Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,335
- 24,232
Mtunzi wa melody ya wimbo wa Taifa letu; Mungu Ibariki Afrika ni mwafrika anaitwa Enock Mankayi Sontonga (Enoch Sontonga - Wikipedia )ambaye aliutunga kama Nkosi Sikelei iAfrika mwaka 1897 huko Afika Kusini.
Mwanzoni wimbo huu uliimbwa kama wa dini ili kupata baraka za Mungu, lakini baadaye wimbo huu ulipendwa sana na kuimbwa katika vikao vya kuomba dua ya waafrika wanyonge huko Afrika Kusini chini ya African National Congress, mwaka 1912.
Ni wimbo na maneno yake yanayogusa sana nafsi.
Kifupi wimbo ulipendwa na wote waafrika waliokuwa wakionewa na kukandamizwa kusini mwa bara la Afrika.
Hivyo basi sasa wimbo huu(melody-instrumental) zipo kaatika mataifa ya Afrika Kusini ,Zambia ,Tanzania , Zimbabwe(baadaye walibaidli), Namibia(baadaye walibadili).
Kila nikisikia maneno ya wimbo huu kwakweli nasisimka kwa kulipenda Taifa langu na watu wake.
Mwanzoni wimbo huu uliimbwa kama wa dini ili kupata baraka za Mungu, lakini baadaye wimbo huu ulipendwa sana na kuimbwa katika vikao vya kuomba dua ya waafrika wanyonge huko Afrika Kusini chini ya African National Congress, mwaka 1912.
Ni wimbo na maneno yake yanayogusa sana nafsi.
Kifupi wimbo ulipendwa na wote waafrika waliokuwa wakionewa na kukandamizwa kusini mwa bara la Afrika.
Hivyo basi sasa wimbo huu(melody-instrumental) zipo kaatika mataifa ya Afrika Kusini ,Zambia ,Tanzania , Zimbabwe(baadaye walibaidli), Namibia(baadaye walibadili).
Kila nikisikia maneno ya wimbo huu kwakweli nasisimka kwa kulipenda Taifa langu na watu wake.