Waraka wa Pili wa Mbunge kwa Wananchi wa Jimbo la Ubungo na watanzania

Nafahamu uzito wa shughuli zako ni Ubungo kwanza. Ubunge ni zaidi ya Ubungo. Ni nini msimamo wako juu ya haya:
-Posho. Kokote ziliko. Bado unazichukua?
-Udini. Huu unainyemelea NCHI yetu taratibu lakini kwa uhakika.
-Bunge. Bunge letu sasa ni kubwa sana. Dar peke yake ina majimbo 7 ya uchaguzi! Ya nini yote haya. Kudai maji toka DAWASCO?
-VITI MAALUM vya Ubunge. Hizi gharama zinazoambatana na viti hivi na uwingi wa viti vyenyewe na jinsi wanavyopatikana unalionaje?
-etc.,etc.


Wildcard,

Asante kwa maswali yako.

Kuhusu posho, nimeshasema: JOHN MNYIKA: Msimamo wangu juu ya suala zima la Posho!, kimsingi sichukui posho kwenye vikao vyote vya madiwani vya Manispaa, vikao vyote vya Jiji, Vikao vyote vya RCC, na bodi ya barabara. Kwa wanaohudhuria nami vikao hivyo wanajua kwamba sina kawaida ya kuchukua. Pia, posho za vikao vya kamati za kibunge ikiwemo kamati ya nishati na madini huwa wakileta mkononi nazikataa. Hata hivyo, hivyo naamini zaidi katika mabadiliko ya kimfumo zaidi ya kuwa suala la mtu mmoja au kada moja katika utumishi wa umma. Ukisoma waraka wangu wa pili kwa wananchi wa ubungo utapata pia nalichukuliaje suala la posho za vikao.

Kuhusu udini, naamini kwamba wapo viongozi ambao wanapandikiza mbegu hiyo kwa maslahi yao ya kisiasa ndio maana kwenye mchango wangu wa kwanza kabisa bungeni nilikemea hali hii na bado ni maoni yangu kwamba kadiri tunavyopigia upatu suala la udini ndio tunapandikiza mbegu hiyo. Tusiingizwe katika mitego ya kuondolewa kwenye mijadala muhimu ya kitaifa, unaweza kurejea hapa:JOHN MNYIKA: Hotuba yangu Bungeni katika Mkutano wa Pili

Kuhusu Bunge na Viti Maalum; nimekuwa nikipigia debe suala la kubadilishwa kwa mfumo wetu wa uchaguzi ili tuwe na mfumo mchanyato/mchanganyiko baina ya wabunge wa kuchaguliwa moja kwa moja na wabunge kutokana na uwakilishi wa uwiano. Nakubaliana na wote wenye maoni kwamba wilaya/halmashauri zetu ndio ziwe majimbo ya kiuchanguzi; kwa kufanya hivyo tutapunguza pia ukubwa wa bunge. Mathalani Dar es salaam nzima itakuwa na wabunge wa kuchaguliwa moja kwa moja watatu; wengine watatokana na uwakilishi wa uwiano. Hii itawezesha pia kuboresha mfumo wa uwakilishi wa wanawake ili uwe na tija zaidi. Unaweza kurejea uchambuzi wangu wa mwaka 209 kuhusu suala hili kupitia: JOHN MNYIKA: Tubadili mfumo wa uchaguzi tupate uongozi bora wenye uwiano wa kijinsia-2Kuhusu sheria ya mabadiliko ya katiba, nashauri uusome kwanza huu waraka kwa ukamilifu wake kwa kuwa maswali uliyouliza mengine waraka tayari umeshayajibu.


Tuendelee kujadiliana.

JJ
 
Hongera mh mnyika, kweli sikupoteza kura yangu. Mungu akusaidie kutimiza wajibu wako kikamilifu.
 
