The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 618
- 1,803
Salaam Wakuu,
Leo tarehe 11/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea.
Kufahamu ilipoishia, soma hapa: Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Januari 10, 2022. Shahidi namba 8 aendelea kutoa ushahidi. Kesi imeahirishwa hadi kesho 11/01/2022
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
UPDATES:
Jaji ameingia Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha;
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Tulimanywa Majige
Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikikupendeza naomba Kuwatambulisha Mawakili
Nashon Nkungu
John Mallya
Dickson Matata
Faraji Mangula
Sisty Aloyce
Michael Mwangasa
Gaston Garubindi
Seleman Matauka
Jaji anaita Washtakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri lina endelea Kusikilizwa na Upande wa Mashtaka tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji nasi pia tupo tayari Kuendelea
Jaji anaandika Kidogo wakati Mahakama Ipo Kimya
Wakili Peter Kibatala anasimama na Kuendelea na Maswali kwa shahidi
Kibatala: Shahidi Tulikuwa tunaendelea Kuhusu Kesi yenu Kuwa Mbowe Alimpa Maelezo Urio na Urio Aweze Kutafuta Watu wa Kufanya Ugaidi
Kibatala: Shahidi, Urio bado Yupo Jeshini na Mwanajeshi aliye kwenye Utumishi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: katika Ushahidi Wako Uliwahi Kuongea Lolote hapa Mahakamani Kwamba Urio akiwa Kama Mwanajeshi wa JWTZ Kushiriki katika Vitendo Vizito Vya Ugaidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulishawahi kuwasiliana na JWTZ kuhusu Mtumishi wao Urio Kushiriki katika ya Matendo ya Ugaidi
Shahidi: Sijafanya
Kibatala: kwa ufahamu wako Uongozi wa JWTZ unafahamu Mwanajeshi wao Urio alikuwa anafanya Vitendo Vya Kutafuta Watu wa Kufanya Ugaidi
Shahidi: Mimi sifahamu
Kibatala: Je Unakubaliana na Mimi Kuwa Vitendo Vya Ugaidi ni Vitendo Vizito na Vinatikisia Psychology na Utulivu wa Nchi
Shahidi: Ndiyo Kibatala: Je unafahamu Kuwa JWTZ Wana kitengo Cha Ujasusi cha Millitary Intelligence, kazi yao ni Pamoja na Kuchunguza Matendo ya Ugaidi?
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Katika Ushahidi Wako Ulizungumzia lolote kuhusu Kushirikiana na Vyombo Vya Usalama na Kijasusi kama TISS?
Shahidi: Mimi sifahamu lakini Viongozi wangu Watakuwa wamefanya
Kibatala: Sasa Viongozi wako Unawaona hapo Kwenye Kizimba?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Kuwa Moja ya Kazi ya Hizo Taasisi ni Kushughulika na Mambo ya Ugaidi
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kuwa iwapo taasisi hizo zingeshirikishwa katika ngazi mbalimbali ya vyombo vya usalama na idara ya uhamiaji na wao wangeshirikishwa?
Shahidi: Hilo mimi siyo wajibu wangu Kibatala: umeanza kuleta ujeuri mahakamani Shahidi: Hapana Kibatala: Sasa Jibu, unafahamu au hufahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Unafahamu Kuwa Mshtakiwa Wa 4 alisafiri Kwenda Nje Mara Kadhaa?
Shahidi: Hapana, Sifahamu
Kibatala: Katika Kikosi chenu wewe ulikuwa Second Command Kama Top leader, Je, Unafahamu timu yenu Kuna Mtu aliwasiliana na Rais Samia Suluhu Hassan?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Unafahamu alipopata taarifa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Mbowe alikuwa anajua atashitakiwa Kwa Ugaidi ndiyo Maana akakimbia nje ya Nchi kukwepa upelelezi?
Shahidi: Hapana... Sifahamu
Kibatala: Kuna kikosi kazi zaidi ya chenu kilikuwa kinafanyia kazi suala hili labda wao walienda kumtaarifu Rais Samia Suluhu Hassan?
Shahidi: Hapana.. Sifahamu
Kibatala: Kesi hii Rais Samia Suluhu Hassan alisema kuna watu wamefungwa katika shauri hili, kwa ufahamu wako kuna watu wamefungwa kwenye shauri hili?
Shahidi: Hilo silijui na siwezi kuliongelea
Kibatala: Kama unajua sema najua au kama hujui sema sijui, Kusema huwezi kuongelea ni ujeuri huo na nitaomba mahakama IKUZIMISHE..
Shahidi: Hilo silifahamu.
Kibatala: Je unafahamu kuwa Kingai alisema kuwa alimuwekea uangalizi Mbowe hata alipokuwa nje ya Nchi?
Shahidi: Hilo Mimi silifahamu Kibatala: Je Kwa ufahamu wako wewe Freeman Mbowe alikimbia nje ya nchi Ilikuweza kukwepa upelelezi
Shahidi: Hilo silifahamu kwa kweli
Kibatala: Je unafahamu Freeman Mbowe kaenda nchi mbalimbali kutoka August 2020 mpaka Mwaka 2021 July?
Shahidi: silifahamu nchi hizo mimi
Kibatala: Je unafahamu mamlaka chunguzi/ pelelezi za Tanzania ziliwahi kuwasiliana na mamlaka chunguzi za hizo nchi?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Je unafahamu kuwa mtu ambaye akiwa kwenye uchunguzi na upelelezi wa kesi nzito huwa anazuiwa hata kusafiri?
Shahidi: Hilo linategemea
Kibatala: Linategemea nini?
Shahidi: Hilo sijui kwa kweli
Kibatala: Iambie sasa mahakama ni uchunguzi upi huo uliokuwa unaendelea ambao Uliwafanya usimkamate Freeman Mbowe Wakati wote
Shahidi: Mambo ya Forensic
Kibatala: Mlifanya mawasiliano kwa mara ya kwanza na taasisi za Forensic Mwezi July 2021 baada ya Freeman Mbowe kukamatwa Je wewe unasemaje?
Shahidi: Sina ninachojua....
Kibatala: Kingine kipi?
Shahidi: Mambo ya Intelligence
Kibatala: Intelligence ipi?
Shahidi: Mambo ya Intelligence mengi siwezi kuyazungumzia hapa
Kibatala: Kwa Sheria Ipi inayokuruhusu wewe shahidi usiseme hayo mambo halafu unataka KUMFUNGA mteja wangu?
Shahidi: Ni Mambo ya watu wengine kwenye upelelezi ikiwemo watu wengine waliokamatwa.
Kibatala: Kuna mtu alimakatwa baada ya September 2020?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Sasa nani unayemzungumzia hapa
Shahidi: Hakuna, Ila wengine wanaendelea kufuatiliwa
Kibatala: Kwa hiyo upelelezi wa kesi hii unaendelea?
Shahidi: Hapana, umeisha
Mahakama: Kicheko!
Kibatala: Je, unafahamu kwamba katika Nchi ambazo Viongozi wake ni MADIKTETA, Huwapa viongozi ambao ni wapinzani wao Kesi Ilikuwatisha
Shahidi: Hilo silifahamu
Kibatala: Nchi Kama Sweden, Marekani na Uingereza zinaweza kumkumbatia mtu ambaye ni gaidi wakati ni waganga wa UGAIDI?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Unafahamu nchi nilizozitaja zinafuatilia kesi hii kwa kutuma wawakilishi wao kuja kufuatilia haki ya Freeman Mbowe?
Shahidi: Hilo Mimi sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kitu kinaitwa TRAVEL ADVISORY
Shahidi: Sijawahi kukutana na kitu kama hicho
Kibatala: Askari Mzoefu Wa Miaka 20 hujawahi Kusikia Kitu hicho
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Upelelezi Wenu wote Mpaka Upelelezi Unakamilika, Urio si Ndiyo alikuwa Informant wenu?
Shahidi: Hilo sijaongelea hilo
Kibatala: Kwa hiyo alikuwa ni Whistler blower
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unaifahamu sheria inaitwa Whistler Blower and Protection Act, Juu ya kulinda WATOA Taarifa?
Shahidi: Hapana sifahamu sheria hiyo
Kibatala: Kwahiyo wewe Afisa wa Polisi na kiongozi wa kikosi Kazi hujui sheria ya Whistle Blower and Witness protection Act
Shahidi: Miye sijawahi kuisoma hiyo sheria natumia miongozo yangu tu
Kibatala: Kwa hiyo hufahamu kuwa Whistle Blower anapokuja kutoa taarifa umuandikishi maelezo ya onyo bali kwa taarifa za sheria hiyo?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Na Bado Mnataka tuendelee Na Kesi hii wakati Whistle Blower hajahojiwa kwa Sheria hiyo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Upelelezi Wenu wote Mpaka Upelelezi Unakamilika, Urio si Ndiyo alikuwa Informant wenu?
Shahidi: Hilo sijaongelea hilo
Kibatala: Kwa hiyo alikuwa ni Whistler blower
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unaifahamu sheria inaitwa Whistler Blower and Protection Act, Juu ya kulinda WATOA Taarifa?
Shahidi: Hapana sifahamu sheria hiyo
Kibatala: Kwa hiyo wewe Afisa wa Polisi na kiongozi wa kikosi Kazi hujui sheria ya Whistle Blower and Witness protection Act
Shahidi: Miye sijawahi kuisoma hiyo sheria natumia miongozo yangu tu
Kibatala: Kwa hiyo hufahamu kuwa Whistle Blower anapokuja kutoa taarifa humuandikishi maelezo ya onyo bali kwa taarifa za sheria hiyo?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Na Bado Mnataka tuendelee Na Kesi hii wakati Whistle Blower hajahojiwa kwa Sheria hiyo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ufahamu Wako Freeman Mbowe aliwapa pesa washtakiwa Personally kutoka Kwake?
Shahidi: Ndiyo aliwapa kutoka kwa Urio
Kibatala: Kwa Hiyo zikipitia kwa Urio ni Personally?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Msomi Mzima hujui maana ya Personally?
