuwa akitaka Serikali ya Tanzania imlipe yeye na mumewe fidia kwa makosa ya raia mmoja wa Tanzania anaitwa Benjamin Mengi.
Huyu mama na mumuewe hakuwahi kujiandikisha TIC ili kujua uwekezaji wake kwenye shamba na hata kupata protection ya kisheria. Sasa juzi kaandika makala kuhusu aid dependence ya Tanzania (Jambo ambalo ni la kweli) lakini akaweka takwimu nyingi sana za uwongo ambazo Watanzania wamezidaka na kuzizungumza Kama za kweli hivi. Baadhi yetu tukamwambia through twitter kwamba takwimu sake sio sahihi.
Pili tukamwambia alipaswa kusema Kama note katika makala yake kwamba yeye ana kesi na Serikali ya Tanzania. Kwamba yeye amekuwa akiilazimisha nchi yake ya Uingereza iinyime muswada Tanzania mpaka hapo Serikali ya Tanzania itakapomlipa fidia!
Mimi naongozwa na msimamo wa wazi kabisa kwamba 'right or wrong my country first' na hivyo siwezi kuruhusu mtu, tena mzungu anayejiita mwekezaji kuitukana nchi nchi yangu kwa sababu tu wamerushana na wafanyabiashara wenzake.
Tena nikajulishwa kwamba mama huyu analipwa na Yusuf Manji ili kuitumia Ugomvi huu dhidi ya Reginald Mengi katika vita vyao vya kila siku.
Hatuweziweka rehani kwa sababu ya magomvi ya watu binafsi.
Nimemwambia huyu mama na ninarudia kusema, muswada hii ni sehemu ya kurejesha Mali zilizonyonywa na ukoloni.
Nimemwambia huyu mama kwamba hata Waingereza wakitaka kuondoa misaada Yao waondoe na wala hatutakufa kwa kukosa misaada Yao. Nimemwambia hivyo na ninarudia hapa. That's me, what you see is what you get.
Huyu aliyeleta hii thread alete mtiririko wote wa mjadala na sio kipande kimoja tu cha mjadala na kuspin atakavyo yeye na wengi humu mmeingia katika mtego wake bila hata kuhoji
ENGLISH TRANSLATION
 
Mkiuu, inasikitisha na inauma sana unapoona kwamba tulilonalo wa TZ ni kulalamika na kutoa visingizio tu. M
bona Malaysia, na nchi zingine za Asia nazo zilitawaliwa na kupata uhuru karibu wakati sawa kama sisi. Lakini angalia walipo sasa kimaendeleo! W
ao ni kazi tu, hakuna visingizio.
Unajuwa sisi tuna tatizo kubwa sana.

Tatizo hilo mara nyingi linapelekea ujinga.

Kwa mfano sisi waafrika tuna ujinga wa kushindwa kuwasoma wenzetu, na ndiyo maana bado tuko hivi tulivyo.

Kuna namna ambayo mbongo zetu haziingiizi some certain stuff iwe iweje...

Ok, hivi unafahamu kuwa kwa mkoloni kila binadamu ana bei yake? Yes a price kama bidhaa ya dukani, hilo ni something ambalo wanaamini kabisa!

Sasa ebu ifikirie hiyo kauli kwa muda, halafu pia ujipange na wewe kama ungekuwa na price, how much is it?Ya viongozi wetu?Ya Taifa? halafu uniambie conclusion yako.

Maybe unaweza kuona bei za watu wa Malysia maybe ni za ghali zaidi, however sisi tuna rasilimali ambazo ni ghali,ni viongozi wetu tu ndo cheap!

Kwahivyo, inatakiwa tuwe na viongozi watakaokuwa alittle more expensive, na siyo u expensive wa binafsi, bali sisi kama Taifa kutokubali rasilimali zetu zichotwe tu kwa namna hii na sisi tunatizama eti kuogopa utawaudhi na kuleta eti sijui national security whatever it is...

Haina mantiki, facts zibaki kuwa facts!

