Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
HATUTAKI TENA KUBURUZWA: WASEMA WAZANZIBAR
Katika ukumbi wa salama Hall, hoteli ya Bwawani mjini zanzibar, kamati ya bunge ya katiba na sheria inayoratibu maoni juu ya mswada wa sheria ya kuandaa utaratibu wa kupata maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya, imechachafywa vikali na wazanzibar wakiwamo wawakilishi, wanasiasa, wanazuoni , wanasheria na wadau mbali mbali visiwani humo.
Hali ilikuwa mbaya kwa tume hiyo iliyoitisha mkutano huo kwa taarifa za haraka haraka, baada ya Mh. Samuel Sitta, kutoa mawasilisho ya mswada huo. Mchangiaaji wa kwanza alikuwa Mh. Hamza Hassan Juma, mwakilishi wa jimbo la Kwamtipura ambaye aliitaka tume hiyo irudi na mswada huo kwa vile Zanzibar haikushirikishwa chochote katika kuuandaa hadi ulivyo sasa.
Huku ukumbi wote ukiwa na hamasa hasa pale aliposimama mwanasheria mkuu wa serikali ya Mapinduzi ya zanzibar bw. Othman Masoud Othman, aliposema kuwa mbali na mswada huo, bunge la Muungano halina Mandate ya kupitisha mswada huo kwa kuwa mamlaka yake kwa mujibu wa katiba ni kurekebisha tu.
Aliongeza kuwa katiba inayotaka kufanyiwa mabadiliko ni katiba ya muungano, ambao upo kwa mujibu wa terms za mkataba wa muungano, hivyo, alishauri kuwa ni lazima pande mbili za muungano zirudi katika mkataba wa muungano na siyo kuja na mswada kama huo.
Wachangiaji waliimbia tume hiyo kuwa kinachotaka kufanyika saivi ni kiini macho chengine kwa wazanzibar kama ilivyozoweleka huko nyuma.
" Mh. mwenyekiti mimi nitaupinga mswada huu katika baraza la Mapinduzi, baraza la wawakilishi na pahala pengine popote nitakapopata nafasi, kwa vile mswada huu hauna maslahi na Zanzibar..." alisema Mh. Mansour Yussuf Himid, waziri wa kilimo na mali asili wa SMZ.
Nao wanasheria wa zanzibar wamesema hawawezi kamwe kukubali mswada huo ujadiliwe huku mambo ya msingi yanayowahusu wazanzibar yakiwekewa vikwazo vya kuyazungumza.
"ndugu mwenyekiti, sisi wazanzibar linalotuhusu katika mkataba huu ni muungano, tuna haki ya kujadili uwepo wake na kutokuwepo kwake, hata namna ya kuwapo kwake ni vipi hili liwekewe vikwazo kulijadili?" alihoji mwanasheria wa kujitegemea Ndg. Awadh Ali Said wakati akichangia mswada huo.
inaendelea kwa kuwa tupo katika break hadi saa nane mchana:
Katika ukumbi wa salama Hall, hoteli ya Bwawani mjini zanzibar, kamati ya bunge ya katiba na sheria inayoratibu maoni juu ya mswada wa sheria ya kuandaa utaratibu wa kupata maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya, imechachafywa vikali na wazanzibar wakiwamo wawakilishi, wanasiasa, wanazuoni , wanasheria na wadau mbali mbali visiwani humo.
Hali ilikuwa mbaya kwa tume hiyo iliyoitisha mkutano huo kwa taarifa za haraka haraka, baada ya Mh. Samuel Sitta, kutoa mawasilisho ya mswada huo. Mchangiaaji wa kwanza alikuwa Mh. Hamza Hassan Juma, mwakilishi wa jimbo la Kwamtipura ambaye aliitaka tume hiyo irudi na mswada huo kwa vile Zanzibar haikushirikishwa chochote katika kuuandaa hadi ulivyo sasa.
Huku ukumbi wote ukiwa na hamasa hasa pale aliposimama mwanasheria mkuu wa serikali ya Mapinduzi ya zanzibar bw. Othman Masoud Othman, aliposema kuwa mbali na mswada huo, bunge la Muungano halina Mandate ya kupitisha mswada huo kwa kuwa mamlaka yake kwa mujibu wa katiba ni kurekebisha tu.
Aliongeza kuwa katiba inayotaka kufanyiwa mabadiliko ni katiba ya muungano, ambao upo kwa mujibu wa terms za mkataba wa muungano, hivyo, alishauri kuwa ni lazima pande mbili za muungano zirudi katika mkataba wa muungano na siyo kuja na mswada kama huo.
Wachangiaji waliimbia tume hiyo kuwa kinachotaka kufanyika saivi ni kiini macho chengine kwa wazanzibar kama ilivyozoweleka huko nyuma.
" Mh. mwenyekiti mimi nitaupinga mswada huu katika baraza la Mapinduzi, baraza la wawakilishi na pahala pengine popote nitakapopata nafasi, kwa vile mswada huu hauna maslahi na Zanzibar..." alisema Mh. Mansour Yussuf Himid, waziri wa kilimo na mali asili wa SMZ.
Nao wanasheria wa zanzibar wamesema hawawezi kamwe kukubali mswada huo ujadiliwe huku mambo ya msingi yanayowahusu wazanzibar yakiwekewa vikwazo vya kuyazungumza.
"ndugu mwenyekiti, sisi wazanzibar linalotuhusu katika mkataba huu ni muungano, tuna haki ya kujadili uwepo wake na kutokuwepo kwake, hata namna ya kuwapo kwake ni vipi hili liwekewe vikwazo kulijadili?" alihoji mwanasheria wa kujitegemea Ndg. Awadh Ali Said wakati akichangia mswada huo.
inaendelea kwa kuwa tupo katika break hadi saa nane mchana: