Wasiomjua Dr. Slaa soma mada hii, kabla ya uanasiasa na baada

mkuu pandisha kiwango tujadili mada; ni afadhali ya mbichi zinalika hizi zimevunda na kuoza kabisa; mkuu tunakula vitu fda approved hivi vya majalalani hata matonya (r.i.p) vilimshinda.

Chama
gongo la mboto dsm

naona umejitoa akili unatema matope
 
Nenda pale karibu na Forodhani kuna bookshop mojawapo ambayo ni zao la TMP Book department ambayo ni publisher, book seller na book distributor. Zomba mambo mengine kuyaelewa unahitaji uyafanyie utafiti vinginevyo tunaandika vingi ambayo hujavijua ninaendeshwaje na vipoje.

Bookshop ya Forodhani (St. Joseph) ipo toka Slaa bado hajaanza shule au kabla ya kuzaliwa, mie nafunguwa macho naikuta na nimezaliwa kabla ya "Uhuru".
 


images

Dr. Slaa

Dr. Slaa si mtu mwenye maneno mengi, ni mtulivu na mkimya kiasi chake, lakini akipanda jukwaani na kuanza kulishambulia huku na kule huwezi kuamini kinachotoka ubongoni mwake. Kimya kingi kina mshindo.

Wengi hawamfahamu Dr. Slaa vilivyo, wengi wanamwona sasa baada ya kuingia bungeni na sasa katika majukwaa ya siasa, ukweli ni mtu mbunifu, mpenda maendeleo na mwenye kujitoa kwa ajili ya wengine bila kujibakiza. Ufahamu wangu wa huyu Dr. Slaa ni wa muda mrefu, lakini wengi wetu wanachukulia mambo ya juu juu tu bila kujua undani na utendaji uliotukuka wa mtu huyu.

Machache kati ya mengi kuhusu Dr Slaa kabla ya kuwa mwanasiasa, kuwa Mwanasiasa na hatimaye kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, ana mlolongo wa mambo mengi ambayo yanaonyesha ubunifu wa hali ya juu, na pia mwepesi kuwaelewa vijana na kuendana nao tofauti na watu wengine wa kizazi chake.

Pamoja na kuwa mwanachama wa CCM, baada ya kuombwa na Wanakaratu agombee ubunge kule baada ya kuchoshwa na mbunge aliyekuwepo wakati huo, CCM iliendelea na mizengwe ile ile kama iliyotokea juzi pale Dodoma kuwaengua watu wanaofaa kwa uongozi. Wanakaratu wakiamua hawataki longolongo, wakamsihi kwamba wameamua awe mbunge wao na wakamwomba achague chama kingine agombee kwani hawamtaki kabisa mbunge aliyepo. Kwa ridhaa ya wananchi akaamua kujitoa CCM na kujitosa kujiunga na Chadema ili agombee ubunge kuridhia matakwa ya wanakaratu.

Kabla ya kuwa mwanasiasa
kuna mengi ya maendeleo ambayo wengi tunayaona huku tusijua kama Dr. Slaa ndiye aliyebuni na kuyaendesha kama ifuatavyo.
  1. Dr. Slaa ndiye amekuwa wa kwanza Tanzania kuagiza big truck for load and unload makontena bandari ya Dar es Salaam wakati akiwa Katibu Mkuu TEC. Ilikuwa ni miaka ya 1980th, hakukuwa hata kampuni au watu binafsi waliothubutu kufanya hivyo. Truck hilo lilikuwa na crane za kupakia na kupakua bila taabu kokote linalokifkishwa container na kwa truck hilo. Baadaye makampuni yakabembeleza wauziwe gari ile, ndipo Barala La maaskofu likawauzia.
  2. Kwa mara ya kwanza baraza la Maaskofu Tanzania lilipoanza kuwa na matumizi ya computer ikiwepo ofisi yake Dr Slaa kama katibu Mkuu, na taasisi za upashanaji habari ambazo zilikuwa chini ya uongozi wake ikiwa ni pamoja na:

  • Gazeti la kiongozi kuanza kutumia mfumo wa computer katika idara ya set up
  • TMP (Tanganyika Mission Press) Kipalapala idara ya uchapishaji (printing) wakitumia Apple computers.
  • TMP Book deparment Tabora mjini) idara ya maduka ya vitabu na usambazaji vitabu wakitumia Apple computers
  • TAPRI idara ya tungo za mawasiliano vitabu TEC iliyokuwa na ofisi zake Seiminari kuu Kipalapala Tabora.