Mbona nimeuliza maswali humu kuna wengine haiwaingii kwenye mbongo zao na hawawezi kujibu, nimeuliza wakoloni waliondoka kwa kupenda?Na ukiondoka pahala bila kupenda hutaandaa mazingira ya kuendelea kupata kile ulichokuwa ukikipata?

Hata wenye migodi si wale wale tu?

Tatizo letu tuna viongozi waoga na wanafiki, wenye kujali kupigiwa saluti zaidi ya kulitumikia taifa, umeshawahi lini kuona hawa viongozi wanaleta msimamo wa kuhakikisha wananchi vilio vyao vinasikilizwa? Kuhakikisha rasilimali zinawasaidia kukuza familia zao na kupata huduma muhimu za jamii?

Fukuzeni hao viongozi waoga wabinafsi, wekeni viongozi kama Gaddafi muone...
 
Wakuu zangu mtanisamehe jana baada ya kusikia msiba mkubwa ulotukuta nilikosa nguvu kabisa ya kuendlea na mijadala nikjasema ngoja nipumzike sikuu hii na kuanza kutafakari safari hii ndefu ambayo tumekuwa tukipoteza mapambanaji kila hatua ya vita hii.. Ni vizuri sana kupoza kichwa na kutazama tumetoka wapi tumefika wapi, na uwezo wetu kuendelea ktk mapambano..

Nashukuru sana kuona michango mingi imejitokeza na sasa hivi swala hili limekuwa pana zaidi ya kauli za Zitto mabazo zimewakera wengine. Lakini haiondoi ukweli kwamba huyu mama kama mkoloni kaitoa haki na tafrisi ya madai yake kwa sababu ya Ukoloni wa mawazo yake kuja Afrika na kununua land ikidai ni haki yake bila kufuata sheria zetu na alipokwamishwa swala la Misaada ndipo likaibuka..

Kaweza vipi kuja kununua land?..kuna utaratibu gani, amekosea wapi ama sisi tumemkosea wapi.. haya ndio maswali yetu kujiuliza..Lakini nyuma ya fikra hizi lazima tukubali kurudi kule kule kwamba viongozi hawa Marais wetu wa nchi za Kiafrika ni MANYAPALA wa mfumo wa kikoloni ambao kwao wao uhuru wa bendera ndio pekee ulotakikana kubadilisha uchumi wa nchi zetu japokuwa mfumo wa biashara bado ni ule ule wa kikoloni unaendelea kuzifanya nchi zetu kuwa Pori na shamba la malighafi...

Watu wanapenda sana kuzungumzia Tiger economy lakini wanashindwa kufahamu kwamba huwezi jenga uchumi wa naona hiyo pasipo kuelewa kwanza kwa nini uchumi huo umeitwa TIGER.. Na kama leo nitazungumzia misingi ya chumi za nchi hizo wengi wenu mtalaani na kusema hatutaki kusikia, kwa sababu mtaona hakuna tofauti KUBWA ule mfumo wa Ujamaa na Kujitegemea (Nyerere).

Hawa jamaa zetu wanachokifanya ni kutengeneza mazingira ya kiuchumi kukidhi mahitaji makubwa na nchi zilizoendelea (developed Countries). Ni uchumi unaozingatia kwanza EXPORT kuliko mahitaji ya ndani.. Wanasema export diven model.... Wakati wahitaji ya ndani (domestic consumpution) kwa mali zinazotoka nje (Imports) yaliwekewa vikwazo vikubwa ikiwa ni pamoja na kodi kubwa kuwadhoofisha uagizaji mali za nje.

Hivyo mgundue tu ya kwamba Ujamaa wa Nyerere umetumika sana ktk nchi hizo isipokuwa ktk mazingira tofauti..Badala ya serikali kuhodhi njia kuu za uzalishaji, jukumu hilo ni la wananchi lakini mambo mengine karibu yote ya Ujamaa na kujitegemea (miiko na maadili) yalitumika ktk kusukuma na kuleta maendeleo ya kiuchumi ktk nchi hizo..

Je, sisi tunaweza?.. Na mjueni fika kwamba kama Cocaine ndio soko zuri na kubwa Ulaya hali nchi yetu ina ardhi nzuri yenye nafaka (from geographical perspective), basi serikali inaweza lifumbia macho uharamu wa kulima Bangi na Cocaine kwa kutazama soko na mahitaji ya nchi tajiri..

