Waziri Mkuu asikitishwa na maazimio ya madaktari

Kauli hii sio kweli sana Matola. Hebu nielimishe kidogo kuhusu yafuatayo:
-Uhusiano wa mojakwamoja wa kikazi kati ya madaktari hawa na waziri wa afya au naibu wake.
-Waziri na naibu wake kwa upande mmoja na madaktari upande mwingine na kati yao kuna wagonjwa wanaohitaji huduma.
-Kama leo hii madaktari wakifanikiwa kushinikiza waziri aondoke au aondolewe kesho watashindwa kufanya hivo kwa WAZIRIMKUU, RAIS?
-Hili shinikizo limekaa KITAALUMA kweli?
-MaDaktari wanatumiwa au kutumika kisiasa? Wanawaumiza WATANZANIA masikini kwa kuwa Dr Mponda hataki kung'oka?
-Ni taaluma hii peke yake iliyonyeti nchi hii? Polisi, DAWASCO, TANESCO, TRA,..., wakigoma kwa staili na mtindo huu je?
Namwomba Rais wetu asiyaendekeze haya. Tuchukue madaktari kutoka Cuba, China au kungineko kwa gharama yoyote ile.
jaribu kupitia post zote za thread hii utapata majibu, fuatilia na thread "jk awekwa kikaangoni na ma dr."
 
Msamiati wa kujiuzuru kiongozi inapoonekana ameharibu kwa nchi hii haupo labda kwa viongozi wengine mbali na hawa tulionao leo hii. I strongly support our doctors regardless of the effects on citizen.

Ikifika j5 hakijaeleweka wekeni tools down mpaka serikali ishike adabu iache tabia ya kudharau wanataaluma
 
Naomba nikujibu tu kwa kifupi, ni kwamba hawa maziri ndio chanzo cha mgogoro huu kufikia hapa ulipo, hili swala lilikuwa ndani ya uwezo wao na kama una kumbukumbu nzuri ni kwamba chokochoko ziliznzia kwa Interns Doctors, swali kwako je ni kweli Serikali haikuwa napesa za kuwalipa posho zao Interns Doctors?
Pili siku zote kuna CONFLICT RESOLUTION je unawezaje kukaa meza moja kusuruhisha tatizo hili meza moja na watu wale wale waliowapuuza Madaktari na kuipotosha Serikari?

Mkuu Waberoya binafsi mimi nilikuwa muhanga wa mgomo ule, Namuuguza mama yangu mzazi huu sasa ni mwezi wa pili, nashukuru Mungu ameshafanyiwa oparesheni pale MOI lakini bado anahudhuria clinic, ni mpumbavu tu peke yake anayeweza kuwapuuza Madaktari, otherwise labda neno hospital uwe unalisoma tu kwenye keyboard.
I strong support our doctors regardless i be will among of victims.
Sijui kama unaniita Waberoya kwa bahati mbaya au makusudi tu! Sio lazima maDaktari wetu hawa waliosoma kwa kodi zetu nyingi waendelee kututesa eti kwa kuwa hawataki maDaktari wenzao kuongoza wizara ile. Jambo hili linakera ingawa umesema ni mpumbavu anayeweza kuwapuuza jamaa hawa. Ngoja mimi niwe MPUMBAVU wa kwanza kuwapuuza kwenye hoja hii endapo kweli watagoma kwa sababu hii peke yake.
MaDaktari wetu watuambie kama serikali imewalazimisha kuongea na akina Dr Mponda. Watuambie pia ni dai lipi jingine ambalo ni la kitaaluma au kimaslahi ambalo serikali imelipuuza. Hatuwezi kuiburuza serikali kwa mtindo huu kwa sababu ya unyeti wa taaluma zetu. Hatuna malaika nchi hii hasa katika UONGOZI. Tukubali kurekebishana, kukosoana na kuombana radhi kiungwana na kwa staha.
Matatizo yaliyoko kwenye sekta ya AFYA sio makubwa kuliko yaliyoko kwenye sekta ya ELIMU, USAFIRI na USAFIRISHAJI, UMASIKINI wa watu wetu, MAJI,...
 
mkuu WildCard kwa uelewa wangu madaktari ukiondoa wale wanaolipiwa ada na wazazi/walezi/wafadhili wanaobakia wanasomeshwa kwa pesa za mkopo wa serikali. Wanalipia hii mikopo pindi wakimaliza chuo na kuanza kufanya kazi. Kwa hiyo hakuna anayesomeshwa bure kwa kodi za wananchi.
 
