BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,377
- 8,120
Msanii wa Comedy kutoka Kenya, amekuwa akifanya vitu ambavyo kikawaida tumezoea kuona vikifanywa na wanasiasa kwa lengo la kutafuta huruma za wananchi waje kumpigia kura wakati wa uchaguzi. Ingawa pia, inaweza kuwa ni pia mipango ya Erico, you never know.
Lakini kitendo cha kufanya tu hivyo vitu ikiwemo kusaidia watu wenye shida mbalimbali kwa kuchangisha fedha au misaada. Pia amekuwa akikosoa waziwazi sera za Serikali yake hadi kuna kipindi alifungwa jela mwezi mmoja lakini akatoka baadaye mapema.
Sasa hivi kaanza kuwatafutia watu kazi ambapo leo amepokea maombi ya watu zaidi ya 12,300 wakihitaji connection zake.