Waziri Sitta: Dowans ni genge la ulaji wa vigogo watatu; tusiwalipe!

Huu ni upuuzi kwa sababu zifuatazo:

  1. Angewataja hao watatu kama kweli kachukizwa. Anaogopa nini?
  2. Mkataba wowote unaoingia una kifungu cha migogoro na chombo kitakachohusika kuitatua pale itakapotokea. Kwa mikataba na mashirika ya nje chombo hicho mara nyingi ni ICC ambacho kinaaminika kuwa neutral. Kudai kuwa mahakama zetu zimerukwa ni kuthibitisha ukweli wa uoga wa mashirika ya nje kutumia vyombo vya usuluhishaji vya nchini kwetu. Inaelekea kuwa imani ya Sitta na wengine ni kuwa tungependelewa. Tabia yetu ya kutumia sababu za kisiasa kuvunja mikataba ya kibiashara matokeo yake ndiyo haya. Hapa hatujaonewa bali tunavuna tulichopanda.
  3. Kutolipa faini hii matokeo yake ni mabaya mno maana credibility yetu itaondoka kabisa. Hatutaweza tena kumpata mwekezaji wa maana kuwekeza nchini maana watajua kuwa sisi ni dhulumati.
Amandla.....

nakushangaa, hujamwelewa sitta, ina maana hao majaji walipelekewa ushahidi feki toka humo nchini kwa kuwa mafisadi walisuka na watendaji humo serikalini, ujue kuwa jaji au hakimu hawezi kufanya maamuzi bila kupewa ushahidi na kuwa kama ushahidi ni feki basi na uamunzi ni feki
 
Hapana wajameni,Sitta ni mnafiki tena narudia ni mnafiki,tunakumbuka wote kipindi ambapo hoja hii inajadiliwa bungeni mwanzoni alitoa ushirikiano mzuri sana kwa watanzania na kuwa kinyume na mafisadi,jamahuu hana mshipa wa kiume anapotishiwa kidogo anapoteza muelekeo na kupoteza dira,baada ya kushambuliwa na kamati kuu na kutoa msimamo juu yake kumfukuza alipoteza kabisa muelekeo na kuanza kuzuia hoja hiyo isiingie bungeni kwa kisingizio cha mda na uchunguzi zaidi,nafikiri amekuwa chanzo cha swala hili kufikia hapo,Sitta mim i binafsi sipendi unafiki wako,unapenda uonekane nje kuwa ni mtu unayejali masilahi ya watanzania kumbe moyoni umeyaweka na kukumbatia ubinafsi.

Kumbuka ni kipindi hicho hicho ukatangaza kuhama CCM na kwenda Chadema kupitia viongozi wa juu wa Chadema,ukawa unafanya mazungumzo ya siri mara kwa mara na ndugu yako Mwakyembe,ukifikiri watanzania wachache hatutagundua hilo,hakuna siri ya watu wawili hapa duniani.baada ya kuaidiwa nafasi ukachane nma mpango huo,na mwakyembe nae akasahau kasi yake ya kuondoka CCM, ni baada ya kupata misukosuko ndani ya majimbo ndipo tena ukakumbuka hawa CCM si wema kwako,walipokutoa katika kinyanganyiro cha uspika ukataka kuondoka tena CCM sasa hupo si kutafuta madaraka kwani ungekuwa na moyo wa kuwatumikia wananchi ungefanya kweli?kuna ajenda gani wewe na Mwakyembe amkuletewa ushahidi juu ya Tanesco na Richmond na Dowans,makaratasi hayo hata leo tukija kuyapekua nyumbani kwako tutayakuta.Baada ya kuitwa na JK siku ambayo wanachagua spika na kuwekwa kiti moto na wakuu wa nchi ukashindwa kutoa maamuzi kwasababu tu yakuahidiwa nafasi,leo umepata nafasi ya uwaziri ni nani asiyejua kuwa umepata uwaziri basi tu usilete vurugu,nini kilikuchemsha na kuanzisha CCJ,yote hayo ni uchu wa madaraka,tafadhari nimechoka kuona unafiki wako tena ukiendelea nitaanika uchafu wako hapa JF wakujadili.