Shahidi: Nilikuwa sijaelewa
Kibatala: Sasa nitafutie sehemu Iliyoandikwa kwamba Kuna pesa iliyotoka kwa Mbowe kuja Kwa Urio, kisha Urio akawapa wao
Shahidi: Hakuna sehemu hiyo
Kibatala: Kwa hiyo katika Maelezo haya Ling'wenya alikabidhiwa pesa na Urio bila kuambiwa imetoka wapi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Soma hapa Katika ukurasa wa tatu Mstari wa mwisho baada ya kukutana na Luteni Dennis Urio. Je, alifahamu anaenda Moshi Kufanya nini?
Shahidi anasoma
"Baada ya Kufika tulikutana na Luteni Denis Urio Bar Moja ya Msavu sikumbuki Jina, Baada ya Kukutana luteni Urio alisema Kuwa Kuna kazi ya kwenda kufanya Moshi ambayo ni VIP Protection"
Amemaliza Kusoma ndugu Shahidi..
Kibatala: Hapo Ling'wenya kwenye Maelezo ya Onyo ambayo mnasema amekiri alisema anaenda Moshi Kufanya nini
Shahidi: Kufanya VIP PROTECTION
Kibatala: Sasa katika Statement hiyo nitafutie Mahala ambapo Urio anamwelekeza Ling'wenya Kuwa anaenda Kufanya Kazi ya Ugaidi Moshi
Shahidi: Hakuna sehemu hiyo anayosema kuwa alipewa Kazi ya kwenda Kufanya Kazi ya Ugaidi
Kibatala: Ni wapi ambapo Ling'wenya anakiri Kuwa alipewa pesa na Mbowe Kwenda Kufanya vitendo vya kigaidi
Shahidi: Hakuna sehemu ambayo anasema alipewa pesa na Mbowe kwenda Kufanya Ugaidi
Kibatala: Kuna Mahala Popote katika Statement Ambapo Freeman Mbowe alipiga simu au Kutuma Meseji Kumshawishi Ling'wenya Kwenda Kufanya Kazi ya Ugaidi?
Shahidi: Hakuna Maelezo hayo..
Kibatala: Kwa maelezo yenu Ni kwamba Luteni Denis Urio ndiye aliyeenda Ofisi wa ya DCI Kuleta taarifa na ndiye akawa INFORMANT wenu, je nini kiliwazuia kumpa vifaa kazi mtu huyu kwa ajili ya KUMREKODI Mbowe akitoa maelekezo ya kutenda UGAIDI au KUMDHURU Sabaya?
Shahidi: Mimi kama mpelelezi sina sauti za Mbowe akipanga ugaidi
Kibatala: Je, tuna video yoyote ambayo inaonyesha Mbowe akipanga ugaidi au kutoa maelekezo ya kutenda ugaidi au kumdhuru sabaya
Shahidi: Ndiyo... Hatuna video yoyote
Kibatala: Je Mliwahi Kumwambia Luten Denis Urio kuwa amrekodi Freeman Mbowe hata Kwa simu alitoa Maelekezo ya Kutenda Vitendo Vya Ugaidi au Kumdhuru Sabaya ili zije Mahakamani Kama Ushahidi wenu?
Shahidi: Hatuna Voice Record kutoka Kwa Urio sisi
Kibatala: Je Mli' Infiltrate Mtu Mwingine Aweze Kupata Records za Freeman Mbowe hata Kama Kwa Kutuma Mwanamke aweze Kumrekodi?? Shahidi: Miye siwezi Kufahamu Kibatala: Wewe ulifahamu lini Kuwepo kwa Luteni Denis Urio kama Whistle Blower?
Shahidi: Kwenye Mwezi wa Nane na Wa Tisa Baada ya Kuwa wamekamatwa wakina Ling'wenya
Kibatala: Mpaka Tarehe hiyo Mlikuwa mnafahamu Freeman Mbowe amemuagiza Luteni Denis Urio Kutenda Vitendo Vya Ugaidi, Je alikuwa amefanya Kosa au alikuwa hajafanya kosa?
Shahidi: Alikuwa amefanya kosa
Kibatala: Lakini Mpaka Wakati huo Mlikuwa hamjaona sababu ya Kumkamata
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Je, ni sahihi nikisema Mlitumia Luten Denis Urio kuwawekea Mtego Vijana hawa ili Kutengenezea Mbowe Kesi ya Kisiasa?
Shahidi: Si kweli, Wewe siyo Mpelelezi
Kibatala: Mimi na wewe nani ajui Upelelezi Wakati nimekuuliza hapa Kuhusu Mbinu za Kazi
Shahidi: Upelelezi ni Mambo Mengi siyo hayo tuh
Kibatala: Upelelezi gani unaujua wewe zaidi ya Kutesa Vijana wa watu ambao walitumikia Nchi na Jeshi?
Shahidi: Sijatesa Mtu Mimi
Kibatala: nakuuliza hapa chini ya kiapo, Unamjua Tito Magoti au humjui?
Shahidi: Simfahamu Tito Magoti kabisa
Kibatala: Nikimleta hapa mahakamani kama shahidi akisema kuwa ulishiriki kumteka je?
Shahidi: Mie sijawahi kumteka
Kibatala: Na Je unasemaje Juu ya taarifa Kuwa wewe ni miongoni wa watu WASIOJULIKANA na UMESHIRIKI KUTEKA na KUTESA watu?
Shahidi: Hapana Mimi sijawahi kuteka mtu Mimi
Kibatala: Je, Unafahamu Kuwa wewe ni Afisa wa Mahakama?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Askari Mzoefu Miaka 20 hujui kuwa PGO inakutambua kama Afisa wa Mahakama
Shahidi: Sijawahi Kujua
Kibatala: Nitafutie Mahala Popote ambapo Ling'wenya anakiri Kukutana katika Kikao cha Kupanga Vitendo Vya Kigaidi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nitafutie Mahala Popote katika Statement hiyo ambapo Ling'wenya anakiri kupanga kwenda Kulipua Soko la Kilombero Arusha
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nitafutie Mahala Popote ambapo Ling'wenya anakiri Kuwa alipanga Kulipua Mkoani Mwanza
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nitafutie Mahala Popote ambapo Ling'wenya anakiri Kuwa Bastola mliyokamata kuwa ilikuwa inatakiwa Kutumika Vipi Katika Vitendo Vya Ugaidi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Ni wapi ambapo Ling'wenya amezungumzia katika Statement hiyo aina ya Vilipuzi?
Shahidi: Hakuna Kibatala: Kwa uzoefu wako wewe Kama Afisa wa Polisi, Unaweza Kulipua bila ya Kuwa na Vilipuzi?
Shahidi: Hapana lazima uwe na Vilipuzi
Kibatala: Kuna Mahala Popote katika Statement hiyo ambapo Ling'wenya ameelezea namna walivyo panga Kumdhuru Sabaya
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Unasema Mliwakamata Ling'wenya na Adamoo Pale Rau Madukani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, kwa Upelelezi Wenu, Uwepo wao pale Rau Madukani Ling'wenya na Adamoo walikuwa katika matembezi yao au Kwa Kwenda Kutekeleza Mpango wa Ugaidi?
Shahidi: Walikuwa Wanatekeleza Mpango wa Ugaidi
Kibatala: Nitafutie hilo katika Statement Ya Ling'wenya hapo sehemu ambapo anasema walikuwa Rau Madukani Kutekeleza Mipango ya Ugaidi
Shahidi: Hapana hakuna sehemu hiyo
Kibatala: Lengai Ole Sabaya ameshahukumiwa Kifungo Kwa Makosa ya Ujambazi na Kudhulumu watu Mali zao
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ni Nyie nyie Ndiyo mlimshitaki Sabaya Kwa Makosa Ya Ujambazi ambaye Hapa Mnasema alitaka kudhuriwa?
Shahidi: Miye ushawahi kuniona kwa Sabaya?
Kibatala: Si nyie Jeshi la Polisi
Shahidi: Aaah! Sawa hapo sawa, Kama Jeshi la Polisi, Mwanzo Hukuwa specific
Kibatala: Ulishawahi Kuongea na Sabaya ukamwambia Kuna watu wanataka Kumdhuru
Shahidi: Hapana
Kibatala: turudi pale Rau Madukani, Baada ya Kuchukua Bastola Katika Maungo ya Adamoo, na Baadae ukamkabidhi Goodluck
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: na Pale hakuwa na Seizure Certificate ikabidi atoke aende Kwenye Gari Kufuata Karatasi ya Seizure Certificate
Shahidi: Sahihi
Kibatala: na Goodluck akaondola na Ile Bastola Kwenda Kwenye Gari, akarudi tena na Ile Bastola
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Lakini Hukusema Hapa Kwamba Goodluck Alisindikizwa Na Mashahidi Huru Kwenda Kuchukua Seizure Certificate Anita na Esther
Shahidi: Ndiyo sikusema
Shahidi: Lakini tayari nilisha kuwa nimesema Namba na Kila Mtu aliokuwa ameona namba
Kibatala: Sasa uliyasema hapa Mahakamani
Shahidi: Hapana
Kibatala: Na Goodluck ile Bastola Uliyo Mkabidhi aende nayo ilikuwa na zile Risasi tatu?
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Sasa unafahamu Kuwa Zile Risasi Zina Calibre Namba Kwenye kitako
Shahidi: Ni sahihi Zina Calibre Namba
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Ulizungumzia hizo tofauti Kuwa Zile Risasi zilikuwa Moja haina namba na Zile Mbili Zina namba tofauti
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: na Unafahamu Kuwa kila Silaha ina Origination yake
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ling'wenya alikwambia wamepata Wapi hiyo silaha
Shahidi: Haja eleza Katika Maelezo Yake
Kibatala: Katika Upelelezi Wenu Mligundua Adamoo alipata wapi hiyo Bastola
Shahidi: ilikuwa ni unlawful
Kibatala: Sijakuuliza hilo, nimekuuliza, Adamoo alipata wapi hiyo Bastola
Shahidi: Hatujui alipata wapi
Kibatala: na hujasema kuwa alipewa na Freeman Mbowe
Shahidi: Sijasema hivyo
Kibatala: na Hayo madawa ya kulevya aliyokutwa nayo Ling'wenya, mlichunguza amepata wapi
Shahidi: Hatukuchunguza
Kibatala: Je, aliwaambia kuwa madawa hayo ya kulevya yana husiana vipi na njama za ugaidi
Shahidi: Hatukugundua yana husiana vipi
Kibatala: Turudi Dar ea Salaam, Je Mlifika Dar es Salaam Saa ngapi Kutoka Moshi ni Saa 10 kwenda Kwenye Saa 11 au Saa 11 kwenda Saa 12 Shahidi' Ilikuwa Saa 11 kwenda Saa 12
Kibatala: Kwahiyo ni Range ya Lisaa limoja tu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Jana ulisema Kumbukumbu Ni Sifa ya Askari Makini
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wale Vijana wengine Watatu Mliwakamata Kwa Sababu walipita 92 KJ
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wewe Si Ndiyo Mpelelezi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa Uliwakamata kwa Sababu ipi au Ndiyo tuseme Jeshi linaonea Wanajeshi Wake waliolitumikia
Shahidi: Hapana Kwa sababu Walikutana kabla kuwa Mwezi July
Kibatala: Kwa hiyo Walikutana wapi
Shahidi: Dar es Salaam
Kibatala: Kwa hiyo Ni Ushahidi Wako Kuwa Ling'wenya alikuwa Dar es Salaam Mwezi July
Shahidi: Hapana Ilikuwa Mwezi wa Nane
Kibatala: Je Unafahamu Kuwa Chadema ilishiriki Uchaguzi Wa Rais, Wabunge Nchi Nzima
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Mbowe aligombea Ubunge Kule Hai
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Hivi Dhana ya Mtu Kupanga Kufanya Ugaidi Kudhuru Wananchi na Kwenda tena kwa hao hao Wananchi akiwa anagombea na Chama Chake
Shahidi: Hiyo ni Mtu Mwenyewe Sasa, miye sifanyii Kazi Dhana
Kibatala: Kuna Mahala Popote Wewe na Kikosi Kazi Chako Kuna Mahala Popote Ulizungumzia Kuripoti kwa Kamanda wa Polisi Kilimanjaro na Moshi kuwa Mna kazi ya Kitaifa Mnafanya
Shahidi: Hapa Sijazungumzia
Kibatala: Kuna Mahala Popote Kwenye PGO inasema Kwamba Maelezo Kaandikishie Mahala ambapo Kesi imefunguliwa
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Je, kuna Mwomgozo Wowote unazungumzia hivyo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Twende sehemu nyingine, Jana Nilisikia Hapa Unazungumzia Kuhusu Tundu Lissu Kupigwa Risasi, Je Tukio la Tundu Lissu Kupigwa Risasi Kwa Lissu ni ugaidi au siyo Ugaidi?
Shahidi: Siyo ugaidi ni uhalifu wa kawaida
Kibatala: tufanye comperative analysis, Inakuwaje kutaka kumdhuru Mhalifu Lengai Ole Sabaya iwe ugaidi ila kupigwa risasi kwa Tundu Lissu isiwe ugaidi?
Shahidi: Kwa sababu Ilikuwa inaendana na maandamano nchi nzima
Kibatala: Kwani Chadema Wamefanya Marangapi Maandamano
Kibatala: Je, maandamano hayo yalikuwa ni Ugaidi?
Shahidi: mimi Sijui
Kibatala: Kuna Mahala popote umesema Kuwa Mlipofika Dar es Salaam mlimfahamisha DCI?
Shahidi: Sijasema
Kibatala: Kuna Mahali Popote ile Umesema Kwamba Gari ilipo haribika mlimpigia simu DCI?
Shahidi: Kimya
Kibatala: Kuna Mahala ulisema pale Aishi Hotel Kingai alishuka kwenda kumtafuta Moses Lijenje
Shahidi: Ndiyo Nilisema
Kibatala: Kingai alikuwa anamfahamau Moses Lijenje..
Shahidi: Hapana, ilaaaaa....
Kibatala: Hakuna cha ila hapa, ushajibu swali hivyo...
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo P12
Kibatala: Shahidi Nionyeshe hapa Sehemu ambayo umejeza description za zile Risasi tatu
Shahidi: Si Kujaza, suala la Risasi kwenye Seizure Certificate
Kibatala: unajua Kuwa Seizure Certificate Ndiyo inaonyesha Chain of Custody ya Mali Mnazokamata?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kielelezo Namba P12 imeandikwa Jina na Saini ya anayekabidhiwa
Shahidi: sahihi
Kibatala: Tusomee Mtu anayekabidhiwa
Shahidi: H 4347 Detective Goodluck
Kibatala: hilo ndiyo Jina lake..?
Shahidi: Ndiyo Kwa Mujibu wa Kazi zetu
Kibatala: ulipo jaza wewe Kuna signature au hakuna
Shahidi: hakuna
Kibatala: Ulielezea Mahakama Kwanini Hakuna signature
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mpaka mnaenda Arusha kwa dada yake Moses Lijenje Arusha, Je Mnafahamu Majina yake?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mlikuwa mnajua Moses Lijenje pale Moshi anakaa Hotel gani?
Shahidi: Hotel Mbalimbali tu
Kibatala: Tutajie Hotel Mbili tu
Shahidi: Hapana sizifahamu!
Kibatala: Nafikiri nimemaliza mheshimiwa jaji
Kibatala sasa anaketi pahali pake, baada ya shughuli ya saa mbili na dakika 20 na shahidi wa jamhuri, SP Jumanne Malangahe
Anasimama Wakili Mwandamizi wa Serikali, Robert Kidando
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kupatiwa Vielelezo P11, 12 na 13
Wakili wa Serikali: Shahidi Ulionyeshwa Kuwa Sehemu ya Jina la H4347 kuna Jina na Hakuna Sahihi lakini Kwenye Jina lako Umeweka Sahihi
Shahidi: Kwa sababu Askari Mdogo hatakiwi Kuweka Saini ya Kukoroga anaweka Namba Yake ya kazi tu
John Mallya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hiyo ni fact Mpya ya Ufafanuzi
Jaji: Rudia Swali ambapo halitaleta Majibu Mapya
Wakili wa Serikali: Shahidi Ulionyeshwa Kuwa Sehemu ya Jina la H4347 Kuna Jina na Hakuna Sahihi lakini Kwenye Jina lako Umeweka Sahihi
Dickson Matata: OBJECTION bado ni fact Mpya hiyo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji sisi tuna Haki hiyo Kwa Mujibu wa Sheria, Siyo Kama tunakatazwa
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji nafikiri wapewa nafasi lakini na sisi tunaomba kurudi upyaaaaa kwenye swali hilo.
Jaji: Sawa ulizeni nitawapa upande wa utetezi nafasi ya kurudi tena...
Wakili wa Serikali: Shahidi Ulionyeshwa Kuwa Sehemu ya Jina la H4347 Kuna Jina na Hakuna Sahihi lakini Kwenye Jina lako Umeweka Sahihi
Shahidi: Kwa sababu Askari Mdogo hatakiwi Kuweka Saini ya Kukoroga anaweka Namba Yake ya kazi tu
Wakili wa Serikali: Kuna Hiki Kielelezo Cha P13 Maelezo ya Onyo ya Mshtakiwa Wa Tatu.. Kwa Mujibu wa statement hii Uliulizwa swali Kama Mohammed Ling'wenya kuhusiana na Mpango Wa Kulipua Vituo Vya Mafuta kuhusu Vilipuzi Ukasema hakukueleza
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali: Sasa Yeye alikueleza nini
Shahidi: alieleza Nchi Nzima Haku specify Sehemu Moja
Wakili wa Serikali: Uliulizwa hapa Kuhusiana na Denis Urio Kuhusiana na Kuweka Mtego ilikumpa Mshtakiwa wa nne Kesi ya Kisiasa
Shahidi: Si Kweli Shahidi alileta Taarifa Mwenyewe wala hakutumwa na Mtu
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusiana Kuwakamata Wakina Gabriel na Khalid, kuwa Mliwakamata sababu walipita 92 kJ Je, Unasemaje?
Shahidi: Si Kweli tukiwa kamata wakiwa sababu Wali zungumza na Washtakiwa Na wakawa wapo tayari Kujiunga
Wakili Mallya: OBJECTION Neno wapo tayari hakusema Jaji anasoma na Kumbukumbu haionyeshi Kuwa walikuwa wanampango wa Kwenda Kujiunga na akina Ligw'enya.
