What if?

Mkuu, wote hapa JF ni wakongwe wa kukata issue. Sitegemei kwamba utakwenda "personal" katika mjadala huu kama inavyoonekana kwenye mistari kadhaa ya posting yako.

Posting yako ndefu bado haituambii kwa vipi TAZARA ni miongoni mwa mafanikio ya SAS ambayo tunaweza kujivunia.

At one point kwenye posting yako unajaribu kutushawishi kwamba Nyerere alikuwa mjamaa kwa kushawishiwa na akina Babu na SAS, sijui haya umeyatoa wapi maana historia ya ujamaa wa JKN haisomeki hivyo. Nisingependa nitumbukie kwenye mada nyingine juu ya ujamaa wa Nyerere, ila ningependa sana nijuwe SAS anapataje credit ya uanzishaji wa TAZARA.
Hakika wewe ndio umekuwa personal toka unaandika hojayako ya kwanza na unaendelea kusema mimi naokoteza na kudanganya nikiwafanya nyie watoto wadogo na kadhalika. Haya ni mawazo yako wewe mimi sikuja hapa kumdanganya mtu isipokuwa kuandika nachokifahamu mimi, sasa iwe wewe unaelewa tofauti ni vizuri ukituletea unachokifahamu kisha watu watapata kupima na hata kuelewa japo kidogo ukweli ni upi.

Ukweli ni kwamba huwezi kuelezea uzuri wa hata kiongozi mmoja ukitumia mifano yako kwa sababu unashindwa kuelewa wajibu wa mtu pasipo kushika madaraka fulani. Sidhani kama unajua hata key players ktk mradi wowote nchini iwe hata kujengwa kwa uwanja wa Taifa zaidi ya kumtaja Mkapa. Kwa hiyo sina muda wa mabishano, unaweza fikiria unavyoweza kufikiria lakini huna unalochangia isipokuwa kutafuta makosa ktk maandishi yangu. Kuhusiana na ukongwe wa kukata issue mkuu wangu hufanyi hivyo hata kidogo kwa sababu hadi sasa hivi hujatueleza wahusika hasa ni kina nani waliotuwezesha mkataba wa Tazara na Salim hayupo ktk list hiyo.

Kuhusiana na swala la Nyerere na Ujamaa sintaweza kuzungumza mengi lakini hata ukichukulia tu mradi wa Tazara, baada ya Nyerere kurudi toka China bado alikuwa akitafuta donors wengine kwa sababu hakuwa na uhakika na China pia kaunda hakuafiki China kutokana na siasa za nchi za magharibi (UK na USA). Na nakumbuka hata Chu el Lai alipotembelea Tanzania, bado Nyerere hakuwa na jibu kwa sababu hizo hizo.

Kwa hiyo unaweza kuendelea na kile unachoamini wewe kwamba Salim hakuchangia chochote ktk ujio wa Tazara na maendeleo ya nchi yetu zaidi ya mitumba. Na sikumbuki lini umewahi kumsifia kiongozi hata mmoja!. Nachosisitiza mimi unapopinga kitu ni vizuri uwe na data sahihi kupinga zile unazokataa sio kupinga ili mradi unapinga kutafuta kujua usichokijua.
Oooh by the way karibu sana T.O. unajua tena Caribana jumamosi usijichimbie huko njoo mjini ili tuzungumze zaidi..
 
So far hapo Chadema ,nani anapewa nafasi ya kuwa mgombea mwenza?
 
Mkuu Mkandara, kama mtoa hoja hana data nitaomba atupe data kuthibitisha hoja yake. Nimejiridhisha kwamba mwenzetu una pendo binafsi na SAS kwa sababu umeshindwa kutueleza mafanikio tunayoweza kujivunia kutoka kwake. Hili sio tatizo kwani kila mmoja wetu anaweza kumpenda kiongozi fulani kwa sababu zisizoelezeka. Lowassa bado anapendwa, Chenge bado anapendwa, Aziz naye kadhalika. Wapo wanaompenda JK kwa sababu zao ambazo hazielezeki kwa watu wengine. Cha muhimu ni kwamba tusitafute sababu zinazoelezeka ili kuhalalisha zile zisizoelezeka. Mfano, si vyema kusema moja ya mafaninikio ya SAS Tz ni TAZARA bila kuwa na uthibitisho, kadhalika si vyema kusema kwamba Nyerere alikuwa mjamaa ati tu kwa sababu alishawishiwa na Babu, SAS, na chama cha Umma pasipo kuleta uthibitisho.