Mura, vita mbere mura.

La sasa kali nina baba mdogo amelazwa hapo muhimbili
sijui hili kasheshe litakuwaje, naomba 'Ikiwa ni mapenzi yako
Baba kikombe hiki kiniepuke'
 
Sijui kama unaniita Waberoya kwa bahati mbaya au makusudi tu! Sio lazima maDaktari wetu hawa waliosoma kwa kodi zetu nyingi waendelee kututesa eti kwa kuwa hawataki maDaktari wenzao kuongoza wizara ile. Jambo hili linakera ingawa umesema ni mpumbavu anayeweza kuwapuuza jamaa hawa. Ngoja mimi niwe MPUMBAVU wa kwanza kuwapuuza kwenye hoja hii endapo kweli watagoma kwa sababu hii peke yake.
MaDaktari wetu watuambie kama serikali imewalazimisha kuongea na akina Dr Mponda. Watuambie pia ni dai lipi jingine ambalo ni la kitaaluma au kimaslahi ambalo serikali imelipuuza. Hatuwezi kuiburuza serikali kwa mtindo huu kwa sababu ya unyeti wa taaluma zetu. Hatuna malaika nchi hii hasa katika UONGOZI. Tukubali kurekebishana, kukosoana na kuombana radhi kiungwana na kwa staha.
Matatizo yaliyoko kwenye sekta ya AFYA sio makubwa kuliko yaliyoko kwenye sekta ya ELIMU, USAFIRI na USAFIRISHAJI, UMASIKINI wa watu wetu, MAJI,...

WildCard, sikuwa napenda kuchangia kwenye thread hii, lakini maoni yako yamenilazimisha. Mchango wangu ni kuwa
(1) Nashukuru umekubali kuwa wewe ni MPUMBAVU wa kwanza, na mimi nasema ni sahihi.

(2) Mawazo yako yanapendekeza kuwa madaktari wetu wanyamaze baada ya kupewa kitu kidogo ili kuridhisha madai yao. Hili kweli ni pendekezo la MPUMBAVU. Hili ndiyo linalopelekea kuwa na viongozi kama Kikwete aliyeshindwa ila kwa kuahidi kitu kidogo hata yasiyowezekana. Haiwezekani kukubali kuridhishwa kwa posho kidogo ili kuwavumilia na kuwakubali viongozi vipofu wasimamie wa-Tanzania wote. Haiwezekani kutumikia wa-Tz wote ukiwa chini ya viongozi fisadi, waongo, wasio serious, wasio na uwezo na wewe ukaridhika na kujituma wakati ukijuwa hakuna vision na hakuna sustainability ya ahadi zao.

(3)Unasema hatuwezi kuiburuza serikali kwa mtindo huu kwasababu ya unyeti wa taaluma. Hili nalo nasema ni wazo la MPUMBAVU wa kwanza. Serikali za watu makini zimeburuzwa na kuleta matumaini mapya, wewe unataka kutupumbaza zaidi kuliko hata upumbavu wako. Angalia huko Ugiriki, serikali imeburuzwa hadi Kiongozi wao akajiuzuru, angalia huko Italia serikali iliburuzwa na Waziri Mkuu yule mzinzi akajiuzuru, mifano ipo mingi na watu waliziburuza serikali zao ili kuleta matumaini mapya wanayohitaji. Madakatri wanasitahili kuungwa mkono katika msimamo wao dhidi ya Uongozi wao unaolindwa na serikali dhalimu ya Kikwete.

(4) Nakubali hatuna viongozi malaika ... tunaweza kuwasamehe katika makosa yao. Lakini makosa ya makusudi, Waziri anatenda kazi kama hakwenda shule. Anatowa maelezo ndani ya Bunge na kupindisha ukweli hadi kufikia hata Bunge linawacha kumwamini na kulazimika kuunda tume ya kufanya uchunguzi..huyo siyo kiongozi na amevuka mipaka ya kiongozi wa kuvumiliwa. Madaktari waungwe mkono. Naamini kwa maelezo yangu upumbavu wako sasa umepungua na unaweza kuukubali ukweli ...
 
Sijui kama unaniita Waberoya kwa bahati mbaya au makusudi tu! Sio lazima maDaktari wetu hawa waliosoma kwa kodi zetu nyingi waendelee kututesa eti kwa kuwa hawataki maDaktari wenzao kuongoza wizara ile. Jambo hili linakera ingawa umesema ni mpumbavu anayeweza kuwapuuza jamaa hawa. Ngoja mimi niwe MPUMBAVU wa kwanza kuwapuuza kwenye hoja hii endapo kweli watagoma kwa sababu hii peke yake.
MaDaktari wetu watuambie kama serikali imewalazimisha kuongea na akina Dr Mponda. Watuambie pia ni dai lipi jingine ambalo ni la kitaaluma au kimaslahi ambalo serikali imelipuuza. Hatuwezi kuiburuza serikali kwa mtindo huu kwa sababu ya unyeti wa taaluma zetu. Hatuna malaika nchi hii hasa katika UONGOZI. Tukubali kurekebishana, kukosoana na kuombana radhi kiungwana na kwa staha.
Matatizo yaliyoko kwenye sekta ya AFYA sio makubwa kuliko yaliyoko kwenye sekta ya ELIMU, USAFIRI na USAFIRISHAJI, UMASIKINI wa watu wetu, MAJI,...



Sio kweli kuwa madaktari hawa wamesomeshwa kwa kodi za watanzania bure, bali wamekopeshwa na ndio maana kama sehemu ya propaganda serikali kupitia asasi zake na baadhi ya redio walitoa majina ya wadaiwa wa mikopo na madaktari walikuwepo, au hukuona jina la Salama Kikwete?


Sio kweli kuwa madaktari hawataki kuongozwa na madaktari wenzao, kwani dr Mwinyi hakuongoza hiyo wizara, waziri aliyepita je? Hivi Mponda ni MD , mbona alishindwa tofautisha intern dr na mwanafunzi wa md? Tuacheni kutetea ujinga, watu twataka watu wadelive na si siasa na undugunization au ushoganization.
 
ndugu zangu madai ya madaktari yanatugusa sisi sote moja kwa moja na ni lazima tuoneshe kuwaunga mkono dhidi ya watawala wetu waovu na wasiosikia
 
Ili kuepusha mgogoro zaidi ktk sakata hili la madai ya madaktari versus govt ni bora ikiwa Mawaziri hao wataondolewa for the sake of public interest, otherwise mgomo utaathiri sana maisha ya watz...!!
 
WildCard, sikuwa napenda kuchangia kwenye thread hii, lakini maoni yako yamenilazimisha. Mchango wangu ni kuwa
(1) Nashukuru umekubali kuwa wewe ni MPUMBAVU wa kwanza, na mimi nasema ni sahihi.

(2) Mawazo yako yanapendekeza kuwa madaktari wetu wanyamaze baada ya kupewa kitu kidogo ili kuridhisha madai yao. Hili kweli ni pendekezo la MPUMBAVU. Hili ndiyo linalopelekea kuwa na viongozi kama Kikwete aliyeshindwa ila kwa kuahidi kitu kidogo hata yasiyowezekana. Haiwezekani kukubali kuridhishwa kwa posho kidogo ili kuwavumilia na kuwakubali viongozi vipofu wasimamie wa-Tanzania wote. Haiwezekani kutumikia wa-Tz wote ukiwa chini ya viongozi fisadi, waongo, wasio serious, wasio na uwezo na wewe ukaridhika na kujituma wakati ukijuwa hakuna vision na hakuna sustainability ya ahadi zao.

(3)Unasema hatuwezi kuiburuza serikali kwa mtindo huu kwasababu ya unyeti wa taaluma. Hili nalo nasema ni wazo la MPUMBAVU wa kwanza. Serikali za watu makini zimeburuzwa na kuleta matumaini mapya, wewe unataka kutupumbaza zaidi kuliko hata upumbavu wako. Angalia huko Ugiriki, serikali imeburuzwa hadi Kiongozi wao akajiuzuru, angalia huko Italia serikali iliburuzwa na Waziri Mkuu yule mzinzi akajiuzuru, mifano ipo mingi na watu waliziburuza serikali zao ili kuleta matumaini mapya wanayohitaji. Madakatri wanasitahili kuungwa mkono katika msimamo wao dhidi ya Uongozi wao unaolindwa na serikali dhalimu ya Kikwete.

(4) Nakubali hatuna viongozi malaika ... tunaweza kuwasamehe katika makosa yao. Lakini makosa ya makusudi, Waziri anatenda kazi kama hakwenda shule. Anatowa maelezo ndani ya Bunge na kupindisha ukweli hadi kufikia hata Bunge linawacha kumwamini na kulazimika kuunda tume ya kufanya uchunguzi..huyo siyo kiongozi na amevuka mipaka ya kiongozi wa kuvumiliwa. Madaktari waungwe mkono. Naamini kwa maelezo yangu upumbavu wako sasa umepungua na unaweza kuukubali ukweli ...
Wengi mnaochagiza mgomo huu mna namna nyingine kujitibu mkiugua. Mna haki ya kuwaunga mkono hawa madaktari wanaoingiza SIASA kwenye TAALUMA yao nyeti. Kama kila kosa watu watatakiwa kuondoka sijui kama Rais atapata muda wa kufanyakazi zingine za URAIS mbali na kuteua na kuapisha kila uchao!
Madaktari wamelundikwa kwa wingi mno kwenye hospitali za serikali hapa Dar. Ndio maana wanapata muda wa kuyafanya haya yanayoendelea. Hospitali mikoani hazina madaktari. Vituo vya AFYA nchi nzima ni vichache mno vyanye Daktari angalau mmoja.
Serikali ulizozitaja kuburuzwa hazikuburuzwa kwa kutumia TAALUMA. Nyingi zimeburuzwa na WANANCHI wa KAWAIDA sana. Tena wengine WAMACHINGA kabisa kama yule kijana wa Tunisia aliyeanzisha mapinduzi ya nchi zote za KIARABU. Namwomba JMK aangalie uwezekano wa kuleta maDaktari kutoka Cuba, China,...,kwa gharama yoyote ile endapo maDaktari hawa WANASIASA wa TANZANIA wataendelea kutimiza azma yao hii ya kitoto.
 
Kweli nimemwamini baadhi ya maneno mabaya tunayosemwa na watu wa mataifa ya nje. Ukifatilia comments za wachangiaji (mchangiaji: Linda Croucher) kufuatia Kongamano la kiuchumi lililofanyika Davos, Switzalnd (http://www.guardian.co.uk/business/2012/jan/26/davos-2012-day-2?commentpage=all#start-of-comments) Linda Croucher alibainisha kuwa tatizo si viongozi, bali ni wale wanaochagua viongozi. Hivyo inaonyesha wengi wetu hatujui kiongozi bora ni nani na tunampata vipi. Baada ya kusoma hii thread, nimeona watu wengi wakiwalaumu Madaktari. Inawezekana wanafanya kishabiki tu, ama hawaelewi kwanini tatizo hili lipo na limefikia hapa. Haiingii akilini mtu kuanza kuwashutumu madaktari wakati madai yao ni ya msingi na ni kwa faida ya wateja wao (ambao ni sisi wananchi). Inaelekea baadhi yetu hatupendi kufuatilia mambo kwa undani. Inakuwaje Kiongozi mkuu wa serikali alaani maovu yaliyofanywa na viongozi wa wizara husika na kuhaidi kuwashughulikia ndani ya kipindi flani. Baada ya huo muda kufika anaanza kusikitika bila kuchukua hatua za msingi walizokubaliana awali. Hapa wanaotaka kuleta maafa si madaktari, bali ni viongozi tuliowachagua wenyewe. Nimepata taarifa kuwa tayari Madaktari wengi wameshakimbia nchi, nafikiri serikali inatambua hili nakuliachilia bila kurekebisha mazingira yaliyo chini ya uwezo wake. Madaktari wengi wanakimbilia Botswana, na ukiangalia uwiano wa Daktari kwa wagonjwa Botswana ni 1:2500 (wakiwamo madaktari wa kitanzania) wakati wanazalisha madaktari wachache sana, wakati Tanzania ni nchi ya mwisho Afrika kwa uwiano wa Daktari na anaotarajia kuwapa huduma (1:50,000). Hivyo ni wazi kabisa serikali hii haijali kabisa maswala ya afya ya wananchi kwani imekuwa inaleta maelezo kuliko votendo katika utekelezaji wa sera za afya. Pia kulingana na utekelezaji mbovu wa sera ya Afya, kumekuwa na vifao vya wajawazito, watoto na magonjwa mengi vinavyoweza kuzuilika. Sasa Madaktari husika wanapolisimamia hili kwa taaluma na dhamana waliyonayo, inatokea watu na viongozi kuwapinga na kuwaona ni wao ndiyo wauwaji. Nikwanini tusiwapigie kelele hawa viongozi wazembe wanaotumia nguvu kubwa kupotosha umma na kukaidi makusudi kushughulikia kwa haraka matatizo ambayo yapo chini ya uwezo wao ili tuweze kuboresha afya ya jamii yetu. Nimesikitika sana kwa jinsi serikali inavyolishughulikia hili swala nyeti kimzahamzaha.
 
