Raia wa Uholanzi amzaba vibao mwalimu mbele ya wanafunzi

Power G

JF-Expert Member
Apr 20, 2011
3,886
1,194
Raia mmoja wa Uholanzi, Marise Koch, amemfanyia kitendo cha udhalilishaji Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Marera iliyopo kata ya Rhotia Wilayani Karatu mkoani Arusha kwa kumpiga vibao mbele ya wanafunzi na walimu wenzake.

Taarifa ambazo NIPASHE imezipata na kuthibitishwa na viongozi wa Idara ya Elimu Wilaya ya Karatu na Jeshi la Polisi, zinasema kutokana na udhalilishaji huo, raia huyo wa Uholanzi ameshafunguliwa jalada lenye namba KRT/RB/835/2012 katika kituo cha polisi Karatu kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Marera, Emmanuel Ginwe, alisema alipigwa vibao viwili na Koch baada ya kuwakuta walimu wa shule hiyo wakipanga ratiba ya shule. Ginwe alisema tukio hilo lililotokea Februari 14, 2012 majira 4:30 asubuhi ambapo Koch ambaye anafadhili shule hiyo kwa kukarabati majengo ya shule, ofisi, nyumba za walimu na kompyuta ndogo za wanafunzi kufanyia michezo na kujifunzia kuandika alifika shule hapo kutembelea kama kawaida. Alisema baada ya kufika shuleni hapo, alikuta walimu wakipanga ratiba ya shule na kuanza kuhoji kwanini walimu hawajaingia madarasani kufundisha wanafunzi ambapo alijibiwa kuwa wamepewa maelekezo ya kuandaa ratiba ya shule na baada ya kumaliza kazi hiyo wataingia madarasani kufundisha.

Hata hivyo majibu ya walimu hao hayakumridhisha Koch na kuamua kwenda ofisini kwa Mwalimu Mkuu na kuanza kumfokea kwamba yeye anafadhili vitu vingi, lakini kumbe walimu hawafundishi na kuanza kukusanya kompyuta zake ndogo kwa lengo la kuzichukua. Mwalimu Mkuu wa shule hiyo hata hivyo alimsihi asichukue kompyuta hizo, lakini alikataa na alipoona anazuiliwa, alipiga vibao mwalimu huyo huku akiendelea kuzikusanya komputa na kumnasa tena vibao tena mwalimu mkuu na kuchukua kompyuta zake 70 kati ya 93 zilizokuwepo na kuondoka zake.

"Nimedhalilishwa sana mbele ya walimu, wanafunzi na mke wangu ambaye ni mwalimu, namshukru Mungu wakati ananipiga vibao japo ni mwanamke sikuweza kujibu mapigo," alisemwa Ginwe.

Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Karatu, Peter Simwanza, alisema kitendo hicho ni cha kiudhalilishaji

Source: NIPASHE

My Take: Misaada inatudhalilisha sana watz tujaribu kuiepuka na kujaribu kutumia rasilimali zetu wenyewe kujiletea maendeleo.
 
Tanzania tunadhalilishwa jamani,yote haya ameyaleta JK kwenda kwake ng'ambo kuhemea kama Rais anahemea wewe hata ukipigwa ngumi huna pa kukimbilia. lakini nasi tuache uvivu
 
Pole sana mwalimu, lakushangaza badala ya kushitakiwa hapa utasikia amepewa adhabu ya kuondoka nchini mara moja.Hapa ndipo uzalendo unapofia kujali wageni kuliko wazawa
 
Sawasawa alivyofanya huyo mama, nyie hamkuona wakati wa kupanga ratiba ila wakati mnatakiwa muwe mnafundisha?

Kafanya sawasawa, hilo ndio tatizo la Watanzania, sababu nyingi na kufanya mambo bila mipango, mtoto analetwa na wazazi anajuwa anakwenda kusomeshwa kumbe waalimu "wanapanga ratiba", pengine ukute kawakuta wanasukana, hiyo ya kupanga ratiba wanazuga tu.

Waandishi wa habari wa huko nendeni mkajuwe mama kakikuta nini, tupate upande wa pili wa habari hii.

Mimi namuunga mkono huyo mama.
 
Wazungu wanawake kwa makofi!
Ulikuwa unaleta ubabe na kukatalia komputer zako?

Mh pole mwalimu muache kutega mfundishe watoto wapasi
 
Raia mmoja wa Uholanzi, Marise Koch, amemfanyia kitendo cha udhalilishaji Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Marera iliyopo kata ya Rhotia Wilayani Karatu mkoani Arusha kwa kumpiga vibao mbele ya wanafunzi na walimu wenzake.

