What can be done to prevent our economy from collapsing?

...Unaifahamu nchi yako vizuri? nani kakwambia wameshindwa kupeleka?

...Unavijua vikwazo vilivyopo kwenye biashara ya chakula nchini? Ukiondoa ada mbalimbali, kuna ubovu wa miundo mbinu pia.

...Labda nikujulishe kidogo. Biashara hufanyika pale inapoleta au kutengeneza faida zaidi. Kama unafahamu vizuri. Wafanyabiashara hawa walipangiwa mpaka bei ya kuuza hayo mahindi. Nikuulize, unafikiri hiyo bei inavutia wao kupeleka mahindi sehemu ambayo hawatapata faida?

...Kwa taarifa yako, kuna hali ya soko kuingiliwa kisiasa kwa kiasi kikubwa na hii ndio inayoondoa maslahi ya kufanya biashara hiyo katika baadhi ya maeneo nchini.

...Narudia tena, tatizo sio uwekezaji wa nje kukosekana na biashara hii hatuhitaji mwekezaji toka nje. Tatizo ni kuingiliwa kwa soko.

Kama umenisoma vizuri post yangu ya mwanzo niliorodhesha matatizo ya nchi hii kama ifuatavyo

Mwanakijiji,

Unakumbuka tulikuwa na debate 2009 kuhusu hali ya kiuchumi ya Tanzania na muelekeo wake. Nikasema uchumi wa Tanzania kwa miaka ijayo kama ukikua sana ni asilimia 4.5%. Uchumi wa nchi unamatatizo na kikubwa ni watu wanaendekeza siasa zaidi ujuzi wa watu. Kuna mambo niliyataja mwaka juzi yanasababisha uchumi wetu kuyumba:-
a. Umeme:
Tatizo la nishati la umeme limechangia kwa kiwango kikubwa kuua uchumi wa Tanzania. Hilo ni kwasababu nishati hii imepotea na hivyo kusababisha uzalishaji wa vitu nchini na huduma nyenginezo kupanda bei maradufu. Na kuchangia ukuaji wa mfumuko wa bei na kuyumba kwa uchumi.

b. Miundo mbinu mibovu:-
Barabara, foleni, mipango miji mibovu vyote vimechangia kuongezeka kwa gharama za maisha na kuyumba kwa uchumi. Mkulima anaona bora auze mchele na sukari nje ya nchi kuliko kuleta Dar kwasababu barabara mbovu. Kama umeangalia statistics za September inflation ya vyakula iko juu kuliko inflation ya vitu vyengine. Sababu kuu ya hayo ni kwamba inflation ya chakula ndio inajumuisha basket of michele, sukari nk. Mchele wa rukwa na mbeya sasa hivi unazidi mchele kutoka pakistan kwa bei. Matokeo yake ni kuongeza importation kuliko kutumia michele ya hapa nchini. Vile vile mipango miji mibovu inachangia ukuaji wa gharama za maisha. Vitu kama foleni za barabara zinamuongezea gharama za maisha mlalahoi kwani vitu kama usafiri wake wa kila siku vinakua maradufu.

c. Ufisadi.
Ufisadi unarudisha nyuma uchumi wa nchi yetu. Hivi sasa ufisadi unatafuna zaidi ya 20% ya GDP na tatizo linakuwa kila mwaka. Hilo linachangia kuzorota kwa shughuli za uzalishaji, an increase in purchasing power of households (maana matajiri ambao ni wafanyakazi wa serikalini na taasisi nyenginezo wana pesa za kuchezea), kuongezeka kwa gharama za maisha.

d. Dollarisation.
Hii nimeshaielezea katika thread hii hapa
https://www.jamiiforums.com/habari-...bot-3-key-policies-to-rescue-shillings-3.html

e. Kuanguka kwa shillingi na athari zake kwenye gharama za maisha. Nimeshaielezea hapa.
https://www.jamiiforums.com/habari-...bot-3-key-policies-to-rescue-shillings-3.html

f. Ukopaji wa serikali usiokuwa na mpangilio.
Serikali yetu inakopa kwa kasi ya ajabu na hakuna mtu ameliangalia kwa uangalifu. Thread moja nilianzisha ya kuorodhesha madeni ya serikali inasemekana deni la serikali ni karibia Trilioni 15 je kuna mtu analijua hilo??? Trilioni 15 inamaanisha kila mtanzania analipa si chini $214 sawa na Tshs 385,200. Bado hujaiangalia level of interest charged for the debt. Na deni linakuwa kwa kasi kwani kama tukifanikiwa kuuza Eurobonds za $500 Billioni our national debt litakuwa karibu Tshs Trilioni 800. Kuna hatari tukawa kama Greece kama hatujawa waangalifu. Zaidi kuna thread nilianzisha kuhusu deni la taifa hii hapa taarifa utaziona zaidi:-

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-na-ndani-na-uwezo-wa-nchi-yetu-kuyalipa.html

Ni vema ukopaji huu ukadhibitiwa na bunge kuzuia nchi kufilisika kwani kasi hii ni hatari kwa mustakabali wa nchi hii.

g. Ukubwa serikali na bunge:
Serikali yetu inajibebesha mizigo isiyokuwa na maana na ukubwa serikali unaliumiza taifa. Tusipokuwa waangalifu tunaelekea kuwa kama ugiriki ambapo uchumi wa nchi unategemea wafanyakazi wa serikali. Serikali inahaja kupunguza gharama za uendeshaji wa serikali yake kusave pesa. Manunuzi ya Magari ya ghali, gharama zisizo na umuhimu na safari za viongozi zisizo na ulazima vinahitaji kusimamiwa. Vyenginevyo ni mzigo kwa taifa.

h. Vyanzo finyu vya kodi. Tuweni wakweli watanzania hasa waliopo katika sekta kujiajiri wengi hawapendi kulipa kodi. Kumekuwa na mianya mingi ya kukwepa kodi na kutokulipa kodi. Mfano biashara za upangishaji nyumba zimekuwa zikiachwa watu hawalipi kodi. Wafanyabishara wa kati na wakubwa wengi hawalipi kodi (including Vodacom). Kuna haja kuongeza vyanzo vya kodi.

i. Tofauti kati ya matajiri na maskini na kupotea tabaka la kati nalo limechangia.

Hayo mwanakijiji ndio matatizo ya nchi yetu. Nilikuwapo!!!

Hata hivyo suala la kuruhusu wawekezaji kutoka nje kuja kuwekeza katika ardhi yetu ni la umuhimu kwa mazingira tuliyonayo sasa. Wafanyabiashara wamepangiwa kuuza bei kwa vile bei wanazouza haziendani na uwezo wa mtanzania kununua. price ceiling ina faida kama hizo ila sio jambo zuri ni vema waboreshe usambazaji wa vyakula nchini.

Wawekezaji wa nje wanauwezo wa kusaidia kutatua hilo na pia kuongeza pato la nchi hii. Fikra kama hizi za kwako zishapitwa na wakati ndugu serikali haiwezi kuwa kila kitu inafanya itashindwa kama ilivyoshindwa kipindi cha nyerere kwasababu government expenditure itakuwa kubwa. Wawekezaji wanasaidia kupunguza tatizo la vijana wasio na ajira nchini, wanaongeza kodi na kusaidia bei za vyakula kushuka.
 
Soma post yangu ya nyuma na swali la Mwanakijiji? Nikuulize wewe unajua mahitaji ya chakula ndani ya nchi na nje ya nchi? Wameshindwa nini kupeleka mahindi yao sehemu za dodoma, Kilimanjaro na kwengineko kulikokuwa na shortage ya chakula? Nikuulize katika hao vijana wangapi wanalima kwa ajili ya kuboresha maisha yao, familia zao? Youth unemployment Tanzania ni 70% wakati graduate unemployment is almost 25% Sekta gani unadhani inaweza kutoa ajira kwa wingi kwa hawa vijana? Vijana wangapi wana mitaji ya kujiendeleza? Wangapi wanaweza kulima kwa kiwango cha kuuza nje ya nchi? Ajira na Uwekezaji zinakuja kwasababu kilimo cha large scale kinasaidia kuongeza supply ya vyakula madukani na kusaidia kushusha bei za vyakula nchini. Uzalishaji ukiongezeka na ajira nayo inaongezeka. Uzalishaji ukiongezeka na kodi ya nchi inaongezeka. Dunia inabadilika na sisi tunahitajika kubadilika kama hujapendezwa na hayo pole sana. Acheni ujinga.
...Wewe ulielimika Ulaya au Marekani au kokote kule, tueleze ni vijana kiasi gani wameajiriwa kwenye mashamba makubwa ya hayo mataifa.

...Waliokufundisha au kukutia kasumba kwa mazungumzo yao, hawakukujulisha jinsi wao walivyoendelea na vijana wao wanapata ajira wapi, tena kwa wingi.

...Viwanda pekee ndio vinaweza kutoa ajira ya maana na kwa wingi kwa vijana. Kwa elimu yako, unafikiri hao vijana 70% wasio na ajira wengi wao wako wapi? vijijini au mijini? Unapoongea kuhusu "graduates 25%" unafahamu ni vijana wangapi wamefeli shule za kata za mijini na hawapo vijijini au walishakimbilia mijini toka vijijini? Je? vijana wamachinga, mama ntilie, n.k wameajiriwa au wamejiajiri au wanatambulika katika takwimu za ajira nchini?
 
Mdondoaji - nijaribu kukuunganishia hili na mojawapo ulilolisema hapo, kama corruption inatafuna kama 20 % ya GDP yetu ni kwa kiasi gani hilo linaathiri maisha ya Waislamu, Wakristu, Wapagani wa Tanzania (collectively - Tanzanians)?
 
Kama umenisoma vizuri post yangu ya mwanzo niliorodhesha matatizo ya nchi hii kama ifuatavyo Hata hivyo suala la kuruhusu wawekezaji kutoka nje kuja kuwekeza katika ardhi yetu ni la umuhimu kwa mazingira tuliyonayo sasa. Wafanyabiashara wamepangiwa kuuza bei kwa vile bei wanazouza haziendani na uwezo wa mtanzania kununua. price ceiling ina faida kama hizo ila sio jambo zuri ni vema waboreshe usambazaji wa vyakula nchini. Wawekezaji wa nje wanauwezo wa kusaidia kutatua hilo na pia kuongeza pato la nchi hii. Fikra kama hizi za kwako zishapitwa na wakati ndugu serikali haiwezi kuwa kila kitu inafanya itashindwa kama ilivyoshindwa kipindi cha nyerere kwasababu government expenditure itakuwa kubwa. Wawekezaji wanasaidia kupunguza tatizo la vijana wasio na ajira nchini, wanaongeza kodi na kusaidia bei za vyakula kushuka.
...Nadhani hujaelewa jinsi ninavyochangia mjadala huu. Nimejibu hoja nilizoziambatanisha na maoni yangu. Hivyo nahusika kwa hizo tu.

...Hamna sehemu niliyosema kuwa serikali ifanye hiki au kile kiuzalishaji au biashara. Tofauti yake nimesema, serikali ipunguze kuingilia soko.

...Na kama haujui. Hiyo bei ni ndogo na ndio maana haivutii hata uwekezaji wa wakulima wa ndani. Hata hao wawekezaji unaowasema wakija itabidi wapandishe bei zaidi ya hiyo ili warudishe gharama na kupata faida. Na katika hili sitashangaa kwa shinikizo la serikali wanakotoka hao wawekezaji au wao wenyewe, serikali ikapunguza kuingilia soko. Tumeyaona haya na hayatakuwa mageni.
 
...Wewe ulielimika Ulaya au Marekani au kokote kule, tueleze ni vijana kiasi gani wameajiriwa kwenye mashamba makubwa ya hayo mataifa.

...Waliokufundisha au kukutia kasumba kwa mazungumzo yao, hawakukujulisha jinsi wao walivyoendelea na vijana wao wanapata ajira wapi, tena kwa wingi.

...Viwanda pekee ndio vinaweza kutoa ajira ya maana na kwa wingi kwa vijana. Kwa elimu yako, unafikiri hao vijana 70% wasio na ajira wengi wao wako wapi? vijijini au mijini? Unapoongea kuhusu "graduates 25%" unafahamu ni vijana wangapi wamefeli shule za kata za mijini na hawapo vijijini au walishakimbilia mijini toka vijijini? Je? vijana wamachinga, mama ntilie, n.k wameajiriwa au wamejiajiri au wanatambulika katika takwimu za ajira nchini?

Mkuu,

Nimesoma Tanzania katika darasa nilikuwa nakaa chini ya sakafu na kuandika sakafuni. Kaptula ikitoboka na kwa kukaa chini. Sio Kasumba ndugu yangu tunafahamishana Umeuliza Marekani, Ulaya vijana wameajiriwa wapi? Unayajua makampuni ya Kellogs, Dell Monte, Gallo na wengineo wana turnover kiasi gani kila mwaka? Wameajiri watu wangapi kila mwaka andika google utapata majibu yake. Ulaya pia makampuni kama Tesco, Morrissons, Aldi, Netto, Lidl na wengineo wananunua maziwa, nyama, ngano nk kwa wakulima wakubwa au syndicate ya wakulima wadogo wadogo.

Sekta ya Kilimo USA inaajiri karibia watu karibu asilimia 3-4% ya population ya marekani. Na inalingizia wamarekani pato la $ 60 Billion kila mwaka. Ulaya mfano Europe Agriculture inaajiri watu wengi na mwajiri mkuu namba tatu Ulaya. Inaliingizia pato la karibu EUR 64 Billioni kila mwaka.

Viwanda ndio vinatoa ajira ila isiwe viwanda tu kwani sio wote katika 70% wanaweza kufanikiwa kupata ajira viwandani. Na ukuaji wa viwanda unategemea na demand and supply of local goods and abroad. Kwa sasa Tanzania inaweza kufaidika na kilimo kwani ndicho kina demand kubwa kuliko Viwanda.

25% ya unemployed graduates ni waliomaliza degree ndugu. Chini ya degree na wasiosoma kabisa wanafikia aslimia 70 ya nguvu kazi hawana ajira na wengi wanakimbilia mijini kama Dar, Arusha, Mwanza na kwengineko.
 
Mwanakijiji... we have adopted a "vapor" business model.... all the signs were there since 2006/7... hadi leo wananchi wanarely on shares, loans za ajabu, on the macro tupo kwenye dependency... strategically tunaweka nchi rehani kwa 1% (wageni) plus 0.0001% (local) kufanya kila ikitu

with our dependency culture, we will never stop kutegemea cha mtu, tumehamia local banks, tuna development partners na FDIs!!!

Simple solution... utilize the primary stakeholder in our life (WENYEWE), TURUDI KULE TULIPOTOKA.... adopt india, china, australia, russia etc models which are not bubble models........... primary stakeholder hapa ni natural resources, tuko mbio tunashindana kugawa, huyu yuko australia, huyu katoka china, yule alikua japan, mwingine yemen, kaka mkuu alipita sweden nk..... CANT BE SOLUTION

ukisoma states economy wanarudi kule walipotoka, wamejua social security ipo ndani kwao na sio a dollar a commodity (cheap 3rd generation stakeholder)

WE ARE BUILDING OUR ECONOMY KWA KUTUMIA MATOFALI YA BARAFU, JUA LINAWAKA, NYUMBA INAYEYUKA... YET SOME ARE TRAVELLING EVRYWHERE KUNUNUA RANGI ZA SILK KUPATA KWENYE MATOFALI YA BARAFU

I AM SORRY I USE THAT LANGUAGE BECAUSE I AM ANGRY AT OUR ECONOMISTS, NIMEWADHARAU WASOMI WA VYUO VYETU WANAOFUNDISHA NADHARIA NA NILISHADHARAU DIRA TUNAYOTUMIA NADHANI HAINA FOUR ANGLES WE KKNOW I THINK NI YA DUARA

turudi kwenye production


ps: NAWAONEA HURUMA SANA WANAONUNUA HISA, TUTAYUMBA KWELI KUMBE TUNGERUDI TO BASICS TUNGEKUA MBALI ZAIDI, WE ARE SWAYED BY THE POWER OF THE COLORS AND BEAUTIFUL FACES OF MARKETING
 
Mdondoaji - nijaribu kukuunganishia hili na mojawapo ulilolisema hapo, kama corruption inatafuna kama 20 % ya GDP yetu ni kwa kiasi gani hilo linaathiri maisha ya Waislamu, Wakristu, Wapagani wa Tanzania (collectively - Tanzanians)?

Mwanakijiji,

Hilo linaathiri watanzania wote kwani kama pato la asilimia 20 la taifa au zaidi linaliwa na mafisadi inamaana uzalishaji wa nchi robo unaenda mifukoni mwa watu fulani na matokeo yake ni ufinyu wa rasilimali kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kuchangia kuongezeka kwa gap baina ya matajiri na maskini nchini. Pia kuondoka kwa tabaka la kati kunachangia kuzorota kwa shughuli za maendeleo kwani ndio walipa kodi wakubwa katika nchi yeyote duniani na watumiaji wakuu wa bidhaa nchini.
 
Mwanakijiji,

Hilo linaathiri watanzania wote kwani kama pato la asilimia 20 la taifa au zaidi linaliwa na mafisadi inamaana uzalishaji wa nchi robo unaenda mifukoni mwa watu fulani na matokeo yake ni ufinyu wa rasilimali kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kuchangia kuongezeka kwa gap baina ya matajiri na maskini nchini. Pia kuondoka kwa tabaka la kati kunachangia kuzorota kwa shughuli za maendeleo kwani ndio walipa kodi wakubwa katika nchi yeyote duniani na watumiaji wakuu wa bidhaa nchini.

Swadakta! Kumbe ni interests yetu sote kupiga vita ufisadi kwa nguvu zetu zote kwa sababu unatugusa sisi sote na vizazi vyetu. Lakini twende mbele zaidi maana najua utakuwa na data nyingi zaidi - maswali yangu mengi ni purely theoretical..

a. Dar-es-Salaam inachangia kwa kiasi gani katika GDP ya Tanzania?
b. Dar-es-Salaam inachangia asilimia ngapi ya kodi zinazokusanywa Tanzana?
 
Hivi huu tunaouita uchumi wetu bado upo kweli au ulisha collapse siku nyingi? Labda swali lingebalika na kuwa how can we resuscitate our collapsed economy? Viashiria kuwa uchumi umekufa na unahitaji kufufuliwa ni:-

(i) Uzalishaji viwandani kupungua kwa sababu ya ukosefu wa umeme;
(ii) Mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa na gharama za maisha;
(iii) Kupungua kwa makusanyo ya kodi za serikali;
(iv) Serikali sisiyoweza kulipa gharama za uendeshaji wake na kutegemea misaada/mikopo;
(v) Mgao endelevu wa umeme unaoathiri siyo tu shughuli za viwandani bali hata biashara ndogodogo;

Wachumi wanisaidie ni viashiria gani vingine zaidi ya hivyo hapo juu vinavyotuambia kuwa uchumi wetu umekufa.

mimi siyo mchumi ila naungana na wewe kusisitiza uliyo taja

nadhani uzalishaji siyo umepungua , bali hakuna uzalishaji.
nchi yetu inatawaliwa na biashara ya pesa haramu-
hakuna usimamizi wa bidhaa zinazo ingia ndani ya nchi
hatujapata kuwa na mipango kabambe ya maendeleo, aidha kama ipo haijawai tekelezwa. kwa mfano huwezi fikiria uzalishaji wakati hatuna nishati. tena biashara kubwa , ya kulipa na ya kudumu kwa serikali ni kuwekeza kwenye nishati. chaajabu huyu mkuu wa nchi anaita suala la nishati ni "suala la dharula".hakuna nchi duniani imepata kufanya nishati "dharula" isipokuwa tanzania.

tuna wigo finyu wa kukusanya kodi. serikali inaona vyanzo vichache na inavibana vyanzo hivyo hivyo.

kwa hali hii nilitarajia hata nchi itangaze kuwa kuna tatizo watu wajifunge mkanda, lakini mkuu wa nchi na wasaidizi wake wapo kimya kama vile mambo ni shwari. mbaya zaidi wengine wanampa pHD ya sheria eti mkuu ni innovative, hiyo innovation ameitoa wapi kama hawezi kufikiri mambo mapya?. tuna kiongozi anaye hujumu nchi na mustakabali wake. sitarajii uchumi ukuwe wakati wakuu wa nchi wakisikia msiba wote ( raisi , waziri mkuu na makamu) wanakwenda kutoa pole- hii ni manake kuwa hawana cha kufanya ndo maana wanaweza kusanyika mahali pamoja wote watatu, hawa watu siyo wavivu, bali hawajui cha kufanya, hata kusimamia hawajui. raisi ma waziri mkuu wanafunga safari kwenda kumsalimia CEO wa vodafone ( ha hahaha).sasa uchumi utakua vipi?? yaani wakuu wawili wanahamisha ofisi kuongea na CEO wa vodafone?? ni kweli hilo ni kipaumbele???.ni aibu tuamke, ili tuwaamshe hawa wakuu wetu
 