Serikali isiyosikivu ya CCM....ni bora kuwalinda watu wawili wazembe kuliko kuokoa watanzania zaidi mil.40 watakoenda kuangaika na wengine kuangamia.
 
kwani madaktari wanadai maslahi yao au wanachodai ni Mawaziri wajiuzulu? Mbona hawaeleweki, wamekuwa wanasiasa?

Madaktari wanaeleweka ila wewe ndiyo huelewi kwa sababu ama hutaki kuelewa, ama ni mbumbumbu au yote mawili. Unashindwa kutofautisha kati ya kudai haki na kufanya siasa. Wanasiasa ndio walioahidi kutekeleza madai ya madaktari, sasa unataka wamdai nani? Wakati wanaahidi, walidhani madaktari ni taahira watasahau, sasa watawala mimacho inawatoka, hawana ubavu wa kutishia kuwafuta kazi. Kwanini wasitumie uungwana wa kukubali matokeo kwamba serikali haina uwezo wa kutekeleza madai yao? Acha chezea daktari taumia sasa. Mwalimu ya shule ya kata iko chezea kichwa ya mtoto ya shule, dokta iko weza nyang'anya roho yako kitaka wakati yoyote.

 
Ni muhimu hao mawaziri waondoke kwanza ndipo majadiliano yaendelee. Tokea mwanzo wizara haikuwa tayari kuyashughulikia matatizo ya madaktari na ushahidi ni taarifa ya Mponda Bungeni. HAKUWA NA NIA YA KUHANGAIKIA MADAI YAO. Hivyo ni vigumu kujadiliana na mtu asiye na nia ya kuwasaidia.

Mkuu asante hapo umewasaidia wagumu wa kuelewa .. ciao
 
Wengi mnaochagiza mgomo huu mna namna nyingine kujitibu mkiugua. Mna haki ya kuwaunga mkono hawa madaktari wanaoingiza SIASA kwenye TAALUMA yao nyeti. Kama kila kosa watu watatakiwa kuondoka sijui kama Rais atapata muda wa kufanyakazi zingine za URAIS mbali na kuteua na kuapisha kila uchao!
Madaktari wamelundikwa kwa wingi mno kwenye hospitali za serikali hapa Dar. Ndio maana wanapata muda wa kuyafanya haya yanayoendelea. Hospitali mikoani hazina madaktari. Vituo vya AFYA nchi nzima ni vichache mno vyanye Daktari angalau mmoja.

Serikali ulizozitaja kuburuzwa hazikuburuzwa kwa kutumia TAALUMA. Nyingi zimeburuzwa na WANANCHI wa KAWAIDA sana. Tena wengine WAMACHINGA kabisa kama yule kijana wa Tunisia aliyeanzisha mapinduzi ya nchi zote za KIARABU. Namwomba JMK aangalie uwezekano wa kuleta maDaktari kutoka Cuba, China,...,kwa gharama yoyote ile endapo maDaktari hawa WANASIASA wa TANZANIA wataendelea kutimiza azma yao hii ya kitoto.