Mimi sina chembe ya chuki na SAS, na kuhoji kwangu juu ya "uhusika wake" na uanzishaji wa TAZARA hakuna maana kwamba nina orodha ya mambo ambayo yalimshinda kufanya. Sijui mapungufu yake wala sijui strengthes zake na data juu ya uhusika wake TAZARA zitaniongezea uelewa wangu juu ya mtu huyu ambaye, kama ilivyokuwa Kambona na Iddi Amini, nimekuwa nikimsikia tangu nikiwa tumboni mwa mama.

That said, naona watanzania wakati umefika wa kutathimini viongozi wetu kwa kuangalia nini wamekifanya sio kile wanachoweza kukifanya.

Mkuu mambo ya Caribana nilisha staafu kwa manufaa ya mabinti za watu teh teh teh, jumamosi nitabaki tu huku bushi nikila uji kwa tango. Wakilisha on behalf.
 
Tangu mwanzoni, chama cha TANU kilipoanzishwa 1954, viongozi walisema tutajenga taifa la kisoshalisti. Soma katiba ya TANU na TANU creed which was also reproduced in the Arusha Declaration to undescore the same point.

Nyerere na viongozi wenzake were already committed to building a socialist nation long before his trip to China. Kama nilivyosema, soma katiba ya TANU na TANU creed pamoja na Arusha Declaration. I know the Arusha Declaration was reprinted somewhere here on Jamii Forums; I just don't remember exactly where.
 
Mkuu Mkandara, kama mtoa hoja hana data nitaomba atupe data kuthibitisha hoja yake. Nimejiridhisha kwamba mwenzetu una pendo binafsi na SAS kwa sababu umeshindwa kutueleza mafanikio tunayoweza kujivunia kutoka kwake. Hili sio tatizo kwani kila mmoja wetu anaweza kumpenda kiongozi fulani kwa sababu zisizoelezeka. Lowassa bado anapendwa, Chenge bado anapendwa, Aziz naye kadhalika. Wapo wanaompenda JK kwa sababu zao ambazo hazielezeki kwa watu wengine. Cha muhimu ni kwamba tusitafute sababu zinazoelezeka ili kuhalalisha zile zisizoelezeka. Mfano, si vyema kusema moja ya mafaninikio ya SAS Tz ni TAZARA bila kuwa na uthibitisho, kadhalika si vyema kusema kwamba Nyerere alikuwa mjamaa ati tu kwa sababu alishawishiwa na Babu, SAS, na chama cha Umma pasipo kuleta uthibitisho.

Mimi sina chembe ya chuki na SAS, na kuhoji kwangu juu ya "uhusika wake" na uanzishaji wa TAZARA hakuna maana kwamba nina orodha ya mambo ambayo yalimshinda kufanya. Sijui mapungufu yake wala sijui strengthes zake na data juu ya uhusika wake TAZARA zitaniongezea uelewa wangu juu ya mtu huyu ambaye, kama ilivyokuwa Kambona na Iddi Amini, nimekuwa nikimsikia tangu nikiwa tumboni mwa mama.

That said, naona watanzania wakati umefika wa kutathimini viongozi wetu kwa kuangalia nini wamekifanya sio kile wanachoweza kukifanya.