Taarifa ambazo NIPASHE imezipata na kuthibitishwa na viongozi wa Idara ya Elimu Wilaya ya Karatu na Jeshi la Polisi, zinasema kutokana na udhalilishaji huo, raia huyo wa Uholanzi ameshafunguliwa jalada lenye namba KRT/RB/835/2012 katika kituo cha polisi Karatu kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Marera, Emmanuel Ginwe, alisema alipigwa vibao viwili na Koch baada ya kuwakuta walimu wa shule hiyo wakipanga ratiba ya shule. Ginwe alisema tukio hilo lililotokea Februari 14, 2012 majira 4:30 asubuhi ambapo Koch ambaye anafadhili shule hiyo kwa kukarabati majengo ya shule, ofisi, nyumba za walimu na kompyuta ndogo za wanafunzi kufanyia michezo na kujifunzia kuandika alifika shule hapo kutembelea kama kawaida. Alisema baada ya kufika shuleni hapo, alikuta walimu wakipanga ratiba ya shule na kuanza kuhoji kwanini walimu hawajaingia madarasani kufundisha wanafunzi ambapo alijibiwa kuwa wamepewa maelekezo ya kuandaa ratiba ya shule na baada ya kumaliza kazi hiyo wataingia madarasani kufundisha.

Hata hivyo majibu ya walimu hao hayakumridhisha Koch na kuamua kwenda ofisini kwa Mwalimu Mkuu na kuanza kumfokea kwamba yeye anafadhili vitu vingi, lakini kumbe walimu hawafundishi na kuanza kukusanya kompyuta zake ndogo kwa lengo la kuzichukua. Mwalimu Mkuu wa shule hiyo hata hivyo alimsihi asichukue kompyuta hizo, lakini alikataa na alipoona anazuiliwa, alipiga vibao mwalimu huyo huku akiendelea kuzikusanya komputa na kumnasa tena vibao tena mwalimu mkuu na kuchukua kompyuta zake 70 kati ya 93 zilizokuwepo na kuondoka zake.

“Nimedhalilishwa sana mbele ya walimu, wanafunzi na mke wangu ambaye ni mwalimu, namshukru Mungu wakati ananipiga vibao japo ni mwanamke sikuweza kujibu mapigo,” alisemwa Ginwe.

Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Karatu, Peter Simwanza, alisema kitendo hicho ni cha kiudhalilishaji

Source: NIPASHE

My Take: Misaada inatudhalilisha sana watz tujaribu kuiepuka na kujaribu kutumia rasilimali zetu wenyewe kujiletea maendeleo.

Amejitakia mwenyewe,kama alitaka kuchukua kompyuta zake wangemwacha aende zake!Umasikini wetu usitufanye kuwa watumwa katika nchi yetu!LOL!
 
Sisi watz tuna matatizo,kwani ratiba huchukua muda gani?si wangepanga baada ya vipindi?au wale ambao hawakua na vipindi muda huo wangeendelea kupanga ratiba,halafu wale wanapotoka kwenye vipindi wanaendelea nayo kisha hawa wengie wakaingia kwenye vipindi vyao muda unapofika?kisha mwisho wa siku wanamaliza na kushare kilichopatikana.Sisi watzee ni wavivu sana,halafu visingizi huwa haviishi.Hiyo ndyio dawa,ijapokua sheria haziruhusu,maana ukiruhusu itakua ni fujo tupu,kila mtu atamzaba mwenzie vibao ,hata kwa kisingizio chake.
 
Tanzania tunadhalilishwa jamani,yote haya ameyaleta JK kwenda kwake ng'ambo kuhemea kama Rais anahemea wewe hata ukipigwa ngumi huna pa kukimbilia. lakini nasi tuache uvivu

Hapo kwenye red unaonyesha ni jinsi gani ubongo wako unavyoujaza ujinga na utegemezi wa kufikiri. angalia usije ukaacha hata kusomesha watoto wako ukitegemea JK yupo!
 
Safi sana ananikumbuka mkuu wa wilaya ya bukoba alioamishwa alivyokuwa anazunguka mashuleni kuchapa walimu bakora sababu badala ya kufundisha wapo wanaendesha bodaboda na kulewa.ratiba ya kufundisha inapangwa mapema si muda wa kufundisha ndio mnapanga ratiba.mi ningekuwa ningempiga mtama kabisa.tena bora alivyochukua hizo computers zake akawape shule nyingine.walimu wawe wanajali muda si kila siku wanapanga ratiba
 
Uforauni huu, umepigwaje makofi na mwananke usirudishe? Tena Wa Kizungu? Aibu tupi!


Raia mmoja wa Uholanzi, Marise Koch, amemfanyia kitendo cha udhalilishaji Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Marera iliyopo kata ya Rhotia Wilayani Karatu mkoani Arusha kwa kumpiga vibao mbele ya wanafunzi na walimu wenzake.

