Watanganyika wenzetu wanavyoteseka Zanzibar

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,320
Baada ya kuchomewa nyumba na biashara zao, wale Watanganyika wenzetu bado wanaendelea kuteseka kwa kuishi maisha mabaya kuliko hata wakimbizi. Kwa sasa wamehifadhiwa katika vyumba viwili vidogo, kimoja wanalala wanaume, kingine wanawake. Ni zingira la kutisha ambapo wanalala zaidi ya watu 40 katika chumba ambamo hamna kitanda, wala godoro wala chandarua na mbu ni wengi.
Kina mama wanaishi na watoto katika chumba hicho kidogo, kwa kweli ni pabaya kuliko hata zizi. cha kusikitisha zaidi, eneo hilo hamna hata choo.

Binafsi naamini serikali haina sababu ya kukaa kimya ikiwaacha wananchi wake wakiteseka ugenini huko kwenye machozi. Lazima kitu kifanyike kuwakomboa hawa wenzetu.
 
na bado wazanzibar wamesema watachangishana fedha kuwawekea wahalifu mawakili waliobora zaidi kujihakikishia ushindini mahakamani

Kuna tetesi kuwa JK yupo upande wao so kiutawala hawawawajibishi.
 
Zanzibar imebadilika sana miaka ya karibuni

Nakumbuka nilienda Znz mara ya kwanza nikiwa likizo ya darasa la nne. Sehemu ya ndugu zangu wanaishi huko. Kusema kweli wakati ule kulikuwa na steriotypes sana wka sisi wabongo. Nakumbuka nilikuwa mdogo lakini nilikuwa nahisi wazi wazi kuwa wabara tulikuwa miaka ile hatupendwi sana visiwani.

Things have changed lakini Zanzibar ni bora zaidi siku hizi hata ukiwa mbara una amani nimestushwa kusikia hayo yaliyotokea.
 
Wanzibari wenyewe wako wachache sana, tukiamua kulipiza si tutawamaliza?
Hebu tuwe na busara kido, mtoto akikunyea mkono, huwezi kuukata.
Tuwasamehe.
 
Baada ya kuchomewa nyumba na biashara zao, wale Watanganyika wenzetu bado wanaendelea kuteseka kwa kuishi maisha mabaya kuliko hata wakimbizi. Kwa sasa wamehifadhiwa katika vyumba viwili vidogo, kimoja wanalala wanaume, kingine wanawake. Ni zingira la kutisha ambapo wanalala zaidi ya watu 40 katika chumba ambamo hamna kitanda, wala godoro wala chandarua na mbu ni wengi.
Kina mama wanaishi na watoto katika chumba hicho kidogo, kwa kweli ni pabaya kuliko hata zizi. cha kusikitisha zaidi, eneo hilo hamna hata choo.

Binafsi naamini serikali haina sababu ya kukaa kimya ikiwaacha wananchi wake wakiteseka ugenini huko kwenye machozi. Lazima kitu kifanyike kuwakomboa hawa wenzetu.

,,,,,Nahitaji kujua hii,,,Hivi hawa wafanyabiashara wamechomewa NYUMBA zao za KUISHI au sehemu zao za BIASHARA???,,manake sielewi imekuaje mtu achomewe sehemu yake ya biashara,mara ghafla hata sehemu ya kulala hakuna tena,au ndo ilikuwa DUKA na KITANDA hapo hapo???,,hata hivyo nawapa pole sana,na hio si tabia ya KIUNGWANA hata kidogo,sidhani hata kama hio DINI inakipengele hicho cha USHENZI uliopindukia,sheria ifuate mkondo wake.
 
Zanzibar imebadilika sana miaka ya karibuni

Nakumbuka nilienda Znz mara ya kwanza nikiwa likizo ya darasa la nne. Sehemu ya ndugu zangu wanaishi huko. Kusema kweli wakati ule kulikuwa na steriotypes sana wka sisi wabongo. Nakumbuka nilikuwa mdogo lakini nilikuwa nahisi wazi wazi kuwa wabara tulikuwa miaka ile hatupendwi sana visiwani.

Things have changed lakini Zanzibar ni bora zaidi siku hizi hata ukiwa mbara una amani nimestushwa kusikia hayo yaliyotokea.

