mkuu pandisha kiwango tujadili mada; ni afadhali ya mbichi zinalika hizi zimevunda na kuoza kabisa; mkuu tunakula vitu fda approved hivi vya majalalani hata matonya (r.i.p) vilimshinda.
Chama
gongo la mboto dsm
naona umejitoa akili unatema matope
mkuu pandisha kiwango tujadili mada; ni afadhali ya mbichi zinalika hizi zimevunda na kuoza kabisa; mkuu tunakula vitu fda approved hivi vya majalalani hata matonya (r.i.p) vilimshinda.
Chama
gongo la mboto dsm
Nenda pale karibu na Forodhani kuna bookshop mojawapo ambayo ni zao la TMP Book department ambayo ni publisher, book seller na book distributor. Zomba mambo mengine kuyaelewa unahitaji uyafanyie utafiti vinginevyo tunaandika vingi ambayo hujavijua ninaendeshwaje na vipoje.
Mkuu Candid Scope umeelezea mazuri sana ya Dr Slaa kana kwamba wengine hawapo, anapokuwepo.
Dr. Slaa
Dr. Slaa si mtu mwenye maneno mengi, ni mtulivu na mkimya kiasi chake, lakini akipanda jukwaani na kuanza kulishambulia huku na kule huwezi kuamini kinachotoka ubongoni mwake. Kimya kingi kina mshindo.
Wengi hawamfahamu Dr. Slaa vilivyo, wengi wanamwona sasa baada ya kuingia bungeni na sasa katika majukwaa ya siasa, ukweli ni mtu mbunifu, mpenda maendeleo na mwenye kujitoa kwa ajili ya wengine bila kujibakiza. Ufahamu wangu wa huyu Dr. Slaa ni wa muda mrefu, lakini wengi wetu wanachukulia mambo ya juu juu tu bila kujua undani na utendaji uliotukuka wa mtu huyu.
Machache kati ya mengi kuhusu Dr Slaa kabla ya kuwa mwanasiasa, kuwa Mwanasiasa na hatimaye kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, ana mlolongo wa mambo mengi ambayo yanaonyesha ubunifu wa hali ya juu, na pia mwepesi kuwaelewa vijana na kuendana nao tofauti na watu wengine wa kizazi chake.
Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM, baada ya kuombwa na Wanakaratu agombee ubunge kule baada ya kuchoshwa na mbunge aliyekuwepo wakati huo, CCM iliendelea na mizengwe ile ile kama iliyotokea juzi pale Dodoma kuwaengua watu wanaofaa kwa uongozi. Wanakaratu wakiamua hawataki longolongo, wakamsihi kwamba wameamua awe mbunge wao na wakamwomba achague chama kingine agombee kwani hawamtaki kabisa mbunge aliyepo. Kwa ridhaa ya wananchi akaamua kujitoa CCM na kujitosa kujiunga na Chadema ili agombee ubunge kuridhia matakwa ya wanakaratu.
Kabla ya kuwa mwanasiasa
kuna mengi ya maendeleo ambayo wengi tunayaona huku tusijua kama Dr. Slaa ndiye aliyebuni na kuyaendesha kama ifuatavyo.
- Dr. Slaa ndiye amekuwa wa kwanza Tanzania kuagiza big truck for load and unload makontena bandari ya Dar es Salaam wakati akiwa Katibu Mkuu TEC. Ilikuwa ni miaka ya 1980th, hakukuwa hata kampuni au watu binafsi waliothubutu kufanya hivyo. Truck hilo lilikuwa na crane za kupakia na kupakua bila taabu kokote linalokifkishwa container na kwa truck hilo. Baadaye makampuni yakabembeleza wauziwe gari ile, ndipo Barala La maaskofu likawauzia.
- Kwa mara ya kwanza baraza la Maaskofu Tanzania lilipoanza kuwa na matumizi ya computer ikiwepo ofisi yake Dr Slaa kama katibu Mkuu, na taasisi za upashanaji habari ambazo zilikuwa chini ya uongozi wake ikiwa ni pamoja na:
- Gazeti la kiongozi kuanza kutumia mfumo wa computer katika idara ya set up
- TMP (Tanganyika Mission Press) Kipalapala idara ya uchapishaji (printing) wakitumia Apple computers.
- TMP Book deparment Tabora mjini) idara ya maduka ya vitabu na usambazaji vitabu wakitumia Apple computers
- TAPRI idara ya tungo za mawasiliano vitabu TEC iliyokuwa na ofisi zake Seiminari kuu Kipalapala Tabora.
Idara hizo zilikuwa na matumizi ya computer na PageMaker & QuakExpress software ambazo kwa graphic designers ilikuwa kitu kigeni kisichozoeka bado Tanzania ukitilia maanani wakati huo tulikuwa na chuo kimoja tu cha ardhi kule Tabora kujifunzia Graphic Design kabla ya Ardhi Dar haijaanza kukamilika. Huo ni ubunifu wa Dr. Slaa kwa wakati huo wakati wengi Tanzania hawajafunguka kuhusu matumizi ya teknologia ya ulimwengu wa dot com.
NB.Wakati huo chuo pekee cha mawasiliano (journalism) Tanzania kilikuwa ni Nyegezi-Mwanza pekee kilichokuwa kikiongozwa na AMECA (Balaza la Maaskofu Katoliki Afrika Mashariki na Kati kimoja kikiwa Kitwe - Zambia, cha Nyegezi kiliendeshwa na TEC Dr. Slaa akiwa msimamizi mkuu kama Katibu Mkuu.
Dr. Slaa atakumbukwa sana kwa makubwa aliyofanya kujenga na kuikuza TEC
- Makao makuu ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) tunayoona siku hizi ni matunda ya ubunifu wa Dr. Slaa alipokuwa Katibu Mkuu pale. Jengo la awali ni lile lililo upande wa mbele zinapotumika ofisi siku hizi ambapo yalikuwa madarasa ya shule ya sekondari ya Masisita Tanzania, ambayo baadaye ilihamishiwa Bigwa Morogoro kupisha kiwanja hicho kuwa makao ya Maaskofu Katoliki Tanzania, awali yalikuwa pale ofisi za St. Joseph, Dar es Salaam. TEC aliyoikuta DR. Slaa ilikuwa na jengo hilo la madarasa na jengo lilolokuwa la utawala wa shule. Dr. akabuni majengo ambayo tunayoana sasa, hata kama hayakukamilika yote waliofuata walikamilisha kazi alioyoianza.
- Kaone maendeleo na majengo katika jimbo la Mbulu ni jitihada za Dr. Slaa na Fr. Narda ambao kwa pamoja walifanya makubwa.
- Kaangalie jimboni kwake huduma za kijamii ambazo amezifanya, utachoka mwenyewe kiasi ambacho CCM imekimbiwa kabisa huko sababu utendaji wa Slaa huko na CCM ni sawa na kulinganisha mlima na kichuguu.
- Dr. Slaa kwa tunaomfahamu ni mwanamapinduzi na mpenda maendeleo, na pengine mengi alikuwa anayafanya yakaonekana mapya mno kwani alikuwa anaona mbali kuliko hawa wakubwa wake, ila sipendi kuliongelea sana hilo.
Chadema yaimarika baada ya Dr. Slaa kuwa mgombea urasi uchaguzi Mkuu uliopita.
Siyo siri Chadema hakikuwa na nguvu tunayoona sasa hivi licha ya kuwa na sera nzuri, lakini leo tunaona nguvu ya Chadema inayoogopewa mno na CCM ni kutokana na Chadema katika dakika za majeruhi kuamua kumwangukia Dr. Slaa agombee urasi ambao Samweli Sitta aliingia mitini baada ya makubaliano nao. Tangu hapo Chadema imekuwa na nguvu ya ajabu.
Je, vijana hao waliokuwemo ndani ya Chadema kabla ya Dr. Slaa kugombea Urais kwa nini hawakuipaisha juu Chadema kama sasa? Baada ya Dr. Slaa kuipaisha Chadema juu sasa tunakuja na kauli mbiu ya kubeza makubwa yaliyofanywa na hawa mnaowaita kizazi cha kabla ya uhuru. Hapana tuwe waungwana, pamoja na kila mmoja kuwa na haki za kugombea nafasi tusigeuze uhuru huo kuwabeza hawa ambao wametufikisha tulipo, na bado tunahitaji mchango wa ushauri, uongozi, hekima na busara zao. Uongozi bora ni kuchanganya mapya na ya kale kwani viatu vya zamani vyaijua njia.
Ubunifu wa Chadema viongozi wakiwa mojawapo waliozaliwa kabla ya Uhuru Dr Slaa na Kamanda Mbowe:
- Dr. Slaa ndiye mbunge ambaye baada ya kuingia bungeni alianza kuchangamcha kwa kuichambua serikali na kasoro zake kitu ambacho katika mabunge yaliyotangulia wabunge walikuwa ni rubber stamp ya serikali.
- Chadema wakiwemo hao unaoona walizaliwa kabla ya uhuru wamebuni mapya katika shughuli na kampeni za uchaguzi Tanzania kuwa zenye mvuto kuanzia mkuktano wa ufunguzi wa kampeni uchaguzi Mkuu uliopita ulifanyika Kidongo Chekundu baada ya Dr. Slaa kushusha makumbora mazitomazito kuituhumu serikali, watendaji wa serikali na CCM, tuhuma ambazo CCM wanazidi kubabaika kuwanyoshea kidole wahusika kisha kuwakumbatia tena hivi karibuni kule Dodoma.
- Mkutano wa Kidongo chekundu Dar es Salaam ndio ulioanza kutufungua macho na masikio Watanzania na kuanza kujifunza elimu ya uraia ambayo tulikuwa tunazibwa na CCM tusiijue.
- Dr. Slaa ndiye aliyetufunza na kutufunua kwamba raia wanayo nguvu ya kuiadabisha serikali haki zao za msingi zinapokiukwa kwa kauli mbiu ya nguvu ya umma (peoples power).
- Utumiaji wa chopper kufikia maeneo magumu kufikika kwa magari na kurahisisha kazi ya kampeni, CCM wakaiga.
- Kuwa na magari yanayotumika kama majukwaa ya mikutano badala ya kupoteza gharama na muda kujenga majukwaa yatakayotumika kwa dakika chache.
Ilani ya Uchaguzi Chadema ndiyo inayotumika na yenye uzito sasa hivi:
- Fukuto la Katiba mpya linaloendelea sasa nchini ni uzao wa ilani ya Chadema na ilani ya Dr Slaa kwamba kinachofuata baada ya Uchaguzi mkuu ndani ya siku 10
- Kikwete kufanya mabadiliko ya barala la mawaziri mara kadhaa ni kutokana na shinikizo la wabunge wa Chadema bungeni.
- Serikali kubana matumizi ya ziada ili kuokoa pesa za walipa kodi
Kuna mengi tu wachangiaji wengine watachangia, ni dhana potovu kuwa na fikra za aina hiyo na kuwabeza wabunifu wa mengi, waliongoza nchi hii, wenye kuturithisha mengi kwa uzoefu na busara zao na walioongoza nchi hii hadi kuwa na utulivu wa aina yake. Leo vijana mnaowasema yanayojilia ni amani kusambaratika na mauaji ambayo ilikuwa hadithi za kusimuliwa kutoka nchi nyingine, leo serikali ya CCM inayoongozwa na Rais kijana kuliko Rais mwingine aliyemtangulia imetwishwa na aibu kubwa ya kitaifa na kimataifa ya mauaji ya raia wasio na hatia.
Kuna nchi ambazo ni kielelezo cha vijana ambao mimi ningewaita watoto kukabidhiwa madaraka ya kuongozia nchi na kusababisha maafa makubwa kwa nchi husika kama Liberia, Ujerumani chini ya Hittler, na kinachoendela huko Zaire ya sintofahamu.
Vijana achaneni na uroho wa madaraka, vema kubaki watumishi na watendaji wazuri serikalini na vyamani kujifunza mbinu za uongozi na kupata uzoefu katika kuongoza nchi.
Kuongoza nchi hakuna shule wala kitabu cha kusomea au chuo. Hekima na busara ya mtu ndio kielelezo cha fanaka katika kuongoza nchi.
- Vijana wana papara,
- wanataka njia ya mkato,
- pagumu wanataka kulazimisha bila busara wala kutumia akili
- Vijana wanalipuka kama moto wa gas
- mambo yakigeuka magumu ni mabavu hutumika.
Hoja zako zipo personal sana so peleka kule jukwaa la mapenzi na mahusiano au fcbk na utapata majibu unayoyataka coz humu ni siasa mwanzo mwisho.
Be a guy
Wewe una mchango gani, au una taarifa gani hadi kumdharau mtoa mada? Hii ni wasifu bayana, tena kuna mengi tu mazuri hajayaandika humu. naye kasema hivyo. Wewe unakurupuka na kuropoka bila kutoa fact.Poor analysis
Fool of bias.
Wewe na molemo mkajipange upya!
kwa uhakika unaonesha jinsi unavyosukumwa na kitu fulani humu jamvini lakini sio great thinker upo upo tu kwa ajili ya kitu fulani maana huelezi cha maana kwemye kila hoja wewe ni kutoa yale uliotumwa.
ukisema imeandikwa kiwango cha chini maanake nini wapi ni kitu gani poor you....fooolish thinker
Wewe bora ukae kimya tunajadiana na Candid Scope kiungwana.
naona umejitoa akili unatema matope
Bookshop ya Forodhani (St. Joseph) ipo toka Slaa bado hajaanza shule au kabla ya kuzaliwa, mie nafunguwa macho naikuta na nimezaliwa kabla ya "Uhuru".
Mkuu Candid Scope umeelezea mazuri sana ya Dr Slaa kana kwamba wengine hawapo, anapokuwepo.
Katika CHADEMA je umaarufu wa chama umepatikana single handedly kwa KUDUMU FIKRA ZA DR SLAA ?
Na je kina Makani, Ngwilulpi, Mtei waanzilishi mbona hawamo kwenye hiyo historia yako?
Mbowe je? Na kujitolea kwake?
Hii isiwe njia tu ya kupolish image ya Dr Slaa kabla ya kutangaza nia ya kuombea Urais, atangaze tu watu wamchambue kwa ndani.
Umeelezea YALIYOPITA ya Dr Slaa ingawaje si kikamilifu.
Je falsafa yake katika kututoa waTanzania kutokana na maadui walewale yaani Ujinga,magonjwa na dhuluma(utawala bora), ziko wapi?
Mipango mikakati ya maendeleo ya nchi kwa ujumla ameiainisha sehemu gani ili watu tuweze kusoma.
Lazima tutambue Watanzania kuwa kuongoza nchi si juhudi za mtu binafsi peke yake, ingawaje kuwa na mtu mwenye mawazo chanya insaidia sana.
Poor analysis
Fool of bias.
Wewe na molemo mkajipange upya!
Huko kwingine kote labda unaweza kuwa umepatia mpaka hapo kwa Kamanda Adolf Hitler hapo umechemka mbaya yaani, huwezi kumweka Kamanda Hitler kundi moja na hao vilaza, Huyo jamaa alikuwa ligi nyingine kabisa, acha kabisa yani!
Kuna nchi ambazo ni kielelezo cha vijana ambao mimi ningewaita watoto kukabidhiwa madaraka ya kuongozia nchi na kusababisha maafa makubwa kwa nchi husika kama Liberia, Ujerumani chini ya Hittler, na kinachoendela huko Zaire ya sintofahamu.
yan kaz aliyafanya ni kulitumikia kanisa sasa watanzania wengne tunahusikaje mchaguen mgalatia mwenzenu awe papa sio rais watz na bado mmesahau kuna masister weng 2 kawazin mpaka mwisho kampora mke wa mtu..
Huko kwingine kote labda unaweza kuwa umepatia mpaka hapo kwa Kamanda Adolf Hitler hapo umechemka mbaya yaani, huwezi kumweka Kamanda Hitler kundi moja na hao vilaza, Huyo jamaa alikuwa ligi nyingine kabisa, acha kabisa yani!
yan kaz aliyafanya ni kulitumikia kanisa sasa watanzania wengne tunahusikaje mchaguen mgalatia mwenzenu awe papa sio rais watz na bado mmesahau kuna masister weng 2 kawazin mpaka mwisho kampora mke wa mtu..
Mafanikio ya kanisa mimi mpagani yananisadia nini?Ungeanalyse jinsi gani ubunifu wake ulivyolisaidia TAIFA .