Mkuu, Nimesoma Tanzania katika darasa nilikuwa nakaa chini ya sakafu na kuandika sakafuni. Kaptula ikitoboka na kwa kukaa chini. Sio Kasumba ndugu yangu tunafahamishana Umeuliza Marekani, Ulaya vijana wameajiriwa wapi? Unayajua makampuni ya Kellogs, Dell Monte, Gallo na wengineo wana turnover kiasi gani kila mwaka? Wameajiri watu wangapi kila mwaka andika google utapata majibu yake. Ulaya pia makampuni kama Tesco, Morrissons na wengineo wananunua maziwa, nyama, ngano nk kwa wakulima wakubwa au syndicate ya wakulima wadogo wadogo. Sekta ya Kilimo USA inaajiri karibia watu karibu asilimia 3-4% ya population ya marekani. Na inalingizia wamarekani pato la $ 60 Billion kila mwaka. Ulaya mfano Europe Agriculture inaajiri watu wengi na mwajiri mkuu namba tatu Ulaya. Inaliingizia pato la karibu EUR 64 Billioni kila mwaka. Viwanda ndio vinatoa ajira ila isiwe viwanda tu kwani sio wote katika 70% wanaweza kufanikiwa kupata ajira viwandani. Na ukuaji wa viwanda unategemea na demand and supply of local goods and abroad. Kwa sasa Tanzania inaweza kufaidika na kilimo kwani ndicho kina demand kubwa kuliko Viwanda. 25% ya unemployed graduates ni waliomaliza degree ndugu. Chini ya degree na wasiosoma kabisa wanafikia aslimia 70 ya nguvu kazi hawana ajira na wengi wanakimbilia mijini kama Dar, Arusha, Mwanza na kwengineko.
...Mdondoaji, ndio maana umejipa jina hilo sio!

...Nadhani tunaanza kuelewana sasa. Hoja yangu kuu ni kwamba, hakuna haja ya kupoteza muda na nguvu kubwa kwenye kilimo chetu. Tunachohitaji ni kuboresha mazingira ya uwekezaji -mimi hapa nitasisitiza wa ndani zaidi- mkubwa, kufanya uchunguzi wa kisanyansi, kuondoa vikwazo -kama, wenye mashamba kuwa na hati za umiliki zitakazo wasaidia kukopa- ili kupunguza gharama za uwekezaji wenyewe. Mambo mengine ulishayataja.

...Tukija kwenye ajira, utagundua kuwa wengi wa hao vijana hawana skills za kuwasaidia kupata hizo kazi -elimu ni mhalifu hapa- na hata uchumi wenyewe haujawa na nafasi hiyo, kwa kuwa hausimamiwi vyema.

...Najua unafahamu viwanda vya nguo vinavyoweza kutoa ajira. Unasema ukuaji wa viwanda unahitaji soko kuwapo, sasa, si unafahamu pia, tunaagiza nguo kwa wingi toka nje ya nchi. Hivyo soko lipo, sio? Bidhaa za plastiki na raba na hata vijiti vya kuchokonoa meno na vile vya kuchomea nyama. Hapa si nafasi ya viwanda ipo? Usisahau pia samani za hovyo toka nje, huku tukidumaza mafundi wetu pale keko, n.k.

...Nawafahamu mpaka wakina Cargill na Monsanto na mbegu zao za GMO. Naomba tusijadili GMO kwasasa. Hata hivyo, unafahamu fika kwamba hao "graduate 25%" hawataajiriwa kwenye kilimo na tunazidi kuwafyatua kama matofali. Je, si ni viwanda na biashara ya huduma ndio itakuwa pona yao? Natumaini unafahamu kuwa sekta zilizochangia vizuri ukuaji uchumi ni hizi mbili na ndizo zenye uwezo wa kuchangia maradufu, wakati mchango wa kilimo ukishuka jinsi uchumi unavyokomaa.

...Ndugu, uliyoyasema kwenye mchango wako wa awali ni ya kweli, ila kwenye kilimo naomba tupishane -ki maoni- kama hivi.
 
Yeyote anayeamini kuwa Tanzania inapaswa kukaribisha wageni katika sekta ya kilimo, mbali na uanzishaji wa viwanda vitakavyosindika mazao yetu, hasa matunda na mboga kwa ajili ya uuzwaji nje, anahitaji kuchunguzwa akili zake. Hakuna nchi yeyote ya Asia au Latin Amerika ambayo imeweza kupiga hatua katika maendeleo kwa kutegemea uwekezaji katika kilimo. Na hao wawekezaji ambao tumewakaribisha Tanzania, it is just a matter of time, tutagundua kuwa kumbe ajenda zao ni tofauti na matazamio yetu.
 
Wakati wa ubinafsishaji,mwalimu aliuliza hizi mali za umma zinazogawiwa kwa watu binafsi na nyingine kuuziwa mabepari baada ya 10 percent nk,na ambao hivi sasa wengi wao ndo hawa mafisadi....Mwalimu aliuliza,je mwanachi ambaye na yeye pia ndiyo mali yake,ni kivipi atahakikishiwa kuwa ananufaika na rasilimali hizo?

Wakamjibu kuwa wananchi watakuwa share holders.Na ilisound good kiasi flani lakini mwalimu bado alikuwa skeptical.

Na kama angekuwa yuko familiarised na hayo mambo ya kuhold stocks,basi angejuwa kuwa hiyo bado haina maana kwamba wananchi wanamiliki rasilimali zao.

Kuna hotuba alizungumzia hilo,you had to read btn the lines.Kama sijakosea,nadhani ni ile hotuba ya "Ikulu si pango la wanyang'anyi"
 
Yeyote anayeamini kuwa Tanzania inapaswa kukaribisha wageni katika sekta ya kilimo, mbali na uanzishaji wa viwanda vitakavyosindika mazao yetu, hasa matunda na mboga kwa ajili ya uuzwaji nje, anahitaji kuchunguzwa akili zake. Hakuna nchi yeyote ya Asia au Latin Amerika ambayo imeweza kupiga hatua katika maendeleo kwa kutegemea uwekezaji katika kilimo. Na hao wawekezaji ambao tumewakaribisha Tanzania, it is just a matter of time, tutagundua kuwa kumbe ajenda zao ni tofauti na matazamio yetu.
...Nadhani tuko kwenye mtazamo mmoja wa hili suala.