Ndugu yangu mimi siamini kama Zanzibar niliyokuwa ninaifahamu ndio hii ambayo inafanya unyama wa namna hii. Hiki kizazi cha sultani kilichachangayika hapo zanzibar serikali isipoangalia vizuri kitamwaga damu. Na hakita mwaga damu hapo Zanzibar tu hata huku bara tusipokuwa makini. Hawa inaonyesha wanamsukumo fulani au wananguvu fulani ndio maana wanajiamini hivyo. Upumbavu wetu na upole wetu utatufanya hawa wajamaaa watumalize kwa kupenda kujikombakomba kwao. Tuangalie wenzetu wa nchi nyingine wanavyokuwa makini na nchi zao. SIsi uroho wa pesa utatufikisha pabaya.

ASANTENI.
 
,,,,,Nahitaji kujua hii,,,Hivi hawa wafanyabiashara wamechomewa NYUMBA zao za KUISHI au sehemu zao za BIASHARA???,,manake sielewi imekuaje mtu achomewe sehemu yake ya biashara,mara ghafla hata sehemu ya kulala hakuna tena,au ndo ilikuwa DUKA na KITANDA hapo hapo???,,hata hivyo nawapa pole sana,na hio si tabia ya KIUNGWANA hata kidogo,sidhani hata kama hio DINI inakipengele hicho cha USHENZI uliopindukia,sheria ifuate mkondo wake.
Hawakuwa na maduka bali walikuwa na mabanda ya miti na makuti,na udongo ndio maana hakikubakia kitu katika kuungua huko,mabanda hayo humo humo kuna kitanda,na cho humo humo,mengine hayana choo wanajisaidia katika ukanda wa bahari.

Suala la sheria kwa kweli inasikitisha hapa zanzbar ,,kwa mfano juzi tu rais alihojiwa kuhusu mambo msije,kuna jengo limeuzwa na serikali,walieka layout ili wanachi watoe maoni,wananchi 300 walitoa maoni kuwa hawataki sehemu hiyo ijengwe huko shangani,sasa rais amehojiwa ametamka kuwa iliyo uza ni serikali,na washauza na hakuna mtu wa kuhoji hilo,sasa jee serikali ni nani ? Ikiwa wananchi 300 wamekata ujenzi katika eneo hilo ?

Ukiangalia lugha chafu kama hizi kwa rais wa zanzbar kuongea kwa wananchi jee kuna sheria hapa kweli ? Jee wananchi watasikilizwa vilio vyao ? Huko eneo la pwani mchangani kulikochomwa moto pia wananchi wakijiji hicho walipeleka malalamiko yao kwa serikali waondolewe wafanya biashara hao na wapatiwe eneo jengine,lakini waliyapuuza malalamiko hayo,wanavyosema kuwa walipewa amri wafanya biashara hao wahame lakini walikuwa bado wanasuasua

Bahati mbaya wananchi wakapandwa na hasira na kuyatia moto,lakini suala hili tunalichukulia kisiasa au kijamii ? Kuna wengine wanasema ni kwa sababu ya muungano,lakini walipohoji wana vijiji wamesema wao wanakata suala hi isipokuwa wanapinga kutokana na mila na desturi zao haziendani na mazingira yale ya biashara sio kwa sababu ya muungano,na walishapeleka malala miko yao kwa serikali.

Hapa zanzbar viongozi wa serikali wamekuwa wakipuuza sana malalamiko ya wananchi hata rais mwenyewe,tumeshuhudia pia hata rais akipingana sana na wanasheria zanzbar kwa kuteuwa mwanasheria mkuu ambaye hakuna na sifa kutokana na katiba ya zanzbar,ilikuwa kasheshe kumtoa,lakini hatimae walishinda.

Mimi siwalaumu walichoma moto wana siwaungi mkono,ila ikiwa kama kweli wananchi hatutaki muungano basi tuachane kwa amani,kuna watu wameowana baina ya pande hizi mbili,tukivunja muungano bado tutakuwa ndugu na udugu hauepukiki,ispokuwa ni nchi na madaraka yake, zanzbar itakuwapo hapa hapa,tanganyika nayo itakuwapo,bahari ya hindi itakuwapo,isipokuwa na mipaka tu,tuwekeane heshima tu.

Tunaombana radhi watanzania wote,haya ni makosa ya viongozi na sio wanachi lazima mufahamu.
 
kama alivyosema baba wa taifa

:mod::mod::mod:......WAPEMBA HAYOOOOO.....WAPEMBA HAYOOOOOOOOO.................!!:mod::mod::mod:
 
Ni roho ya ubaguzi!

nilisoma na mzenji mmoja chuoni, alinambia et wabara tunawapelekea ukimwi (makahaba wote wa zenji ni Wabara), na madawa ya kulevya, na alisema ipo siku wabara wataona pagumu zenji, tulibishana sana. Sasa ndo nimejua alichomaanisha,

Na kama angekua zenji mpaka sasa ningejua anahusika na kama hausiki amefurahi sana. ila yeye kwa sasa yupo India anasoma masters

Cooorupt Mind!
Zanzibarian u should Style up!
 
Siungi mkono mtu yoyote kufanyiwa ubaya kutokana na jinsia, dini au rangi yake

lakini pia sisi kama binadam tumeumbwa na kumepewa akili ya kufikiri

sasa kama unaishi sehemu na unaona hutakiwi au hali yako na maisha yako yanakuwa hatarini kwanini usihame?

Nchi ni kubwa sana ...mtu kama hawezi kuishi unguja anaweza kuhamia Bukoba, Moshi, Iringa , Nyarugusu na hata Dodoma

Mambo mengine tusisubiri serikali itusaidue mengine yako ndani ya uwezo wetu ni kiasi cha kuyatekeleza tuuu....eti serikali ikulinde..kha! serikali imeshindwa kulinda watu wanaishi gongo la mboto na Ukonga ndio ikulinde weye!

Hebu tujaribu kuwa realistic saa zingine
 
Mkianza kubaguana wazanzibari na wabara, hamtoishia hapo hiyo dhambi itaendelea kuwatafuna mzanzibari mtagundua kumbe zanzibar kuna wapemba na waunguja. Na bara kuna wachaga na wasukuma, wahaya, wakurya na makabila kibao tu.

kukonclude sisi wote ni kiumbe cha mwenyezi Mungu, tumeumbwa wote kwa mfano wa Mungu sasa wewe nani unaanza kuleta ubaguzi.
Mungu akusaidie wewe uliye mbaguzi na ugundue kuwa ni dhambi kubwa unafanya.
 
Hawakuwa na maduka bali walikuwa na mabanda ya miti na makuti,na udongo ndio maana hakikubakia kitu katika kuungua huko,mabanda hayo humo humo kuna kitanda,na cho humo humo,mengine hayana choo wanajisaidia katika ukanda wa bahari.

Suala la sheria kwa kweli inasikitisha hapa zanzbar ,,kwa mfano juzi tu rais alihojiwa kuhusu mambo msije,kuna jengo limeuzwa na serikali,walieka layout ili wanachi watoe maoni,wananchi 300 walitoa maoni kuwa hawataki sehemu hiyo ijengwe huko shangani,sasa rais amehojiwa ametamka kuwa iliyo uza ni serikali,na washauza na hakuna mtu wa kuhoji hilo,sasa jee serikali ni nani ? Ikiwa wananchi 300 wamekata ujenzi katika eneo hilo ?

Ukiangalia lugha chafu kama hizi kwa rais wa zanzbar kuongea kwa wananchi jee kuna sheria hapa kweli ? Jee wananchi watasikilizwa vilio vyao ? Huko eneo la pwani mchangani kulikochomwa moto pia wananchi wakijiji hicho walipeleka malalamiko yao kwa serikali waondolewe wafanya biashara hao na wapatiwe eneo jengine,lakini waliyapuuza malalamiko hayo,wanavyosema kuwa walipewa amri wafanya biashara hao wahame lakini walikuwa bado wanasuasua

Bahati mbaya wananchi wakapandwa na hasira na kuyatia moto,lakini suala hili tunalichukulia kisiasa au kijamii ? Kuna wengine wanasema ni kwa sababu ya muungano,lakini walipohoji wana vijiji wamesema wao wanakata suala hi isipokuwa wanapinga kutokana na mila na desturi zao haziendani na mazingira yale ya biashara sio kwa sababu ya muungano,na walishapeleka malala miko yao kwa serikali.