Mkuu mambo ya Caribana nilisha staafu kwa manufaa ya mabinti za watu teh teh teh, jumamosi nitabaki tu huku bushi nikila uji kwa tango. Wakilisha on behalf.
Mkuu niemsema hakuna mtu anaweza kuthibitisha kitu chochote kwa mrtazamo wako..Hata huyo Lowassa anayepingwa kama sii mbora huwezi kunithibitishia kitu chochote kwa ubaya wala uzuri wake na naweza kubisha ktk mtindo wako hata kama kuna ukweli. Kifupi sielewi unatakamimi nisema kitu gani yaani Salim alikufanya nini na wapi au?..
Kifupi nitakueleza vitu ambavyo sikupenda kabisa kuvilaza hapa kijiweni.

Mwaka 1993 au 94 nilikutana na Abrahman Babu aliyekuja hapa T.O kuhutubia Waeritrea kuhusiana na Uhuru wao. Marehemu Babu ni mmoja wa viongozi anayeheshimiwa sana Eritrea kwa mchango wake dhisi ya Utawala wa Ethiopia. I met him personally na kuzungumza naye mambo mengi sana yanayohusu Tanzania bara na visiwani..In fact I learned a lot na mengine huyamwaga hapa inapobidi. Siwapendi watu hawa kwa sababu ya kupenda tu kama unavyofikiria na wala siudhani kama hapa JF kuna matu anapenda au kuchukia mtu pasipo sababu kama unavyodhania.

Hivyo basi kama wewe huamini mchango wa Salim kuhusiana na Tazara nakuomba wewe andika unachokijua kinyume kuhusu Tazara ni rahisi sana, kisha mimi na wengine tutapata kuelimika lakini kubisha tu kwamba Salim hakuhusika hali hujui ni kina nani walihusika ni ubishi usiokuwa na maana.
Mkuu sawa umekataa Salim hakuhusika wala hana mchango ktk maendelo ya Tanzania basi wewe sema waliohusika na sio Salim.
Ni hayo tu mkuu wewe tupe waliohusika baada ya kupinga hoja!
 
Tangu mwanzoni, chama cha TANU kilipoanzishwa 1954, viongozi walisema tutajenga taifa la kisoshalisti. Soma katiba ya TANU na TANU creed which was also reproduced in the Arusha Declaration to undescore the same point.

Nyerere na viongozi wenzake were already committed to building a socialist nation long before his trip to China. Kama nilivyosema, soma katiba ya TANU na TANU creed pamoja na Arusha Declaration. I know the Arusha Declaration was reprinted somewhere here on Jamii Forums; I just don't remember exactly where.

Concerning Nyerere and his socialist beliefs long before independence, it's true that he articulated that position way back then.

I don't know where else the Arusha Declaration, which embodies those beliefs, is reprinted here on Jamii Forums. But I know it's reprinted in its entirety in a book by Nyerere's "Ted Sorensen," as one Jamii Forum member once described Godfrey Mwakikagle here on Jamii Forums, which is a misleading characterisation of Mwakikagile and his work.

I posted on Jamii Forums an entire chapter from Mwakikagile's book, "Nyerere and Africa: End of an Era," which contains the whole Arusha Declaration. The chapter is on page 81 of "Nyerere: The Man, the Myth and the Legend," a thread started by Game Theory.
 
Shwari,
Mkuu hizi habari za kwamba mwalimu alikuwa socialist before Uhuru wetu ningependa sana mnipe mifano hai au hata ujumbe alowahi kuandika au kusema. Nachojua mimi kuundwa kwa TANU ilitokana na kuunda nguvu ya pamoja ktk kuutafuta Uhuru wetu (Pan African Idealism).. Ikiwa katiba ya TANU 1954 inasema:- TUTAJENGA TAIFA LA KISOCIALIST naomba sana mtu aniwekee hapa kipande hicho tu kwa sababu nakumbuka vizuri Nyerere alipokutana na Mao Tse Tung alimwambia mapema kwamba Tanzania ni nchi isiyofungamana na Upande wowote na it is not for sale!

Nachojua mimi na pengine mtabisha pia ni kwamba Kambona idealistic, was a known socialist, na ndio maana alikuja ungana na kina Kassim Hanga mengine mnayajua. Sasa sioni sababu kama walikuwa pamoja na falsafa sawa iweje watake kumpindua mwenzao..

Ushahidi mwingine ni kwamba Nyerere alitumiwa na Uingereza na USA kabla na baada ya Uhuru na ndio maana hata wakati wa mutiny, Mkuu aliingia mitini akaomba Uingereza kumsaidia. Na kama mnakumbuka Mapinduzi ya Zanzibar na maasi ya wanajeshi East Africa (maana ilitokea hata Kenya na Uganda wakati huo huo) ilikuwa kama kitu kimepangwa vile.

Zipo report kibao za CIA na wanahabari wengi tu zinaonyesha jinsi UK na Marekani walivyokuwa wakimshawishi juu ya wasiwasi yao na Mapinduzi ya Zanzibar, kwamba asipoangalia nchi itachukuliwa na Masocialist..meaning hiyo mutiny ilikuwa ni ya kisiasa zaidi ya ugaidi wa wanajeshi na ndio maana kilichofuatia mwalimu alivunja vyama vya upinzani na kubakiza chama kimoja. Again why CIA wamfuate mwalimu hali wakijua fika kwamba TANU ilikuwa chama cha Kisocialist?..
 
Shwari,
Mkuu hizi habari za kwamba mwalimu alikuwa socialist before Uhuru wetu ningependa sana mnipe mifano hai au hata ujumbe alowahi kuandika au kusema. Nachojua mimi kuundwa kwa TANU ilitokana na kuunda nguvu ya pamoja ktk kuutafuta Uhuru wetu (Pan African Idealism).. Ikiwa katiba ya TANU 1954 inasema:- TUTAJENGA TAIFA LA KISOCIALIST naomba sana mtu aniwekee hapa kipande hicho tu kwa sababu nakumbuka vizuri Nyerere alipokutana na Mao Tse Tung alimwambia mapema kwamba Tanzania ni nchi isiyofungamana na Upande wowote na it is not for sale!

Nachojua mimi na pengine mtabisha pia ni kwamba Kambona idealistic, was a known socialist, na ndio maana alikuja ungana na kina Kassim Hanga mengine mnayajua. Sasa sioni sababu kama walikuwa pamoja na falsafa sawa iweje watake kumpindua mwenzao..

Ushahidi mwingine ni kwamba Nyerere alitumiwa na Uingereza na USA kabla na baada ya Uhuru na ndio maana hata wakati wa mutiny, Mkuu aliingia mitini akaomba Uingereza kumsaidia. Na kama mnakumbuka Mapinduzi ya Zanzibar na maasi ya wanajeshi East Africa (maana ilitokea hata Kenya na Uganda wakati huo huo) ilikuwa kama kitu kimepangwa vile.

Zipo report kibao za CIA na wanahabari wengi tu zinaonyesha jinsi UK na Marekani walivyokuwa wakimshawishi juu ya wasiwasi yao na Mapinduzi ya Zanzibar, kwamba asipoangalia nchi itachukuliwa na Masocialist..meaning hiyo mutiny ilikuwa ni ya kisiasa zaidi ya ugaidi wa wanajeshi na ndio maana kilichofuatia mwalimu alivunja vyama vya upinzani na kubakiza chama kimoja. Again why CIA wamfuate mwalimu hali wakijua fika kwamba TANU ilikuwa chama cha Kisocialist?..

"THE ARUSHA DECLARATION: SOCIALISM AND SELF-RELIANCE

Part One: The TANU Creed

The policy of TANU is to build a socialist state. The principles of socialism are laid down in the TANU constitution...."
 