Wakili wa Serikali: Basi Mheshimiwa Jaji Neno Mpango wa Kujiunga liondoke
Wakili wa Serikali: Tufafanulie Exactly Ni Mwezi upi Khalid na Gabriel Walikutana Mshtakiwa Wa tatu Dar es Salaam
Shahidi: Ni Mwezi wa Saba
Wakili wa Serikali: Ulitoa Taarifa hapa Kwamba ACP Kingai Kuwa hakuwepo Tarehe 09 August 2020 hakuwepo Mbweni, Hebu Tufafanulie hapo
Shahidi: Ni Kwa sababu tulikuwa na Shughuli Ya Kuendelea Kumtafuta Mtuhumiwa Khalfani Bwire
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Pia Kuhusiana na Upekuzi na Ukamataji Pale Rau Madukani Kwamba Baada ya Kukamata Bastola Ulimtuma Goodluck Kwenye Gari na Ukasema Hakuna aliyekwenda na Goodluck Kufuata Seizure Certificate Tufafanulie kwanini Ikitokea hivyo
Shahidi: Baada ya Kukamata Nilisema Namba na wote walisikia, Ndipo Nikamtuma Goodluck na Yeye Mwenyewe ndiye aliyerudi na hiyo silaha
Wakili MALLYA: OBJECTION hayo Ni Majibu Mapya tena Yanajikoroga na Majibu ya awali
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kuwa Kama Unajua Kuwa Mshtakiwa Freeman Mbowe alikamatwa Mwanza akiwa Kwenye Mkutano wa Katiba Ukasema ufahamu, Je Nini Unachofahamu Shahidi: Ni nacho fahamu ni kuwa alikamatwa Mwanza Kwa tuhuma Za Ugaidi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kama Ulikuwa na Maslahi Binafsi na Washtakiwa
Shahidi: Niliwa kamata kwa Sababu ya tuhuma ambazo zimekuwa reported Polisi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu na Askari aliyesimamisha Daladala na Kuhusu Taarifa za Yule Dereva, Ukasema Hapakuwa na Umuhimu
Shahidi: Hapa Kuwa na Umuhimu Kwa sababu Tulimkamata Kisheria na Ndiyo Maana Mpaka Sasa Yupo Mahakamani
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu simu Mbili za Mshtakiwa Ukasema hilo hujalitolea Ushahidi
Shahidi: Ni Kwa sababu siyo Mimi niliye Mkamata wala Kufanyia Upekuzi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu Mshtakiwa Wa tatu Kufanya VIP protection Ukasema Siyo Kosa, Ulikuwa unamaanisha nini
Shahidi: Kwa sababu siyo Kosa kama Unafanya Kwa nia Njema ila Ni Kosa Unafanya Kama Jinai
Dickson Matata: OBJECTION hapo Mbele Majibu nayapinga sababu Hakusema Mwanzo
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Katika Kielelezo hicho pia, Kuhusiana Kile Kilicho hamasishwa Kufanya Maandamano Nchi Nzima ni Kosa au Siyo Kosa Ukasema inategemea
Shahidi: Kufanya Maandamano Kwa Kufuata Sheria Siyo Kosa
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kuhusu Mkoa gani Umetwajwa Kufanya Maandamano, Ukasema Hakuna Je ni Kitu gani kimesemwa
Shahidi: Kufanya Maandamano Nchi Nzima na Mikoa ipo Ndani ya Nchi
Wakili wa Serikali: katika Statement hiyo Umeulizwa Kuhusiana na suala la Mshtakiwa Wa Tatu Kupewa pesa pale Morogoro Kwa jili ya VIP protection Ukasema Siyo Kosa Sababu inategemea na Malengo
Wakili DICKSON MATATA: OBJECTION swali hilo Siku sema hivyo
Wakili wa Serikali: Sawa narudia
Wakili wa Serikali: katika Statement hiyo Umeulizwa Kuhusiana na suaa la Mshtakiwa Wa Tatu Kupewa pesa pale Morogoro Kwa jili ya VIP protection Ukasema Siyo Kosa
Shahidi: Ni Kwa sababu kama unatuma Kwa nia Njema siyo Kosa Wakili
DICKSON MATATA: Mheshimiwa Jibu la Swali hilo Kwamba nia Njema, Nia njema Haikutajwa
Jaji: Umechelewa Kusimama, Nitakupa nafasi ya Kuhoji tena
Wakili wa Serikali: Nilisikia Unasema Kuwa Watuhumiwa Wataandikwa Kwenye Detention Register Pale tu Watakapo Pokelewa, Unamaanisha Nini
Shahidi: Nilikuwa namaanisha Kwamba Pale wanapokelewa na Kuwekwa Mahabusu Ndiyo Wanaandikishwa Kwenye Detention Register
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Pia Kuhusiana na Ule Muda wa Ukamataji Ukasema Ilikuwa ni Saa 7 Mchana na Pia Uliandika Kwenye Hati ya Upekuzi.. Na Ukasema Muda huo Ulikuwa Muda Sasa Sana Je Ulikuwa Umaanisha Nini
Shahidi: Nilikuwa namaanisha Haijavuka hiyo Saa Saba
Wakili wa Serikali: Pia Uliulizwa hapa Kwamba Siku ya Tarehe 09 August 2020 Ndiyo Siku Uliwapeleka Kituo cha Polisi Mbweni wewe na Mahita, Ukasema Siyo Kweli, Je Unamanisha Nini
Shahidi: Siyo Kweli Kwamba tuliwapeleka Kituo cha Polisi Mbweni Tarehe 09 August Bali Ilikuwa tarehe 08 August 2020
Wakili wa Serikali: Pia Umeulizwa Kwamba Mlienda Arusha, Ukaulizwa Kama ikiwa Unamfahamu Majina ya Huyo Dada yake Lijenje, Nyumba au Mtaa Ukasema Ufahamu, Hebu tufafanulie
Shahidi: Ni Kwa sababu wao Watuhumiwa ndiyo walikuwa wanatupeleka kila sehemu
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu Kutomkamata Mshtakiwa Wa Nne Baada ya Wengine watatu Kukamatwa zaidi ya Mwaka Mmoja Ukasema Upelelezi Ulikuwa unaendelea, Je Ni Upelelezi upi
Shahidi: Masuala la Forensics na Upelelezi Mwingine Ulikuwa unaendelea
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Pia Maswali Kuwa katika Bastola hiyo Uliyo kamata ilikuwa ina Maeneo ambayo yangeweza Kutoa Finger Prints Ukasema ni Kweli, lakini haujaleta Mahakamani
Shahidi: Ni kweli Siku leta Ushahidi Wa Finger Prints Kwa sababu Hapakuwa na Mahaka Kwamba Silaha hiyo ilikuwa haina Ubishi kuwa inamilikiwa na Mtuhumiwa
Wakili wa Serikali: Jana Uliulizwa kuhusu Katazo la Ku unLoad Silaha, Ukasema inategemea, Je Ulikuwa Unamanisha nini
Shahidi: Ni si Silaha ambayo imekuwa eneo la Tukio ndiyo haitakiwi Kuwa Unload lakini Silaha ambayo unataka Ku seize na Umeipata Kwa Mtu Unaruhusiwa Ku unload Kuona Kuna Kitu gani, Ndiyo Nilichomanisha..
Wakili wa Serikali: Uliulizwa hapa Kuhusu Mshtakiwa Wa tatu kuhusu Kwenda Kwa Mlinzi wa Amani ila Ukasema Hukuona sababu ya kwenda na wala Hakuhitaji
Shahidi: Ni Kwa sababu alikuwa tayari Kujaza Maelezo na Hakuona haja ya Kwenda Kwa Mlinzi wa Amani
Wakili wa Serikali: Uliulizwa utendaji wa shughuli Zenu Mmekuwa Mkishirikiana na Mamlaka Mbalimbali, Tufafanulie ni Ushirikiano Gani mnapeana
Shahidi: tunashirikiana na vyombo mbalimbali vya Usalama lakini kwa ngazi za Juu
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba kukomea hapo hatutokuwa na swali lingine
Jaji: Kuna maeneo mawili ambayo mnayarudia upande wa utetezi
Wakili Peter Kibatala: Shahidi Ni kweli wakati unatoa ushahidi wako unaomba kutoa vielelezo hukufafanua kuwa kuna maofisa ambao hawatakiwi kusaini?
Shahidi: Hayo Sikusema
Kibatala: Uliposema maofisa wa chini ulimaanisha nini?
Shahidi: Kuanzia Staff sergeant kurudi chini
Kibatala: Detective Coplo anatakiwa kusaini?
Shahidi: Hatakiwi kusaini Kibatala: kwa ruhusa ya Mahakama naomba usome Hapa Shahidi "F5914 Detective Coplo Hafidh Mohammed"
Kibatala: Huyo ni Afisa wa chini au siyo?
Shahidi: Ni Afisa wa chini
Kibatala: Amesaini au hajasaini?
Shahidi: AMESAINI
Wakili Dickson Matata: Mheshimiwa Jaji naomba P13
Matata: Shahidi, Jana wakati nakufanyia Dodoso Nilikuuliza Mtu Kupewa nauli na pesa ya matumizi Njiani ni Kosa au Siyo Kosa Ukasema Siyo Kosa Leo Wakati Unafanyiwa Re-examination Ukasema Siyo Kosa kama ulipewa kwa nia Njema
Sasa chukua hiyo Statement Nionyeshe Sehemu ambayo Mohammed Ling'wenya amesema alipewa hiyo Pesa ya Nauli na Matumizi ya Njiani Kwa nia Ovu
Shahidi: Hakuna Aliposema
Wakili Matata: Mheshimiwa Jaji sina Swali Lingine
Jaji aandika Kidogo
Mahakama Ipo Kimya Kidogo
Jaji Baada ya Maswali hayo Kuulizwa Upande wa Serikali Maswali Lolote?
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Hakuna swali Mheshimiwa Jaji
Jaji: Mmemaliza na shahidi wa 8?
Wakili wa Serikali: Ndiyo Mheshimiwa Jaji
Jaji: Shahidi Tunakuahukuru Kwa Ushahidi Wako
Shahidi anatoka na kuondoka kizimbani
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Huyo ndiye shahidi tuliyekuwa naye leo Hivyo tunaomba hairisho la Kesi hii ili kuja Kuendelea Kesho Kutwa Alhamisi tarehe 13 January 2022 Ambapo tutaleta shahidi mwingine kuja kuendelea na ushahidi
Na Pamoja na kwamba sasa ni saa saba mchana hatukuweza kujua shahidi Huyu angeweza Kumalizia Saa ngapi Hivyo tunaomba hairisho Mpka kesho kutwa kama nilivyo Omba, Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji
Wakili Peter Kibatala: Hatuna Pingamizi Mheshimiwa Jaji
Jaji: Basi maombi ya hairisho yanakubaliwa mpaka kesho kutwa alhamisi ya tarehe 13 January 2022 Washtakiwa wataendelea kuwa rumande chini ya magereza mpaka siku hiyo Jaji anatoka
Tuendelee na kesi hii hapa keshokutwa tarehe 13
Leo tarehe 11/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea.