Hivyo hata human occupancy na matumizi ya mazingira (Phisical nad cultural) yalikuwa ktk kutazama soko nje kuwalisha wenye nazo. Hata mjini ukienda mwenye Hotel anayewalenga watalii lunch huuza Tsh 40,000 hadi laki lakini uswahilini unakuta ni Tsh 3,000 na hakika hasara utaikuta sana kwetu uswahili na ndio maana wenye migawaha hawatoki, matumizi yao ni makubwa kuliko mapato.

Leo hii utawasikia CCM wakiweka madai kwamba Azimio la Arusha halikufa!..halikufa wakati tunaagiza zaidi toka nje kuliko ku export?, halikufa wakati mikakati mingi ya maendeleo inalenga Domestic consumption kuliko exports..Halikufa wakati Maazimio yote ya kiuchumi haijengi msukumo wa wananchi kutawala njia za Uchumi ktk kukidhi mahitaji ya nchi zilizoendelea badala yake tumewarudisha wakoloni kuja kwa njia nyingine kuhodhi rasilimali zetu kukidhi mahitaji yao huko nje!. Halafu IMF wanatupa sifa za kwamba uchumi wetu unakuwa kwa asilimia 7 wakati expenses zetu (consumption) ya mali zao inapanda kwa zaidi ya asilimia 10 kila mwaka!.

Hee jamani wakuu zangu, hata ktk maisha ya kawaida ukiwa shamba lako linazalisha magunia 100 ya mahindi ukaongeza ukubwa wa shamab hadi ukazalisha magunia 1,000 huwezi kusema ni maendeleo ikiwa uzalishaji wa magunia hayo unazidi thamani ya mahitaji yako. Wengine tuilianza na mishahara ya Tsh 700 kwa mwezi wakati wa Nyerere, leo hii wanapata Tsh millioni lakini wanashindwa hata kujenga kibanda cha choo. Huwezi kusifia ongezeko la mshahara kwa kutazama takwimu toka Tsh 700 hadi millioni kama ni mafanikio hata kidogo.

Narudi pale pale, ya kwamba hawa wazungu hata kama wangekuwa waafrika wenzangu kama wana mawazo sawa na huyu mama na kufiiria misaada ni mtego wa sisi kuendelea na Utumwa wa fikra tuwashabikie misaada tunayoipata kama ndio hatuna jinsi, believe me sintokubaliana nao hata siku moja kwa sababu ni akili ya UTUMWA sawa kabisa na akili ya MANYAPALA wanayoitukuza viongozi wetu kina Kikwete na wengineo...
 
FJM

Tafadhali soma background ya Jambo hili kabla hujahukumu. Nimeeleza nini kilileteleza mjadala kati ya mimi na mwanamama wa kiingereza Sarah kiasi cha kumwambia wakitaka waondoe misaada Yao.

Ninaamini ukoloni uliofanyika Afrika ulikuwa na madhara zaidi kuliko Malaysia, Singapore na kwingine kokote. Ukoloni uliofanyika Afrika una madhara makubwa zaidi ya Kisaikolojia kuliko mahala pengine au jamii nyingine duniani.

Ukoloni uliofanyika Afrika mizizi yake bado haijakatwa. Bado mfumo wa uchumi wa dunia umelifanya bar a la Adrika kuwa Soko la malighafi. Bado wakoloni wana ushahiwishi mkubwa sana katika sera zetu mbalimbali.

Miaka 50 Baada ya Uhuru tusiendelee kusema matatizo yetu yanatokana na ukoloni. Hii ndio lugha wakoloni wanapenda kuisikia kutoka kwetu. Lugha inayowaondoa kwenye picha. Lugha inayowaonyesha wao wanatusaidia kwa usamaria mwema. Lugha hii sitaisema kamwe maana najua bado nchi hii imeshikwa na makucha ya ukoloni.

Leo hii Barrick kwa mfano hawakulipa kodi Tanzania mwaka 2010 lakini wamelipa kodi UK. Kuna Mgodi kule Uingereza? City of London is the largest tax haven. Tax dodging investors have camped within the ring fenced cityn of London exploiting developing countries billions of USD every year through tax avoidance.

Hivi vi misaada hivi ni vi reparation tu ambayo haipo kwenye makubaliano tu. Unaweza kuiita vingine. Lakini nchi Kama Uingereza wala isijidai au kujitapa na misaada Yao kwetu. Wanachukua zaidi kutoka kwetu kuliko tunavyopata katika misaada. Wakitaka wachukue misaada Yao. Tutabaki Kama Taifa

aksante kaka mkuu, u are right,wasiokuelewa ni wale ni wale waliopigika vichwani!
 
Katika siku za hivi karibuni kulikuwa na mjadala mkubwa katika mtandao wa twitter na sehemu nyingine na Jamii forums kuhusu misaada inayotolewa na nchi ambazo zilitutawala.

Nilichangia mjadala huo twitter Nilisema uingereza wana moral obligation yakutusaidia, Walinipinga waliniambia naongea Non sense kama Mtu ninayependa changamoto, Nilichukua wasaha huo kutafakari, Kama kweli mantiki yangu ilikuwa ni sahihi na kama kweli Mantiki ya mheshimiwa Zitto zuberi kabwe ni sahihi. Kwamba waingereza wanapaswa kutulipa fidia kwa colonial exploitation. Pengine nieleze kwanini nilisema uingereza wana moral obligation ya kutusaidia kama uwezo wao wa ndani wa ki nchi unawatosheleza na kama misaada wanayotupatia tunaitumia kuleta mabadiliko yetu ya kimaendeleo. Niweke sawa hapa hawana ulazima wa kutusaidia kama jina lenyewe lilivyo msaada ni kitu cha Mtu kupenda.


Ili kuweka picha vizuri Tukumbuke Taifa letu lilipopata uhuru Lilikuwa ni la namna gani, ili tujue kama kulikuwa na haja ya uingereza kutusaidia ilituimarike na tuweze kujitawala wenyewe.

Tulikuwa na wasomi wachache mno Ambao wasingeweza kuliendesha taifa hili, Tulikuwa Hatuna skills za kutosha ilibidi waingereza watusaidie na walikuwa na moral obligation hiyo. Lakini mtoto hukua na kujitegemea. Mtoto asiyekua ni mgonjwa ana mdumao.

Hawana haki ya kuendelea kutusaidia ikiwa sisi wenyewe hatufanyi jitihada za kujitegemea na kusimama wenyewe kwa miguu yetu. Ni miaka Hamsini toka uhuru wetu sasa huo ni umri wa mtu mzima, Kama tumeshindwa kujitegemea mpaka sasa hawana haki ya kutusaidia.

Madai ya mheshimiwa zitto kabwe juu ya kulipwa kwetu fidia kutokana na ukoloni sidhani kama yanazingatia uhalisia wa Tulivyokuwa kabla ya Tanganyika ya mjerumani na baadae muingereza. Ukoloni huu huu ndio ulitufanya tuwe Taifa na tuwe na maendeleo hayo madogo tuliyonayo. Hatukuwa na elimu ya kutuwezesha kujenga nyumba bora, barabara, reli na vitu vingine vya dunia ya kisasa. Tukumbuke wenzetu walitupita mbali kwa maendeleo na mpaka sasa tunaona kwa dhahiri maendeleo waliyopiga katika kila nyanja.


Tulikuwa Taifa la vikabila vingi kila kabila na chifu wake. Tuko pamoja leo hii ni madhara ya ukoloni. Tumepata Mwanga huu wa elimu kwa tabu na mateso. Sisi sote tunaamini maisha haya ya sasa ni bora zaidi kuliko yale ya kale walioishi babu zetu.
Iweje kama wakati huu tuna akili zetu tunashindwa ku process madini yetu na vito vyetu ili kuongeza thamani kwa wakati huu, hayo madini kwa wakati huo yawe na dhamani? Mimi sidhani kama tulikuwa tunajua hizo almasi na dhahabu zina thamani. Ni haki yao kuchukua hatuna moral authority kuwadai.

