Mpigadili Tz
JF-Expert Member
- May 4, 2015
- 1,042
- 1,821
Habari zenu wakuu,
Mimi ni mfanya biashara katika biashara yangu pia nimeweka mambo ya huduma za kipesa za mitandao (Wakala), sasa jana majira ya saa tisa kuna mtu alikuja akasema:
Jamaa: niwekee Tigo pesa laki 8 na voda niwekee laki moja
Mimi: poa (jamaa akanipa pesa nikazihesabu zikawa sahihi laki 9).
Jamaa: Ah niwekee na 7500 tigo pesa na 3000 voda nifanye kama ya kutolea maana baadae nitazitoa.
Mimi: poa (jamaa akanipa 10500)
Jamaa: Ah sikia basi nipe hizo pesa nimeghairi (mimi nikamkabidhi)
Jamaa: lakini poa we niwekee tu maana kutembea nazo pia naona ovyo (jamaa akanikabidhi tena).
Mimi nikazichukua zile pesa nikazieka katika droo nikamuekea kisha akaondoka dah! Nakuja kuzicheki zipo laki mbili zilizojaa 2000 na 10000 tatu, nikajaribu kuwapigia Voda wamesema jamaa kashazitoa ila nenda polisi alafu nenda TCRA, nikwapigia Tigo wamesema jamaa kashazitoa nikwauliza mtanisaidiaje wamesema hatuna cha kukusaidia.
HIVI WAKUU NINI NAWEZA KUFANYA?
Mimi ni mfanya biashara katika biashara yangu pia nimeweka mambo ya huduma za kipesa za mitandao (Wakala), sasa jana majira ya saa tisa kuna mtu alikuja akasema:
Jamaa: niwekee Tigo pesa laki 8 na voda niwekee laki moja
Mimi: poa (jamaa akanipa pesa nikazihesabu zikawa sahihi laki 9).
Jamaa: Ah niwekee na 7500 tigo pesa na 3000 voda nifanye kama ya kutolea maana baadae nitazitoa.
Mimi: poa (jamaa akanipa 10500)
Jamaa: Ah sikia basi nipe hizo pesa nimeghairi (mimi nikamkabidhi)
Jamaa: lakini poa we niwekee tu maana kutembea nazo pia naona ovyo (jamaa akanikabidhi tena).
Mimi nikazichukua zile pesa nikazieka katika droo nikamuekea kisha akaondoka dah! Nakuja kuzicheki zipo laki mbili zilizojaa 2000 na 10000 tatu, nikajaribu kuwapigia Voda wamesema jamaa kashazitoa ila nenda polisi alafu nenda TCRA, nikwapigia Tigo wamesema jamaa kashazitoa nikwauliza mtanisaidiaje wamesema hatuna cha kukusaidia.
HIVI WAKUU NINI NAWEZA KUFANYA?