mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 11,855
- 8,253
Kwa wale wakazi wa Dar kuanzia miaka ya mwishoni mwa `1980 na mwanzoni mwa miaka ya 1990 pale kituo cha polisi Msimbazi kulikuwa na askari mmoja mkakamavu kwelikweli ambaye alikuwa kiboko cha makonda na madereva jeuri na sugu wa daladala,wakati wote alikuwa akitembea na vitendea kazi vyake muhimu kama vile bastola,pingu na rungu huku buti zake zikishine na uniform zake zikiwa safi na zimepigwa pasi kwa kutumia wanga,hata inzi alikuwa anaogopa kutua kwenye nguo zake,yuko tofauti na askari wa siku hizi ambao wanavitambi,uniform chafu na sifa yake kuu ilikuwa ni UKAKAMAVU NA KUTOCHUKUA KITU KIDOGO,alikuwa ahongeki.