...Tunapaswa kufahamu kuwa maendeleo ya viwanda ndio huleta maendeleo ya kilimo na si kinyume chake. Mathalani, huwezi zalisha mifugo bora kama hamna mahitaji ya nyama, ngozi, maziwa, n.k kutoka viwandani. Maana, viwanda hivi ndio vitaamrisha hata aina ya teknologia utakayotumia katika kilimo chako, ili, uweze kukidhi viwango na mahitaji.

...Tuna piga pori lisilo katika kutafuta maendeleo ya nchi yetu. Mbaya zaidi, hawa jamaa wanaoitwa wazungu na ndugu zao wanafahamu hili na kuendelea kutushawishi tupotee kabisa.

...Mahesabu rahisi hapa ni kuiga walivyofanya wao huko kwao -tukizingatia mazingira yetu- na hasa kwa kuangalia historia ya maendeleo yao.

...Mdondoaji, unakumbuka ni kisa gani kilichowafanya mababu wa wamarekani wa sasa kupigana vita ya kuuondoa ukoloni wa waingereza? Si ilikuwa kukataliwa kuwa na viwanda bali wao wazalishe malighafi pekee kwa ajili ya viwanda vya nchi ya malkia. Kati ya watu wote Adam Smith akishadadia dhana hii potofu.
 
Swadakta! Kumbe ni interests yetu sote kupiga vita ufisadi kwa nguvu zetu zote kwa sababu unatugusa sisi sote na vizazi vyetu. Lakini twende mbele zaidi maana najua utakuwa na data nyingi zaidi - maswali yangu mengi ni purely theoretical..

a. Dar-es-Salaam inachangia kwa kiasi gani katika GDP ya Tanzania?
b. Dar-es-Salaam inachangia asilimia ngapi ya kodi zinazokusanywa Tanzana?

Mkoa wa Dar ndio unaongoza kwa uchangiaji mkubwa wa uzalishaji nchini partly kwasababu kodi inayotokana na sekta ya huduma nchini. Service sectors including mabenki na biashara occupy almost 50% of country GDP. Agriculture inachangia asilimia 25 au zaidi na Viwanda asilimi 22%. Kilimo kimeporomoka na kuhamia katika huduma.
 
Some few months ago (In April to be precise) I wrote this thread: https://www.jamiiforums.com/hoja-nzito/125963-on-the-brink-what-is-troubling-tanzanian-economy.html

In it I asked these questions:



Na watu wengi walitoa majibu ya kina na mengine ya kudokeza. Leo hii hali ya uchumi inazidi kuwa tete hasa kama factors nyingine zote zikichukuliwa. Kwa mfano hatujui kama lile jengo la serikali lililonunliwa limenunuliwa kwa mkopo au cash na hilo la kutoa kiasi hicho cha fedha kutoka kwa Tanzani kuna athari gani katika uchumi wetu (as far as I know haikununuliwa kwa mkopo - I stand to be corrected).

Sasa katika hali inayoendelea sasa hivi kweli kuna namna yoyote ya kuokoa uchumi au ndio kama wenzentu wanavyosema finally the "the chickens are coming home to roost".

Je ndio wakati wa CCM na serikali yake kujikuta wanalazimishwa kulipa gharama ya sera na utendaji wao? Je ndio wakati ambapo Tanzania hatimaye itajikuta inalazimishwa kulipa gharama ya kuruhusu mfumo wa utawala wa kifisadi? Je, nani ataitwa kuikoa Tanzania endapo uchumi utaanza kuwa vurugu hasa bidhaa za kila siku (vitunguu, nyanya, mikate n.k) zitakapoonekana kuwa ni za juu kuliko uwezo wa watu wetu wengi?
Mzee Mwanakijiji,niliiona hii thread kule kwenye jukwaa la siasa,nikawa siioni tena.Nilitaka nichangie mawili matatu halafu tuone kama yatakuwa yametoa mwangaza wowote kwenye hoja yako hii...

Kwa kifupi nchi yetu ni masikini.Na kwahivyo mara nyingi uncertainity about future value of our domestic currency is always there.

Hilo linasababisha nonfinancial firms, banks pamoja na serikali yenyewe ku issue debt dominated in foreign currency ie US dollars rather than domestic currency.

This leads to decline in the price level. Kwa hiyo unaweza kuona kuwa, kwasababu mikataba ya madeni iko dominated in foreign currency, when the domestic currency declines, the result is that the debt burdens of domestic firms increases.

Na kwasababu ASSETS re typically dominated in domestic currency, balance sheets za hizo firms zita detoriate, pamoja na declination of its networth.

Kwanza kabla hata ya financial institutions kuwa na less resources for lending, bado kuna tatizo kubwa la umeme ambalo lina discourage investments.

Binafsi sijawahi kuamini kwamba uchumi wetu uko hai.

Uchumi wetu una characteristics zote za depression and even more. Yani hakuna hata jina la kuupa.

Kwasababu tuna act kama nchi yetu inaendeshwa kwa viwanda which is not true, kilimo which is also not true. Kwahiyo kufanya analysis inakuwa ngumu.

Ni uchumi "Shaghalabhagala"

Financial crisis yoyote huanzia stage one ambayo ni mismanagemenent of financial liberization.

Hili kwetu limetokea tulipofungua milango kwa wawekezaji. Hii proccess inaitwa "Financial Globalization", ambapo hata mabenki yetu sasa yanaruhusiwa kukopa kukopa kutoka abroad.

Hizi benki zinalipa high interest rates ili kuweza ku attract foreign capital, na hivyo hiyo inapelekea wao kukopa zaidi na zaidi.

Hata hivyo mwisho wake si mzuri kwasababu it leads to banks balance sheets deterioration, hence cutting down on their lending.

Stage ya pili ni currency crisis.

Kutokana na baadhi ya/ama yote endapo yatatokea kwenye stage 1, washiriki wa foreign exchange market wataona kuwa wana opportunity kwani sasa wanaweza kutengeneza faida kubwa sana tu just kwa kutabiri kuwa pesa itashuka thamani hence, stage 2 which is currency crisis

Sasa swali linakuja hapa: ni kivipi detoriation ya banks balance sheets inaweza kusababisha currency crisis?

Ukweli ni kwamba serikali hapa inaogopa kufanya kama alivyofanya Mkapa alipokuwa akijaribu kudhibiti mfumuko wa bei. Kwa kupandisha interest rates.

However, kama serikali itapandisha interest rates, then ina maana the banks must pay more to obtain funds.

Hili in return, linapunguza faida za benki, which may lead to insolvency.

Kwahiyo hapo benki kuu na serikali wako kwenye dilemna, on one hand, kama wakipandisha interest rates too much, basi they will destroy the already weakened banks. On the other hand, if they dont, then they cant maintain the value of their currency.

Na kwajinsi ninavyoona, serikali imeamuwa kufuata policy ya devaluation.

Hilo litawezekana only kama benki kuu ita exhaust holdings of foreign currency reserves.

Wakishaishiwa na resources za ku intervine kwenye foreign exchange market, basi hawana njia zaidi ya ku allow devaluation.

Govt Fiscal imbalances pia ni mojawapo ya factors zinazoweza ku trigger financial crisis, kwasababu zina pelekea kudorora kwa banks balance sheets. Hapa pia fiscal imbalance inaweza ku directly trigger currency crisis.

When govt budget deficits spin out of control, foreign and domestic investors begin to suspect that the country may not be able to pay back its govt debt and so they will start pulling money out of the country and selling the domestic currency, which can eventually collapse it.

Stage ya 3 ambayo ndiyo full fledge financial crisis inatokea mara baada ya mikataba ya madeni sasa majority yake kuwa in foreign currency ie dollar.

Hili linapekea deni letu kuwa kubwa zaidi in terms of domestic currency!

That is it takes more Tz shillings to pay back the dollarized debt! Na kwasababu bidhaa nyingi ziko priced in a domestic currency, then thamani ya makampuni haipandi in terms of tz shillings.

Wakati huo huo hatahivyo, deni linapanda in terms of tz shillings.

This leads to depreciation of domestic currency which in turn increases the value of debt relative to assets, hence the declination of the firms networth. This leads to decline in investments and economic activities. Again, binafsi naamini umeme pia unaplay part let alone hizi facts!

Kwa kifupi kwasababu madeni mengi ya kwetu yanashikiliwa kwa foreign currency kama dola, basi pesa yetu inaposhuka thamani, deni letu nalo linapanda in terms of our domestic currency, huku thamani ya assets ikiwa inabakia pale pale.

Hili mwishowe hupelekea mfumuko wa bei kama mnavyoona kwasasa.

Kwamba Mkullo atasaidia hapo? Ni kutizama tulipojikwaa, tatizo ni serikali yote.

Ni lazima tujuwe kwanza asili matatizo yetu kabla hatujataka kuyatatua.
 
MWKJJ: Naomba kuchangia haya:
Mosi: Kwa mtizamo wangu ni kwamba,Uongozi umepoteza mwelekeo kwa kutotoa vipaumbele katika kuuza nje vitu. Uagizaji wa vitu kutoka nje ni mkubwa kiasi cha kukomba 'akiba' chache tuliyonayo katika hazina yetu.
Pili: Sera mbovu 'political Impunity' na ukosefu wa utashi wa kisiasa: fuatilia kuanzia madini, kuuza nje nyama, samaki n.k. Uratibu katika eneo hili huku ICU na tayari kupelekwa chumba cha maiti 'morgue';
Tatu: Serikali inategemea asilimia zote kukusanya kodi kwa kina pangu pakavu. Hatari ya hili ni kuwa ikitokea 'turmoil' kama ya madaktari wetu basi nachelea kusema serikali yetu itatangazwa 'muflisi' 'bankrupt'
Angalizo:
· Tunashindwaje kuwa kama Botswana kwenye suala la madini?
· Tunashindwaje kuwa kama Rwanda kwenye suala la utashiwa kisiasa na utawala wa sheria?
· Tunashindwaje, kukuza mambo yetu na kuuza bidhaa na si malighafi? Kama Africa Kusini au Korea?
Mwisho: Neno kwa walioko madarakani:
"I cannot give you the formula for success, but I can give you the formula for failure--which is: Try to please everybody '

Herbert Bayard Swope
 
Hakuna serikali inayoendelea bila kukusanya Kodi. Na kuweka malengo ya makusanyo na kubalance kutegemea na Mfumuko wa bei. Hii ni muhimu ukiachilia mbali hayo mengine ya kibenki
 
Sisi na mataifa ya west, ni kama wapenzi ambao kuna mmoja hataki kumwacha mwenzake moja kwa moja kutokana na sababu mbali mbali.
Kutokana na mlolongo wa matukio ya kiuchumi nk, tunaweza kuona kuwa kila kitu kiko planned kwa kudhibiti masoko na ama makoloni nk.

