mtuporimtupori
Member
- Mar 24, 2009
- 76
- 14
Kuna swala linanitatiza kidogo naomba wenzangu mnipe maoni yenu.
Mimi na wife tunaenjoy maisha yetu ya kuwa pamoja kwa kama miaka miwili sasa tukiwa huku mwisho wa reli, Kigoma na tumebahatika kupata watoto wawili mapacha, Kabla hatuajaanza uhusiano wetu wife alikuwa tayari ana mtoto wa kike wa kama miaka 12 hivi ambaye alimpata akiwa anasoma sekondari na kwa mujibu wa maelezo yake uhusiano wake na baba wa mtoto kimapenzi uliisha siku nyingi. Hivyo tumekuwa tukiishi na mtoto huyu kama binti yangu wa kumzaa bila kumbagua na anapohitaji kwenda kumsalimia baba yake mzazi (ambaye naye yupo hapa hapa Kigoma) tumekuwa tukimpa nafasi hiyo. Kuna swala moja ambalo limekuwa likinikosesha amani. Baba wa mtoto (ambaye siyo wangu biologically) amekuwa akija au kumtuma dereva wake home kila siku za wiki kumchukua mtoto kumpeleka na kumrudisha kutoka shuleni ambapo awali alikuwa antumia school bus. Nimeshamwambia wife mara kibao kwamba sijisikii vizuri huyu jamaa anapokuja nyumbani kila siku kwa ajili ya mwanae na kwamba ingekuwa bora awe anafuatwa na school bus au wapange kituo cha kukutana na mtoto na siyo nyumbani kwetu kila siku. Mara zote tukiongelea suala hili na wife anakuwa mkali na kuniambia kwamba nasema hivyo kwa kuwa huyo siyo binti yangu wa kumzaa. Kwa kweli nampenda sana mke wangu na nisingependa tuwe tunakwaruzana kwa ajili ya hili.
Hii wenzangu mnaona imekaaje?
Mimi na wife tunaenjoy maisha yetu ya kuwa pamoja kwa kama miaka miwili sasa tukiwa huku mwisho wa reli, Kigoma na tumebahatika kupata watoto wawili mapacha, Kabla hatuajaanza uhusiano wetu wife alikuwa tayari ana mtoto wa kike wa kama miaka 12 hivi ambaye alimpata akiwa anasoma sekondari na kwa mujibu wa maelezo yake uhusiano wake na baba wa mtoto kimapenzi uliisha siku nyingi. Hivyo tumekuwa tukiishi na mtoto huyu kama binti yangu wa kumzaa bila kumbagua na anapohitaji kwenda kumsalimia baba yake mzazi (ambaye naye yupo hapa hapa Kigoma) tumekuwa tukimpa nafasi hiyo. Kuna swala moja ambalo limekuwa likinikosesha amani. Baba wa mtoto (ambaye siyo wangu biologically) amekuwa akija au kumtuma dereva wake home kila siku za wiki kumchukua mtoto kumpeleka na kumrudisha kutoka shuleni ambapo awali alikuwa antumia school bus. Nimeshamwambia wife mara kibao kwamba sijisikii vizuri huyu jamaa anapokuja nyumbani kila siku kwa ajili ya mwanae na kwamba ingekuwa bora awe anafuatwa na school bus au wapange kituo cha kukutana na mtoto na siyo nyumbani kwetu kila siku. Mara zote tukiongelea suala hili na wife anakuwa mkali na kuniambia kwamba nasema hivyo kwa kuwa huyo siyo binti yangu wa kumzaa. Kwa kweli nampenda sana mke wangu na nisingependa tuwe tunakwaruzana kwa ajili ya hili.
Hii wenzangu mnaona imekaaje?