Hapa zanzbar viongozi wa serikali wamekuwa wakipuuza sana malalamiko ya wananchi hata rais mwenyewe,tumeshuhudia pia hata rais akipingana sana na wanasheria zanzbar kwa kuteuwa mwanasheria mkuu ambaye hakuna na sifa kutokana na katiba ya zanzbar,ilikuwa kasheshe kumtoa,lakini hatimae walishinda.

Mimi siwalaumu walichoma moto wana siwaungi mkono,ila ikiwa kama kweli wananchi hatutaki muungano basi tuachane kwa amani,kuna watu wameowana baina ya pande hizi mbili,tukivunja muungano bado tutakuwa ndugu na udugu hauepukiki,ispokuwa ni nchi na madaraka yake, zanzbar itakuwapo hapa hapa,tanganyika nayo itakuwapo,bahari ya hindi itakuwapo,isipokuwa na mipaka tu,tuwekeane heshima tu.

Tunaombana radhi watanzania wote,haya ni makosa ya viongozi na sio wanachi lazima mufahamu.

Ghibuu, acha uongo, sisi Zanzibar tunaijua kuliko unavyodhani wewe, usije ukashangaa tunaonana kila siku, Walio chomewa wana nyumba imara na maduka imara, na wengine wemewaajiri Wazanzibari, na maduka yenyewe ni ya Kitalii, Tourism Souvernir na wengi wa Wazanzibari isipokuwa wahindi ndio wenye maduka ya namna hii, wengi ni Wakenya, Wabara na Wahindi, sawa inawezekana yalikuwepo pia mabanda madogo, lakini eneo la Mnarani kulikuwa na makaazi.
Unajua history ya Kijiji cha wabara cha KIBANDA UGALI Kiwengwa? alivunja Rais Karume mwaka 2005 na Kujenga Hoteli 2 moja yake, Sultan Sands Hotel, na hekalu la mkewe Mama Shadya, eti alishauriwa na ZATI shirikisho la wawekezaji wa Kitalii ambayo mwenyekiti wake ni Simai Said Mohamed, mdogo wake Hassan Kichwa, wamiliki ya Mercury Restaurant hapo Bandarini, cha ajabu huyo Simai amepewa Uwakilishi, na usiniambie kuwa hii familia ni safi ya Kina Simai, ila nasemaje, kulikuwepo wawekezaji wengi wa bara hapo Kibanda ugali, walitumia pesa nyingi sana kujenga nyumba za maana na biashara kubwa kubwa za Kitalii, siku moja bila taarifa, saa kumi usiku, Greda au makatapila yalifika na kuanza kubinua kila nyumba bila hata kuamsha watu, walitoka wanawake na watoto uchi wakijiuliza ni mwisho wa dunia? lakini badala ya Jeshi tiifu kwa Rais wa Zanzibar la JKU liliwacheka tu na kuwaamuru wasionekane popote maeneo ya karibu. pia miezi 3 iliopita unakumbuka Kendwa? maduka yote na minisupermarket nyingi za wabara zilizostawi, ilitoka amri kwa viongozi wa Juu zivunjwe mara moja, mbona za wanzibari hazivunjwi?
 
Ghibuu, acha uongo, sisi Zanzibar tunaijua kuliko unavyodhani wewe, usije ukashangaa tunaonana kila siku, Walio chomewa wana nyumba imara na maduka imara, na wengine wemewaajiri Wazanzibari, na maduka yenyewe ni ya Kitalii, Tourism Souvernir na wengi wa Wazanzibari isipokuwa wahindi ndio wenye maduka ya namna hii, wengi ni Wakenya, Wabara na Wahindi, sawa inawezekana yalikuwepo pia mabanda madogo, lakini eneo la Mnarani kulikuwa na makaazi.
Unajua history ya Kijiji cha wabara cha KIBANDA UGALI Kiwengwa? alivunja Rais Karume mwaka 2005 na Kujenga Hoteli 2 moja yake, Sultan Sands Hotel, na hekalu la mkewe Mama Shadya, eti alishauriwa na ZATI shirikisho la wawekezaji wa Kitalii ambayo mwenyekiti wake ni Simai Said Mohamed, mdogo wake Hassan Kichwa, wamiliki ya Mercury Restaurant hapo Bandarini, cha ajabu huyo Simai amepewa Uwakilishi, na usiniambie kuwa hii familia ni safi ya Kina Simai, ila nasemaje, kulikuwepo wawekezaji wengi wa bara hapo Kibanda ugali, walitumia pesa nyingi sana kujenga nyumba za maana na biashara kubwa kubwa za Kitalii, siku moja bila taarifa, saa kumi usiku, Greda au makatapila yalifika na kuanza kubinua kila nyumba bila hata kuamsha watu, walitoka wanawake na watoto uchi wakijiuliza ni mwisho wa dunia? lakini badala ya Jeshi tiifu kwa Rais wa Zanzibar la JKU liliwacheka tu na kuwaamuru wasionekane popote maeneo ya karibu. pia miezi 3 iliopita unakumbuka Kendwa? maduka yote na minisupermarket nyingi za wabara zilizostawi, ilitoka amri kwa viongozi wa Juu zivunjwe mara moja, mbona za wanzibari hazivunjwi?

Sawa mie mungo wewe unajua zaidi,lakini hizo nyumba kama ni tufali basi haliungui na kama tufali linaungua basi Dunia imemaliza kwa sababu katika ilo eneo hakikubaki kitu,,,nasema yalikuwa ni mabanda na makazi humo humo,,wacha ubishi,

UKWELI KUHUSU VIBANDA VILIVYOCHOMWA MOTO
mzalendo_balozi-564x272.jpg


Ukweli kuhusu vibanda vilivyojengwa vya wafanyabiashara ya vinyago eneo la Pwani Mchangani, Kaskazini Unguja ni kama hivi: Ukweli ambao SMZ-GNU hautaki kuusema kwa faida yao na matakwa yao zaidi ya kisiasa. Soma maelezo sahihi na uchambuzi wa kina:
- Vibanda hivi vimejengwa bila kibali cha aina yeyote ile au ya umiliki wa ardhi. Na kama kipo tunaomba tuonyeshwe. Balozi Seif Ali Iddi anajua hilo, lakini amekurupuka na kuzungumza siasa zaidi ya kutaka kukamilisha agenda yake ya Tanganyika. Nina challenge balozi Seif Ali Iddi atuonyeshe hati miliki ya hao wamachinga wa hapo. Jamani, tuzungumze sheria, na haki, sio hamasa wala siasa au chuki.
- baada ya kuvamia, wamejenga kanisa, jambo lililowakera wananchi wazawa wa hapo. Balozi Seif Ali Iddi anisute kama sio kweli.
- wanakijiji/wazawa, walilalamika kwa serikali, za wilaya, mkoa na serikali kuu kuhusu kadhia hiyo, hakuna lililochukuliwa, smz imepuuza madai ya wananchi wake. Leo, yametokea mengine, wanajaribu kugeuza kibao kwa wenyeji. Uonevu gani huu, ndani ya nchi yetu. Madai ya wananchi yapo hai, tena kwa maandishi na kesi ipo, files zipo. Madai yao yapo halali kabisa, lakini walipuuzwa kwa sababu wao ni wenyeji, na wamekuzwa watu wageni wasiokuwa na hata saa moja ya kuishi Zanzibar. Sasa, OK, tujaalie SMZ iamue kuwalipa watoto wa wafalme, wataanzia wapi; any document ya kuhalilisha malipo au uhalali wa umiliki wao hapo, kisheria; tusiende kisiasa.
* Jamani, tunataka kuambiwa nini na Balozi Seif Ali Iddi, Charlie Chaplin. Nilisema awali kuwa huyu Seif NO.2 siye/hatufai. Na kadhalika Seif NO.1; pia ni mzigo kwetu kwa maslahi ya Zanzibar.
Hiyo ni SET NO .1
SET NO.2 ya mazungumzo yetu:
- hoteliers pia wamelalamika sana na watu hawa – NO action. Kamisheni ya utalii pia wamekereka na watu hawa – no action: kwa sababu wanaiharibu sekta yote ya utalii Zanzibar.Hoteli nyingi ama zinakosa biashara kwa kuwepo vibanda vile pale. How? wageni wao wanaibiwa, wanakuwa harrased na hotels zinakosa ‘positve image/good image' kwa kuzungukwa na vibanda hivyo. Hoteli ya fur star worth over 20m dollars, imezungukwa na kibanda cha shilingi elfu kumi. Uoza mtupu. Sekta ya utalii inakufa kutokana na wauza ugali na vinyago hawa. Hii ni serious, na naomba SMZ na nyie wote muitazame huko, kama angle ya biashara zaidi /sio siasa zaidi.
SET NO.3 ya amzungumzo yetu:
- biashara gani walikuwa wanafanya hawa watoto wa wafalme?
1. Kuuza Vinyago
2.Kuuza pombe/madawa ya kulevya
3.Uhalifu wa kupindukia.
4.Ukahba.
Katika uhalifu, iliwahi kukamatwa hata silaha katika mabanda hayo, ingawa polisi imebana kimya. Haya na mengine , mstahiki balozi seif ali iddi hataki kuyasema wala hatoyasema maisha.
Angalia ufedhuli wa watu hawa, jana wanasoma risala mbele ya Seif Ali Iddi na kusema kuwa kama serikali haitochukua hatua, wao watachukua hatua mikononi mwao. Huyu eti ni VP 2 wa nchi, na watu wanamwambia watavunja sheria, yeye na timu yake, wanacheka. Watu wanafikiria kulipiza kisasi, au kuuwa, au kufanya hujma, yeye mwenzetu anaona rahaaa, na anacheka kwa kuraha. Keli tumepata vingozi au tumepatikana.
Lakini yote hayo ya nini? Hayo ni mambo yamepanga na system. Inawezekana waliochoma moto ni serikali au hata hoteliers, au hata wengine xxxx! ili kukamilisha agenda yao. Mnaijua?
Jawabu: katiba mpya. Kwa vile mmeikataa, sasa wanabuni tension, ili kukamilisha agenda hiyo.
Bottomline: lazima katiba mpa iwe by 2014, kama alivyosema au anavyotaka JK.
Sasa Zanzibar kuanzia siku mliyoikataa mswada wa katiba mpya, mpaka 2014 – mtaona mambo mengi ya ajabu ajabu – popobawa atarudi, wale ramba ramba watarudi, vitisho, na visa, na mikasa mingi tu mtaiona. Ushindi lazima, na lazima katiba mpya ipite, na lazima Zanzibar tuifute katika ramani ya dunia…kwa utaalamu na kisayansi.
Tusisahau kuwa katika kuchomwa moto vibanda hivi upo mkono wa kanisa.
Unajua huko nyuma sana, nilisema kwa sauti kubwa kuwa Seif NO.1 na NO.2 hawatufai, na ni lame duck – niliambiwa sijui niko CUF, wengine wakasema mimi CCM. Ahhhh…jamani: mimi atayesema ni CUF – basi mimi ni CUF aliyekata kamba zizini; na atayesema mimi CCM; basi mimi ni CCM mfu – sina mbele, sina nyuma. GNU, narudia tena haitufai; inazidi kutuletea matatizo.
- Na Maalim seif mwenyewe (menyewe….baba dogo veve, amekiri juzi jamat khan) kuwa hawawezi kutatua matatizo ya wananchi, na ametoa visingizio miteni kidogo. Mwisho hana la kusema anasingizia eti pirates wa Somalia, ndio wamesababisha kupanda kwa bei ya vyakula. Balahau bora sasa ukae na uandike vitabu vya comedy. Maalim Seif bora aungane na akina Chimbeni Kheri au Mr.Bean, watupatie tales za vichekesho.
Mwisho,nimesitikitika zaidi kuona waandishi kama Salma Said, naye amejaa tele katika hamasa na kuandika lugha mbovu kabisa, iweje yeye aandike neno ‘vibanda vya wabara'. si aseme tu, vibanda vya wafanya biashara……yaani wazanzibari wote tumetekwa akili zetu na watu hawa.
Inasikitisha sana.
 
Back
Top Bottom