TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Mgombea ubunge Chadema ahamia CCM
Saturday, 04 September 2010
Julieth Ngarabali, Kibaha
MGOMBEA wa Ubunge wa Jimbo la Singida Magharibi, kwa tiketi ya Chadema, Nkhambaku Elisha amesitisha kugombea nafasi hiyo na kurudi CCM.
Elisha alihamia Chadema kwa hasira akitokea CCM baada ya kuenguliwa na Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) licha ya kuongoza katika kura za maoni.
Tukio hilo la mgombea ubunge kusitisha kampeni zake na kuhamia chama kingine ni la kwanza kutokea mwaka huu.
Uamuzi huo wa Elisha unampa mgombea wa CCM katika jimbo hilo, Mohamed Misanga kushinda uchaguzi huo bila kutumia nguvu nyingi.
Elisha aliongoza kwenye kura za maoni kwa tiketi ya CCM, lakini jina lake lilitupwa na Nec kupewa aliyeshika nafasi ya pili.
Mgombea huyo alifikia hatua hiyo jana, wilayani Kibaha, ilikofanyika mikutano miwili ya kampeni ya CCM katika Wilaya za Kibaha na Bagamoyo.
Katika kura za hizo za maoni, Elisha aliongoza kwa kura 3,499 akifuatiwa na Mohamed Misanga kwa kura 3,433, lakini Nec ilimwengua.
Hatua hiyo inadaiwa kuwa ndiyo iliyomfanya mgombea huyo apate jazba na kuamua kujiunga na Chadema ambao nao walimpitisha kugombea jimbo.
Akizungumza katika mkutano huo wa CCM mkoani Pwani, alisema alichanganyikiwa jina lake lilipoenguliwa na Nec wakati alikuwa akiongoza kwenye kura za maoni.
Alisema hasira ndizo zilizomfanya ahamie Chadema kwa kuwa alitamani kuwaongoza wananchi kupitia ubunge, lakini aligundua kuwa nafasi yake ya baadaye kisiasa itakuwa ndani ya CCM na si chama kingine.
Alisema alianza kupeperusha bendera ya Chadema kwa kishindo lakini hasira zilipoisha
akagundua kuwa alikosea na aliposhauriana na ndugu na marafiki aliamua kurudi CCM.
Kuhusu usaliti, Elisha alisema kuwa yeye si msaliti lakini hawezi kuzuia watu wengine kumwona kuwa ni msaliti kwa kuwa suala hilo lipo katika vyama vyote, bali jambo la msingi kwake ni kuwa ndani ya CCM.
Mgombea Ubunge wa jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu alisema chama kinatambua umuhimu wa Elisha na ndiyo maana waliamua kumshauri na akakubali kurudi CCM.
Naye Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba aliwataka wanachama wenzake waliokimbilia upinzani kwa hasira warudi nyumbani ili wajiandae na chaguzi zijazo.
Kampeni za Dk Slaa
Mwandishi wetu, Salim Said anaripoti kuwa siku sita za mwanzo za msafara wa kampeni za mgombea urais Chadema, Dk Wilibrod Slaa ziliambatana na matukio kadhaa, huku ummati mkubwa watu ukijitokeza katika mikutano aliyofanya katika mikoa ya Manyara na baadhi ya majimbo ya Dodoma na Morogoro.
Katika siku hizo sita, Dk Slaa akiwa ameongozana na mchumba wake Josephine, alionyesha kukubalika kwake katika wilaya za Kiteto, Babati, Hanang, Mbulu zote za mkoani Manyara na Mikumi mkoani Morogoro pamoja na Singida Vijijini.
Mwanzo wa msafara
Baada ya ufunguzi wa Agosti 25 mwaka huu jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alianza msafara wa kampeni Agosti 30 mwaka huu katika majimbo mbalimbali ya Morogoro pamoja na Mikumi.
Wakati Dk Slaa akiwa jukwaani anahutubia katika jimbo la Mikumi mkoani Morogoro alasiri, alipita mwendesha baiskeli ya matairi matatu (Guta), na kumwambia, "Freeman Mbowe usiwadanganye wananchi…Freeman Mbowe usiwadanganye wananchi."
Lakini Dk Slaa alimjibu, "Msikilizeni huyo hajui hata anayoyasema kwa sababu kutokana na hali yake hapaswi kusema maneno haya, kwani hafanani hata na sisi, lakini mwacheni msimfanye chochote."