Kwa siasa zetu tunakoelekea,itakuwa wakristo wanaleta mtu wao na waislam wao,hata hivyo tumekuwa tukifanya hivyo chini ya ccm rulling,sema hatuweki wazi kilugha na utaratibu ni kwamba wakristo na waislam hao ni wa ccm nec ,na mpango wao ni kubadilisha kila baada ya miaka kumi...nimefurahi mwananchi kama Mkandara akijali maslahi ya Taifa na kuweka udini pembeni na kumsapoti Dr Slaa.Nakubali ingekuwa vyema kwa upande wao wachague na wao mtu makini,Slaa ni Rais wa waislam na wakristo,ila si mbaya akipata msaada wa waislam ili kuindoa ile dhana ya udinii ambayo inaligawa Taifa....ccm wakileta udini watashindwa kwani wakristo ni wengi zaidi na kama wakidhani ccm haiwapendi ama haimpendi Slaa eti bcoz alikuwa father ama ni mkristu ambaye chama chake ni cha "wakristo"then watawapa kila sababu wakristo hao kusimama naye kwasababu ina maana kwamba ccm nacho ni chama cha waislam,na hapo ndo mgawanyiko wa kidini.Hata hivyo chama cha ccm kimekuwa kikitumia udhaifu ho kuwalaghai waislam,kuanzia kuundwa kwa BAKWATA hadi hili la mahakama ya kadhi..Kazi kwetu watanzania

Ndugu zangu waislam nawashauri msidanganyike kirahisi hivyo kama ambavyo tumekuwa tukiona wanasiasa wakifanya,kuvaa kibarakashia tu inatosha kumpa kura mwanasiasa kwasababu ameoyesha anajali uislam?Mrema alishindwa walimwibia kura,mwalimu mwenyewe mwanzoni mwa kampeni za Tanu alivaa kibarakishia ili luwavutia waislam,However i believe si lazima uwe msilam ili kujali maslahi ya waislam kwa viongozi wazalendo kama Dr Slaa na wengineo wengine wakiwa washa tangulia mbele ya haki....Mwalimu alifanya mambo mengi symbolically to bring the nation together,nuttin wrong with that,lakini wakija wengine na kufanya the same,haina maana they care about you,ndio maana mzungu alituwezea sana na kututawala,wao walikuja na kijifanya kama sisi kwa kuishi na kujifunza lugh na tamaduni zetu na sisi tukadhani wanatijali ndipo kibao kikageuzwa.....si lazima eti wakivaa kibarakishia ama hata kanzu kwamba watajali maslahi yenu,si mmeona ccm?

Same aplies to christians,si kila mtu anayejigamba ukristo anawapenda wakristo wenzake nk.
Watachoweka mezani kwamba watafanya nini kwa maslahi ya taifa ndiyo yana matter...Yani as a nation we will be successfull kama wote wakiwa na haki ya elimu,kazi nzuri nk,hakutakuwa na ubaguzi,na ukiwepo sheria kali zitungwe na ikibainika kuna mwenye kuleta ubaguzi wa kidini sheria ichukue mkondo wake.Si lazima mataifa ya kiislam ama kikisto yatusiadie ili tupate maendeleo.....Wao hawawapiganii nyie wala watoto wenu kwasababu tu ninyi ni waislam wema,no! wana interesst zao za kitaifa,na sisi tuna zetu,taifa letu ni la wote,mataifa yao wao ni ya kiislam ama kikiristo,na kama wewe ni msilam sana ama mkristo kwanini wasiwahamishie huko ama watoe hifadhi kwa mamia ya raia wasiokuwa na hatia wakiuwawa?sasa si mnaona utofauti hapo?

Wenzetu wanapigania territories na ego,mwarabu akitaka utamaduni wao uwe superior,wakristo nao na jews na hata nazi!

Dini za wenzetu ni tamaduni zao ndugu zanguni,tamaduni ambazo zimekuwa popular kwasababu zilitangazwa in any means necessary including wakristo crusaders na waislam jihadists,kwa sababu dunia imeba dilika,mbinu nazo zimebadilika,za kisiasa na kiuchumi,yani pesa with strings attached,no free lunch ndugu zanguni.Mkitaka maendeleo ni maslahi ya taifa kwanza asiwadanganye mtu mtaendelea kwa kupigania tamaduni za wenzenu na maslahi yao na mataifa yao,waingereza utaona waliitawala dunia na ndio maana lugha yao inatumika almost everywhwre,ingekuwa ni maasai walitawala,basi ni kimasai kingekuwa popular nk

