Wosia wa Mwl. Nyerere - Mimi ninang'atuka na siasa ya Tanzania

Bibie,
Nakwambiaje? Katika lugha yetu hatuna neno ng'ata kwa maana ya kuuma. Kuuma ni kuuma tu. Ukishaelewa hivyo ndipo utaweza kuelewa kwamba hakuna uhusiano baina ya maneno hayo mawili. Ng'ata ni kuuma kwa meno. Lakini kung'atuka ni neno la Kizanaki ambalo maana yake ni kuondoka kwenye kiti (specific). Kwa mfano huwezi kulitumia neno hilo kwa mtu anayetoka kitandani. Ni mahususi tu juu ya kiti. Na ndiyo maana limeingizwa katika kamusi ya Kiswahili likiwa na maana ya kuondoka kwa hiari kutoka nafasi ya uongozi ( Kamusi ya Kiswahili Sanifu, toleo la pili, ukurasa wa 306)

Ni kamusi gani hiyo Jasusi? Ya TUKI au BAKITA?
 
Tatizo ni kwamba Huwa Hatusomi between the Lines,

'Mmi ninang'atuka lakin bila CCM madhubuti nchi itayumba'

Maana yake hapa mwalimu Alimaanisha Kama CCM haipo madhubuti basi Iwaachie wengine hadi itakapo kuwa madhubuti basi ndo irejee.CCM legelege na nchi itakuwa legelege.
 
Ukitaka kujuwa maana ya kung'atuka ni rahisi sana, kwanza ujuwe "kung'ata" kama umesha juwa kung'ata ni nini basi ujuwe Nyerere alitung'ata na baada ya kuona hii mijitu hata unapoing'ata yenyewe bado tu ipo "ndiyo baaaba" akachoka kung'ata, unaing'ata mijitu kwa miaka zaidi ya ishirini yenyewe ipo tu, inakenuwa meno kama vile hawana hisia za kung'atwa, baada ya taya kumuuma aka "ng'atuka". Alikuwa hana jipya jingine taabani kwa kun'gata.

Kung'ata = Kuuma kwa kutumia meno.
Kung'atuka = Kuwachia kuuma kwa kutumia meno.

Sikubaliani na maana iliyotajwa hapo juu na bado ninaamini kua kung'atuka ni kuondoka sehemu kwa kulazimiswa na mazingira kama yule aliyesema kua akitokea mtu mzima inabidi ung'atuke kumpisha kiti. I any case mjadala wangu haupo ktk hilo ninacotaka ni kutathmini maneno ya Mwl na uhalisia wake ktk wakati tulionao
 
Ukitaka kujuwa maana ya kung'atuka ni rahisi sana, kwanza ujuwe "kung'ata" kama umesha juwa kung'ata ni nini basi ujuwe Nyerere alitung'ata na baada ya kuona hii mijitu hata unapoing'ata yenyewe bado tu ipo "ndiyo baaaba" akachoka kung'ata, unaing'ata mijitu kwa miaka zaidi ya ishirini yenyewe ipo tu, inakenuwa meno kama vile hawana hisia za kung'atwa, baada ya taya kumuuma aka "ng'atuka". Alikuwa hana jipya jingine taabani kwa kun'gata
Kung'ata = Kuuma kwa kutumia meno.
Kung'atuka = Kuwachia kuuma kwa kutumia meno.
Have never thought of the word that way...he had played with this countries' history that I think we can have less strength going forward with it and him as part of it.
 
mimi nashangaa hawa wanaohangaika na kile kibabu. nchi ilimshinda karibu kila nyanja, afya, elimu, etc. kaliweza kudhibiti rushwa tu na kulinda rasilimali zetu. The rest was zero.

sasa hauoni kama hilo ni la muhimu zaid? na haujui kuwa adui mkuu wa maendeleo ya nchi ni rushwa na matumiz mabaya ya rasilimal? so kwa hilo naamin Nyerere hakua zero
 
Acheni kumtukuza nyerere jamani. faiza kasema kweli kabisaa kuwa nyerere alikuwa anag'ata na mpaka katuchoka kung'ata. wewe fikiria alivyobuluza watu katika operesheni ya vijiji iliyojulikana kama sogeza! Tazama alivyotubuluza kula ugali wa njano, unga mchafu wa muhogo na kulilia sukari kwa folleni!