Kulia jukwaani
Baada ya hapo, Agosti 31, Dk Slaa alihamishia msafara wake mkoa Dodoma ambapo alianzia mikutano yake katika Jimbo la Mtera, ambalo lilikuwa linaongozwa na John Malecela kwa miaka zaidi ya 30 sasa.
Akiwa hapo Dk Slaa alimwaga mchozi jukwaani baada ya kuelezwa hali ngumu ya maisha inayowakumba asilimia kubwa ya wananchi wa Mtera.
"Nimelia kwa sababu ya hali ngumu ya maisha yenu ambayo mmenieleza, lakini pia nimekumbuka wenzenu 50, waliofukiwa wakiwa hai katika machombo ya madini ya Bulyanhulu mkoani Shinyanga ambayo mkataba wake ulisainiwa na na Jakaya Kikwete," alisema Dk Slaa.
Ufafanuzi wa ndoa yake
Baada ya makombora mengi kutupwa katika baadhi ya magazeti kutoka kwa baadhi ya viongozi wa CCM kuhusu ndoa mpya ya Dk Slaa, ikidaiwa kuwa ina utata, inamtesa na kwamba amepora mke wa mtu, aliamua kuvunja ukimya.
Septemba 2, mwaka huu, akiwa katika mkutano wa hadhara, Babati Mjini Dk Slaa kwa mara ya kwanza aliamua kutoa ufafanuzi juu ya ndoa yake hiyo, na kumtambulisha kwa mara ya pili mchumba wake mbele ya umati wa watu.
Utambulisho wa kwanza wa Josephine Mushumbusi ulifanyika siku ya uzinduzi wa kampeni za Chadema katika viwanja vya Jangwani, jijini Dar es Slaam Agosti 28 mwaka huu.
"Ni kweli niliishi na mwanamke nje ya ndoa na kuzaa naye watoto wawili, lakini nilipotaka kufunga ndoa sikutaka kufunga naye niliamua kufunga na huyu. Hebu mama Slaa nyanyuka wakuone," alisema Dk Slaa katika uwanja wa Kibaya Babati Mjini.
Kumnadi Rose Kamili
Katika mkutano wa kwanza wa Septemba 3, uliofanyika katika uwanja wa Endasaki, Dk Slaa alisimama jukwaani na Kamili ambaye aliishi naye na kuzaa naye kabla hawajatengana na kumnadi kwa wananchi huku akitaka wamchague kwa kura nyingi.
Wakati hayo yakiendelea jukwaani, Josephine alikuwa amekaa katika meza kuu iliyokuwa katika hema lililojengwa kwa ajili ya wageni hao.
Dk Slaa alimsifia Kamili ambaye alikuwa diwani wa CCM kwamba ni kiongozi makini na anaweza kumaliza ufisadi ndani ya halmashauri ikiwa atafanikiwa kupata ubunge wa jimbo hilo, ambalo sasa linaloongozwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Mary Nagu.
Akiwa katika kijiji cha Rose Kamili cha Basutu, Dk Slaa aliahidiwa kura zote za wananchi wa hapo kwa kuwa ni kwake, kwa watoto, shemeji na wake zake.
"Dk Slaa usiwe na wasiwasi, hapa ni kwako, kwa watoto wako, shemeji na wake zako, hivyo nakuahidi kuwa utapata kura zote za watoto, wakwe na shemeji zako," aliahidi Rose Kamili.
Basuto wanajua bado Dk Slaa na Kamili ni mke na mume
ya waliohudhuria ambao ni wa asili ya kimasai wakirukaruka na mishale kana kwamba wamepandisha mori, katika kushangilia.
Katika hali ya isiyo ya kawaida baadhi ya wagombea hao akiwamo Dk Slaa walilazimika kujinadi kwa kutumia lugha za makabila, baada ya kudaiwa kuwa wananchi wengi wa Babati, Hanang na Mbulu ambao ni Wairaq, Wamasai, Wambulu na Wabarbei hawaelewi Kiswahili vizuri.
Dk Slaa alisema lengo lake la kutaka kuingia Ikulu ni kuwakomboa Watanzania na sio kwenda kula mayai na kujilimbikizia mali
Source: Mwananchi Jumamosi
Saturday, 04 September 2010
Julieth Ngarabali, Kibaha
MGOMBEA wa Ubunge wa Jimbo la Singida Magharibi, kwa tiketi ya Chadema, Nkhambaku Elisha amesitisha kugombea nafasi hiyo na kurudi CCM.
Elisha alihamia Chadema kwa hasira akitokea CCM baada ya kuenguliwa na Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) licha ya kuongoza katika kura za maoni.
Tukio hilo la mgombea ubunge kusitisha kampeni zake na kuhamia chama kingine ni la kwanza kutokea mwaka huu.
Uamuzi huo wa Elisha unampa mgombea wa CCM katika jimbo hilo, Mohamed Misanga kushinda uchaguzi huo bila kutumia nguvu nyingi.
Elisha aliongoza kwenye kura za maoni kwa tiketi ya CCM, lakini jina lake lilitupwa na Nec kupewa aliyeshika nafasi ya pili.
Mgombea huyo alifikia hatua hiyo jana, wilayani Kibaha, ilikofanyika mikutano miwili ya kampeni ya CCM katika Wilaya za Kibaha na Bagamoyo.
Katika kura za hizo za maoni, Elisha aliongoza kwa kura 3,499 akifuatiwa na Mohamed Misanga kwa kura 3,433, lakini Nec ilimwengua.
Hatua hiyo inadaiwa kuwa ndiyo iliyomfanya mgombea huyo apate jazba na kuamua kujiunga na Chadema ambao nao walimpitisha kugombea jimbo.
Akizungumza katika mkutano huo wa CCM mkoani Pwani, alisema alichanganyikiwa jina lake lilipoenguliwa na Nec wakati alikuwa akiongoza kwenye kura za maoni.
Alisema hasira ndizo zilizomfanya ahamie Chadema kwa kuwa alitamani kuwaongoza wananchi kupitia ubunge, lakini aligundua kuwa nafasi yake ya baadaye kisiasa itakuwa ndani ya CCM na si chama kingine.
Alisema alianza kupeperusha bendera ya Chadema kwa kishindo lakini hasira zilipoisha
akagundua kuwa alikosea na aliposhauriana na ndugu na marafiki aliamua kurudi CCM.
Kuhusu usaliti, Elisha alisema kuwa yeye si msaliti lakini hawezi kuzuia watu wengine kumwona kuwa ni msaliti kwa kuwa suala hilo lipo katika vyama vyote, bali jambo la msingi kwake ni kuwa ndani ya CCM.
Mgombea Ubunge wa jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu alisema chama kinatambua umuhimu wa Elisha na ndiyo maana waliamua kumshauri na akakubali kurudi CCM.
Naye Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba aliwataka wanachama wenzake waliokimbilia upinzani kwa hasira warudi nyumbani ili wajiandae na chaguzi zijazo.
Kampeni za Dk Slaa
Mwandishi wetu, Salim Said anaripoti kuwa siku sita za mwanzo za msafara wa kampeni za mgombea urais Chadema, Dk Wilibrod Slaa ziliambatana na matukio kadhaa, huku ummati mkubwa watu ukijitokeza katika mikutano aliyofanya katika mikoa ya Manyara na baadhi ya majimbo ya Dodoma na Morogoro.
Katika siku hizo sita, Dk Slaa akiwa ameongozana na mchumba wake Josephine, alionyesha kukubalika kwake katika wilaya za Kiteto, Babati, Hanang, Mbulu zote za mkoani Manyara na Mikumi mkoani Morogoro pamoja na Singida Vijijini.
Mwanzo wa msafara
Baada ya ufunguzi wa Agosti 25 mwaka huu jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alianza msafara wa kampeni Agosti 30 mwaka huu katika majimbo mbalimbali ya Morogoro pamoja na Mikumi.
Wakati Dk Slaa akiwa jukwaani anahutubia katika jimbo la Mikumi mkoani Morogoro alasiri, alipita mwendesha baiskeli ya matairi matatu (Guta), na kumwambia, "Freeman Mbowe usiwadanganye wananchi…Freeman Mbowe usiwadanganye wananchi."
Lakini Dk Slaa alimjibu, "Msikilizeni huyo hajui hata anayoyasema kwa sababu kutokana na hali yake hapaswi kusema maneno haya, kwani hafanani hata na sisi, lakini mwacheni msimfanye chochote."