Idara hizo zilikuwa na matumizi ya computer na PageMaker & QuakExpress software ambazo kwa graphic designers ilikuwa kitu kigeni kisichozoeka bado Tanzania ukitilia maanani wakati huo tulikuwa na chuo kimoja tu cha ardhi kule Tabora kujifunzia Graphic Design kabla ya Ardhi Dar haijaanza kukamilika. Huo ni ubunifu wa Dr. Slaa kwa wakati huo wakati wengi Tanzania hawajafunguka kuhusu matumizi ya teknologia ya ulimwengu wa dot com.

NB.
Wakati huo chuo pekee cha mawasiliano (journalism) Tanzania kilikuwa ni Nyegezi-Mwanza pekee kilichokuwa kikiongozwa na AMECA (Balaza la Maaskofu Katoliki Afrika Mashariki na Kati kimoja kikiwa Kitwe - Zambia, cha Nyegezi kiliendeshwa na TEC Dr. Slaa akiwa msimamizi mkuu kama Katibu Mkuu.​

Dr. Slaa atakumbukwa sana kwa makubwa aliyofanya kujenga na kuikuza TEC

  1. Makao makuu ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) tunayoona siku hizi ni matunda ya ubunifu wa Dr. Slaa alipokuwa Katibu Mkuu pale. Jengo la awali ni lile lililo upande wa mbele zinapotumika ofisi siku hizi ambapo yalikuwa madarasa ya shule ya sekondari ya Masisita Tanzania, ambayo baadaye ilihamishiwa Bigwa Morogoro kupisha kiwanja hicho kuwa makao ya Maaskofu Katoliki Tanzania, awali yalikuwa pale ofisi za St. Joseph, Dar es Salaam. TEC aliyoikuta DR. Slaa ilikuwa na jengo hilo la madarasa na jengo lilolokuwa la utawala wa shule. Dr. akabuni majengo ambayo tunayoana sasa, hata kama hayakukamilika yote waliofuata walikamilisha kazi alioyoianza.
  2. Kaone maendeleo na majengo katika jimbo la Mbulu ni jitihada za Dr. Slaa na Fr. Narda ambao kwa pamoja walifanya makubwa.
  3. Kaangalie jimboni kwake huduma za kijamii ambazo amezifanya, utachoka mwenyewe kiasi ambacho CCM imekimbiwa kabisa huko sababu utendaji wa Slaa huko na CCM ni sawa na kulinganisha mlima na kichuguu.
  4. Dr. Slaa kwa tunaomfahamu ni mwanamapinduzi na mpenda maendeleo, na pengine mengi alikuwa anayafanya yakaonekana mapya mno kwani alikuwa anaona mbali kuliko hawa wakubwa wake, ila sipendi kuliongelea sana hilo.

Chadema yaimarika baada ya Dr. Slaa kuwa mgombea urasi uchaguzi Mkuu uliopita.

Siyo siri Chadema hakikuwa na nguvu tunayoona sasa hivi licha ya kuwa na sera nzuri, lakini leo tunaona nguvu ya Chadema inayoogopewa mno na CCM ni kutokana na Chadema katika dakika za majeruhi kuamua kumwangukia Dr. Slaa agombee urasi ambao Samweli Sitta aliingia mitini baada ya makubaliano nao. Tangu hapo Chadema imekuwa na nguvu ya ajabu.

Je, vijana hao waliokuwemo ndani ya Chadema kabla ya Dr. Slaa kugombea Urais kwa nini hawakuipaisha juu Chadema kama sasa? Baada ya Dr. Slaa kuipaisha Chadema juu sasa tunakuja na kauli mbiu ya kubeza makubwa yaliyofanywa na hawa mnaowaita kizazi cha kabla ya uhuru. Hapana tuwe waungwana, pamoja na kila mmoja kuwa na haki za kugombea nafasi tusigeuze uhuru huo kuwabeza hawa ambao wametufikisha tulipo, na bado tunahitaji mchango wa ushauri, uongozi, hekima na busara zao. Uongozi bora ni kuchanganya mapya na ya kale kwani
viatu vya zamani vyaijua njia.

