Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Pamoja na maneno mazuri ya faraja kuwa Tanzania karibia inakombolewa...bado napata mashaka na mbinu za Ukombozi tulizonazo. Huwezi Kuamini kinachoendelea katika baadhi ya Wilaya nchini.....ambapo yaani hata harufu ya CDM kuisikia ni kwa machale.
Nilibahatika kuingia katika kikao cha Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba (Rural) yenye kata 29 nilisikitika kuona kuwa kati ya hizo kata 29, kata 28 zinaongozwa na CCM na kata moja tu ya Katoro inaongozwa na CUF. Yaani hapa upinzani umeoneshwa na CUF pekee japokuwa bado na yenyewe haitoshi.
Wakati kikao kianendelea Viongozi wa Vyama vya upinzani walikuwa wanakribishwa kuhudhuria kikao hicho. Waliokaribishwa ni Viongozi wa CCM na CUF kwa siku ya kwanza. Siku ya Pili alihudhuria wa CCM na NCCR Mageuzi na CUF. Ikabidi niulize; imekuwaje NCCR Mageuzi wamefika hapa wakati hawana hata Kata moja? Jibu nililopewa ni kuwa "angalau NCCR wanaonekana as chama cha Upinzani, hata kama hawana kata hata moja wao ni "ACTIVE" maeneo haya. Baada ya hapo nikajiuliza inakuwa je Chama kinachopigiwa chapuo kuchukua nchi hakina jitihada yoyote ili kijihakikishie ushindi?
Nimewahi kusema hapa kuwa CDM hapa Bukoba mjini haionekani.......hatuoni initiative zozote za kukipromote chama. Viongozi wa Mkoa wako wapi? Niliwahi kusema Chama kama chama kiitishe mkutano wa wanachama wake kioneshe mpango kazi wake kama tatizo ni la ki budget wanachama wenyewe tujipange na kukiwezesha kuwafikia wananchi lakini wapi. Ofisi au Makao makuu naambiwa ni Ijuganyondo.....pembeni mwa mji. Hata kutoonekana kwa ofisi mjini ni udhaifu........
Tatizo nini? Inawezekana kuna wilaya Nyingine CDM haina hata kata moja!! Naomba tena Uongozi wa CDM ueleze kinaga ubaga nini mpango wake wa Kukiimarisha chama Mkoani Kagera .,....Hususan Wilaya Hii ya Bukoba? Siwezi kuwasemea wengine hapa nchini. Naomba anayeona kulegalega kwa CDM mahali pake aombe ufafanuzi kwa viongozi ili watoe majibu ya pamoja. Nisipojibiwa kwa hili siongei tena.
Nasuburi maelezo hapa........tumejiuliza wengi ...tunasubiri majibu na makakati.
Nilibahatika kuingia katika kikao cha Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba (Rural) yenye kata 29 nilisikitika kuona kuwa kati ya hizo kata 29, kata 28 zinaongozwa na CCM na kata moja tu ya Katoro inaongozwa na CUF. Yaani hapa upinzani umeoneshwa na CUF pekee japokuwa bado na yenyewe haitoshi.
Wakati kikao kianendelea Viongozi wa Vyama vya upinzani walikuwa wanakribishwa kuhudhuria kikao hicho. Waliokaribishwa ni Viongozi wa CCM na CUF kwa siku ya kwanza. Siku ya Pili alihudhuria wa CCM na NCCR Mageuzi na CUF. Ikabidi niulize; imekuwaje NCCR Mageuzi wamefika hapa wakati hawana hata Kata moja? Jibu nililopewa ni kuwa "angalau NCCR wanaonekana as chama cha Upinzani, hata kama hawana kata hata moja wao ni "ACTIVE" maeneo haya. Baada ya hapo nikajiuliza inakuwa je Chama kinachopigiwa chapuo kuchukua nchi hakina jitihada yoyote ili kijihakikishie ushindi?
Nimewahi kusema hapa kuwa CDM hapa Bukoba mjini haionekani.......hatuoni initiative zozote za kukipromote chama. Viongozi wa Mkoa wako wapi? Niliwahi kusema Chama kama chama kiitishe mkutano wa wanachama wake kioneshe mpango kazi wake kama tatizo ni la ki budget wanachama wenyewe tujipange na kukiwezesha kuwafikia wananchi lakini wapi. Ofisi au Makao makuu naambiwa ni Ijuganyondo.....pembeni mwa mji. Hata kutoonekana kwa ofisi mjini ni udhaifu........
Tatizo nini? Inawezekana kuna wilaya Nyingine CDM haina hata kata moja!! Naomba tena Uongozi wa CDM ueleze kinaga ubaga nini mpango wake wa Kukiimarisha chama Mkoani Kagera .,....Hususan Wilaya Hii ya Bukoba? Siwezi kuwasemea wengine hapa nchini. Naomba anayeona kulegalega kwa CDM mahali pake aombe ufafanuzi kwa viongozi ili watoe majibu ya pamoja. Nisipojibiwa kwa hili siongei tena.
Nasuburi maelezo hapa........tumejiuliza wengi ...tunasubiri majibu na makakati.