Fanya kazi na acha maneno.Wewe nakufananisha na mtoto Zitto mnauma na kupuliza kama panya.
Unazungumzia Sitta kukalia nyaraka za siri za Dowans huku na wewe una siri za Sitta umezikalia kwa hiyo usimlaum mwenzako.
 
Huyu Sitta naye mpuuzi tuu asituchezee akili,alikuwa spika na alikuwa anajua kila kitu na uwezo wa kutumia bunge lake kumalizia hii issue kirahisi sana,seems alikuwa anajua kila kitu lakini hakuwahi kusema lolote la maana au kuwachukulia hatua za kibunge alipokuwa spika maana uwezo huo alikuwa nao,then asichezee watu akili maana huyu mzee ndio alikuwa wa kwanza kuwatukana wapinzani walioleta hii issue bungeni na kuwatishia kuwafukuza na mpaka leo analeta upuuzi wake wa kuongea lugha zake za mtaani eti vigogo fulani (WTF?),huyu mzee ni part ya matatizo ya uongozi wa ile nchi na watu kama hawa must go ndio labda tutaendelea mbele...TZ imepoteza billions and billions kwa ajiri ya wanafiki kama hawa,miaka mitano imepita billions zimepotea na many more zitapotea na hakuna cha umeme wala mitambo ni blah blah tuu,wamekuja na report yao fake lakini lakini mpaka leo no arrest no prosecution sana sana tunazidi kuwalipa tuu,cha ajabu Energy minister ambaye ni mhusika mkubwa na wizara yake ndio kapewa zawadi kuteuliwa kuwa waziri tena....hii serikali ya JK is a big joke na ndio matatizo yote ya ile nchi,and this guy Sitta need to shut up maana he is just another tool ya kufanikisha ufisadi,leo kafanyiziwa in his ambitious za kuwa spika ndio anajidai anakuja na upupu wake eti vigogo watatu...next time chagua CHADEMA!
Koba
Acha hasira baada ya hasira tuambie ni yupi mnafiki mkubwa aliyetuletea mitambo feki na kututia hasara au Sitta anayeropoka.

kwenye bold tuambie ile nchi ni nchi gani......... au wewe si mkazi wa nchi ile ila umetumwa tu kuandika habari zake.
 
Huu ni upuuzi kwa sababu zifuatazo:


3. Kutolipa faini hii matokeo yake ni mabaya mno maana credibility yetu itaondoka kabisa. Hatutaweza tena kumpata mwekezaji wa maana kuwekeza nchini maana watajua kuwa sisi ni dhulumati.


Amandla.....
Wakati na soma kuna mwalimu wangu alikuwa anapenda sana kutumia neno wekiazi kwa wale wanafunzi wake waliokuwa wazito kuelewa.

Nilikuwa na jaribu kutafakariki hivi hawa wa dowans ni wawekezaji au matapeli kama walivyo matapeli wengine? walichowazdii wenzao ni kuwa wao ni matapeli wa kimataifa. Ingekuwa yule mwalimu wangu kasoma hii hoja yako asinge jishauri kukuita we kiazi
 
nakushangaa, hujamwelewa sitta, ina maana hao majaji walipelekewa ushahidi feki toka humo nchini kwa kuwa mafisadi walisuka na watendaji humo serikalini, ujue kuwa jaji au hakimu hawezi kufanya maamuzi bila kupewa ushahidi na kuwa kama ushahidi ni feki basi na uamunzi ni feki

Hivi kweli unaweza ku-appeal kesi kwa kudai kuwa ushahidi ulioletwa na wakili WAKO ni feki? Mahakama yeyote kila siku inaangalia ushahidi uliombele yake na ulioletwa na wanaoshindana au wawakilishi wao. Kama kuna mtu alipeleka ushahidi feki basi jawabu ni kumshughulikia huyo na sio kukataa hukumu. Hapo watakapowashitaki wale wote waliosababisha tushindwe basi ndipo nitakapowaona waona wa maana.