Ndipo hapo tunaweza kugunduwa kuwa hatuwezi kuya fix matatizo yetu bila kuwahusisha hawa west kwasababu tayari wanatudai pesa nyingi sana na kuna makubaliano ya baadhi ya policies kwa kupitia world financial institutions, policies ambazo ukiangalia kwa umakini hazitusaidii bali kutubana zaidi.

Ni shida sana kuona kwamba hatutaweza kutoka kwenye matatizo haya kwasababu tumeshaingia kwenye shimo ambalo kutoka inahitaji almost "kuanza upya" Hatuwezi kuzungumzia kuuneemesha uchumi bila kuingiliwa na masharti ya wale wanaotudai...

Kwanza tujiulize ni kivipi madeni haya yamekuwa mzigo ambao haubebeki?

Kwenye miaka ya sitini, serikali ya marekani ilikuwa ikitumia pesa nyingi kuliko mapato, na hivyo ikaendelea ku print more dollars. Consequently, the dollar depreciated. Mwaka 1973, nchi zinazozalisha mafuta zilipandisha bei zao. Kwahiyo with the scenario that their exports now bought less, and they deposited their huge profits in Western banks.

Interest rates began to plummet and commercial banks mainly "London Club" kwa wakati ule, walianza lavish lending to the Third World without much thought about how the money would be used or whether the recipients had the ability to repay it.Kama hilo halikutosha, baadaye wakaja na biletaral agreements through "Paris Club"
 
Serikali za Dunia ya Tatu zilitake advantage na kuchukua mikopo katika viwango vya chini sana riba kwa sababu fedha hizo ni kweli kwamba zilikuwa zikihitajika kwenye shughuli za kudumisha maendeleo na kukabiliana na adha ya kupanda kwa gharama za mafuta. However ni kiasi kidogo sana cha fedha hizi kiliweza kuwanufaisha wananchi wa kawaida. Kiasi kikubwa kilielekezwa kwenye manunuzi ya vifaa kijeshi ili kuzilinda serikali za kifisadi na kikandamizaji.

Nyingine zilienda kwenye miradi mikubwa ya "maendeleo" ambayo hata hivyo imeonekana kuwa na thamani kidogo kulinganisha hata na pesa zilizotumika.

Rushwa, matumizi yasiyo ya lazima, na uzembe pia viliconsume na bado zinaendelea kuconsume kiasi kikubwa cha mikopo, na hili ni tatizo ambalo bado lipo.

Pia kwakuwa tulitegemea ushauri kutoka nchi za Magharibi, nchi za dunia ya tatu wengi tulianza kupanda mazao ya biashara. Hii ilipelekes "glut" kwenye soko, hence bei kushuka. Wakati riba na bei ya mafuta vilianza kupanda, mauzo ya nje yalizidi kueleta mapato kidogo zaidi na zaidi. Nchi zinazoendelea, ilibidi kukopa fedha zaidi just ili waweze tu kulipa riba.


Mwaka 1982, mataifa mengi ya ulimwengu wa tatu, yaliwaambia wadai wake hawatoweza kulipa madeni yao. Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Benki ya Dunia walijitolea kuprovide mikopo mipya under strict conditions, (you can relate to Mwalimu's back and forth with them) ili kusaidia kulipa riba.

Lakini madeni yalizidi kuongezeka na kukua, na mikopo mipya ndiyo iliyoongezea mzigo zaidi. West hawakutaka kupoteza mikopo yao, hivyo wakaja pamoja na kupata msaada wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa ajili ya mpango wa kuya reschedule madeni.

Tangu wakati huo IMF na Benki ya Dunia - ambazo ni taasisi kuu mbili za kimataifa za fedha - wamekuwa wakihusika katika mikopo ya fedha na rescheduling za madeni katika nchi ambazo hazwezi kulipa riba ya mikopo yao.


Lakini mikopo yao inaongeza mzigo wa madeni na pia ina kuja na masharti. Serikali lazima zikubali kuimpose strict economic programs, kuna ile inayojulikana kama Programu Structural Adjustment (SAPs), hii program ni kwa nchi hizo ili wewezeshwe ku reschedule madeni yao au kukopa fedha zaidi.

SAPs ina measures ama hatua zilizoundwa ili kusaidia nchi kuweza kulipa madeni yake kwa more hard currency, kuongeza mauzo ya nje na kupunguza imports, pamoja na ku promote economic stabilty.

Hii program ya SAPs imeziathiri sana nchi za Afrika kusini mwa Sahara, ambazo chumi zake tayari ni maskini zaidi duniani.

Serikali ili kuweza kutekeleza SAPs, kwa kawaida kinachofanyika ni: kupunguza matumizi kwenye huduma ya afya,(tumeona issues za madakatari na kudorora kwa afya) elimu na huduma za jamii, ku devalue sarafu ya taifa,(hili nilishalizungumzia) kupunguza ruzuku ya chakula, ajira na kukatwa mshahara kwa wafanyakazi wa serikali, na kuhimiza ubinafsishaji wa viwanda vya umma.

Kwa kifupi hata hayo masharti ambayo wanatulazimishia ili tuweze kulipa madeni ukiangalia kwa umakini ndo yanayozidi kutudidimiza, inakuwa kama vile wanatutumia sisi kama pahala pa kufanya majaribisho ya sera kabla hawajazitumia kwao, kwa hiyo tumebakia kuwa genie pigs in almost every aspect of life.
 
Back
Top Bottom