Ubunifu wa Chadema viongozi wakiwa mojawapo waliozaliwa kabla ya Uhuru Dr Slaa na Kamanda Mbowe:

  • Dr. Slaa ndiye mbunge ambaye baada ya kuingia bungeni alianza kuchangamcha kwa kuichambua serikali na kasoro zake kitu ambacho katika mabunge yaliyotangulia wabunge walikuwa ni rubber stamp ya serikali.
  • Chadema wakiwemo hao unaoona walizaliwa kabla ya uhuru wamebuni mapya katika shughuli na kampeni za uchaguzi Tanzania kuwa zenye mvuto kuanzia mkuktano wa ufunguzi wa kampeni uchaguzi Mkuu uliopita ulifanyika Kidongo Chekundu baada ya Dr. Slaa kushusha makumbora mazitomazito kuituhumu serikali, watendaji wa serikali na CCM, tuhuma ambazo CCM wanazidi kubabaika kuwanyoshea kidole wahusika kisha kuwakumbatia tena hivi karibuni kule Dodoma.
  • Mkutano wa Kidongo chekundu Dar es Salaam ndio ulioanza kutufungua macho na masikio Watanzania na kuanza kujifunza elimu ya uraia ambayo tulikuwa tunazibwa na CCM tusiijue.
  • Dr. Slaa ndiye aliyetufunza na kutufunua kwamba raia wanayo nguvu ya kuiadabisha serikali haki zao za msingi zinapokiukwa kwa kauli mbiu ya nguvu ya umma (peoples power).
  • Utumiaji wa chopper kufikia maeneo magumu kufikika kwa magari na kurahisisha kazi ya kampeni, CCM wakaiga.
  • Kuwa na magari yanayotumika kama majukwaa ya mikutano badala ya kupoteza gharama na muda kujenga majukwaa yatakayotumika kwa dakika chache.

Ilani ya Uchaguzi Chadema ndiyo inayotumika na yenye uzito sasa hivi:


  • Fukuto la Katiba mpya linaloendelea sasa nchini ni uzao wa ilani ya Chadema na ilani ya Dr Slaa kwamba kinachofuata baada ya Uchaguzi mkuu ndani ya siku 10
  • Kikwete kufanya mabadiliko ya barala la mawaziri mara kadhaa ni kutokana na shinikizo la wabunge wa Chadema bungeni.
  • Serikali kubana matumizi ya ziada ili kuokoa pesa za walipa kodi

Kuna mengi tu wachangiaji wengine watachangia, ni dhana potovu kuwa na fikra za aina hiyo na kuwabeza wabunifu wa mengi, waliongoza nchi hii, wenye kuturithisha mengi kwa uzoefu na busara zao na walioongoza nchi hii hadi kuwa na utulivu wa aina yake. Leo vijana mnaowasema yanayojilia ni amani kusambaratika na mauaji ambayo ilikuwa hadithi za kusimuliwa kutoka nchi nyingine, leo serikali ya CCM inayoongozwa na Rais kijana kuliko Rais mwingine aliyemtangulia imetwishwa na aibu kubwa ya kitaifa na kimataifa ya mauaji ya raia wasio na hatia.

Kuna nchi ambazo ni kielelezo cha vijana ambao mimi ningewaita watoto kukabidhiwa madaraka ya kuongozia nchi na kusababisha maafa makubwa kwa nchi husika kama Liberia, Ujerumani chini ya Hittler, na kinachoendela huko Zaire ya sintofahamu.

Vijana achaneni na uroho wa madaraka, vema kubaki watumishi na watendaji wazuri serikalini na vyamani kujifunza mbinu za uongozi na kupata uzoefu katika kuongoza nchi.

Kuongoza nchi hakuna shule wala kitabu cha kusomea au chuo. Hekima na busara ya mtu ndio kielelezo cha fanaka katika kuongoza nchi.

  • Vijana wana papara,
  • wanataka njia ya mkato,
  • pagumu wanataka kulazimisha bila busara wala kutumia akili
  • Vijana wanalipuka kama moto wa gas
  • mambo yakigeuka magumu ni mabavu hutumika.
Mkuu Candid Scope umeelezea mazuri sana ya Dr Slaa kana kwamba wengine hawapo, anapokuwepo.

Katika CHADEMA je umaarufu wa chama umepatikana single handedly kwa KUDUMU FIKRA ZA DR SLAA ?
Na je kina Makani, Ngwilulpi, Mtei waanzilishi mbona hawamo kwenye hiyo historia yako?

Mbowe je? Na kujitolea kwake?
Hii isiwe njia tu ya kupolish image ya Dr Slaa kabla ya kutangaza nia ya kuombea Urais, atangaze tu watu wamchambue kwa ndani.

Umeelezea YALIYOPITA ya Dr Slaa ingawaje si kikamilifu.
Je falsafa yake katika kututoa waTanzania kutokana na maadui walewale yaani Ujinga,magonjwa na dhuluma(utawala bora), ziko wapi?
Mipango mikakati ya maendeleo ya nchi kwa ujumla ameiainisha sehemu gani ili watu tuweze kusoma.

Lazima tutambue Watanzania kuwa kuongoza nchi si juhudi za mtu binafsi peke yake, ingawaje kuwa na mtu mwenye mawazo chanya insaidia sana.
 
Dk.Slaa ni almasi ya chadema na ya watanzania wapenda mema.
Mungu ambariki sana.
 
Hoja zako zipo personal sana so peleka kule jukwaa la mapenzi na mahusiano au fcbk na utapata majibu unayoyataka coz humu ni siasa mwanzo mwisho.

Be a guy

Wewe bora ukae kimya tunajadiana na Candid Scope kiungwana.
 
Last edited by a moderator:
Poor analysis
Fool of bias.
Wewe na molemo mkajipange upya!
Wewe una mchango gani, au una taarifa gani hadi kumdharau mtoa mada? Hii ni wasifu bayana, tena kuna mengi tu mazuri hajayaandika humu. naye kasema hivyo. Wewe unakurupuka na kuropoka bila kutoa fact.
 
kwa uhakika unaonesha jinsi unavyosukumwa na kitu fulani humu jamvini lakini sio great thinker upo upo tu kwa ajili ya kitu fulani maana huelezi cha maana kwemye kila hoja wewe ni kutoa yale uliotumwa.

ukisema imeandikwa kiwango cha chini maanake nini wapi ni kitu gani poor you....fooolish thinker

Sijaanza mjadala rasmi mmeanza matusi; sasa nikiingia si mtatoka povu? Saint Ivuga anagalia watu wako wanavyotaka kuharibu majadala

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Mafanikio ya kanisa mimi mpagani yananisadia nini?Ungeanalyse jinsi gani ubunifu wake ulivyolisaidia TAIFA .
 
Bookshop ya Forodhani (St. Joseph) ipo toka Slaa bado hajaanza shule au kabla ya kuzaliwa, mie nafunguwa macho naikuta na nimezaliwa kabla ya "Uhuru".

Hujanielewa, naijua vizuri historia ya vitu hivi. Bookshop ya St. Joseph nakuonyesha kwamba ni uzao wa TMP book department ya Tabora ambayo inaendesha publishing, bookseller na distribution kwa maduka mengine kama hayo nchini kama St Joseph Bookshop, Moshi Bookshop nk. Vitabu vyake vinachapishwa kule kule Tabora na TMP Printing Department iliyoko Kipalapala. Unachoona bookshop pale St. Joseph Bookshop ni uzao wa TMP Printing Department na TMP Book Department vilivyoko Tabora.

Idara hizo awali zilikuwa zinaendeshwa na White Fathers, alini siku TMP inaendeshwa na Benedictine Monks na ile Book Department inaendeshwa na Grail Sister wa Same/ Kilimanjaro.

Nilichoeleza ni kwamba Dr. Slaa alisanivu update ya taasisi hizo kwa kuanzisha mfumo wa kutumia computer. Zamani Printing Press ya Tanganyika Missiona Press (TMP) ilikuwa inatumia mitambo ya kizamani ya monotype ya kurudufu herufi kwa kuchapa kutumia mfumowa letter press.

Wakati wa Dr. Slaa mfumo huo aliubadilisha na kuanzisha mfumo wa computer ambayo uchapaji wake ni wa kisasa kwa kutumia offset printing.

Jaribu kusoma vizuri maelezo yangu, maana inaelekea hukunielewa bado.
 
yan kaz aliyafanya ni kulitumikia kanisa sasa watanzania wengne tunahusikaje mchaguen mgalatia mwenzenu awe papa sio rais watz na bado mmesahau kuna masister weng 2 kawazin mpaka mwisho kampora mke wa mtu..
 
Mkuu Candid Scope umeelezea mazuri sana ya Dr Slaa kana kwamba wengine hawapo, anapokuwepo.

Katika CHADEMA je umaarufu wa chama umepatikana single handedly kwa KUDUMU FIKRA ZA DR SLAA ?
Na je kina Makani, Ngwilulpi, Mtei waanzilishi mbona hawamo kwenye hiyo historia yako?

Mbowe je? Na kujitolea kwake?
Hii isiwe njia tu ya kupolish image ya Dr Slaa kabla ya kutangaza nia ya kuombea Urais, atangaze tu watu wamchambue kwa ndani.

Umeelezea YALIYOPITA ya Dr Slaa ingawaje si kikamilifu.
Je falsafa yake katika kututoa waTanzania kutokana na maadui walewale yaani Ujinga,magonjwa na dhuluma(utawala bora), ziko wapi?
Mipango mikakati ya maendeleo ya nchi kwa ujumla ameiainisha sehemu gani ili watu tuweze kusoma.

