Kwa miezi miwili sasa kama ukiwa makini kila ukimsikia msemaji wa simba sc ahmed ally akiongea na media utagundua kuwa hayuko serious kabisa na kwa 99%. anachokifanya ni mzaha mwingi pamoja na ukomedi wake ambao wala hauna tija katika suala zima la ufanisi wa timu hasa katika upande wa mawasiliano na mahusiano
Yaani mchezaji akitokea Cameroon tunaambiwa Samuel eti kapendekeza, akitokea ivory coast eti didier drogba kapendekeza, akitokea senegal eti sadio mane kapendekeza na najua kwa sasa anatamani mchezaji atokee ama nigeria au south afrika aseme kuwa akina nwako kanu na ben macarthy ndiyo wamewapendekeza
Ushauri wangu kwa uongozi wa simba sc ni kwamba ianze kutafuta a competent club spokesperson wa kuendana na dunia ya sasa ya ushindani katika masuala mazima ya communication, media, pr and corporate affairs ila siyo kwa huyu ahmed ally kwani hatoshei na naendelea kusisitiza kuwa huyu siyo mwana simba sc 100% kama hata na wale wengine nao ali wao nae hata siyo mwana mafuriko ya vyura kwa 100% kwani hata marafiki na ndugu zake baadhi wameshasema hilo kitambo tu isipokuwa tajiri wa magodoro kachagua kuweka pamba masikioni