Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,268
- 17,097
Napenda kuwafahamisha kuwa mimi Gamba Jipya, sina uhusiano wowote na Bwana Willy, kitu kilichopo hapa ni kuwa mimi ni muumini wa siasa/uongozi wa vijana, na mara ninapoona kijana wa Kitanzania mwenye nia njema kabisa akiwa na ari na shauku ya kupanda ngazi ili awe kiongozi ili baadaye asaidie mustakabali wa Taifa hili huwa nampa sana support yangu.
Ni vijana wangapi hapa jamvini wanaweza kwenda vijiji ground zero kujaribu kuongea/kusikiliza na kukusanya kero za watanzania wenzake na pale anapokuwa na uwezo kuwasaidia ama yeye mwenyewe ama kuwasilisha kero hizo sehemu husika, wangapi wanafanya au wamefanya hivyo?..kuna wengine mnaishi hapo Dar es Salaam lakini hata kwenda Bagamoyo ground zero kujionea maisha na kusikia kilio cha Mtanzania wa kawaida ili baadaye ujue ni kwa kiasi kipi unaweza saidia watanzania wenzako hamjafanya, huyu jamaa ameweza kuonyesha njia, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, tubadilike, tuache chuki, wivu, uvivu na majungu, Nenda ground zero kama kina Zitto, Mnyika, Kibanda, January etc, kukaa nyuma ya laptop yako kamwe hakuta saidia ujenzi wa taifa hili.
Turudi kwenye kujadili hoja na si vioja vya kuandama watu.
Mwenyezi Mungu awabariki sana, Nadhani sasa tuko pamoja kwa maslahi ya Taifa
Unamdanganya nani?.......wewe FMES na hili GAMBA JIPYA....LE MUTUZ....BAHARIA....how could you have all these aliases?