Mimi nawashukuru kwa kutupa mwanga na kutuleta pamoja kuwa Taifa. Bila wao tusingekuwa kama tulivyo sasa. Tukumbuke kwamba uingereza nayo ilitawaliwa na warumi katika karne ya nne na wao walikuwa vikabila vingi waliunganishwa na warumi, warumi waliweka mtawala wao kule uingereza waliwatumikisha na kuchukua utajiri ambao wao pia waingereza walikuwa hawajui kama ni thamani. Siku zote Mataifa yenye nguvu na maarifa yatayatawala mataifa mengine na kuwafanya watumwa. Ni lazima tujue tulipotoka na wapi tunataka kuelekea kama Taifa.


Tukishindwa kutumia akili zetu na jitihada zetu tusimlalamikie mtu. Haiwezekani watu wakose ardhi katika mataifa mengine sisi tunayo lakini hatuitumii ipasavyo wasiichukue. Mimi ni mwafrika na ninaunga mkono ukoloni, Walikuwa na haki ya kuitumia ardhi tuliyokuwa hatuitumii kwa uzalishaji. Tusijidanganye utajiri wa nchi unatokana na nguvu, juhudi na maarifa ya watu na viongozi wao. Tuache porojo na kumtafuta mchawi. Maendeleo yetu tutayaleta sisi wenyewe kwa umoja wetu na juhudi zetu katika kuleta maendeleo.


Wakati wazungu wakitoka kutafuta masoko na malighafi tulikuwa wapi? Wakati wakitengeneza meli na bunduki za kututiisha tulikuwa wapi? Wakati wakitengeneza mizinga tulikuwa wapi na sasa hivi tunafanya nini kujikomboa tuache upumbavu. Lazima tukubali sisi ni wajinga na tuwe tayari kupambana na ujinga wetu. Taifa lenye watu wenye akili na busara huwezi kulitawala wala watu wake kuwachukua utumwa. Taifa la watu wenye umoja watu wake huwezi kuwafanya hivyo.


Miaka hamsini baada ya uhuru bajeti bado tunategemea wahisani kwa karibu ya nusu, Hatuwezi kuendesha serikali yetu wenyewe khalafu tujiite watu wenye akili? Tujiite watu huru? Tujiite watu wenye kufikiria? Walituita subhuman na wataendelea kutuita subhuman kama hatutafanya jitihada za kujiheshimu. Ngoja niwawekee maneno ya Pw Botha aliyoongea kwa Watu weusi.


'' Pretoria imetengenezwa na watu Weupe kwa ajili ya watu Weupe na hatuna haja ya kuuthibitisha umma au mtu Mweusi kuwa sisi ni watu bora, tumekuwa tukiwaambia watu Weusi jambo hili kwa njia elfu.''


'' Afrika Kusini ya leo haikutengenezwa katika mawazo ya kawaida, tumeitengeneza kwa kutumia akili nyingi, jasho na damu. Mnaposema kuwa tunawabagua Weusi sielewi. Hivi ni Afrikaners ndio waliojaribu kusitisha kizazi cha Aborigines wa Australia? Je, ni Afrikaners waliotenga na kuwanyanyasa watu Weusi Marekani Kaskazini kwa kuwaita niggaz?''


''Sisi sio wanafiki kama Wazungu wenzetu wafanyavyo kwamba wanawapenda watu weusi. Ukweli kuwa Weusi wanaofanana na binadamu na kutenda mambo kama binadamu hayawahalalishi wao kuwa watu wenye akili timamu au binadamu aliyetimia. Kanunguyeye si nungunungu na mijusi hawawezi kuwa mamba eti kwa sababu tu wanafanana.''



Nimeyaandika hayo maneno kwa makusudi mnichukie lakini nitasema ukweli. Na katika dunia ya leo tumefanya nini kujikomboa? Tumeendelea kumpelekea kikombe mtu yule yule aliye tudharau na kutunyanyasa. Lazima tujitambue na tuwe tayari kujirekebisha sio kulalamika tunatukanwa.


