Sumba-Wanga
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 5,349
- 1,224
Ningependa post hii ibaki hapa hapa kwani siasa za Tanzania ni chanzo cha tatizo hili.
Alihamisi iliyopita nilipita katika shule fulani pale Dodoma, shule hii ipo maeneo ya maili mbili kule CDA, ni moja ya shule za kata. Sina uhakikwa wa jina la shule ile ila ipo karibu sana na shule ya Azimio. Anyway, nilichokuta pale shuleni mida ya saa sita ni kwamba walimu wote walikuwa wamekaa nje na wanafunzi wanapiga kelele kweli kweli madarasani. Kimsingi nilikereka na nilisema ingekuwa shule yangu ningewanasa vibao walimu waliokuwa wamekaa nje. Siasa zetu ni za kipumbavu sana. Hatuna tabia ya kuwajibika kabisa.
Kimsingi mimi namuunga mkono huyo mfadhili. Tena kama inawezekana angewatandikwa walimu wote. Fikiri tarehe 14 mwezi wa pili wanapanga ratiba! Inaingia akilini kweli? Shule za serikali zilifunguliwa tarehe 16 mwezi wa kwanza halafu walimu wakakwambia kwamba tarehe 14 mwezi wa pili wanapanga ratiba. Huu ni upumbavu! Kwa mtindo huu, nchi hii haitaendelea hata siku moja. Nimewahi kuwa mwalimu wakati wa likizo ya mkapa, kimsingi sikuwa na mda wa kusogoa na wanafunzi wangu walifaulu, tena masomo ya sanyansi. Inakuwaje walimu washindwe kuwafundisha kwa miaka minne?
Jamani tuungane kupinga udhalimu huu wanaofanyiwa watoto wetu. Tukiendelea kusema tunadhalilishwa, tutakufa na umasikini. Ni upumbavu kwenda shuleni na kusogoa! Ni upumbavu kwenda ofisini na kupiga hadithi bila kufanya kazi. Ni wizi kulipwa bila kufanya kazi. Tunaua taifa.
Acheni ushambiki huyu mwalimu alipaswa kutandikwa vibao.
tena achukuliwe hatua kali,huo ni udhalilishwaji mkubwa sana,ufadhili wake usiwe kigezo cha kudhalilisha watanzania,siku hizi hata mwanafunzi hachapwi fimbo hovyo.