Waziri Membe aitabiria ushindi CHADEMA uchaguzi mkuu ujao

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Waziri wa mambo ya nje Bernard Membe amekitabiria ushindi chama cha Demokrasia na maendeleo-CDM katika uchaguzi mkuu unaokuja.

Waziri Membe amesema chama cha CDM kimetokea kupendwa na wananchi katika kila kona ya nchi na hata operesheni yao ya kusini imekitikisa chama tawala.

Waziri Membe aliyasema hayo katika chakula cha mchana alichowaandalia viongozi wa CDM nyumbani kwake waliokuwa katika jimbo lake la Mtama.

Viongozi hao ni mjumbe wa kamati kuu Godbless Lema,kamanda James Millya na viongozi wakuu waandamizi.

Waziri Membe aliwaambia viongozi hao ameishi nchi mbalimbali duniani zenye demokrasia ya hali ya juu hivyo hatashangazwa hata kidogo CDM kuingia Ikulu.

Kuhusu kesi iliyotengua ubunge Lema waziri Membe amedai kushtushwa na kusema kwa vile amekata rufaa anaamini mahakama ya rufaa itamrejeshea ubunge wake.


Source:
Mtanzania Jumapili.

Updates......
Katika taarifa ya habari ITV saa mbili usiku waziri Membe ameonyeshwa akiwakaribisha viongozi wa CDM nyumbani kwake kijijini Jimboni Mtama na kukaririwa akiwashutumu wabunge wanaolalamika kuvamiwa na CDM majimboni mwao katika vuguvugu la M4C.

Membe amesema wabunge hao hawajui ni nini maana ya siasa ya vyama vingi.
 
Waziri Membe aliyasema hayo katika chakula cha mchana alichowaandalia viongozi wa CDM nyumbani kwake waliokuwa katika jimbo lake la Mtama.

Tunamkaribisha kwenye M4C
Inanikumbusha enzi za professa mkuu wa Siasa huko Kwa watani wetu Kenya. Enzi hizo ukikaribishwa ugali, jioni nyumbani kwa Rais Moi, kinachofuata ni kuhama chama.

Sasa masikio yetu yapo juu juu , je ni lini BENARD MEMBE atahamia chadema?????

Stay tuned and let's take a political break as opposed to a commercial break.
 
Hatuna sababu ya kumshambulia Benard Membe, hakuna mtu anayekuwa mtenda dhambi wa milele, isipokuwa shetwani! Ameongea maneno yenye upako wa Mungu, tuyaheshimu na kuyafanyia kazi kwa tahadhali ya hali ya juu. Ubarikiwe Membe.
 
Ccm wanajua hila ya jk, wanajua 2015 hapatoshi wamebaki kufanya mipasho bora membe amesaliti amri.
 
Hakuna cha unafiki hapo ndugu. Siasa si uadui, Chama kimoja kinatawala leo kesho kinatawala kingine.

Ni kweli mkuu tusimshambulie.Membe amesema ukweli hata kama unauma kwa chama chake
 
Hatuna sababu ya kumshambulia Benard Membe, hakuna mtu anayekuwa mtenda dhambi wa milele, isipokuwa shetwani! Ameongea maneno yenye upako wa Mungu, tuyaheshimu na kuyafanyia kazi kwa tahadhali ya hali ya juu. Ubarikiwe Membe.

Tunasubiri kauli ya Nape kwa.matamshi haya ya Membe
 
Kama kweli amefanya hivyo, basi ni mtu mkweli asiyetaka kuficha ukweli kwa mgongo wa kukipendezesha chama kinachoshindwa kuangalia maslahi ya umma. Ubinafsi mpaka kwenye masaburi.
 
Membe ameongea yaliyo moyoni kwake. Pia, ameonyesha busara. Hata Maige ameshatoa kauli kama hii zaidi ya mara 1. Mwendawazimu Nepi ndio amebaki kichwa ngumu.
 
Wana CCM wote wanatambua kuwa CHADEMA inachukua dola 2015,lakini ni wanaCCM wachache wanaoweza kutamka hili japo moyo wanajua ukweli!wengine wanashindwa kutamka kwa kuhofia ugali wao,wengine kuhofia posho.ROHO I RADHI,LAKINI MWILI NI DHAIFU
 
MH, Membe ni mwana siasa aliyekomaa kama amewakaribisha wapinzani wake katika chakula na kuongea hivo tutegemee makubwa hapa katikati kabla ya 2015
 
Akiiona Nape hii anazimia!!
Utamsikia akiny** mdomoni "wanaokisariti chama cha mapinduzi wawajibishwe!!" Subirini muone...!
 
Membe we ni shujaa kwa kusema ukweli japo wengine roho zinawauma but no way out, sema tu bro.
 
Back
Top Bottom