Wakati marekani ikitengeneza ndege isiyokuwa na rubani sisi tunafanya nini? Tumekuwa watu wa kuagiza kila kitu. Hata mashirika yetu wenyewe tuliyoyajenga ya reli na shirika la ndege na mengine ya umma kwa faida yetu na vizazi vyetu tumeshindwa kuyaendeleza Tunayaua wataachaje kutuita manyani?


Kama tunawafuata na kuwalalamikia matatizo yetu badala ya kuyatatua wenyewe kwanini wasitudharau?. Kama tunaweza kutumiwa kuanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa faida ya mabeberu kwanini wasitukebehi? Tumeshindwa kujiongoza hadi leo miaka hamsini bado tunategemea misaada kwanini wasituone tuna mapungufu? Kama wanatusaidia Pesa ya maendeleo yetu wenyewe tunaitafuna na kuitumia kuhongea kwanini wasituone tuna kasoro?


Katika journal ya A+C ya 1997. Wahisani walilalamika kwamba misaada yao hawaoni kama inaleta mabiliko kwa mataifa yanayopokea misaada hiyo kutokana na corruption, inefficiency na maladmistration, mpaka leo malalamiko ni ya aina hiyo hiyo. Tunashindwaje kutumia pesa hata ya msaada kuleta mbadiliko yetu wenyewe khalafu tunataka tuheshimiwe? Wanalalamika pesa nyingi inapotea bila madhara yaliyokusudiwa.


Wenyewe wana matatizo ya kiuchumi kwa sasa bado tunategemea watusaidie sisi ni watu wa namna gani? Kwa nini hatutaki kujiheshimu? Tuko makini kweli katika kuleta mabadiliko katika Taifa letu? Bunge, mahakama na serikali kuu wako makini kweli kuhakikisha nchi yetu inasonga mbele? Tutaondokanaje na matatizo yetu ya kiuchumi tuliyonayo kwa sasa? Hii Inahitaji umoja na tafakari zaidi kwa watu wenye uzalendo na kujitolea.

Namwambia mweshimiwa zitto zuberi kabwe Waingereza hawana haki hiyo ya kutulipa kutokana na ukoloni. Kama wao wasivyokuwa na haki ya kuwadai Warumi. Tusipojitayarisha na kujijenga tutatawaliwa mpaka sasa hadi milele. Lakini fursa ya kujitegemea ipo ni utayari wetu na jitihada zetu za pamoja na umoja wetu. Kuwaambia waingereza watulipe kwasababu walitutawala na kuchukua resources zetu wakati wenyewe tulikuwa bado hatujajitawala sidhani kama ni sahihi. Tulikuwa bado ni makabila madogo madogo ya wakulima na wafugaji, Tulikuwa hatuijui hata hiyo dhahabu maana yake nini na mpaka sasa tunashindwa kui process sababu ya Uvivu wa kufikiri wa viongozi wetu na utayari wao kulifanya taifa hili lijitegemee. Nasema sidhani labda niwasikilize wadau huenda mkawa na hoja nzito zaidi yangu.
 
Narudi pale pale, ya kwamba hawa wazungu hata kama wangekuwa waafrika wenzangu kama wana mawazo sawa na huyu mama na kufiiria misaada ni mtego wa sisi kuendelea na Utumwa wa fikra tuwashabikie misaada tunayoipata kama ndio hatuna jinsi, believe me sintokubaliana nao hata siku moja kwa sababu ni akili ya UTUMWA sawa kabisa na akili ya MANYAPALA wanayoitukuza viongozi wetu kina Kikwete na wengineo...

Kama tunawafuata na kuwalalamikia matatizo yetu badala ya kuyatatua wenyewe kwanini wasitudharau?. Kama tunaweza kutumiwa kuanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa faida ya mabeberu kwanini wasitukebehi? Tumeshindwa kujiongoza hadi leo miaka hamsini bado tunategemea misaada kwanini wasituone tuna mapungufu? Kama wanatusaidia Pesa ya maendeleo yetu wenyewe tunaitafuna na kuitumia kuhongea kwanini wasituone tuna kasoro?

