HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,566
Dear Miss Judith,
Nimesukumwa na upendo mwingi wa dhati uliojaa furaha kukuandikia waraka huu mfupi kukupongeza na kukutakia heri ktk maisha yako mapya ya ndoa unayokaribia kuyaanza hivi karibuni, taarifa niliyoipata kupitia thread yako ya Mwaka Mpya na Maisha Mapya... Ooh, Glory to God!
Maamuzi haya si madogo, ni maamuzi ya kuunganisha koo mbili zilizokuwa hazifahamiana na kujikuta zikijenga umoja wa kifamilia na undugu. Hapa ndipo Mawifi, Mashemeji, Wajomba, Mashangazi, Mama Mdogo, Wakwe na ndg wengine wapya huzaliwa.
Ndoa mara nyingi hufurahiwa na wengi, lakini pia wapo wachache ambao kamwe hawafurahii kusikia taarifa hizi. Wapo ambao wangependa kuona hufanikiwi, wanapenda kukuona ukiharibikiwa, mipango yako ikikwama na hufurahia kuona ukikosa furaha na amani ktk maisha yako. Watu hawa huanza kama marafiki na baadaye kukuletea umbea na maneno mabaya. Kataa maneno ya umbea, chuki, majivuno, kiburi, infedility na mengine yafananayo na hayo! Utapoteza ndoa!
Nakushauri, ili ndoa yako idumu, jitahidi sana kutimiza majukumu yako kama mama wa kiafrika. Mpende Mumeo, kumbuka kuwa Kazi ya mama ni kutunza familia, contrary na kazi ya baba ambayo ni kulinda familia! Maandiko yanasema Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake na mpumbavu huvunja nyumba yake , pia baba ni kichwa cha nyumba Ubeijing usikutawale sana, ukizidi ni hatari, nimeshuhudia ukivunja ndoa nyingi. Pika, fua na shiriki kazi za ndani ukisaidiwa na msichana/mvulana wa kazi. Upendo huo, utamvuta baba pia akusaidie ktk majukumu ya ndani. Nakushauri ujifunze kuwa mnyenyekevu kwa mumeo, atakupenda, kukusaidia na kamwe hata kuacha.
Usijisahau ukasema mumeo mtarajiwa kaokoka hivyo hawezi kukamata nyumba ndogo, utakuja kulia! Tumeshuhudia watumishi wa Mungu wakinasa ktk kupata utamu usio halali! Kumbuka kumchunga kwa kumuombea na kumtunza vyema. Mfanye aone nyumbani ni sehemu ya kimbilia au tulizo la moyo wake, atakupenda daima.
Sababu za kuvunjika ndoa, ni nyingi na baadhi yake ni kutokuwa muaminifu ktk ndoa, kutokuwa na upendo wa dhati, tamaa za pesa & mali, kutokujisheshimu, kukosa mapenzi ya dhati, kulipiza kisasi, ndoa kuingiliwa na ndg, majirani & marafiki, kutokuridishana ktk mapenzi, mitazamo tofauti nk. Jiepushe na hayo ili udumu ktk ndoa yako.
Kuna yale mambo mema ambayo mlionyeshana wakati wa uchumba wenu.Yale mema na mazuri yaliyowasukuma mpaka mkaamua kufunga pingu za Maisha, hayo myadumishe, yatawadumisha pia. Usisahau mipango ya maendeleo. Kumbuka kuwapenda ndg wa pande zote, ila usiwape nafasi ya kutawala ndoa, ishi nao kwa hekima hasa mawifi!
Nakutakia mema yote ya ndoa yakukute. Ndoa yako izae matunda ya watoto wa kukutosha, wake kwa waume, na amani na upendo utawala familia yako Mpya.
Mungu awe nawe daima,
Wako,
HorsePower
Nimesukumwa na upendo mwingi wa dhati uliojaa furaha kukuandikia waraka huu mfupi kukupongeza na kukutakia heri ktk maisha yako mapya ya ndoa unayokaribia kuyaanza hivi karibuni, taarifa niliyoipata kupitia thread yako ya Mwaka Mpya na Maisha Mapya... Ooh, Glory to God!
Maamuzi haya si madogo, ni maamuzi ya kuunganisha koo mbili zilizokuwa hazifahamiana na kujikuta zikijenga umoja wa kifamilia na undugu. Hapa ndipo Mawifi, Mashemeji, Wajomba, Mashangazi, Mama Mdogo, Wakwe na ndg wengine wapya huzaliwa.
Ndoa mara nyingi hufurahiwa na wengi, lakini pia wapo wachache ambao kamwe hawafurahii kusikia taarifa hizi. Wapo ambao wangependa kuona hufanikiwi, wanapenda kukuona ukiharibikiwa, mipango yako ikikwama na hufurahia kuona ukikosa furaha na amani ktk maisha yako. Watu hawa huanza kama marafiki na baadaye kukuletea umbea na maneno mabaya. Kataa maneno ya umbea, chuki, majivuno, kiburi, infedility na mengine yafananayo na hayo! Utapoteza ndoa!
Nakushauri, ili ndoa yako idumu, jitahidi sana kutimiza majukumu yako kama mama wa kiafrika. Mpende Mumeo, kumbuka kuwa Kazi ya mama ni kutunza familia, contrary na kazi ya baba ambayo ni kulinda familia! Maandiko yanasema Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake na mpumbavu huvunja nyumba yake , pia baba ni kichwa cha nyumba Ubeijing usikutawale sana, ukizidi ni hatari, nimeshuhudia ukivunja ndoa nyingi. Pika, fua na shiriki kazi za ndani ukisaidiwa na msichana/mvulana wa kazi. Upendo huo, utamvuta baba pia akusaidie ktk majukumu ya ndani. Nakushauri ujifunze kuwa mnyenyekevu kwa mumeo, atakupenda, kukusaidia na kamwe hata kuacha.
Usijisahau ukasema mumeo mtarajiwa kaokoka hivyo hawezi kukamata nyumba ndogo, utakuja kulia! Tumeshuhudia watumishi wa Mungu wakinasa ktk kupata utamu usio halali! Kumbuka kumchunga kwa kumuombea na kumtunza vyema. Mfanye aone nyumbani ni sehemu ya kimbilia au tulizo la moyo wake, atakupenda daima.
Sababu za kuvunjika ndoa, ni nyingi na baadhi yake ni kutokuwa muaminifu ktk ndoa, kutokuwa na upendo wa dhati, tamaa za pesa & mali, kutokujisheshimu, kukosa mapenzi ya dhati, kulipiza kisasi, ndoa kuingiliwa na ndg, majirani & marafiki, kutokuridishana ktk mapenzi, mitazamo tofauti nk. Jiepushe na hayo ili udumu ktk ndoa yako.
Kuna yale mambo mema ambayo mlionyeshana wakati wa uchumba wenu.Yale mema na mazuri yaliyowasukuma mpaka mkaamua kufunga pingu za Maisha, hayo myadumishe, yatawadumisha pia. Usisahau mipango ya maendeleo. Kumbuka kuwapenda ndg wa pande zote, ila usiwape nafasi ya kutawala ndoa, ishi nao kwa hekima hasa mawifi!
Nakutakia mema yote ya ndoa yakukute. Ndoa yako izae matunda ya watoto wa kukutosha, wake kwa waume, na amani na upendo utawala familia yako Mpya.
Mungu awe nawe daima,
Wako,
HorsePower