Tulipata uhuru lakini bado tunanyeyekea wakoloni wale wale tuliowakimbiza, kwa mambo kama ya common wealth nk,ni utumwa voluntarily,ila kwasbabu manyapara sasa ni viongozi wetu wenye suti wenye kuuza rasilimali kasoro watu!Basi ndo utofauti.Wao wana mamilioni AKA "vijisenti" vya wananchi kwenye akaunti huko nje!Sasa ina maana kuwa ziko nyingi ambazo hatujui na kauli ile ilikuwa ya kuwashtuwa wenzake kuwa mkinilima nitataja hayo majisenti yenu na kuprove kuwa vynagu ni vijisenti tu!
 
"THE ARUSHA DECLARATION: SOCIALISM AND SELF-RELIANCE

Part One: The TANU Creed

The policy of TANU is to build a socialist state. The principles of socialism are laid down in the TANU constitution...."
Mkuu Arusha declaration ni ya mwaka 1967, mimi nataka kuona Katiba ya Tanu ya mwaka 1954 ikisema tutalijenga Taifa kisocialist! au mahala mwalimu akisema au ku support usocialist kabla ya kukutana na kundi la masocialist nilowataja.
 
Mkuu Arusha declaration ni ya mwaka 1967, mimi nataka kuona Katiba ya Tanu ya mwaka 1954 ikisema tutalijenga Taifa kisocialist! au mahala mwalimu akisema au ku support usocialist kabla ya kukutana na kundi la masocialist nilowataja.

When the Arusha Declaration was promulgated in February 1967, it included the TANU creed and socialist principles enunciated in 1954.

Katiba ya TANU haikuandikwa 1967, na haikubadilishwa 1967. Azimio la Arusha incorporated the TANU creed and provisions of the TANU constitution adopted in 1954.
 
When the Arusha Declaration was promulgated in February 1967, it included the TANU creed and socialist principles enunciated in 1954.

Katiba ya TANU haikuandikwa 1967, na haikubadilishwa 1967. Azimio la Arusha incorporated the TANU creed and provisions of the TANU constitution adopted in 1954.
Mkuu nipe somo maanake nimezisoma lakini sioni Ujenzi wa Taifa kwa Usocialist. Nachojua mimi ni hadi tulipotangaza Azimio la Arusha as a declaration ndipo tulipokubali Itikadi hiyo kuwa Principals zitakazo tumika ku achieve haya. Kabla ya hapo ilikuwa Pan african idealism (Dira yetu) na nchi zote za kiafrika ziliamini hivyo pasipo kutangaza mrengo wake.

WHEREAS TANU believes:
(a) That all human beings are equal;
(b) That every individual has a right to dignity and respect;
(c) That every citizen is an integral part of the nation and has the right to take an equal part in Government at local, regional and national level;
(d) That every citizen has the right to freedom of expression, of movement, of religious belief and of association within the context of the law;
(e) That every individual has the right to receive from society protection of his life and of property held according to law;
(f) That every individual has the right to receive a just return for his labour;
(g) That all citizens together possess all the natural resources of the country in trust for their descendants;
(h) That in order to ensure economic justice the state must have effective control over the principal means of production; and
(i) That it is the responsibility of the state to intervene actively in the economic life of the nation so as to ensure the well-being of all citizens, and so as to prevent the exploitation of one person by another or one group by another, and so as to prevent the accumulation of wealth to an extent which is inconsistent with the existence of a classless society.
 
Nyerere's socialist ideas began to crystallise at Endinburgh University, partly influenced by Fabian socialism. Kulikuwa na Fabian socialists katika chuo hicho and in the city of Edinburgh where Nyerere first went in October 1949. He used to attend their meetings and exchange ideas with them.

Aliporudi Tanganyika 1952, he already had socialist ideas hata kabla ya TANU kuanzishwa. Pia kuna uwezekano hata kabla ya kwenda Uingereza, he was already thinking along socialist lines, hasa ukiona kwamba emphasis yake ilikuwa on African socialism. Hakujifunza ujamaa wa Kiafrika alipokwenda Uingereza. Babu alikuwa hazungumzii ujamaa wa Kiafrika kama Nyerere.
 
Nyerere's socialist ideas began to crystallise at Endinburgh University, partly influenced by Fabian socialism. Kulikuwa na Fabian socialists katika chuo hicho and in the city of Edinburgh where Nyerere first went in October 1949. He used to attend their meetings and exchange ideas with them.

Aliporudi Tanganyika 1952, he already had socialist ideas hata kabla ya TANU kuanzishwa. Pia kuna uwezekano hata kabla ya kwenda Uingereza, he was already thinking along socialist lines, hasa ukiona kwamba emphasis yake ilikuwa on African socialism. Hakujifunza ujamaa wa Kiafrika alipokwenda Uingereza. Babu alikuwa hazungumzii ujamaa wa Kiafrika kama Nyerere.
Mkuu hapa ndipo mnapokosea. Nyerere ku attend meetings za Fabian socialism haina maana alikuwa msocialist isipokuwa ilikuwa kupata elimu ya Usocialist. Nyerere pia alikuwa aki attend misikitini na hata kusoma Kuran haina maana alikuwa Muislaam.

Hata wewe hapo unaujua Usocialist kwa kupitia kusoma vitabu na pengine ku attend meetings zao hii haina maana wewe ni msocialist isipokuwa unajifunza. Fabian kilikuwa chombo chini ya Labour party ambao walikuwa wakiunga sana mkono Uhuru wa nchi zetu na kupinga colonialism. I wouldn't call Labour Party a socialist party for simple reason that they promote equality. It's how you intend to achieve that ndicho kinakufanya uwe Socialist au vinginevyo.

Na hakika tutakapo rudisha dira yetu ya Kitaifa regardless ya tofauti ya itikadi ndipo wananchi wataweza kuchagua itikadi wanayoona inayofaa kuwawezesha kufanikiwa. Leo hii sote hapa tunazitaka sana hizo imani za TANU lakini maadam tumepoteza mwongozo huo ni vigumu hata vyama vya Upinzani ku form ideology inayolenga kufanikisha malengo hayo..
 
Mkuu hapa ndipo mnapokosea. Nyerere kuttend meetings za Fabian socialism haina maana alikuwa msocialist isipokuwa ilikuwa kupata elimu ya Usocialist. Nyerere pia alikuwa aki attend misikitini na hata kusoma Kuran haina maana alikuwa Muislaam.

Hata wewe hapo unaujua Usocialist kwa kupitia kusoma vitabu na pengine ku attend meetings zao hii haina maana wewe ni msocialist isipokuwa unajifunza. Fabian kilikuwa chombo chini ya Labour party ambao walikuwa wakiunga sana mkono Uhuru wa nchi zetu na kupinga colonialism. I wouldn't call Labour Party a socialist party for simple reason that they promote equality. It's how you intend to achieve that ndicho kinakufanya uwe Socialist au vinginevyo.
Right on the bones,as indicated on my previous contributions.....Ama wahat do you think about mwalimu's treatment of the muslims?
 
Jmushi
Issue ya udini Tanzania ni tatizo kubwa sana,imeshachukua sura mpya.

No more nationalism which meanz we are heading to a failing state.Kiongozi yoyote makini anayeitakia mema Tz anatakiwa aweze ku address hii issue kwa ukweli wake then ipatikane suluhu ya pamoja ili kujenga imani baina yetu ambayo hivi sasa imepotea kabisa.

Tutaandika sana humu JF kwa majina yetu matatu matatu na tutaonekana tuko wengi twaunga mkono CHADEMA,lakini in reality huko mitaani,vijijini etc hizi sauti za vuvuzela haziwafikii kabisaaa.
 
With the breaking newz on Dr.Slaa's broken arm (now moving around with POP), I just can't imagine what if! Keep your eyes/ears wide open & be ready for the unexpected!
 
Back
Top Bottom