Haya ndiyo maajabu ya serikali za CCM. Zote baba mmoja, mama mmoja.
Ukisikia mtendaji au waziri kuwa ni mzalendo au mchapakazi kweli kweli, basi ujue hapo huyo kawazidi wenzake kwenye ile sifia sifia kama kigezo #1.
Kigezo #2 kipo kwenye kuwakamua wananchi kwa maslahi ya aliyeko kwenye kiti cha enzi. Wasilaumiwe makarani kwenye hili. Ukisikia fulani tenguzi huwa hazimhusu, basi bila shaka atakuwa kawazidi mno wenzake kwenye zile hesabu za siku (mawasilisho).
"Afya, Tamisemi, mambo ya ndani, fedha nk, zinatakiwa pesa."
Hapo ikibidi punda na afe tu ila mzigo lazima ufike.
Yaonyesha hutakiwa kuwa na tabia za wale chawa wetu. Ikikushinda ujue utenguzi utakuhusu asubuhi na mapema tu.
Nani asiyeyajua mashindano ya hadharani kwenye hii sifia sifia hata pasipo stahili? Kila mmoja akijtahidi kumpiku mwenzake.
Tunahitaji mustakabala mpya ambapo watendaji watawajibika kwa watu, siyo kwa kiti cha enzi bila kujali hali.
Ukisikia mtendaji au waziri kuwa ni mzalendo au mchapakazi kweli kweli, basi ujue hapo huyo kawazidi wenzake kwenye ile sifia sifia kama kigezo #1.
Kigezo #2 kipo kwenye kuwakamua wananchi kwa maslahi ya aliyeko kwenye kiti cha enzi. Wasilaumiwe makarani kwenye hili. Ukisikia fulani tenguzi huwa hazimhusu, basi bila shaka atakuwa kawazidi mno wenzake kwenye zile hesabu za siku (mawasilisho).
"Afya, Tamisemi, mambo ya ndani, fedha nk, zinatakiwa pesa."
Hapo ikibidi punda na afe tu ila mzigo lazima ufike.
Yaonyesha hutakiwa kuwa na tabia za wale chawa wetu. Ikikushinda ujue utenguzi utakuhusu asubuhi na mapema tu.
Nani asiyeyajua mashindano ya hadharani kwenye hii sifia sifia hata pasipo stahili? Kila mmoja akijtahidi kumpiku mwenzake.
Tunahitaji mustakabala mpya ambapo watendaji watawajibika kwa watu, siyo kwa kiti cha enzi bila kujali hali.