Alituletea walimu wa UPE na hakutaka kabisaa kujenga shule za secondari wala kujenga vyo vya ualimu! halafu wakuu wa wilaya wote tanzania walikuwa ni dalasa la saba!

watu tuliogea sabuni za mkaa na aliwanyima wanamuziki na wasanii kuwa na hati miliki. walijikuta wote wapo masikini sana kama kina ahmedi kipande, malijani shabani, shem kalenga na balisidya. wapi duniani ukatembea ukakuta wanamuziki ni masikini ?

leo watu kutaka kusema eti, mwalimu katuachia usia ni utoto wa juu sana na usiopingika. Faiza kasema kweli na hata gazeti la Alnur limesema kweli kuwa mtu huyu katutoa pazuri na kutufikisha pabaya.
 
Acheni kumtukuza nyerere jamani. faiza kasema kweli kabisaa kuwa nyerere alikuwa anag'ata na mpaka katuchoka kung'ata. wewe fikiria alivyobuluza watu katika operesheni ya vijiji iliyojulikana kama sogeza! Tazama alivyotubuluza kula ugali wa njano, unga mchafu wa muhogo na kulilia sukari kwa folleni!

Alituletea walimu wa UPE na hakutaka kabisaa kujenga shule za secondari wala kujenga vyo vya ualimu! halafu wakuu wa wilaya wote tanzania walikuwa ni dalasa la saba!

watu tuliogea sabuni za mkaa na aliwanyima wanamuziki na wasanii kuwa na hati miliki. walijikuta wote wapo masikini sana kama kina ahmedi kipande, malijani shabani, shem kalenga na balisidya. wapi duniani ukatembea ukakuta wanamuziki ni masikini ?

leo watu kutaka kusema eti, mwalimu katuachia usia ni utoto wa juu sana na usiopingika. Faiza kasema kweli na hata gazeti la Alnur limesema kweli kuwa mtu huyu katutoa pazuri na kutufikisha pabaya.
Sasa hivi mna umeme wa mgao haulalamiki. Shirika la ndege Air Tanzania mmeliua haulalamiki. Mashirika mengi ya umma na benki zetu tumegawia wageni haulalamiki. Watu wanafukuzwa kutoka vijijini wanaingizwa "wawekezaji" haulalamiki. Akutukanaye hakuchagulii tusi.
 
mimi nashangaa hawa wanaohangaika na kile kibabu. nchi ilimshinda karibu kila nyanja, afya, elimu, etc. kaliweza kudhibiti rushwa tu na kulinda rasilimali zetu. The rest was zero.

kama nchi ilimshinda aliwezaje kudhibiti mali zenu na rushwa? Mlitibiwa bure na mlisoma bure. Wewe unafahamu ulichochangia kweli, au unafuata mkumbo? Nyerere was the great leader ambae msimtegemee kumpata kirahisi hapa tz nakuhakikishia. Huko mnapomjadili vibaya mnapotoka mbaya. Dhambi ya chuki kwa mtu inocent itawamaliza.
 
kama nchi ilimshinda aliwezaje kudhibiti mali zenu na rushwa? Mlitibiwa bure na mlisoma bure. Wewe unafahamu ulichochangia kweli, au unafuata mkumbo? Nyerere was the great leader ambae msimtegemee kumpata kirahisi hapa tz nakuhakikishia. Huko mnapomjadili vibaya mnapotoka mbaya. Dhambi ya chuki kwa mtu inocent itawamaliza.

bure maana yake nini? mkuu kwani mlikuwa hamlipi kodi?

matibabu yapi yalikuwa yanapatikana vipi? ulanguzi na rushwa
 
Kung'atuka kwa uelewa wangu mdogo kunachukua muelekeo wa mtu kulazimika kuacha kitu fulani bila ya hiari yake pengine mazingira yamemfanya achukue uamuzi huo. Sina uhakika kwa asilimia 100 kua Mwl alitumia neno hilo kwa mantiki hiyo possibly.
Ambacho nilikikusudia sana ni kutathmini maneno ya Mwl kwa ujumla na ukweli wake ktk wakati tulionao na sio neno mojamoja na ninadhani kua maneno ya Mwl kwa ujumla yanaeleweka no matter kung'tuka itakua na maana gani.

Naomba mchango wako sister au kama ni brother please. Thanks.

Mimi nimejaribu kulielezea neno ng'atuka kwa uasilia wake ili ieleweke kuwa Nyerere hakuachia kwa kupenda imemlazimu ang'atuke na aliposema anang'atuka wengi hawakumuelewa anamaanisha nini.

Nyerere alijitahidi sana lakini kwa nchi kashindwa kabisa, hakuna zaidi ya kimoja tu alichokifanya kilichokuwa na mafanikio. Hicho kimoja wengi wanakijuwa ni nini na ndicho hicho kinachopelekea kuombewa Utakatifu hakuna zaidi ya hapo.
 
Mimi nimejaribu kulielezea neno ng'atuka kwa uasilia wake ili ieleweke kuwa Nyerere hakuachia kwa kupenda imemlazimu ang'atuke na aliposema anang'atuka wengi hawakumuelewa anamaanisha nini.

