black-tz
Member
- Jul 20, 2021
- 38
- 55
Mambo vipi.
Masela wasome hii watapata kitu
Kuna mwana hapa mtaani ana mwanamke wanaishi pamoja kama miaka miaka mitatu sasa. Wana mtoto mmoja wa miaka miwili. Ila mwanamke alishawai kuwa na mtoto na mtu mwingine kabla ya mchizi.
Ila hawaishi na huyo mtoto yupo kwa bibi ake uswahilini huko
Miaka yote hiyo Mwanamke alikuwa fresh tu ila akaanza mizinguo kama miezi 6 iliyopita. Kuna muda hataki kumpa jamaa tendo, kawa jeuri mpaka anamtukana mchizi sometimes.
Sasa mchizi akawa anaenda kwa ndugu wanasuluhisha haipiti week mambo yanajirudia.
Mwisho wa siku jamaa ikabidi aanze uchunguzi ajue ni nini hasa kinasababisha hayo yote.
Akaja kugundua wife ana simu mbili, moja huwa anaiacha kwa jirani shoga yake wanawasiliana na baba mtoto wake mapenzi motomoto wanataka kurudiana.
Jamaa akamwambia wife aende kwao atamfata azungumze na wazazi wake akaenda zake job. Kurudi usiku kakuta wife kasafisha nyumba kaondoka na kila kitu, mchizi kwenda nyumbani kwao mwanamke hawampi ushirikiano wowote na hawataki arudiane tena na mtoto wao na kaambiwa ata mtoto siyo wake.
Jamaa anapitia wakati mgumu sana ila kaamua tu kuanza moja maisha mengine yaendelee.
Masela wasome hii watapata kitu
Kuna mwana hapa mtaani ana mwanamke wanaishi pamoja kama miaka miaka mitatu sasa. Wana mtoto mmoja wa miaka miwili. Ila mwanamke alishawai kuwa na mtoto na mtu mwingine kabla ya mchizi.
Ila hawaishi na huyo mtoto yupo kwa bibi ake uswahilini huko
Miaka yote hiyo Mwanamke alikuwa fresh tu ila akaanza mizinguo kama miezi 6 iliyopita. Kuna muda hataki kumpa jamaa tendo, kawa jeuri mpaka anamtukana mchizi sometimes.
Sasa mchizi akawa anaenda kwa ndugu wanasuluhisha haipiti week mambo yanajirudia.
Mwisho wa siku jamaa ikabidi aanze uchunguzi ajue ni nini hasa kinasababisha hayo yote.
Akaja kugundua wife ana simu mbili, moja huwa anaiacha kwa jirani shoga yake wanawasiliana na baba mtoto wake mapenzi motomoto wanataka kurudiana.
Jamaa akamwambia wife aende kwao atamfata azungumze na wazazi wake akaenda zake job. Kurudi usiku kakuta wife kasafisha nyumba kaondoka na kila kitu, mchizi kwenda nyumbani kwao mwanamke hawampi ushirikiano wowote na hawataki arudiane tena na mtoto wao na kaambiwa ata mtoto siyo wake.
Jamaa anapitia wakati mgumu sana ila kaamua tu kuanza moja maisha mengine yaendelee.