Kufahamu ilipoishia, soma hapa: Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Januari 10, 2022. Shahidi namba 8 aendelea kutoa ushahidi. Kesi imeahirishwa hadi kesho 11/01/2022
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
UPDATES:
Jaji ameingia Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha;
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Tulimanywa Majige
Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikikupendeza naomba Kuwatambulisha Mawakili
Nashon Nkungu
John Mallya
Dickson Matata
Faraji Mangula
Sisty Aloyce
Michael Mwangasa
Gaston Garubindi
Seleman Matauka
Jaji anaita Washtakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri lina endelea Kusikilizwa na Upande wa Mashtaka tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji nasi pia tupo tayari Kuendelea
Jaji anaandika Kidogo wakati Mahakama Ipo Kimya
Wakili Peter Kibatala anasimama na Kuendelea na Maswali kwa shahidi
Kibatala: Shahidi Tulikuwa tunaendelea Kuhusu Kesi yenu Kuwa Mbowe Alimpa Maelezo Urio na Urio Aweze Kutafuta Watu wa Kufanya Ugaidi
Kibatala: Shahidi, Urio bado Yupo Jeshini na Mwanajeshi aliye kwenye Utumishi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: katika Ushahidi Wako Uliwahi Kuongea Lolote hapa Mahakamani Kwamba Urio akiwa Kama Mwanajeshi wa JWTZ Kushiriki katika Vitendo Vizito Vya Ugaidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulishawahi kuwasiliana na JWTZ kuhusu Mtumishi wao Urio Kushiriki katika ya Matendo ya Ugaidi
Shahidi: Sijafanya
Kibatala: kwa ufahamu wako Uongozi wa JWTZ unafahamu Mwanajeshi wao Urio alikuwa anafanya Vitendo Vya Kutafuta Watu wa Kufanya Ugaidi
Shahidi: Mimi sifahamu
Kibatala: Je Unakubaliana na Mimi Kuwa Vitendo Vya Ugaidi ni Vitendo Vizito na Vinatikisia Psychology na Utulivu wa Nchi
Shahidi: Ndiyo Kibatala: Je unafahamu Kuwa JWTZ Wana kitengo Cha Ujasusi cha Millitary Intelligence, kazi yao ni Pamoja na Kuchunguza Matendo ya Ugaidi?
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Katika Ushahidi Wako Ulizungumzia lolote kuhusu Kushirikiana na Vyombo Vya Usalama na Kijasusi kama TISS?
Shahidi: Mimi sifahamu lakini Viongozi wangu Watakuwa wamefanya
Kibatala: Sasa Viongozi wako Unawaona hapo Kwenye Kizimba?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Kuwa Moja ya Kazi ya Hizo Taasisi ni Kushughulika na Mambo ya Ugaidi
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kuwa iwapo taasisi hizo zingeshirikishwa katika ngazi mbalimbali ya vyombo vya usalama na idara ya uhamiaji na wao wangeshirikishwa?
Shahidi: Hilo mimi siyo wajibu wangu Kibatala: umeanza kuleta ujeuri mahakamani Shahidi: Hapana Kibatala: Sasa Jibu, unafahamu au hufahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Unafahamu Kuwa Mshtakiwa Wa 4 alisafiri Kwenda Nje Mara Kadhaa?
Shahidi: Hapana, Sifahamu
Kibatala: Katika Kikosi chenu wewe ulikuwa Second Command Kama Top leader, Je, Unafahamu timu yenu Kuna Mtu aliwasiliana na Rais Samia Suluhu Hassan?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Unafahamu alipopata taarifa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Mbowe alikuwa anajua atashitakiwa Kwa Ugaidi ndiyo Maana akakimbia nje ya Nchi kukwepa upelelezi?
Shahidi: Hapana... Sifahamu
Kibatala: Kuna kikosi kazi zaidi ya chenu kilikuwa kinafanyia kazi suala hili labda wao walienda kumtaarifu Rais Samia Suluhu Hassan?
Shahidi: Hapana.. Sifahamu
Kibatala: Kesi hii Rais Samia Suluhu Hassan alisema kuna watu wamefungwa katika shauri hili, kwa ufahamu wako kuna watu wamefungwa kwenye shauri hili?
Shahidi: Hilo silijui na siwezi kuliongelea
Kibatala: Kama unajua sema najua au kama hujui sema sijui, Kusema huwezi kuongelea ni ujeuri huo na nitaomba mahakama IKUZIMISHE..
Shahidi: Hilo silifahamu.
Kibatala: Je unafahamu kuwa Kingai alisema kuwa alimuwekea uangalizi Mbowe hata alipokuwa nje ya Nchi?
Shahidi: Hilo Mimi silifahamu Kibatala: Je Kwa ufahamu wako wewe Freeman Mbowe alikimbia nje ya nchi Ilikuweza kukwepa upelelezi
Shahidi: Hilo silifahamu kwa kweli
Kibatala: Je unafahamu Freeman Mbowe kaenda nchi mbalimbali kutoka August 2020 mpaka Mwaka 2021 July?
Shahidi: silifahamu nchi hizo mimi
Kibatala: Je unafahamu mamlaka chunguzi/ pelelezi za Tanzania ziliwahi kuwasiliana na mamlaka chunguzi za hizo nchi?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Je unafahamu kuwa mtu ambaye akiwa kwenye uchunguzi na upelelezi wa kesi nzito huwa anazuiwa hata kusafiri?
Shahidi: Hilo linategemea
Kibatala: Linategemea nini?
Shahidi: Hilo sijui kwa kweli
Kibatala: Iambie sasa mahakama ni uchunguzi upi huo uliokuwa unaendelea ambao Uliwafanya usimkamate Freeman Mbowe Wakati wote
Shahidi: Mambo ya Forensic
Kibatala: Mlifanya mawasiliano kwa mara ya kwanza na taasisi za Forensic Mwezi July 2021 baada ya Freeman Mbowe kukamatwa Je wewe unasemaje?
Shahidi: Sina ninachojua....
Kibatala: Kingine kipi?
Shahidi: Mambo ya Intelligence
Kibatala: Intelligence ipi?
Shahidi: Mambo ya Intelligence mengi siwezi kuyazungumzia hapa
Kibatala: Kwa Sheria Ipi inayokuruhusu wewe shahidi usiseme hayo mambo halafu unataka KUMFUNGA mteja wangu?
Shahidi: Ni Mambo ya watu wengine kwenye upelelezi ikiwemo watu wengine waliokamatwa.
Kibatala: Kuna mtu alimakatwa baada ya September 2020?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Sasa nani unayemzungumzia hapa
Shahidi: Hakuna, Ila wengine wanaendelea kufuatiliwa
Kibatala: Kwa hiyo upelelezi wa kesi hii unaendelea?
Shahidi: Hapana, umeisha
Mahakama: Kicheko!
Kibatala: Je, unafahamu kwamba katika Nchi ambazo Viongozi wake ni MADIKTETA, Huwapa viongozi ambao ni wapinzani wao Kesi Ilikuwatisha
Shahidi: Hilo silifahamu
Kibatala: Nchi Kama Sweden, Marekani na Uingereza zinaweza kumkumbatia mtu ambaye ni gaidi wakati ni waganga wa UGAIDI?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Unafahamu nchi nilizozitaja zinafuatilia kesi hii kwa kutuma wawakilishi wao kuja kufuatilia haki ya Freeman Mbowe?
Shahidi: Hilo Mimi sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kitu kinaitwa TRAVEL ADVISORY
Shahidi: Sijawahi kukutana na kitu kama hicho
Kibatala: Askari Mzoefu Wa Miaka 20 hujawahi Kusikia Kitu hicho
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Upelelezi Wenu wote Mpaka Upelelezi Unakamilika, Urio si Ndiyo alikuwa Informant wenu?
Shahidi: Hilo sijaongelea hilo
Kibatala: Kwa hiyo alikuwa ni Whistler blower
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unaifahamu sheria inaitwa Whistler Blower and Protection Act, Juu ya kulinda WATOA Taarifa?
Shahidi: Hapana sifahamu sheria hiyo
Kibatala: Kwahiyo wewe Afisa wa Polisi na kiongozi wa kikosi Kazi hujui sheria ya Whistle Blower and Witness protection Act
Shahidi: Miye sijawahi kuisoma hiyo sheria natumia miongozo yangu tu
Kibatala: Kwa hiyo hufahamu kuwa Whistle Blower anapokuja kutoa taarifa umuandikishi maelezo ya onyo bali kwa taarifa za sheria hiyo?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Na Bado Mnataka tuendelee Na Kesi hii wakati Whistle Blower hajahojiwa kwa Sheria hiyo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Upelelezi Wenu wote Mpaka Upelelezi Unakamilika, Urio si Ndiyo alikuwa Informant wenu?
Shahidi: Hilo sijaongelea hilo
Kibatala: Kwa hiyo alikuwa ni Whistler blower
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unaifahamu sheria inaitwa Whistler Blower and Protection Act, Juu ya kulinda WATOA Taarifa?
Shahidi: Hapana sifahamu sheria hiyo
Kibatala: Kwa hiyo wewe Afisa wa Polisi na kiongozi wa kikosi Kazi hujui sheria ya Whistle Blower and Witness protection Act
Shahidi: Miye sijawahi kuisoma hiyo sheria natumia miongozo yangu tu
Kibatala: Kwa hiyo hufahamu kuwa Whistle Blower anapokuja kutoa taarifa humuandikishi maelezo ya onyo bali kwa taarifa za sheria hiyo?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Na Bado Mnataka tuendelee Na Kesi hii wakati Whistle Blower hajahojiwa kwa Sheria hiyo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ufahamu Wako Freeman Mbowe aliwapa pesa washtakiwa Personally kutoka Kwake?
Shahidi: Ndiyo aliwapa kutoka kwa Urio
Kibatala: Kwa Hiyo zikipitia kwa Urio ni Personally?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Msomi Mzima hujui maana ya Personally?
Shahidi: Nilikuwa sijaelewa
Kibatala: Sasa nitafutie sehemu Iliyoandikwa kwamba Kuna pesa iliyotoka kwa Mbowe kuja Kwa Urio, kisha Urio akawapa wao
Shahidi: Hakuna sehemu hiyo
Kibatala: Kwa hiyo katika Maelezo haya Ling'wenya alikabidhiwa pesa na Urio bila kuambiwa imetoka wapi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Soma hapa Katika ukurasa wa tatu Mstari wa mwisho baada ya kukutana na Luteni Dennis Urio. Je, alifahamu anaenda Moshi Kufanya nini?
Shahidi anasoma
"Baada ya Kufika tulikutana na Luteni Denis Urio Bar Moja ya Msavu sikumbuki Jina, Baada ya Kukutana luteni Urio alisema Kuwa Kuna kazi ya kwenda kufanya Moshi ambayo ni VIP Protection"
Amemaliza Kusoma ndugu Shahidi..
Kibatala: Hapo Ling'wenya kwenye Maelezo ya Onyo ambayo mnasema amekiri alisema anaenda Moshi Kufanya nini
Shahidi: Kufanya VIP PROTECTION
Kibatala: Sasa katika Statement hiyo nitafutie Mahala ambapo Urio anamwelekeza Ling'wenya Kuwa anaenda Kufanya Kazi ya Ugaidi Moshi
Shahidi: Hakuna sehemu hiyo anayosema kuwa alipewa Kazi ya kwenda Kufanya Kazi ya Ugaidi
Kibatala: Ni wapi ambapo Ling'wenya anakiri Kuwa alipewa pesa na Mbowe Kwenda Kufanya vitendo vya kigaidi
Shahidi: Hakuna sehemu ambayo anasema alipewa pesa na Mbowe kwenda Kufanya Ugaidi
Kibatala: Kuna Mahala Popote katika Statement Ambapo Freeman Mbowe alipiga simu au Kutuma Meseji Kumshawishi Ling'wenya Kwenda Kufanya Kazi ya Ugaidi?
Shahidi: Hakuna Maelezo hayo..
Kibatala: Kwa maelezo yenu Ni kwamba Luteni Denis Urio ndiye aliyeenda Ofisi wa ya DCI Kuleta taarifa na ndiye akawa INFORMANT wenu, je nini kiliwazuia kumpa vifaa kazi mtu huyu kwa ajili ya KUMREKODI Mbowe akitoa maelekezo ya kutenda UGAIDI au KUMDHURU Sabaya?
Shahidi: Mimi kama mpelelezi sina sauti za Mbowe akipanga ugaidi
Kibatala: Je, tuna video yoyote ambayo inaonyesha Mbowe akipanga ugaidi au kutoa maelekezo ya kutenda ugaidi au kumdhuru sabaya
Shahidi: Ndiyo... Hatuna video yoyote
Kibatala: Je Mliwahi Kumwambia Luten Denis Urio kuwa amrekodi Freeman Mbowe hata Kwa simu alitoa Maelekezo ya Kutenda Vitendo Vya Ugaidi au Kumdhuru Sabaya ili zije Mahakamani Kama Ushahidi wenu?
Shahidi: Hatuna Voice Record kutoka Kwa Urio sisi
Kibatala: Je Mli' Infiltrate Mtu Mwingine Aweze Kupata Records za Freeman Mbowe hata Kama Kwa Kutuma Mwanamke aweze Kumrekodi?? Shahidi: Miye siwezi Kufahamu Kibatala: Wewe ulifahamu lini Kuwepo kwa Luteni Denis Urio kama Whistle Blower?
Shahidi: Kwenye Mwezi wa Nane na Wa Tisa Baada ya Kuwa wamekamatwa wakina Ling'wenya
Kibatala: Mpaka Tarehe hiyo Mlikuwa mnafahamu Freeman Mbowe amemuagiza Luteni Denis Urio Kutenda Vitendo Vya Ugaidi, Je alikuwa amefanya Kosa au alikuwa hajafanya kosa?
Shahidi: Alikuwa amefanya kosa
Kibatala: Lakini Mpaka Wakati huo Mlikuwa hamjaona sababu ya Kumkamata
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Kibatala: Je, ni sahihi nikisema Mlitumia Luten Denis Urio kuwawekea Mtego Vijana hawa ili Kutengenezea Mbowe Kesi ya Kisiasa?
Shahidi: Si kweli, Wewe siyo Mpelelezi
Kibatala: Mimi na wewe nani ajui Upelelezi Wakati nimekuuliza hapa Kuhusu Mbinu za Kazi
Shahidi: Upelelezi ni Mambo Mengi siyo hayo tuh
Kibatala: Upelelezi gani unaujua wewe zaidi ya Kutesa Vijana wa watu ambao walitumikia Nchi na Jeshi?
Shahidi: Sijatesa Mtu Mimi
Kibatala: nakuuliza hapa chini ya kiapo, Unamjua Tito Magoti au humjui?
Shahidi: Simfahamu Tito Magoti kabisa
Kibatala: Nikimleta hapa mahakamani kama shahidi akisema kuwa ulishiriki kumteka je?
Shahidi: Mie sijawahi kumteka
Kibatala: Na Je unasemaje Juu ya taarifa Kuwa wewe ni miongoni wa watu WASIOJULIKANA na UMESHIRIKI KUTEKA na KUTESA watu?
Shahidi: Hapana Mimi sijawahi kuteka mtu Mimi
Kibatala: Je, Unafahamu Kuwa wewe ni Afisa wa Mahakama?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Askari Mzoefu Miaka 20 hujui kuwa PGO inakutambua kama Afisa wa Mahakama
Shahidi: Sijawahi Kujua
Kibatala: Nitafutie Mahala Popote ambapo Ling'wenya anakiri Kukutana katika Kikao cha Kupanga Vitendo Vya Kigaidi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nitafutie Mahala Popote katika Statement hiyo ambapo Ling'wenya anakiri kupanga kwenda Kulipua Soko la Kilombero Arusha
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nitafutie Mahala Popote ambapo Ling'wenya anakiri Kuwa alipanga Kulipua Mkoani Mwanza
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nitafutie Mahala Popote ambapo Ling'wenya anakiri Kuwa Bastola mliyokamata kuwa ilikuwa inatakiwa Kutumika Vipi Katika Vitendo Vya Ugaidi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Ni wapi ambapo Ling'wenya amezungumzia katika Statement hiyo aina ya Vilipuzi?
Shahidi: Hakuna Kibatala: Kwa uzoefu wako wewe Kama Afisa wa Polisi, Unaweza Kulipua bila ya Kuwa na Vilipuzi?
Shahidi: Hapana lazima uwe na Vilipuzi
Kibatala: Kuna Mahala Popote katika Statement hiyo ambapo Ling'wenya ameelezea namna walivyo panga Kumdhuru Sabaya
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Unasema Mliwakamata Ling'wenya na Adamoo Pale Rau Madukani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, kwa Upelelezi Wenu, Uwepo wao pale Rau Madukani Ling'wenya na Adamoo walikuwa katika matembezi yao au Kwa Kwenda Kutekeleza Mpango wa Ugaidi?
Shahidi: Walikuwa Wanatekeleza Mpango wa Ugaidi
Kibatala: Nitafutie hilo katika Statement Ya Ling'wenya hapo sehemu ambapo anasema walikuwa Rau Madukani Kutekeleza Mipango ya Ugaidi
Shahidi: Hapana hakuna sehemu hiyo
Kibatala: Lengai Ole Sabaya ameshahukumiwa Kifungo Kwa Makosa ya Ujambazi na Kudhulumu watu Mali zao
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ni Nyie nyie Ndiyo mlimshitaki Sabaya Kwa Makosa Ya Ujambazi ambaye Hapa Mnasema alitaka kudhuriwa?
Shahidi: Miye ushawahi kuniona kwa Sabaya?
Kibatala: Si nyie Jeshi la Polisi
Shahidi: Aaah! Sawa hapo sawa, Kama Jeshi la Polisi, Mwanzo Hukuwa specific
Kibatala: Ulishawahi Kuongea na Sabaya ukamwambia Kuna watu wanataka Kumdhuru
Shahidi: Hapana
Kibatala: turudi pale Rau Madukani, Baada ya Kuchukua Bastola Katika Maungo ya Adamoo, na Baadae ukamkabidhi Goodluck
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: na Pale hakuwa na Seizure Certificate ikabidi atoke aende Kwenye Gari Kufuata Karatasi ya Seizure Certificate
Shahidi: Sahihi
Kibatala: na Goodluck akaondola na Ile Bastola Kwenda Kwenye Gari, akarudi tena na Ile Bastola
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Lakini Hukusema Hapa Kwamba Goodluck Alisindikizwa Na Mashahidi Huru Kwenda Kuchukua Seizure Certificate Anita na Esther
Shahidi: Ndiyo sikusema
Shahidi: Lakini tayari nilisha kuwa nimesema Namba na Kila Mtu aliokuwa ameona namba
Kibatala: Sasa uliyasema hapa Mahakamani
Shahidi: Hapana
Kibatala: Na Goodluck ile Bastola Uliyo Mkabidhi aende nayo ilikuwa na zile Risasi tatu?