Nyerere alijitahidi sana lakini kwa nchi kashindwa kabisa, hakuna zaidi ya kimoja tu alichokifanya kilichokuwa na mafanikio. Hicho kimoja wengi wanakijuwa ni nini na ndicho hicho kinachopelekea kuombewa Utakatifu hakuna zaidi ya hapo.
Bibie,
Hata kama Nyerere aling'atuka baada ya kutambua kuwa hakuna hata kimoja alichofanya kilichofanikiwa nadhani tunastahili kumsifia. Mtu anayetambua kuwa ameshindwa na kumpisha mwenzake ajaribu si mtu wa kubeza. Afrika imejaa mifanyo ya ving'ang'anizi ambavyo hata licha ya kufeli vinabakia tu mamlakani mpaka waje wachomolewe kwenye mitaro ya maji na kusokomezwa milingoti matakoni. Kwa hili Nyerere bado ni above the rest.
 
Kwa hiyo Kuuma kizanaki ni Kiswahili kuuma? Kama ni hivyo basi uelewe kuwa kuna maneno ya Kizanaki yanatokana na Kiswahili na Kung'ata ni neno Msafiri sana la Kiswahili ni kama nilivyolieleza huko juu, Kama lipo au halipo kwenye kamusi inategemea na huyo mwandishi wa hiyo kamusi, kuna maneno mengi sana hupatikana katika kamusi mojawapo kukosekana katika kamusi nyingine na kamusi za maana ni zile zinazoishi au kwa maana nyingine zinazoongezewa maneno kila baada ya muda fulani.

Sikupingi hilo neno Wazanaki wanalitumia vipi nnachokueleza ni uasili wa hilo neno na kwanini Nyerere alilitumia, unaweza kuniambia kuwa Nyerere alikosa neno kuwachia madaraka au kustaafu? La hasha, akiyajuwa sana lakini alitumia hilo kwa maana yake na nimeshaelezea kwa maana ipi. Fikiri.
 
Bibie,
Hata kama Nyerere aling'atuka baada ya kutambua kuwa hakuna hata kimoja alichofanya kilichofanikiwa nadhani tunastahili kumsifia. Mtu anayetambua kuwa ameshindwa na kumpisha mwenzake ajaribu si mtu wa kubeza. Afrika imejaa mifanyo ya ving'ang'anizi ambavyo hata licha ya kufeli vinabakia tu mamlakani mpaka waje wachomolewe kwenye mitaro ya maji na kusokomezwa milingoti matakoni. Kwa hili Nyerere bado ni above the rest.

Hakuondoka kwa hiyari "aling'atuka", tafadhali usichanganye kustaafu na kung'atuka.
 
Nyerere alijitahidi sana lakini kwa nchi kashindwa kabisa, hakuna zaidi ya kimoja tu alichokifanya kilichokuwa na mafanikio. Hicho kimoja wengi wanakijuwa ni nini na ndicho hicho kinachopelekea kuombewa Utakatifu hakuna zaidi ya hapo.
Katika kipindi chake tulikuwa na umeme Dar kama kawa sasa hivi hapo mchafukoge giza totoro ndo kawaida. watu walisoma bure kwasababu kodi zao zilitumika ipasavyo leo hii kuendesha mashangini ndo sifa. Sasa hivi nchi inauzawa kwa republicans wewe unaona poa tuu.Deni la ndani na la nje linaongezeaka huoni tatizo, eti nchi kukopa kwenye benki za ndani kulipa mishahara wewe unaona ni maendeleo. Huu ujinga haukuwepo wakati wa nyerere.
 
Katika kipindi chake tulikuwa na umeme Dar kama kawa sasa hivi hapo mchafukoge giza totoro ndo kawaida. watu walisoma bure kwasababu kodi zao zilitumika ipasavyo leo hii kuendesha mashangini ndo sifa. Sasa hivi nchi inauzawa kwa republicans wewe unaona poa tuu.Deni la ndani na la nje linaongezeaka huoni tatizo, eti nchi kukopa kwenye benki za ndani kulipa mishahara wewe unaona ni maendeleo. Huu ujinga haukuwepo wakati wa nyerere.

Unashindwa kuelewa kuwa wakazi wa Dar wameongezeka sana toka Nyerere alipong'atuka. Halafu Nyerere aliiacha hii nchi ina megawati ngapi za umeme na asilimia ngapi ya Watanzania walikuwa wanapata umeme? Nyerere umeme wa Dar aliukuta, alipokuja kuhamia Dar na kukaribishwa nyumbani kwa kina Sykes alikuta kuna umeme upo Dar.
 
Back
Top Bottom