Namwambia mweshimiwa zitto zuberi kabwe Waingereza hawana haki hiyo ya kutulipa kutokana na ukoloni. Kama wao wasivyokuwa na haki ya kuwadai Warumi. Tusipojitayarisha na kujijenga tutatawaliwa mpaka sasa hadi milele. Lakini fursa ya kujitegemea ipo ni utayari wetu na jitihada zetu za pamoja na umoja wetu. Kuwaambia waingereza watulipe kwasababu walitutawala na kuchukua resources zetu wakati wenyewe tulikuwa bado hatujajitawala sidhani kama ni sahihi. Tulikuwa bado ni makabila madogo madogo ya wakulima na wafugaji, Tulikuwa hatuijui hata hiyo dhahabu maana yake nini na mpaka sasa tunashindwa kui process sababu ya Uvivu wa kufikiri wa viongozi wetu na utayari wao kulifanya taifa hili lijitegemee. Nasema sidhani labda niwasikilize wadau huenda mkawa na hoja nzito zaidi yangu.

Wakuu vyema sana.

Lakini habari mbaya ni kwamba aina ya viongozi tulio nao sasa hivi fikra zao zinawatuma kuona misaada kama ni haki yao (malipo ya ukoloni). Ndio maana mzee Kiranga akapinga suala la Zitto kutumia notion ya reparations kujustify hiyo misaada!!

Hapa kinachotakiwa ni kuwa na viongozi ambao suala la msaada lisiwe ni agenda kabisa ya serikali; yaani viongozi ambao watakataa kwa namna yoyote kuendekeza na kutegemea misaada.

Jamani, misaada inalevya. Naamini ili linaeleweka. Katika dunia ya sasa hivi, nchi kama zetu kuendelea ni rahisi sana. Kila kitu kipo, ni suala la kuamua na kuweka vipaumbele. Sisi hatuna haja ya kugundua chochote, nchi za magharibi zimeshagundua kila kitu wakati zikikabiliana na changamoto za kimaendeleo nyakati zile nchi hizo zinaanza kusonga mbele.

Kwanini tusiwekeze katika technological transfer? Kuchukua tu teknolojia za wenzetu na kuja kuzitumia kwaajili ya maendeleo yetu. Sasa sijui sisi tunataka kugundua? Tutagundua nini sasa? Uwa nashangaa mainjia wetu pale CoET (UDSM), wana kitengo cha teknolojia na maendeleo. Hivyo vitu wanavyotengeneza (wenyewe wanasema "wanagundua - innovations") ni vituko na vichekesho. Yaani wanatengeneza vitu ambavyo Ulaya na Marekani vimetumika enzi za industrial revolution!! Hivi nini kinawashinda kwao kutransfer technology kutoka Ulaya na Marekani na kuja kuitumia (pengine kwa kumodify kidogo kucater needs zetu) hapa kwetu?

Pia tujiulize, hivi hao wazungu (Ulaya hususani, kwa sababu walioenda Marekani wengi wao walienda na innovative ideas kutoka Ulaya), hawakua na shida kabla hawajaendelea? Walikua nazo; sasa walifanya nini ili waweze kuzikabili na kuondokana na shida hzio, waligundua mbinu (waliumiza vichwa, hapa ndipo wavumbuzi wa mambo mbalimbali walijitokeza) na namna ya kuzikabili na kuondokana na shida hizo.

Sasa sisi kama taifa, kuzikabili shida zetu tunafanya nini?! Akili zetu zimelala katika kuwaza misaada, badala ya kuwaza namna gani tuumize vichwa (tena sasa kama nilivyosema hatuna haja ya kuumiza kichwa kama kina Alexander Bell, Newton and the like) ili kuzikabili shida na changamoto mbalimbali, tunawaza kuomba. Na hii tabia imesambaa kuanzia kwa rais hadi kwa raia wa kawaida (yaani wameshaona misaada kama ni sehemu ya kusukuma gurudumu la maendeleo).

Nakumbuka siku zile Bush jr. alikvyokuja mara kwanza Tanzania, kuna kikundi cha waislamu walitaka kuandamana kuonyesha hisia zao juu ya Bush jr. na sera zake za "shock and awe". Basi, pale bungeni kuna mbunge mmoja (nimemsahau jina) alisimama na kuropoka kwamba anawashangaa hao waislamu kwa kuandamana kwao wakati Bush jr. anakuja na mapesa mengi ya misaada, kuandamana huko kutayafanya mataifa mengine yashindwe kutoa misaada kutokana na kutoridhika kwetu!! Sasa fikira kauli na fikra kama hizo zinatoka kwa kiongozi tena mtunga sheria!!

Mwisho: uwa nikifikiria juu ya kiongozi ambae anaweza kweli kusimama kidete katika kutotegemea na kuomba omba misaada (grants and aids) napata shida na kizunguzungu!! Simwoni kwa Tanzania yetu hii ya sasa (niliwaza CHADEMA inaweza kutoa kiongozi huyo kwa sasa, lakini nacho pia moja ya vyanzo vyake vya mapato ni misaada kutoka kwa vyama rafiki vya kisiasa vya ndani na nje ya nchi; na misaada na ruzuku kutoka ndani na nje ya nchi). Na bila kupata kiongozi wa namna hiyo kuendelea kwetu kutakua ndoto za alfu ulela.
 
Wakuu vyema sana.

Lakini habari mbaya ni kwamba aina ya viongozi tulio nao sasa hivi fikra zao zinawatuma kuona misaada kama ni haki yao (malipo ya ukoloni). Ndio maana mzee Kiranga akapinga suala la Zitto kutumia notion ya reparations kujustify hiyo misaada!!
Ni sawa lakini lazima ujue kwamba baada ya Uhuru kulikuwepo na makubaliano mengi tu ya kiutawala Memorundum of understanding. Na kama unakumbuka uasi wa wanajeshi wetu mwaka 1964 uingereza walipeleka majeshi yao Tz why?..Sasa ni vigumu sana kukataa ya Zitto ikiwa kuna kaukweli fulani maana itakuwa ajabu sana leo Iraq ikatae kwamba misaada wanayoipata haitokani na repatarions.. unaweza kutumia neno ama lugha yoyote ile unayotaka lakini ukweli upo pale pale kwamba marekani wanisaidia Iraq kwa sababu hizo na kuiweka kama koloni lao kinamna na WaMarekani raia wanatukana kila siku kwa nini wanatumia fedha zao nyingi kuisaidia Iraq nchi.

Nakumbuka mwaka 1982 Kenya waliwakatalia marekani kuweka kambi yao ya jeshi la Majini pakawa na utata mkubwa sana Marekani wakasema wanakata misaada yao, Kenya bila kujali wakaugeuza kibao na kurudi kwa Muingereza..Kwa hiyo utaona kwamba viongozi wetu ni Manyapala, ingawa najua fika Nyerere alipotangaza Azimio la Arusha na kusema Tanzania ni nchi isiyofungamana na upande wowote ndipo aliwakosha wote..Na kama alitangaza hivyo pamoja na baadhi ya nchi ina maana zilikuwepo nchi zinazofungamana! na ukizitazama hizi nchi zote utakuta ktk kundi la mkoloni alowatawala.
Nakumbuka siku zile Bush jr. alikvyokuja mara kwanza Tanzania, kuna kikundi cha waislamu walitaka kuandamana kuonyesha hisia zao juu ya Bush jr. na sera zake za "shock and awe". Basi, pale bungeni kuna mbunge mmoja (nimemsahau jina) alisimama na kuropoka kwamba anawashangaa hao waislamu kwa kuandamana kwao wakati Bush jr. anakuja na mapesa mengi ya misaada, kuandamana huko kutayafanya mataifa mengine yashindwe kutoa misaada kutokana na kutoridhika kwetu!! Sasa fikira kauli na fikra kama hizo zinatoka kwa kiongozi tena mtunga sheria!!
Kusema kweli mimi nimepoteza imani kubwa na wanasiasa wa Tanzania, kuna kitu kinanambia kwamba tunachezewa akili zetu tu maana haiwezekani mambo yamekaa vibaya lakini hakuna mtu hata mmoja anajitokeza kupigania haki na kuinua maisha ya WAKULIMA na WAFANYAKAZI..Something ain't right!..hasa napoona viongozi wanagombania madaraka, kuingia/kung'ang'ania Ikulu au Ubunge!..
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom