Yaliyojiri Bungeni Dodoma, Septemba 06, 2016: Mbunge wa Kilolo ataka michezo ifutwe nchini

kalulukalunde

JF-Expert Member
May 27, 2016
1,056
1,083
MKUTANO wa Nne wa Bunge la 11 umeanza leo mjini Bungeni Dodoma, huku miswada sita ukiwemo wa Sheria ya Upatikanaji wa Habari ukitarajiwa kuchukua nafasi kubwa.

Pia wabunge mbalimbali wa upinzani ambao mwanzo waligoma kuendelea na vikao vya bunge lililopita kwa madai ya Naibu Spika kutowatendea haki wabunge wa upinzani.

Mbunge wa Jimbo la Kilolo Venance Mwamoto ameuliza swali bungeni kwanini serikali isifute michezo nchini kutokana mwenendo mbaya wa matokeo?

Tujadiliane kwanini serikali isiifute michezo nchini???


Wadau mnaonaje chango wa mbunge wetu?View attachment 394610


-------------------------------------

MKUTANO wa Nne wa Bunge la 11 unatarajiwa kuanza leo mjini hapa, huku miswada sita ukiwemo wa Sheria ya Upatikanaji wa Habari ukitarajiwa kuchukua nafasi kubwa.

Katika mkutano huo, wabunge wa kambi ya upinzani ambao walisusia siku kadhaa za mkutano uliopita, wamesema kwamba watahudhuria.
Mbunge wa Vunjo, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), alithibitisha jana kwamba wabunge wa upinzani wataingia bungeni.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano ya Bunge kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana, jumla ya maswali 110 yanatarajiwa kuulizwa na wabunge na kujibiwa na Serikali.

Aidha, Waziri Mkuu anatarajiwa kuulizwa maswali 16 ya papo kwa hapo. Taarifa hiyo ilisema miswada sita ya sheria iliyosomwa kwa mara ya kwanza katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na baadaye kupelekwa katika kamati husika ili ifanyiwe kazi, itaendelea kushughulikiwa katika hatua zinazofuata ikiwa ni pamoja na kusomwa kwa mara ya pili, kamati ya Bunge zima na kusomwa kwa mara ya tatu.

Miswada hiyo ni pamoja na ule wa Sheria ya Upatikanaji wa Habari ya mwaka 2015, Muswada wa Sheria ya Utathmini na Usajili wa Wathamini wa mwaka 2016, Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serika wa mwaka 2016.

Pia utakuwepo Muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Wanataaluma wa Kemia wa mwaka 2016, Muswada wa Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo wa mwaka 2016 na Muswada wa Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi ya mwaka 2016.

Kufikia jana, mji wa Dodoma ulikuwa umefurika wageni balimbali wakiwemo wabunge na maofisa wa serikali wanaohamia tayari kuanza kuendesha shughuli zao katika makao makuu mapya ya Serikali, mjini hapa.
 
Wangekaza tu posho mchezo. jamaa wamesubiri usuruhishi watu wamewapotezea, wameziba madomo weee watu wamewashangaaa, wametoa matamko watu ndo kwanza wakaitisha tulia marathon kumpongeza naibu spika sasa akili zimewakaa. Mdogo mdogo wanarudi

nimekumbuka ule wimbo Wa Christian Bella amerudi ana lia weeee
 
Wale jamaa wapendwa wetu safari hii wakitoka wazibe macho na masikio na sio midomo tena, snema inoge.
 
Nyambafu wangekaza tuuu posho mchezo. jamaa wamesubiri usuruhishi watu wamewapotezea, wameziba madomo weee watu wamewashangaaa, wametoa matamko watu ndo kwanza wakaitisha tulia marathon kumpongeza naibu spika sasa akili zime wakaa. mdogo mdogo wanarudi

nimekumbuka ule wimbo Wa Christian Bella amerudi ana lia weeee
myopic
 
sio bunge mkutano wa ccm maana kama ni bunge leo ningesikia wanapiga kura ya kutokuwa na imani na uchwara kwa kusigina KATIBA ova
 
wangekaza tuuu posho mchezo. jamaa wamesubiri usuruhishi watu wamewapotezea, wameziba madomo weee watu wamewashangaaa, wametoa matamko watu ndo kwanza wakaitisha tulia marathon kumpongeza naibu spika sasa akili zimewakaa. mdogo mdogo wanarudi

nimekumbuka ule wimbo Wa Christian Bella amerudi ana lia weeee
What a waste of time and space...
 