Kulia jukwaani
Baada ya hapo, Agosti 31, Dk Slaa alihamishia msafara wake mkoa Dodoma ambapo alianzia mikutano yake katika Jimbo la Mtera, ambalo lilikuwa linaongozwa na John Malecela kwa miaka zaidi ya 30 sasa.
Akiwa hapo Dk Slaa alimwaga mchozi jukwaani baada ya kuelezwa hali ngumu ya maisha inayowakumba asilimia kubwa ya wananchi wa Mtera.
"Nimelia kwa sababu ya hali ngumu ya maisha yenu ambayo mmenieleza, lakini pia nimekumbuka wenzenu 50, waliofukiwa wakiwa hai katika machombo ya madini ya Bulyanhulu mkoani Shinyanga ambayo mkataba wake ulisainiwa na na Jakaya Kikwete," alisema Dk Slaa.
Ufafanuzi wa ndoa yake
Baada ya makombora mengi kutupwa katika baadhi ya magazeti kutoka kwa baadhi ya viongozi wa CCM kuhusu ndoa mpya ya Dk Slaa, ikidaiwa kuwa ina utata, inamtesa na kwamba amepora mke wa mtu, aliamua kuvunja ukimya.
Septemba 2, mwaka huu, akiwa katika mkutano wa hadhara, Babati Mjini Dk Slaa kwa mara ya kwanza aliamua kutoa ufafanuzi juu ya ndoa yake hiyo, na kumtambulisha kwa mara ya pili mchumba wake mbele ya umati wa watu.
Utambulisho wa kwanza wa Josephine Mushumbusi ulifanyika siku ya uzinduzi wa kampeni za Chadema katika viwanja vya Jangwani, jijini Dar es Slaam Agosti 28 mwaka huu.
"Ni kweli niliishi na mwanamke nje ya ndoa na kuzaa naye watoto wawili, lakini nilipotaka kufunga ndoa sikutaka kufunga naye niliamua kufunga na huyu. Hebu mama Slaa nyanyuka wakuone," alisema Dk Slaa katika uwanja wa Kibaya Babati Mjini.
Kumnadi Rose Kamili
Katika mkutano wa kwanza wa Septemba 3, uliofanyika katika uwanja wa Endasaki, Dk Slaa alisimama jukwaani na Kamili ambaye aliishi naye na kuzaa naye kabla hawajatengana na kumnadi kwa wananchi huku akitaka wamchague kwa kura nyingi.
Wakati hayo yakiendelea jukwaani, Josephine alikuwa amekaa katika meza kuu iliyokuwa katika hema lililojengwa kwa ajili ya wageni hao.
Dk Slaa alimsifia Kamili ambaye alikuwa diwani wa CCM kwamba ni kiongozi makini na anaweza kumaliza ufisadi ndani ya halmashauri ikiwa atafanikiwa kupata ubunge wa jimbo hilo, ambalo sasa linaloongozwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Mary Nagu.
Akiwa katika kijiji cha Rose Kamili cha Basutu, Dk Slaa aliahidiwa kura zote za wananchi wa hapo kwa kuwa ni kwake, kwa watoto, shemeji na wake zake.
"Dk Slaa usiwe na wasiwasi, hapa ni kwako, kwa watoto wako, shemeji na wake zako, hivyo nakuahidi kuwa utapata kura zote za watoto, wakwe na shemeji zako," aliahidi Rose Kamili.
Basuto wanajua bado Dk Slaa na Kamili ni mke na mume
ya waliohudhuria ambao ni wa asili ya kimasai wakirukaruka na mishale kana kwamba wamepandisha mori, katika kushangilia.
Katika hali ya isiyo ya kawaida baadhi ya wagombea hao akiwamo Dk Slaa walilazimika kujinadi kwa kutumia lugha za makabila, baada ya kudaiwa kuwa wananchi wengi wa Babati, Hanang na Mbulu ambao ni Wairaq, Wamasai, Wambulu na Wabarbei hawaelewi Kiswahili vizuri.
Dk Slaa alisema lengo lake la kutaka kuingia Ikulu ni kuwakomboa Watanzania na sio kwenda kula mayai na kujilimbikizia mali
Source: Mwananchi Jumamosi