Kwako Lowassa ni mwekezaji wa maana, kama ni hivyo bora tusimpate mwekezaji wa type hiyo.
Ninavyojua mimi kesi imeshinda kampuni ya Dowans na sio Lowassa. Sasa kama una ushahidi kuwa Dowans ndio Lowassa ungeuweka ili wananchi wajue.

Wawekezaji wa maana wanaangalia track record yetu inapokuja kwenye haki ya mwekezaji. Kwa vile track rekodi yetu si ya kujivunia ndiyo maana tunaishia wawekezaji matapeli kama hawa wakina Dowans na City Water. Tunachotakiwa kufanya ni kujifunza kutoka yote haya na kufanyadue diligence tunapoingia kwenye mikataba na kuhakikisha kuwa tunapotaka kuivunja tunafanya hivyo kufuatana na makubaliano yaliyomo kwenye mkataba na si ya kwenye majukwaa ya siasa! Zaidi ya hapo tutaendelea kuliwa tu hata kwenye mahakama zetu wenyewe. Au mmesahau wakina Valambia na yule mwenye petrol station Mwanza? Zote hizo zilisimamiwa na wazungu?

Amandla...........
 
Hizo pesa zitalipwa haraka sana na serikali hilo ni ndili la vigogo lilishapangwa kabla ya uchaguzi.
 
Sitta Mss**ge tena sana tu. Still anatumia ufisadi as a tool kuwa maarufu, insted on eradicating ufisadi. Kwanza taja hayo majina, pili kama unasema wasilipe hizo hela, what are your effin suggestions on what to do next? tatu Dr Rashid (who is so damn competent) aliwaonya wewe na wabunge wenzako kuhusu issue ya Dowans, ukamwona yeye ****--sasa leo ni aje?

Kiukweli, Sitta should not be taken serious kiiivyo.

And kuhusu huu us**nge wa mgao umbao unaboa sana, all I can say is shame on this goverment. They are failing us. Crashing our spirits and dreams. Its 2010 and there is no power, na hili joto. Shame on this government, they are not serious. But people like Sitta who are the root of matatizo and are being wanafki, hao ndio noma zaidi.
 
Sitta Mss**ge tena sana tu. Still anatumia ufisadi as a tool kuwa maarufu, insted on eradicating ufisadi. Kwanza taja hayo majina, pili kama unasema wasilipe hizo hela, what are your effin suggestions on what to do next? tatu Dr Rashid (who is so damn competent) aliwaonya wewe na wabunge wenzako kuhusu issue ya Dowans, ukamwona yeye ****--sasa leo ni aje?

Kiukweli, Sitta should not be taken serious kiiivyo.

And kuhusu huu us**nge wa mgao umbao unaboa sana, all I can say is shame on this goverment. They are failing us. Crashing our spirits and dreams. Its 2010 and there is no power, na hili joto. Shame on this government, they are not serious. But people like Sitta who are the root of matatizo and are being wanafki, hao ndio noma zaidi.

.
Wezi wetu ni serikali yetu, mafisadi wetu ni viongozi wetu, mikataba mibovu ni urithi wa vilaza tulivyovikabizi zamana kwa kufikiri ni wazalendo kumbe ni mumiani yenye tamaa ni kiu ya utajiri haramu kama mbwa na damu. Fikiria kwamba eti richmond ambayo ndio iliyofaulishia mitambo yake kwa dowans ambaye ni yule yule richmond serikali yetu tukutu haikuwa inamfahamu mmiliki ilhali ilikuwa ikimlipa pesa lukuki. Kisa hiki ni sawa na cha kagoda ambacho serikali ilishindwa kumfahamu mmiliki japokuwa ilikiri kupitia rais wetu kuwa pesa za kagoda zilirudishwa. Na kwa ukweli mmiliki wa dowans ndiye yule yule mwizi wa kagoda ambaye rais wetu na serikali yake kwa hili fisadi wamefyata mkia. mh Sitta yupo sahihi na dhamira yake iko hai inamsuta kuwa genge moja na hawa mafya wasio na uruma hata kidogo na umasikini wa watanzania. Mchezo wanaotaka kutuchezea ni sawa kabisa na ule wa kisi ya mauaji ya Zombe. Serikali hii tukutu ikishirikiana na mahakama zake zilizowekwa mifukoni tayari na ufisadi zulizongwa kimaamuzi hata kufikia mahali pa kutoweza kupambanua kati ya dhulma na haki. Sitta tunakuunga mkono na tutaendelea kukuunga mkono japo wewe mwenyewe umeshindwa kutambua kwamba upo katikati ya lundo la samaki waliooza. Wanaokuamulia mahali pa wewe kukaa ama kuondoka. Tunakuombea Mungu akushindie kwani umejichagulia kuwa katika kundi ka watetea haki ambao siku zote kundi kama lako limekua katika mstari mwekundu yaani kujihatarisha wenyewe.
 
