Mkuu Sikonge,Hili ni gumu kwa akina Masanja tu, ila kwa watoto wa wakubwa ni RAHISI sana na wana PASSPORT mbilimbili au tatutatu. Tuseme uko nje, unaukana ubongo. Unarudi Tz na kuchonga pass mpya. Hivi ni shida kuchonga pale pass? Ukikwama Bongo, si unaenda hata Rwanda/Burundi kama siyo Kenya na Uganda? Pia kama mtu kaweza kuchukua Uraia wa UINGEREZA, wa Tanzania utamshinda? Mnaongelea nini hapa? Kama watu waliweza kwenda BoT na kuchota pesa, itakuwa Pass? Hebu fikirieni mara mbili kabla ya kuandika. Nalaani sikuomba URAIA wa Gabon nilipopita kule.
Looh! hilo la uraia wa Gabon limenichekesha sana. Kuna ndugu yangu huwa ananiambia anaombe apewe ubalozi hata kama ni Chechenya. Huwa nacheka lakini jamaa anasema balozi ni balozi tu hata kama ni kwenye nchi yenye matatizo.
Sheria za uraia zinasema kama una uraia wa nchi mbili kwa mfano UK na Tanzania, ukifanya kosa Tanzania, uraia wako wa UK haukusaidii na wala UK authority haiwezi kukutetea kama raia wao. Hiyo ndio hasara ya uraia wa nchi mbili.
Sasa huyu kijana kafanya makosa kwenye nchi ambayo ana gamba lake, hapo UK watamrudisha TZ kama Mtanzania tu. Suala la kwamba ana passport pia ya Uingereza hawataliweka tena maanani. Angefanya kosa nchini Kenya hapo suala lake lingeshughulikiwa kama Mwingereza.
Huu mtandao ukiuchangamkia sana unageuka kuwa kilevi kama drugs tu na mwisho wake unaingia hata kwenye madudu ya ajabu ajabu.
Nchi zilizoendelea huwa hawakurupuki kukamata mtu. Wakishahisi unahusika basi watakuchunguza hata miezi kabla ya kukushutua. Inaelekea jamaa walimjua mapema na wakaamua kuwacha tu aendelee na utundu wake mpaka walipokuwa na uhakika kwamba ni yeye.