Taarifa ambazo NIPASHE imezipata na kuthibitishwa na viongozi wa Idara ya Elimu Wilaya ya Karatu na Jeshi la Polisi, zinasema kutokana na udhalilishaji huo, raia huyo wa Uholanzi ameshafunguliwa jalada lenye namba KRT/RB/835/2012 katika kituo cha polisi Karatu kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Marera, Emmanuel Ginwe, alisema alipigwa vibao viwili na Koch baada ya kuwakuta walimu wa shule hiyo wakipanga ratiba ya shule. Ginwe alisema tukio hilo lililotokea Februari 14, 2012 majira 4:30 asubuhi ambapo Koch ambaye anafadhili shule hiyo kwa kukarabati majengo ya shule, ofisi, nyumba za walimu na kompyuta ndogo za wanafunzi kufanyia michezo na kujifunzia kuandika alifika shule hapo kutembelea kama kawaida. Alisema baada ya kufika shuleni hapo, alikuta walimu wakipanga ratiba ya shule na kuanza kuhoji kwanini walimu hawajaingia madarasani kufundisha wanafunzi ambapo alijibiwa kuwa wamepewa maelekezo ya kuandaa ratiba ya shule na baada ya kumaliza kazi hiyo wataingia madarasani kufundisha.

Hata hivyo majibu ya walimu hao hayakumridhisha Koch na kuamua kwenda ofisini kwa Mwalimu Mkuu na kuanza kumfokea kwamba yeye anafadhili vitu vingi, lakini kumbe walimu hawafundishi na kuanza kukusanya kompyuta zake ndogo kwa lengo la kuzichukua. Mwalimu Mkuu wa shule hiyo hata hivyo alimsihi asichukue kompyuta hizo, lakini alikataa na alipoona anazuiliwa, alipiga vibao mwalimu huyo huku akiendelea kuzikusanya komputa na kumnasa tena vibao tena mwalimu mkuu na kuchukua kompyuta zake 70 kati ya 93 zilizokuwepo na kuondoka zake.

“Nimedhalilishwa sana mbele ya walimu, wanafunzi na mke wangu ambaye ni mwalimu, namshukru Mungu wakati ananipiga vibao japo ni mwanamke sikuweza kujibu mapigo,” alisemwa Ginwe.

Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Karatu, Peter Simwanza, alisema kitendo hicho ni cha kiudhalilishaji

Source: NIPASHE

My Take: Misaada inatudhalilisha sana watz tujaribu kuiepuka na kujaribu kutumia rasilimali zetu wenyewe kujiletea maendeleo.
 
Sawasawa alivyofanya huyo mama, nyie hamkuona wakati wa kupanga ratiba ila wakati mnatakiwa muwe mnafundisha?

Kafanya sawasawa, hilo ndio tatizo la Watanzania, sababu nyingi na kufanya mambo bila mipango, mtoto analetwa na wazazi anajuwa anakwenda kusomeshwa kumbe waalimu "wanapanga ratiba", pengine ukute kawakuta wanasukana, hiyo ya kupanga ratiba wanazuga tu.

Waandishi wa habari wa huko nendeni mkajuwe mama kakikuta nini, tupate upande wa pili wa habari hii.

Mimi namuunga mkono huyo mama.

Umeona eeh, na si ajabu walikuwa wanasogoa tu na si kupanga ratiba. Hizi shughuli zinatakiwa kufanywa kipindi cha likizo; ingawa siungi mkono kupigwa vibao, lkn kuchukua vitu vyake namsupport.
 
Wana Jf tuwe wakweli. Kwanini watoto wetu wanafeli. Huyu mzungu kaona ubabahishaji wa hawa waalimu na hana pa kuwasemeha kwa sababu system yote ndiyo hivyo. Akaamua kuhukumu mwenyewe. Je tunamuona mzungu kafanya kosa. Kosa lake nini wakati baadhi ya watoto wetu wanafika darasa la saba hawajuhi kuandika. Tuache ushabiki tujiangalie wenyewe. Huyu mzungu alitaka wawe madarasani kufundishwa. Hii si kwa faida yetu?. Sasa kama hii serikali yetu kama haiwezi kuwatoa watu wazembe mpaka wageni wanatusaidia si ni aibu. Serikali imeshindwa kuwatoa mafisadi walioiba pesa na wanajulikana sasa yeye mzungu hafanyeje. Huyu mzungu alikuwa anafkisha ujumbe kwa jamii yetu kwamba kuna uozo mwingi kwenye idara zetu za serikali. Viongozi fanyeni kazi kusafisha kwa sababu hawa wazungu wanatuona mataahira tu watu wasioweza kufikiri.
 
Back
Top Bottom