Samatime Magari
Senior Member
- Feb 10, 2017
- 103
- 388
Kumiliki gari na kumaintain gari ni vitu viwili tofauti, ndo maana unaweza kuta mtu ananunua gari kwa furaha anafanya na sherehe mambo ya maintenance yakianza inakua balaa..
.
Unaanza kuona gari kama JINI Kabula, Sasa Leo nataka tuguse kidogo issue ya kutumia maji ya Bomba [tap water]katika gari [upozaji wa engine]..
.
Lakini kabla hatujaanza ni muhimu tukapata picha ya mfumo huu wa upozaji Engine na ufanyaji kazi wake..
.
Mfumo wa Upozaji wa Engine unatumia Radiator, Fan, Water pump, Expansion tank na thermostart [Hizi ndo main parts za upozaji wa Engine]...
.
Radiator ni kifaa chenye pipes ndogo ndogo ambapo maji huzunguka [huzungushwa na water pump] yakitoka kwenye engine, Maji haya hupulizwa na fan yakipata joto ili yapoe na kurudi kwenye Engine kufanya upozaji..
.
.
Moja ya common mistakes ambayo tunaifanya ni kutumia maji kupoza engine, Maji ni rahisi kuyapata ndo maana always ikija issue ya upozaji wa engine maji ndo inakuaga first option..
.
Wengi wetu hatujui jinsi radiator inavyofanya kazi na engine ya gari ndo maana huwa tunakimbilia kutumia maji badala ya coolant..
.
Kuna tofauti kubwa ya kutumia coolant na maji, Maji ndio yatafanya upozaji wa engine lakini hayafanyi kazi kama coolant inavyofanya..
.
Ingawa wengi tunatumia maji ila nikufahamishe tu coolant ndio liquid sahihi katika kupoza engine na inashauriwa kubadilishe Kila baada ya miaka 2..
.
Coolant inahakikisha ina maintain locomotive [movement za engine parts] ziwe efficiency huku ikongeza life span ya engine..
.
.
Maji yanapata joto faster kuliko coolant[boils faster at lower temperature], Maeneo ya Joto risk ya Engine block kupata crack au kutanuka ni kubwa kama unatumia plain water hasa kwa safari ndefu..
.
Block ikitanuka Piston Rings wont seal properly na gari itaanza kula oil. Coolant imekua formulated na properties ambazo zina protect Engine kupata kutu [corroded].. .
.
Ukitumia maji kuna Inner parts za engine unazipa kutu as Engine imetengenezwa na Cast iron ambayo inadhurika na kutu.. . Water pump yenye meno ya chuma ukitumia maji inaliwa na kutu..
.
Sababu maji husababisha kutu kwenye Engine ile kutu inaleta tope, Tope ambalo baadae litaenda kuzungushwa kwenye Radiator na kusababisha kuziba...
.
Radiator pia imetengenezwa na Aluminium na Aluminium hulika na chumvi iliyopo kwenye maji [sulphates na carbonates]..
.
Boiling Point ya coolant iko chini tofauti na maji same to Evaporation maji yana evaporate faster., Sytem ya upozaji ikiwa na leakage kidogo tu au ikiingiza hewa sababu ya evaporation lazima gari ichemeshe.. .
.
.
Kwa nchi zenye baridi sana [Below 0°] huwezi tumia maji kabisa, Unaweza park gari ukakuta maji yameganda Lakini ukitumia coolant haito ganda Maji yakiganda yanatanuka [kama umewahi kuweka soda kwenye freezer ukasahau kuitoa utakua unajua nachomaanisha hapa]..
.
Coolant imekua formulated ikiwa na uwezo wa kulainisha bearing ya water pump, Pia ina uwezo wa kukusanya Joto vyema zaidi [Head gasket unaipa ufanisi na maisha marefu].. .
.
Ukitumia maji kwa muda mrefu water pump inawahi kufa sababu ya bearing[hazitaki maji], Utasikia water pump inaanza kutoa kelele flani ukiwasha gari ukisikia hivyo jua tayari..
.
Baadhi ya gari za kisasa Kama gari za Ulaya kama R R, Parts ambazo zinapitisha coolant kwenye oil cooler ukiwa unatumia maji kwa muda mrefu inaweza sababisha oil cooler kutoboka.. .
.
Na ukiona maji yanapungua kwa gari yako na hakuna leakage jua kwamba head gasket ina tatizo, Sasa kuna coolant ambazo watu huwa wanachanganya na maji.. .
.
Nipende kusema kama ni recommendation za manufacture wa hiyo coolant basi changanya.. . Akirecommend naamini ukichanganya itakua ina meet manufacturer's specifications.. . Kama hujaambiwa basi usichanganye ..
.
.
Nikukumbushe Bila coolant joto litakalokua linazalishwa na engine yako kutoka na internal combustion ni kubwa[overheating}. Joto hili linaweza kuleta madhara kwa Engine ya gari yako kama nilivyoelezea hapo Juu na ukaingia gharama kubwa kufix tatizo..
.
Maji kama maji hayako adequate kufanya upozaji wa engine ipasavyo hasa kwa engine zinazorun muda mrefu, Nikukumbushe madhara yanayotokana na Joto kwenye Engine huwa ni gharama kuyafix sababu unagusa ndani ya engine.. . Ni muhimu kuwa makini na hili swala kabla halijawa mwiba..
.
Thermostat sijamgusa ila napokea sana maswali kuhusu atolowe au asitolewe, Siku nyingine tutamgusa ila kiufupi kama gari yako ina ECU usiitoe.. .
.
Reason being inafanya kazi na sensors za Joto Oxygen Oil etc ili kusaidia kiasi cha hewa na mafuta katika ufanyaji kazi wa Engine..
.
.
Nimalize kwa Kusema Najua kuna wadau watachagua maji kuliko coolant, Sio jambo zuri ila kama hauna coolant kwa muda huo basi tumia pure distilled water.. .
.
Haya maji yanakua yametolewa baadhi ya contaminants and minerals na wataalamu wanasema ni bora kuliko tap water, Natumaini umejifunza kitu kama Jibu ni ndio basi usisahau ku share na Wengine wapate Madini.. .
.
Kama unahitaji ushauri au kuagiza gari Japan, UK Singapore, etc au kununua hapa nchini [showroom au mkononi] Karibu, tutafanya mchakato wako wa kupata gari kuwa salama na unaojali muda wako..
.
Tunafanya kazi na dealers wa nje na nchini wanaotupa gari nzuri zenye ubora na bei poa kwa ajili yako simpy njoo ofisini Kigamboni au whatsapp [0714547598]na hitaji lako utakua sorted na ushauri juu..
.
Hata kama uko mkoani unaweza wasiliana nasi ukaagiza gari yako then malipo ukafanyia huko huko [at cost] yani unatumiwa invoice kama ilivyo mpaka gari itapofika then utaletewa au utakuja kuichukua..
.
Asante
Samatime Car Dealers Company Limited
0714547598