KWA HAWA MAFISADI WA DOWANS NA WAFADHILI WAO 'MWENDO WA KUWANYATIA MMOJA BAADA YA MWINGINE, FAMILIA ZAO PAMOJA NA MALI ZAO NDIO JIBU KWETU VIJANA TANGU SASA:

Wenye magendo na nia ya dhati kuendelea kuhujumu uchumi na KUTAFUNA RASILMALI YA TAIFA BILA HURUMA, nadhani siku si nyingi sana Wa-Tanzania tutalazimika kidogo kuweka AMANI yetu kabatini na UTAWALA WA KIJANJA WA SHERIA na kuzipitia baadaye kidogo ili vijana kwanza tukamalizane kiaina na nyie. Hapo adabu itakwepo.

Ndio, nadhani njia pekee tuliobaki nayo ni hii hapa. Hakika, itabidi na familia zenu popote pale walipo nao kama hawaoni kwamba mnafanya KUFURU vitendo vyenu vinatuelekeza kuchukua hatua za makusudi kabisa ili sasa tuanze tu na nyinyi pamoja na familia zenu popote pale mlipo - KWA MWENDO WA KUWANYATIENI BILA YA KELELE ZOZOTE ZA MWIZI MWIZI - halafu matamu yake yatakua fundisho tosha kwa wengine wengi wa aina yenu.

Nyinyi si ni wajanja, na wanasheria wote mnao, taasisi zote muhimu tayari mmezinunua ndani na nje ya nchi sio??????????? Sawa basi!!! Huu ujinga tutaufumbia macho hadi lini. Ole wake mtu atumie sehemu ya KODI YANGU kuwalipeni ninyi MASHETANI WAKUBWA!!!!!!!!!!

Nao wanafamilia zenu wamekataa katakata kuwashaurini kutufanyia taifa letu huu UBAKAJI WA KUTISHA WA AINA HII, OK!!!!!!!!!! Hivi kwanza wanachi mnaowakilishwa na watu kama hawa mnajisikieje????

Kaka nakubaliana na wewe kuhusu kuweka kando dhana ya 'Tanzania ni kisiwa cha amani' kivp tujitwishe kauli mbiu hii ilhali rasilimali mhimu wachache wanahujumu?
Hivi kwanza tujiulize ilikuwaje Sitta atie kapuni suala laRichmond pale Bungeni? Lile lilikuwa jukwaa zuri kwake tena akiwa kama refa kuonyesha uzalendo halisi anaojibebesha kwa Nchi yake
sahzi hana jukwaa tena ambalo litatufanya sisi watanzania kuona live ya kile anchoongea na kukitetea.
Kuwepo ndani ya Baraza la Mawaziri nauhakika hata kama akiraise ishu ngumu kama hii itazimwa juujwaju coz we dont know n we cant see what issues will be resolved upon the consent of the Cabinet of Ministers so Sitta ulishiriki na uliruhusu mazishi ya mjadala wa Richmond make wewe ndiye mhusika mkuu wa kuulizwa.
Jamani twendeni tu msituni tukadai kivingine haki zetu na malekebisho mengi ya utaratibu wa kiutawala Nchini mwetu na hapo ndipo tutapata viongozi halisi na wenye kumwogopa Mungu na Wawekao masrahi ya Taifa mbele.
Tukitumia mfumo huu wa Demokrasia ya kimapokeo wataendelea kuchakachua ili wabaki madarakani.
Hamuoni Ivory Cost yanayotokea?
Hamuoni wenzetu SouthAfrika walivyojikomboa kutoka mikononi mwa Makaburu???
Tuwamulikie kwa tochi ya betrii ngapi ili muone haya??
Tupaze sauti zetu kwa ving'ora ganiili masikio yenu yafunguke?
tutumie mbinu ipi kuwabana mafsadi? Sheria hapana, uwajibishaji hapana mbona EL alijihudhuru na leo hii bado anatuonea?
Tumlilie Mungu hadi lini?
FUNGENI MIKANDA TWENDENI VITANI
SABABU,NIA na KWANINI TWENDE vyote tunavyo.
 