Kwa maelezo yako hayo (bolded) sasa nimekubali jina ulilopewa na wewe ukakubali kwa furaha bado linakufaa
Sina zaidi ya kueleza isipokuwa kukutakia maisha marefu ya kuvuta hewa ya bure, na uhuru wa kuishi bure ... kwa sababu sasa nimeelewa si kila bin-Adam anayeishi anao ufaham wa kwa nini anaishi, na nini kinampasa kwa jamii, nini jamii yake inastahili, na kadhalika
 
Kufuatia kikao cha madaktari kilichoazimia kuendelea na mgomo waliousitisha ifikapo jumatano (7/03/2012) kwa kutotekelezwa baadhi ya makubalionao walioafikiana na serikali chini ya Waziri mkuu Mizengo Pinda.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema amesikitishwa na tishio hilo akisema kwa sasa Serikali ipo katika mchakato wa utekelezaji wa makubaliano mbalimbali na wanataaluma hao.


Source: Mwananchi 5/03/2012

Swali la msingi:

Ni kweli serikali imeshindwa kuendelea na mchakato huo wakati ikiwa imewawajibisha Mawaziri husika kama walivyokubaliana? Kwananmna hiyo basi, mawaziri hawa waliopelekea matatizo yaliyo pita watakuwa wanashiriki katika mchakato huo ambapo Madaktari na sisi wananchi tukiwa hatuna imani na viongozi hao. Inatuwia vigumu sana kuona Mh. Pinda unasikitishwa na maazimio ya Madaktari mlioafikiana awali.

Kwani muda walioafikiana si umekwisha pita? Kwanini yeye aliafiki muda ambao dhahiri anajua serikali haitoweza kuutimiza, alifikiri kutumia siasa ktk nyanja nyingine ni jambo la kumaliza matatizo? Basi mwaache yamkute
 
Msamiati wa kujiuzuru kiongozi inapoonekana ameharibu kwa nchi hii haupo labda kwa viongozi wengine mbali na hawa tulionao leo hii. I strongly support our doctors regardless of the effects on citizen.

Ikifika j5 hakijaeleweka wekeni tools down mpaka serikali ishike adabu iache tabia ya kudharau wanataaluma

Adabu tutaishika sisi wananchi wenyewe na siyo viongozi wa serikali
 
Sijui kama unaniita Waberoya kwa bahati mbaya au makusudi tu! Sio lazima maDaktari wetu hawa waliosoma kwa kodi zetu nyingi waendelee kututesa eti kwa kuwa hawataki maDaktari wenzao kuongoza wizara ile. Jambo hili linakera ingawa umesema ni mpumbavu anayeweza kuwapuuza jamaa hawa. Ngoja mimi niwe MPUMBAVU wa kwanza kuwapuuza kwenye hoja hii endapo kweli watagoma kwa sababu hii peke yake.
MaDaktari wetu watuambie kama serikali imewalazimisha kuongea na akina Dr Mponda. Watuambie pia ni dai lipi jingine ambalo ni la kitaaluma au kimaslahi ambalo serikali imelipuuza. Hatuwezi kuiburuza serikali kwa mtindo huu kwa sababu ya unyeti wa taaluma zetu. Hatuna malaika nchi hii hasa katika UONGOZI. Tukubali kurekebishana, kukosoana na kuombana radhi kiungwana na kwa staha.
Matatizo yaliyoko kwenye sekta ya AFYA sio makubwa kuliko yaliyoko kwenye sekta ya ELIMU, USAFIRI na USAFIRISHAJI, UMASIKINI wa watu wetu, MAJI,...

ujue mgomo wenyewe kwa upande mmoja una faida kwetu na upande mwingine una hasara ambayo 2tawapoteza wagonjwa walio wengi na faida ni kuwepo kwa vipimo ambavyo tutaweza kupimwa kwa bei nzuri ambayo itakuwa angalao kwa waTZ walio wengi wanaweza kulipa, hivi kwani ni kweli serikali wameshindwa kununua hivyo vifaa?
 
pinda amepinda, na hata maneno yake yamepinda,
jana nilicheka nilivyocheki kibonzo cha wiki mlimani TV, pinda anahutubia kuhusu matumizi bora ya lugha ya kiswahili bila hata aibu anaongea kiswanglish, PINDA KAPINDA NA KAULI ZAKE ZIMEPINDA. nchi inaongozwa na magazeti siku nyingi, hatuna viongozi wenye kauli mda mrefu sana.

magufuli na Mwandri wapo.sio wote
 
Back
Top Bottom