"Aidha, Waziri Mkuu anatarajiwa kuulizwa maswali 16 ya papo kwa hapo."
Naomba mwenye kujua anisaidie hapa,kama maswali yanaitwa ya papo
kwa papo,inakuwaje yanafahamika idadi yake? kama tunakadria namba ya
watu watakaouliza maswali kuwa ni kadhaa,inafahamikaje kama mtu hatakuwa na maswali
mawili au zaidi? Au ndo ule mtindo wa wauliza maswali kuwasilisha watakacholiuliza
mapema ili kitafutiwe majibu afu sisi tunaita ya papo kwa papo?
 
Wadau amani iwe kwenu.

CHADEMA, CUF na UKAWA kwa ujumla ni washari. Wanadhihirisha kuwa hawapo tayari kwa suluhu japo wanajifanya wao ndio wanachokozwa Bungeni. Wanajifanya wastaarabu kumbe si lolote. Wamejiandaa kwa mapambano Bungeni ambayo kwa hakika hawatayaweza.

Nimewaona wabunge wa Upinzani wote wakiwa wamevalia suti nyeusi. Nimeongea na mmoja wa wabunge wa UKAWA ambaye ni source wangu akaniambia kuwa wanaomboleza kifo cha demokrasia nchini. Akasema kuwa wamepania bunge hili kuhamishia harakati za UKUTA ndani ya Bunge. Akasema kuwa wamepewa maelekezo na Edward Lowasa na Maalim Seif kuwa katu wasikubali muafaka wowote na wabunge wa CCM. Akasema kuwa Lowasa na Maalim Seif wameafikiana kuwa sasa hakuna suluhu bali jino kwa jino.

Hakika nimetafakari sana kauli hizo na nimeziona kuwa hazina tija kwa mustakabali wa demokrasia nchini. Hii ni kutokana na ukweli kwamba CCM tutaendelea kuutumia wingi wetu na wao wataendelea kuathirika kwa uchache wao.

Kwa tabia za hawa wabunge wa Upinzani, tumuache Rais Magufuli awaambie ukweli
 
Wadau amani iwe kwenu.

CHADEMA, CUF na UKAWA kwa ujumla ni washari. Wanadhihirisha kuwa hawapo tayari kwa suluhu japo wanajifanya wao ndio wanachokozwa Bungeni. Wanajifanya wastaarabu kumbe si lolote. Wamejiandaa kwa mapambano Bungeni ambayo kwa hakika hawatayaweza.

Nimewaona wabunge wa Upinzani wote wakiwa wamevalia suti nyeusi. Nimeongea na mmoja wa wabunge wa UKAWA ambaye ni source wangu akaniambia kuwa wanaomboleza kifo cha demokrasia nchini. Akasema kuwa wamepania bunge hili kuhamishia harakati za UKUTA ndani ya Bunge. Akasema kuwa wamepewa maelekezo na Edward Lowasa na Maalim Seif kuwa katu wasikubali muafaka wowote na wabunge wa CCM. Akasema kuwa Lowasa na Maalim Seif wameafikiana kuwa sasa hakuna suluhu bali jino kwa jino.

Hakika nimetafakari sana kauli hizo na nimeziona kuwa hazina tija kwa mustakabali wa demokrasia nchini. Hii ni kutokana na ukweli kwamba CCM tutaendelea kuutumia wingi wetu na wao wataendelea kuathirika kwa uchache wao.

Kwa tabia za hawa wabunge wa Upinzani, tumuache Rais Magufuli awaambie ukweli

Ulitaka wavae Tshirt za KIJANI?
 
Back
Top Bottom