Jasusi ni kweli Valambia hajalipwa, take my words, atalipwa!.
Mikataba iko governed na law of contract, yaani makubaliano ya hiari na kwenye makubaliano hayo lazima kuna kipengele cha iwapo mmoja atashindwa kutekeleza mkataba, nini kilitakiwa kufanyika sambamba na mmoja akiamua kuuvunja mkataba nini kifanyike.

Hizi ni points za kisheria na sio politics. Sitta anataka kuleta tena politics kwenye issue za kisheria. Kwa vile yeye ni mwanasheria, nilitegemea aseme hatulipi kwa hoja za kisheria na sio za kisiasa.

Mimi ni miongoni mwa niliomuunga mkono Zitto pale mwanzo kuwa ama tuzinunue ama tuzitaifishe hizo jenereta za Dowans bila kuchanganya na politics. Sitta na timu yake wakapoliticize kuonekana kuzinunua ni ufisadi, mara PPRA mara ohh.., pure politics!

Ule ulikuwa ni ufa hatukuuziba, sasa tutajenga ukuta.
Nimesisitiza mara nyingi, Tanzania kwa upande wa serikali, hatuna kabisa wanasheria makini, tumejaza watu waliosoma tuu sheria na kupewa vyeti vya LL.B na LL.M lakini hakuna kitu!

Kwa vile hukumu hiyo ya ICC lazima iwe registed mahakama zetu ili iwe applicable kwa Tanzania, serikali yetu na Tanesco bado wanayo nafasi ya kuwatumia wanasheria wa ukweli, wakaiponda ponda hiyo hukumu ya ICC na kuwapatia Watanzania haki yao dhidi ya hiki kiini macho cha Dowans, sio tuu, tusilipe hata senti tano, bali pia tuitafishe hiyo mitambo kwa ku quatify loss Tanzania kama nchi, tuliyoipata kwa Richmond waliposhindwa kutimiza wajibu wao, ambao Dowans ndio wameubeba!.

Wanasheria wengi wa serikali either wana pass au second class lower division. Wale wenye vichwa vikali hawafanyi kazi serikali.
 
Sitta Mss**ge tena sana tu. Still anatumia ufisadi as a tool kuwa maarufu, insted on eradicating ufisadi. Kwanza taja hayo majina, pili kama unasema wasilipe hizo hela, what are your effin suggestions on what to do next? tatu Dr Rashid (who is so damn competent) aliwaonya wewe na wabunge wenzako kuhusu issue ya Dowans, ukamwona yeye ****--sasa leo ni aje?

Kiukweli, Sitta should not be taken serious kiiivyo.

And kuhusu huu us**nge wa mgao umbao unaboa sana, all I can say is shame on this goverment. They are failing us. Crashing our spirits and dreams. Its 2010 and there is no power, na hili joto. Shame on this government, they are not serious. But people like Sitta who are the root of matatizo and are being wanafki, hao ndio noma zaidi.

Mkuu,

Sitta kataja kabisa majina ila gazeti lenyewe ndilo limeyahifadhi
 
if mr Sitta knows who's behind this, then I don't see why he's hesistating to come forward and spell out the beans. Unless he does so, he's a hypocryte!!
 
kuna watu humu siwataji wanamlaum sitta kwa kusemea nje ya baraza la mawaziri yaani angetolea maoni yake ndani ya vikao lakini kwenye sataka la zitto walikuwa wanasema ni uhuru wake kuongea na vyombo vya habari, naomba msiwe ndumilakuwili katika hili naye sitta ana uhuru wa kuongea na vyombo vya habari.

kaka huenda hao ni mojawapo wa mawaziri ambao wanakuja kuangalia tunachowaumbua. Jf ina inforamer wengi kaka
 
hivi mbona tuna uma uma maneno?hawa jamaa watatu si wapigwe risasi wafie mbali?tunaogapana hadi lini?
hivi nchi nzima hamna vijana wa kazi wanaoweza kuwapiga risasi kwa wakati tofauti hawa jamaa tumalize utata?
yaani wana nikera sana.najua familia zao zitajisikia vibaya kwa usemi huu ila no way coz kwenye sheria wanatushinda coz wanatumia pesa zetu kuhonga majaji wenye njaa.
mda ndo huu,jamani tusisubiri yesu ashuke tuwashikishe adamu hawa majambazi.
Majambazi ndo hawa tena NO 1.

 
if mr Sitta knows who's behind this, then I don't see why he's hesistating to come forward and spell out the beans. Unless he does so, he's a hypocryte!![/QUOT
Spill what??????of all tanzania citizens,SITA tu ndo mwanaume aliyejitokeza hata kutoa kaulia,badala ya kumuunga mko tunaleta politics.
Mnataka mwambiwe vip watz,hebu tuingie mtaani mara moja tuwamalize hawa majambazi!
ikibidi wapigiwe NDURU kila wakionekana natuwashambulie hasa.
For sure SITA is the man,he know what is talking!tumunge mkono watz!
 
Huu ni upuuzi kwa sababu zifuatazo:


  1. Angewataja hao watatu kama kweli kachukizwa. Anaogopa nini?
  2. Mkataba wowote unaoingia una kifungu cha migogoro na chombo kitakachohusika kuitatua pale itakapotokea. Kwa mikataba na mashirika ya nje chombo hicho mara nyingi ni ICC ambacho kinaaminika kuwa neutral. Kudai kuwa mahakama zetu zimerukwa ni kuthibitisha ukweli wa uoga wa mashirika ya nje kutumia vyombo vya usuluhishaji vya nchini kwetu. Inaelekea kuwa imani ya Sitta na wengine ni kuwa tungependelewa. Tabia yetu ya kutumia sababu za kisiasa kuvunja mikataba ya kibiashara matokeo yake ndiyo haya. Hapa hatujaonewa bali tunavuna tulichopanda.
  3. Kutolipa faini hii matokeo yake ni mabaya mno maana credibility yetu itaondoka kabisa. Hatutaweza tena kumpata mwekezaji wa maana kuwekeza nchini maana watajua kuwa sisi ni dhulumati.

Amandla.....

Nadhani wewe ni mwana familia wa hawa watu 3.Unataka Sita ataje nini wakati gazeti linasema aliwatajia majina ila kwasababu zao wana withheld.
Umetumwa sio
 
Mimi nataka maisha yazidi kuwa magumu ili next time wawe makini wakati wa kuchagua viongozi.
Maji hakuna (mimi nina kisima changu)
Umeme wa mgawao ( Mimi nimeweka solar power),
Hospitali dawa hakuna ( Mimi nina kadi ya AAR gold),
Walimu na vifaa mashuleni hakuna ( Mwanangu anasoma shule private class)

Wananchi wa hali ya chini tunaowatetea ndiyo hao hao wanaotuangusha kwa kudanganywa danganywa na mafisadi uchwala na ndiyo hao hao kama wakitaka katiba mpya leo lazima itapatikana - siyo sisi tulio maofisni.

Well said brov,they real real irritating me!!!!!
 
Sita ametaja majina ila Gazeti limeficha na kwa kuanza kudadavua mmoja aliyekuwa akipokea malipo ya Richmond ambayo baadaye ilikuwa Dowans ni;
1. Rostam Aziz
2. Andrew Chenge
3. Edward Lowasa
Hao tuchukue hatua sasa.

Ndugu, shukrani sana !!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom