Yaliyojiri mkutano wa CUF Morogoro leo, CHADEMA wana sera ya kutaja mafisadi tu

Naona wachangiaji wote wanamwagika kipovu, punguzeni jazba mutaturoesha mimate hapa ukumbini! Hata kama yanauma ukweli ndio huo.
 
Habara ndio nini? Na kwanini wamshutumu MR CLEAN badala ya CHEKA

wewe kansa ya udini inaendelea kukutafuna taratibu bahati mbaya hujijui...maana hata post zako sasa ndio nimeanza kuzitilia mashaka mwanzoni nilikua nachangia kwa nia moja ya kujenga kumbe mwenzetu una yako yaliyo nyuma ya pazia "udini",ndio mana unaweweseka na hoja ya rais kutoka zanzibar....issue kumbe ni dini.sasa nimekusoma.
 
Na sera ya CUF ni kuishambulia Chadema, hawana jipya, naona hilo ndiyo sharti walilopewa na mume wao CCM ili kudumisha ndoa yao. Ama kweli ndoa ndoano.
 
Habara toka Morogoro Jioni ya leo Mh. Mustapha Wandwi na Mh. Mbalala Maharagande walieleza yafuatayo;
1. Zaidi ya kutoa orodha ya mafisadi Tz CHADEMA hawana jipya zaidi.
2. Nchi hii iliharibika awamu ya 3 ya Mh. Mkapa na si marais wengine
3. CUF imeimarika zaidi katika uchaguzi wa mwaka 2010 kuliko 2005 kwa kuongeza wabunge 2 Bara tofauti na 2005.
4. CUF inazidi CHADEMA wabunge wa majimbo.
5. CUF ndiyo chama chenye wabunge Pemba na Ugunja na CHADEMA hakina hata mmoja.
6. Waziri wa SMZ kutoka CUF ndiye amepandisha bei ya karafu kutoka Tsh 3,500 Okt 2011 hadi Tsh 25,000 bei ya hivi sasa.
7. CUF ndiyo imeoa CCM tofauti ya CHADEMA wanaodai CUF imeolewa na CCM visiwani.
8. Wanaandaa mapokezi makubwa ya Prof wa Uchumi Dunia atakaporudi toka Marekani mwezi ujao.
9. Prof. Lipumba ni kati ya maprofesa 4 tu walioajiriwa na serikali ya Marekani kati ya maprofesa 300 waliofanya usaili ili waajiriwe
na Marekani.
10. Mkutano ulizidisha dakika 15 muda wa kawaida, licha ya polisi kutaka wafunge lakini walikataliwa.
11. Hakukuwa na kumkumbuka walau dakika moja kumkumbuka mwanasiasa aliyefariki Mh. Regia Mtema.
12. Hamad Rashid si mwanachama wa CUF anatapatapa tu.
Maajabu sana haya! mada nyinginezo hazihitaji hata mtu kuchangia yaani ujinga mtupu na uswahili.. Nyie CUF kinachouzwa kwa wananchi ni sera sio habari za kusodoana tosi! Hee mbona mnatuletea siasa za mduara na nyama ya bata!
 
Maajabu sana haya! mada nyinginezo hazihitaji hata mtu kuchangia yaani ujinga mtupu na uswahili.. Nyie CUF kinachouzwa kwa wananchi ni sera sio habari za kusodoana tosi! Hee mbona mnatuletea siasa za mduara na nyama ya bata!

Unamaanisha nini kusema uswahili? aisee kweli umebobea katika kuwatukuza....mabosi wako kawawa type!
 
hapo kwenye red; hivi ni nani kamwoa mwenzie? Kwani kati ya dr.shein na seif, ni nani mwenye sauti ndani ya nyumba? Yule ambaye akikoroma mambo yanakuwa sawa sawia?
Seif hana sauti hata kwa makamu wa pili balozi seif idd,. yaani kama shein hayupo makamu wa pili ndio anakaimu nafasi ya urais, ikitokea leo hii shein akakoma kuwa rais makamu wa pili balozi idd ndiye atakayekuwa rais wa muda kusubiri uchaguzi, seif yeye sana kumwagilia maua na kutengeneza chai kule ikulu hana lolote ndio maana anangangania ukatibu mkuu na hamad
 
Pia kuhusu item Na. 4 - hawakutaja kwamba idadi ya kura walizopata wabunge wao wote haizidi ile idadi ya kura alizopata Mbunge Halima Mdee peke yake kule Kawe.
 
Huyo Mustapha Wandwi alipata kura 253 Vedastus Manyinyi 14,000 v.j Nyerere 21,000 hana jipya
 
CUF udini umewajaa sana.Wakimtaja JK wanaona ni tusi kwa uislam!

Ni kweli mkuu kwani tatizo la cuf ni udini tu ulowajaa but enewei koz siku zote mfamaji haishi kutapatapa, so kwa ushaauri wangu kwa cuf hiyo fedha ya ruzuku waitumie kuanzisha mashamba ya karafuu na mahakama ya kadhi.
 
Hawa CUF kweli wameisha huku bara! Yaani badala ya kuzungumzia mikakati ya kukiinua chama chao huku bara wanaanza kukiponda CDM! CDM inaingiaje katika hili?

CDM kutaja mafisadi na kufanya maandamano ni mbinu moja ya kisiasa ya kupata umaarufu, na si dhambi!Mnaona wivu sana kwa kuwa imewasaidia sana CDM katika harakati za kuisambaratisha CCM hadi kufikia viongozi wake hawaelewani, wamebaki kusema hovyo na kuonyeshana vidole!

Eti wanajivunia Profesa! Lol! Mbona usomi wake hauleti tija kwenu huku Bara na unazidi kuwadidimiza? Kule Zimbabwe Mugabe ana digrii 6, lakini tazama nchi inavyoyumba kiuchumi -- kazi yake kubwa ni vita dhidi ya wazungu! Ajabu ni kwamba yeye anawafukuza, sisi huku tunawakaribisha!

Hawa kina Mtatiro, maharagande na Wandwi na viongozi wengine wa CUF huku Bara wameonjeshwa hela za CUF wanazo-control Maalim Seif na Jussa na sasa wanasapoti sera za Maalim kwa ajili ya Zanzibar. Seif hana habari kabisa na Bara! Narudia -- hana habari kabisa na Bara. Niko tayari kurudia hili hata mara elfu!

Angekuwa ana habari na Bara wakati huu angekuwa anatembelea wilayani huko kuona kwa nini chama kinazorota na kutafuta mbinu za kukiimarisha.

Mwaka huu CUF Bara mtajibeba tu -- hamna akili kabisa ya kujiangalia kipi kinawasibu Bara, mbali na kumsikiliza Seif na Jussa!
 
Maajabu sana haya! mada nyinginezo hazihitaji hata mtu kuchangia yaani ujinga mtupu na uswahili.. Nyie CUF kinachouzwa kwa wananchi ni sera sio habari za kusodoana tosi! Hee mbona mnatuletea siasa za mduara na nyama ya bata!

Si wapemba wengi,ndio maana siasa za mduara,mipasho na kuzodoana wana ziweza!mtatiro na lipumba ni watu waliokosea njia kuingia kwy chama cha mipasho!
 
Mi naona hizi ni hisia za aliyeleta hii thread ila kaamua kututajia morogoro kwa kuwa watu wengi hatuwezi kufanya uchunguzi kujiridhisha na habari hii, kama ni kweli kwa nini asitupie hata kapicha ka simu ya mchina, anatuletea hii thread kutaka kupima upepo wa mtazamo wetu kwa chama chake. ukiainisha hizo hoja zake yaani kuanzia ya kwanza mpaka ya mwisho utagundua kuwa hata kama wewe ni mnazi wa cuf huwezi kuhudhuria mkutano kwa maada za kijinga kama hizi. Cha kushangaza kwa mazoea ya wengi hapa jf wameanza kuchangia pasipo hata kujihoji wao kwa hiki kilichoandikwa kina mantiki gani na mstakabari wake, ila siwezi kuwalaumu kwa kuwa hapa mara nyingi imezoeleka ku-comment kwa mazoea ya unazi wa vyama. Huu ni ushauri wa bure tu wala hulazimishwi kuukubali ama kuukataa kama vipi upotezee.

Mkuu ni kweli cuf jana walikua na mkutano wao hapa Moro,wametumia nguvu mno kuutangaza huo mkutano wao lakini mkutanoni walitokea watu wasiozidi 50,tena ni wale "washadadiaji" wasiojua chochote kinacho endelea kwenye nchi yao
 
Cuf ni copy ya ccm, na hiki chama 2shakizika since uchaguzi mkuu ulopita na hata igunga walikiona ' so matokeo ya igunga ni salamu kwa wanacuf wote. CUF UZENI KARAFUU KWANI CHADEMA SIO LEVEL ZENU.
 
Back
Top Bottom