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Sasa unafahamu Kuwa Zile Risasi Zina Calibre Namba Kwenye kitako
Shahidi: Ni sahihi Zina Calibre Namba
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Ulizungumzia hizo tofauti Kuwa Zile Risasi zilikuwa Moja haina namba na Zile Mbili Zina namba tofauti
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: na Unafahamu Kuwa kila Silaha ina Origination yake
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ling'wenya alikwambia wamepata Wapi hiyo silaha
Shahidi: Haja eleza Katika Maelezo Yake
Kibatala: Katika Upelelezi Wenu Mligundua Adamoo alipata wapi hiyo Bastola
Shahidi: ilikuwa ni unlawful
Kibatala: Sijakuuliza hilo, nimekuuliza, Adamoo alipata wapi hiyo Bastola
Shahidi: Hatujui alipata wapi
Kibatala: na hujasema kuwa alipewa na Freeman Mbowe
Shahidi: Sijasema hivyo
Kibatala: na Hayo madawa ya kulevya aliyokutwa nayo Ling'wenya, mlichunguza amepata wapi
Shahidi: Hatukuchunguza
Kibatala: Je, aliwaambia kuwa madawa hayo ya kulevya yana husiana vipi na njama za ugaidi
Shahidi: Hatukugundua yana husiana vipi
Kibatala: Turudi Dar ea Salaam, Je Mlifika Dar es Salaam Saa ngapi Kutoka Moshi ni Saa 10 kwenda Kwenye Saa 11 au Saa 11 kwenda Saa 12 Shahidi' Ilikuwa Saa 11 kwenda Saa 12
Kibatala: Kwahiyo ni Range ya Lisaa limoja tu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Jana ulisema Kumbukumbu Ni Sifa ya Askari Makini
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wale Vijana wengine Watatu Mliwakamata Kwa Sababu walipita 92 KJ
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wewe Si Ndiyo Mpelelezi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa Uliwakamata kwa Sababu ipi au Ndiyo tuseme Jeshi linaonea Wanajeshi Wake waliolitumikia
Shahidi: Hapana Kwa sababu Walikutana kabla kuwa Mwezi July
Kibatala: Kwa hiyo Walikutana wapi
Shahidi: Dar es Salaam
Kibatala: Kwa hiyo Ni Ushahidi Wako Kuwa Ling'wenya alikuwa Dar es Salaam Mwezi July
Shahidi: Hapana Ilikuwa Mwezi wa Nane
Kibatala: Je Unafahamu Kuwa Chadema ilishiriki Uchaguzi Wa Rais, Wabunge Nchi Nzima
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Mbowe aligombea Ubunge Kule Hai
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Hivi Dhana ya Mtu Kupanga Kufanya Ugaidi Kudhuru Wananchi na Kwenda tena kwa hao hao Wananchi akiwa anagombea na Chama Chake
Shahidi: Hiyo ni Mtu Mwenyewe Sasa, miye sifanyii Kazi Dhana
Kibatala: Kuna Mahala Popote Wewe na Kikosi Kazi Chako Kuna Mahala Popote Ulizungumzia Kuripoti kwa Kamanda wa Polisi Kilimanjaro na Moshi kuwa Mna kazi ya Kitaifa Mnafanya
Shahidi: Hapa Sijazungumzia
Kibatala: Kuna Mahala Popote Kwenye PGO inasema Kwamba Maelezo Kaandikishie Mahala ambapo Kesi imefunguliwa
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Je, kuna Mwomgozo Wowote unazungumzia hivyo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Twende sehemu nyingine, Jana Nilisikia Hapa Unazungumzia Kuhusu Tundu Lissu Kupigwa Risasi, Je Tukio la Tundu Lissu Kupigwa Risasi Kwa Lissu ni ugaidi au siyo Ugaidi?
Shahidi: Siyo ugaidi ni uhalifu wa kawaida
Kibatala: tufanye comperative analysis, Inakuwaje kutaka kumdhuru Mhalifu Lengai Ole Sabaya iwe ugaidi ila kupigwa risasi kwa Tundu Lissu isiwe ugaidi?
Shahidi: Kwa sababu Ilikuwa inaendana na maandamano nchi nzima
Kibatala: Kwani Chadema Wamefanya Marangapi Maandamano
Kibatala: Je, maandamano hayo yalikuwa ni Ugaidi?
Shahidi: mimi Sijui
Kibatala: Kuna Mahala popote umesema Kuwa Mlipofika Dar es Salaam mlimfahamisha DCI?
Shahidi: Sijasema
Kibatala: Kuna Mahali Popote ile Umesema Kwamba Gari ilipo haribika mlimpigia simu DCI?
Shahidi: Kimya
Kibatala: Kuna Mahala ulisema pale Aishi Hotel Kingai alishuka kwenda kumtafuta Moses Lijenje
Shahidi: Ndiyo Nilisema
Kibatala: Kingai alikuwa anamfahamau Moses Lijenje..
Shahidi: Hapana, ilaaaaa....
Kibatala: Hakuna cha ila hapa, ushajibu swali hivyo...
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo P12
Kibatala: Shahidi Nionyeshe hapa Sehemu ambayo umejeza description za zile Risasi tatu
Shahidi: Si Kujaza, suala la Risasi kwenye Seizure Certificate
Kibatala: unajua Kuwa Seizure Certificate Ndiyo inaonyesha Chain of Custody ya Mali Mnazokamata?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kielelezo Namba P12 imeandikwa Jina na Saini ya anayekabidhiwa
Shahidi: sahihi
Kibatala: Tusomee Mtu anayekabidhiwa
Shahidi: H 4347 Detective Goodluck
Kibatala: hilo ndiyo Jina lake..?
Shahidi: Ndiyo Kwa Mujibu wa Kazi zetu
Kibatala: ulipo jaza wewe Kuna signature au hakuna
Shahidi: hakuna
Kibatala: Ulielezea Mahakama Kwanini Hakuna signature
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mpaka mnaenda Arusha kwa dada yake Moses Lijenje Arusha, Je Mnafahamu Majina yake?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mlikuwa mnajua Moses Lijenje pale Moshi anakaa Hotel gani?
Shahidi: Hotel Mbalimbali tu
Kibatala: Tutajie Hotel Mbili tu
Shahidi: Hapana sizifahamu!
Kibatala: Nafikiri nimemaliza mheshimiwa jaji
Kibatala sasa anaketi pahali pake, baada ya shughuli ya saa mbili na dakika 20 na shahidi wa jamhuri, SP Jumanne Malangahe
Anasimama Wakili Mwandamizi wa Serikali, Robert Kidando
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kupatiwa Vielelezo P11, 12 na 13
Wakili wa Serikali: Shahidi Ulionyeshwa Kuwa Sehemu ya Jina la H4347 kuna Jina na Hakuna Sahihi lakini Kwenye Jina lako Umeweka Sahihi
Shahidi: Kwa sababu Askari Mdogo hatakiwi Kuweka Saini ya Kukoroga anaweka Namba Yake ya kazi tu
John Mallya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hiyo ni fact Mpya ya Ufafanuzi
Jaji: Rudia Swali ambapo halitaleta Majibu Mapya
Wakili wa Serikali: Shahidi Ulionyeshwa Kuwa Sehemu ya Jina la H4347 Kuna Jina na Hakuna Sahihi lakini Kwenye Jina lako Umeweka Sahihi
Dickson Matata: OBJECTION bado ni fact Mpya hiyo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji sisi tuna Haki hiyo Kwa Mujibu wa Sheria, Siyo Kama tunakatazwa
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji nafikiri wapewa nafasi lakini na sisi tunaomba kurudi upyaaaaa kwenye swali hilo.
Jaji: Sawa ulizeni nitawapa upande wa utetezi nafasi ya kurudi tena...
Wakili wa Serikali: Shahidi Ulionyeshwa Kuwa Sehemu ya Jina la H4347 Kuna Jina na Hakuna Sahihi lakini Kwenye Jina lako Umeweka Sahihi
Shahidi: Kwa sababu Askari Mdogo hatakiwi Kuweka Saini ya Kukoroga anaweka Namba Yake ya kazi tu
Wakili wa Serikali: Kuna Hiki Kielelezo Cha P13 Maelezo ya Onyo ya Mshtakiwa Wa Tatu.. Kwa Mujibu wa statement hii Uliulizwa swali Kama Mohammed Ling'wenya kuhusiana na Mpango Wa Kulipua Vituo Vya Mafuta kuhusu Vilipuzi Ukasema hakukueleza
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali: Sasa Yeye alikueleza nini
Shahidi: alieleza Nchi Nzima Haku specify Sehemu Moja
Wakili wa Serikali: Uliulizwa hapa Kuhusiana na Denis Urio Kuhusiana na Kuweka Mtego ilikumpa Mshtakiwa wa nne Kesi ya Kisiasa
Shahidi: Si Kweli Shahidi alileta Taarifa Mwenyewe wala hakutumwa na Mtu
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusiana Kuwakamata Wakina Gabriel na Khalid, kuwa Mliwakamata sababu walipita 92 kJ Je, Unasemaje?
Shahidi: Si Kweli tukiwa kamata wakiwa sababu Wali zungumza na Washtakiwa Na wakawa wapo tayari Kujiunga
Wakili Mallya: OBJECTION Neno wapo tayari hakusema Jaji anasoma na Kumbukumbu haionyeshi Kuwa walikuwa wanampango wa Kwenda Kujiunga na akina Ligw'enya.
Wakili wa Serikali: Basi Mheshimiwa Jaji Neno Mpango wa Kujiunga liondoke
Wakili wa Serikali: Tufafanulie Exactly Ni Mwezi upi Khalid na Gabriel Walikutana Mshtakiwa Wa tatu Dar es Salaam
Shahidi: Ni Mwezi wa Saba
Wakili wa Serikali: Ulitoa Taarifa hapa Kwamba ACP Kingai Kuwa hakuwepo Tarehe 09 August 2020 hakuwepo Mbweni, Hebu Tufafanulie hapo
Shahidi: Ni Kwa sababu tulikuwa na Shughuli Ya Kuendelea Kumtafuta Mtuhumiwa Khalfani Bwire
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Pia Kuhusiana na Upekuzi na Ukamataji Pale Rau Madukani Kwamba Baada ya Kukamata Bastola Ulimtuma Goodluck Kwenye Gari na Ukasema Hakuna aliyekwenda na Goodluck Kufuata Seizure Certificate Tufafanulie kwanini Ikitokea hivyo
Shahidi: Baada ya Kukamata Nilisema Namba na wote walisikia, Ndipo Nikamtuma Goodluck na Yeye Mwenyewe ndiye aliyerudi na hiyo silaha
Wakili MALLYA: OBJECTION hayo Ni Majibu Mapya tena Yanajikoroga na Majibu ya awali
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kuwa Kama Unajua Kuwa Mshtakiwa Freeman Mbowe alikamatwa Mwanza akiwa Kwenye Mkutano wa Katiba Ukasema ufahamu, Je Nini Unachofahamu Shahidi: Ni nacho fahamu ni kuwa alikamatwa Mwanza Kwa tuhuma Za Ugaidi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kama Ulikuwa na Maslahi Binafsi na Washtakiwa
Shahidi: Niliwa kamata kwa Sababu ya tuhuma ambazo zimekuwa reported Polisi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu na Askari aliyesimamisha Daladala na Kuhusu Taarifa za Yule Dereva, Ukasema Hapakuwa na Umuhimu
Shahidi: Hapa Kuwa na Umuhimu Kwa sababu Tulimkamata Kisheria na Ndiyo Maana Mpaka Sasa Yupo Mahakamani
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu simu Mbili za Mshtakiwa Ukasema hilo hujalitolea Ushahidi
Shahidi: Ni Kwa sababu siyo Mimi niliye Mkamata wala Kufanyia Upekuzi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu Mshtakiwa Wa tatu Kufanya VIP protection Ukasema Siyo Kosa, Ulikuwa unamaanisha nini
Shahidi: Kwa sababu siyo Kosa kama Unafanya Kwa nia Njema ila Ni Kosa Unafanya Kama Jinai
Dickson Matata: OBJECTION hapo Mbele Majibu nayapinga sababu Hakusema Mwanzo
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Katika Kielelezo hicho pia, Kuhusiana Kile Kilicho hamasishwa Kufanya Maandamano Nchi Nzima ni Kosa au Siyo Kosa Ukasema inategemea
Shahidi: Kufanya Maandamano Kwa Kufuata Sheria Siyo Kosa
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kuhusu Mkoa gani Umetwajwa Kufanya Maandamano, Ukasema Hakuna Je ni Kitu gani kimesemwa
Shahidi: Kufanya Maandamano Nchi Nzima na Mikoa ipo Ndani ya Nchi
Wakili wa Serikali: katika Statement hiyo Umeulizwa Kuhusiana na suala la Mshtakiwa Wa Tatu Kupewa pesa pale Morogoro Kwa jili ya VIP protection Ukasema Siyo Kosa Sababu inategemea na Malengo
Wakili DICKSON MATATA: OBJECTION swali hilo Siku sema hivyo
Wakili wa Serikali: Sawa narudia
Wakili wa Serikali: katika Statement hiyo Umeulizwa Kuhusiana na suaa la Mshtakiwa Wa Tatu Kupewa pesa pale Morogoro Kwa jili ya VIP protection Ukasema Siyo Kosa
Shahidi: Ni Kwa sababu kama unatuma Kwa nia Njema siyo Kosa Wakili
DICKSON MATATA: Mheshimiwa Jibu la Swali hilo Kwamba nia Njema, Nia njema Haikutajwa
Jaji: Umechelewa Kusimama, Nitakupa nafasi ya Kuhoji tena
Wakili wa Serikali: Nilisikia Unasema Kuwa Watuhumiwa Wataandikwa Kwenye Detention Register Pale tu Watakapo Pokelewa, Unamaanisha Nini
Shahidi: Nilikuwa namaanisha Kwamba Pale wanapokelewa na Kuwekwa Mahabusu Ndiyo Wanaandikishwa Kwenye Detention Register
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Pia Kuhusiana na Ule Muda wa Ukamataji Ukasema Ilikuwa ni Saa 7 Mchana na Pia Uliandika Kwenye Hati ya Upekuzi.. Na Ukasema Muda huo Ulikuwa Muda Sasa Sana Je Ulikuwa Umaanisha Nini
Shahidi: Nilikuwa namaanisha Haijavuka hiyo Saa Saba
Wakili wa Serikali: Pia Uliulizwa hapa Kwamba Siku ya Tarehe 09 August 2020 Ndiyo Siku Uliwapeleka Kituo cha Polisi Mbweni wewe na Mahita, Ukasema Siyo Kweli, Je Unamanisha Nini
Shahidi: Siyo Kweli Kwamba tuliwapeleka Kituo cha Polisi Mbweni Tarehe 09 August Bali Ilikuwa tarehe 08 August 2020
Wakili wa Serikali: Pia Umeulizwa Kwamba Mlienda Arusha, Ukaulizwa Kama ikiwa Unamfahamu Majina ya Huyo Dada yake Lijenje, Nyumba au Mtaa Ukasema Ufahamu, Hebu tufafanulie
Shahidi: Ni Kwa sababu wao Watuhumiwa ndiyo walikuwa wanatupeleka kila sehemu
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusu Kutomkamata Mshtakiwa Wa Nne Baada ya Wengine watatu Kukamatwa zaidi ya Mwaka Mmoja Ukasema Upelelezi Ulikuwa unaendelea, Je Ni Upelelezi upi
Shahidi: Masuala la Forensics na Upelelezi Mwingine Ulikuwa unaendelea
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Pia Maswali Kuwa katika Bastola hiyo Uliyo kamata ilikuwa ina Maeneo ambayo yangeweza Kutoa Finger Prints Ukasema ni Kweli, lakini haujaleta Mahakamani
Shahidi: Ni kweli Siku leta Ushahidi Wa Finger Prints Kwa sababu Hapakuwa na Mahaka Kwamba Silaha hiyo ilikuwa haina Ubishi kuwa inamilikiwa na Mtuhumiwa
Wakili wa Serikali: Jana Uliulizwa kuhusu Katazo la Ku unLoad Silaha, Ukasema inategemea, Je Ulikuwa Unamanisha nini
Shahidi: Ni si Silaha ambayo imekuwa eneo la Tukio ndiyo haitakiwi Kuwa Unload lakini Silaha ambayo unataka Ku seize na Umeipata Kwa Mtu Unaruhusiwa Ku unload Kuona Kuna Kitu gani, Ndiyo Nilichomanisha..
Wakili wa Serikali: Uliulizwa hapa Kuhusu Mshtakiwa Wa tatu kuhusu Kwenda Kwa Mlinzi wa Amani ila Ukasema Hukuona sababu ya kwenda na wala Hakuhitaji
Shahidi: Ni Kwa sababu alikuwa tayari Kujaza Maelezo na Hakuona haja ya Kwenda Kwa Mlinzi wa Amani
Wakili wa Serikali: Uliulizwa utendaji wa shughuli Zenu Mmekuwa Mkishirikiana na Mamlaka Mbalimbali, Tufafanulie ni Ushirikiano Gani mnapeana
Shahidi: tunashirikiana na vyombo mbalimbali vya Usalama lakini kwa ngazi za Juu
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba kukomea hapo hatutokuwa na swali lingine
Jaji: Kuna maeneo mawili ambayo mnayarudia upande wa utetezi
Wakili Peter Kibatala: Shahidi Ni kweli wakati unatoa ushahidi wako unaomba kutoa vielelezo hukufafanua kuwa kuna maofisa ambao hawatakiwi kusaini?
Shahidi: Hayo Sikusema
Kibatala: Uliposema maofisa wa chini ulimaanisha nini?
Shahidi: Kuanzia Staff sergeant kurudi chini
Kibatala: Detective Coplo anatakiwa kusaini?
Shahidi: Hatakiwi kusaini Kibatala: kwa ruhusa ya Mahakama naomba usome Hapa Shahidi "F5914 Detective Coplo Hafidh Mohammed"
Kibatala: Huyo ni Afisa wa chini au siyo?
Shahidi: Ni Afisa wa chini
Kibatala: Amesaini au hajasaini?
Shahidi: AMESAINI
Wakili Dickson Matata: Mheshimiwa Jaji naomba P13
Matata: Shahidi, Jana wakati nakufanyia Dodoso Nilikuuliza Mtu Kupewa nauli na pesa ya matumizi Njiani ni Kosa au Siyo Kosa Ukasema Siyo Kosa Leo Wakati Unafanyiwa Re-examination Ukasema Siyo Kosa kama ulipewa kwa nia Njema
Sasa chukua hiyo Statement Nionyeshe Sehemu ambayo Mohammed Ling'wenya amesema alipewa hiyo Pesa ya Nauli na Matumizi ya Njiani Kwa nia Ovu
Shahidi: Hakuna Aliposema
Wakili Matata: Mheshimiwa Jaji sina Swali Lingine
Jaji aandika Kidogo
Mahakama Ipo Kimya Kidogo
Jaji Baada ya Maswali hayo Kuulizwa Upande wa Serikali Maswali Lolote?
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Hakuna swali Mheshimiwa Jaji
Jaji: Mmemaliza na shahidi wa 8?
Wakili wa Serikali: Ndiyo Mheshimiwa Jaji
Jaji: Shahidi Tunakuahukuru Kwa Ushahidi Wako
Shahidi anatoka na kuondoka kizimbani
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Huyo ndiye shahidi tuliyekuwa naye leo Hivyo tunaomba hairisho la Kesi hii ili kuja Kuendelea Kesho Kutwa Alhamisi tarehe 13 January 2022 Ambapo tutaleta shahidi mwingine kuja kuendelea na ushahidi
Na Pamoja na kwamba sasa ni saa saba mchana hatukuweza kujua shahidi Huyu angeweza Kumalizia Saa ngapi Hivyo tunaomba hairisho Mpka kesho kutwa kama nilivyo Omba, Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji
Wakili Peter Kibatala: Hatuna Pingamizi Mheshimiwa Jaji
Jaji: Basi maombi ya hairisho yanakubaliwa mpaka kesho kutwa alhamisi ya tarehe 13 January 2022 Washtakiwa wataendelea kuwa rumande chini ya magereza mpaka siku hiyo Jaji anatoka
Tuendelee na kesi hii hapa keshokutwa tarehe 13