Lazima tutambue Watanzania kuwa kuongoza nchi si juhudi za mtu binafsi peke yake, ingawaje kuwa na mtu mwenye mawazo chanya insaidia sana.

Ukiangalia na kusoma vizuri mada hii sijasema wengine hawakufanya mazuri kukijenga Chadema, ila nimesema Chadema imeanza kupaa kwa nguvu sana baada ya Dr. Slaa kugombea urais.

Timu za mpira utasikia jina la mchezaji fulani anayefunga mabao kwa wingi kuiwezesha timu kupata ushindi. Hii haina maana anacheza uwanja mzima peke yake, timu nzima inacheza kufa na kupona, anayejitokeza kwa namna ya pekee ni yule mahiri wa kutikisa nyavu.

Natanguliza shukrani kama utanielewa kwa jibu hilo.
 



Kuna nchi ambazo ni kielelezo cha vijana ambao mimi ningewaita watoto kukabidhiwa madaraka ya kuongozia nchi na kusababisha maafa makubwa kwa nchi husika kama Liberia, Ujerumani chini ya Hittler, na kinachoendela huko Zaire ya sintofahamu.

Huko kwingine kote labda unaweza kuwa umepatia mpaka hapo kwa Kamanda Adolf Hitler hapo umechemka mbaya yaani, huwezi kumweka Kamanda Hitler kundi moja na hao vilaza, Huyo jamaa alikuwa ligi nyingine kabisa, acha kabisa yani!
 
yan kaz aliyafanya ni kulitumikia kanisa sasa watanzania wengne tunahusikaje mchaguen mgalatia mwenzenu awe papa sio rais watz na bado mmesahau kuna masister weng 2 kawazin mpaka mwisho kampora mke wa mtu..

Please, mimi mleta mada nimeleta kwa maana nzuri ya kuonyesha wasifu kisiasa wa mhusika, matusi kama hayo wengine wenye ustaarabu hatuja yazoea na wala kanisa likohudumia hawajatoa wala kulalamikia hayo unayoongea wewe. Tuachane na chuki za kiwango hicho vinginevyo kishe mmoja toka familia yako akiwa chama tofauti utakuwa kumchukulia jambia kumbe ni ushindana kwa hoja tu na mfumowa wa njia ya kupita tunakotaka kufika ni kumoja ingwa njia nyingine ni rahisi zaid. Hesabu ni moja lakini ina njia nyingi za kupata jibu.
 
kinacho nishangaza mimi ni kuona mpaka leo hii bado kuna vijana wako CCM!!! Zamani nilikuwa nafikiria kwamba tukifika mwaka 2005 vijana wote wangekuwa opposition waungane pamoja kuiondoa madarakani.KITENDO CHA NCHI YETU KUWA MASIKINI MPAKA LEO NI SABABU TOSHA YA KUIFURUSHA MADARAKANI HII SERIKALI DHALIMU.Dr waukweli ongoza mapambano hadi kieleweke.
 
Huko kwingine kote labda unaweza kuwa umepatia mpaka hapo kwa Kamanda Adolf Hitler hapo umechemka mbaya yaani, huwezi kumweka Kamanda Hitler kundi moja na hao vilaza, Huyo jamaa alikuwa ligi nyingine kabisa, acha kabisa yani!

Nimebahatika kukaa Ujerumani kwa nusu mwaka hivi, na wengi hasa wazee walioishi kipindi cha Adolf Hitler, huwezi kuamini wanavyomwona dhalimu wa kupindukia na matatizo aliyowasababishia hadi kuishia kuchimba viazi kwa mikono sababu ya nguvu zote za uchumi kupeleka kupigana vita. Inatisha na wanatoa machozi wangine wakikusimua, na inatia huruma sana. Wazee wengi wanasema ujana wake ni tatizo mojawapo kwani hakuwa tayari kusikia ushauri, aliendesha serikali kiimla.
 
yan kaz aliyafanya ni kulitumikia kanisa sasa watanzania wengne tunahusikaje mchaguen mgalatia mwenzenu awe papa sio rais watz na bado mmesahau kuna masister weng 2 kawazin mpaka mwisho kampora mke wa mtu..

Udini udini udini!!!! mpaka lini wa-Tz.
Badala ya kujadili mada au kuiacha ipite kama huna cha kujadili, unaandika utumbo kama huu na kuingiza mawazo finyu ya udini na tuhuma za kejeli. Halafu nawe unajiita great thinker, oh ghosh!
 
Back
Top Bottom