Heshima yako mheshimiwa mnyika watu wa ubungo wanatembea kifua mbele kuwa mwakilishi wao. Nipo jimbo la Kawe na kamanda Halima mdee , huku ameushughulikia vizuri mgogoro wa ardhi ,vipi kuhusu majimbo ya kawe na Ubungo kupakana chini uwakilishi wa chadema...mkakati wa kimaendeleo kwenye hii zone ya chadema ili ccm ifutike kabisa ukoje??? Naomba majibu mh.mbunge JJM .
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Asante kamanda pamoja sana; kila unyao wako unapokanyaga hapo Mungu amekupa so onyesha njia wengine wafuate nyuma kila siku!
 
Mh. Mnyika big up kwa sana. Bado tunaomba ufuatilie suala la kibosile wa dawasco kujiunganishia maji kata ya Mbezi Lois mtaa wa Makabe baada ya kufanikiwa kuuzima mradi wa maji uliokuwa unatekelezwa na wachina, na kwa sasa amekua suplier mkubwa wa maji eneo hili kwa bei ya tsh 200 kwa ndoo.

Anawezapia kusambaza maji usiku na kujaza matenki na visima majumbani kwa garama kubwa kwa kuunganisha mipira/mabomba marefu inayosemekana ameyafisadi hukohuko dawasco. Plse Mnyika do something, maana jitihada za kuwaona viongozi wengne wa eneo akiwepo diwani zimegonga mwamba. tunashindwa kujua labda nao wamebloo kwa huyo jamaa "jimama" la dawasco.

Huduma ya Maji kwa wapiga kura wako ni miongoni mwa ahadi na vipaumbele vyako. Fika ujionee misururu mireeeefu ya raia na ndoo za maji. Daah, safari mbado ndefu.

Asante; unaweza kuongeza maelezo ya ziada na kama kuna vielelezo ukanipatia? Anaitwa nani na yuko nyumba gani? Kuhusu Makabe kuna fedha tumetenga toka kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo la Ubungo kwa ajili ya by pass. Aidha, kuna hatua ambazo tulikubaliana na DAWASCO siku ile ya maandamano ya maji. Kwa sasa kuna tatizo la maji limeongezeka kutokana na baadhi ya mabomba kuharibiwa na mafuriko. Tuendelee kushirikiana mpaka kieleweke

JJ
 
heshima yako mkuu, MI NINGEPENDA KUJUA JE NI KWELI SERIKALI YA TANZANIA IMEFILISIKA KABISA?
 
Katika waraka wangu wa kwanza kwenu niliwapa mrejesho kuhusu uwakilishi wa Mbunge katika mkutano wa pili wa Bunge. Nawaandikia waraka huu “Uhuru na Mabadiliko” katika mwaka 2011 wa kumbukumbu ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika ambayo sasa inaitwa Tanzania bara.

Lengo la waraka huu wa pili (Tazama Kiambatanisho) ni kuungana nanyi katika mwaka huu kutafakari kila mmoja wetu kuhusu taifa letu lilipotoka, lilipo na tunapotaka liende katika kipindi cha miaka 50 toka Uhuru na kutumia fursa hiyo pia kutafakari kuhusu jimbo letu katika kipindi cha mwaka mmoja toka uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na kuwatakia heri ya mwaka mpya wa 2012.

Waraka huu wote, isipokuwa aya ya kwanza na aya hii ya tatu, niliuandika tarehe 9 Disemba 2011; hata hivyo sikuutoa siku hiyo kutokana na ‘macho na masikio’ ya wengi kuelekezwa katika ‘sherehe’ za siku hiyo pamoja na matarajio kuhusu hotuba ya Mkuu wa Nchi kugusa masuala mapana kuhusu mwelekeo wa taifa. Nimeona niutoe waraka huu katika kipindi cha kuelekea mwisho wa mwaka, na ni wakati muafaka wa kutafakari zaidi baada ya ‘sherehe’ kwa kuwa mpaka sasa Rais Jakaya Kikwete hajatoa hotuba nyingine ndefu kama alivyoahidi tarehe 9 Disemba na pia taifa linamaliza majonzi yaliyotokana na maafuriko yaliyoleta maafa katika mkoa wa Dar es salaam.

Kwa hali hii ni wakati muafaka wa kurudi nyuma na kutafakari kiwango cha fedha tulichotumia kwenye ‘sherehe’ za uhuru; huku taifa likiwa halina hata vifaa vya msingi vya uokoaji wakati wa maafa. Ni wakati muafaka wa kutafakari, ‘mafanikio’ ya miaka 50 ya uhuru, tukiwa na matatizo ya mipango miji na kutetereka kwa misingi ya utawala wa sheria katika mkoa wa Dar es Salaam ambao ulitangazwa kuwa jiji mwaka huo huo wa uhuru.

Nimeutoa waraka huu leo katika kata ya Mabibo jirani na Loyola eneo ambalo linabeba kumbukumbu ya kihistoria kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kwa Jimbo la Ubungo. Hivyo waraka huu umedokeza baadhi ya wajibu wa msingi ambao mbunge ameutekeleza katika Jimbo la Ubungo katika kipindi cha mwaka mmoja.

Naelewa kwamba wapo wengine ambao walitumia mwaka huu wa 2011 wa maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru kufanya ‘sherehe’ ama kufanya ‘maonyesho ya kijeshi’, lakini binafsi nimeona pamoja na yote niwaandikie tutumie kutafakari. Ni wakati wa kila mmoja wetu kujiuliza ameifanyia nini nchi na pia kujiuliza nchi na wananchi wenzake wamemfanyia nini katika miaka 50 ya uhuru wetu. Tafakari hii haiwezi kuwa ya siku moja ya tarehe 9 Disemba bali ni mchakato endelevu wa kujitambua na kuchukua hatua. Tuna kila sababu ya kukumbuka na kuadhimisha siku ya uhuru, lakini hatuna sababu nyingi za kusherehekea tena kwa gharama kubwa tukilinganisha baina ya umri, rasilimali na mafanikio tuliyoyapata.

Tunaelezwa kwamba Tanganyika ilipata uhuru bila kupigana vita hivyo maonyesho ya kijeshi ni ishara tu ya kujipanga kwetu katika kulinda uhuru wa mipaka yetu; lakini ilipaswa sikukuu ya leo iwe ni ya kuonyesha matunda ya miaka 50 ya uhuru.
Mwaka 1958 wakati Mwalimu Julius Nyerere akihutubia Umoja wa Mataifa (UN) kutaka Uhuru wa Tanganyika dhidi ya mkoloni alieleza kwamba tunapodai uhuru kutoka kwa Waingereza sio kwamba tunataka ili watupe tu utawala, bali ni kwa sababu wameshindwa kuondoa umaskini, wameshindwa kuelimisha Watanganyika na pia wameshindwa kutoa huduma za afya.

Tarehe 9 Disemba 1961 kupitia hotuba zake mbili kwa nyakati na matukio tofauti Nyerere akarudia kuwatangaza maadui watatu wa taifa- umaskini, ujinga na maradhi na akataka kila mmoja awapige vita. Siku hiyo hiyo, Nyerere akatangaza kuwa adui mkubwa ni umaskini! Miaka michache baada ya uhuru akarejea kumtaja adui mwingine mkubwa zaidi ambaye aliwahi kumweleza hata wakati wa kudai uhuru; naye ni ufisadi. Kwa hiyo vita yetu kwa sasa ni ya maadui wanne; ufisadi, umaskini, ujinga na maradhi. Katika kutathmini tulipotoka, tulipo na kupanga tunapotaka kwenda ni muhimu tukawatazama maadui hawa miongoni mwetu wananchi na katika nchi yetu kwa ujumla.

Nawashukuru tena kwa kunipa heshima ya kunituma kuwawakilisha na kuwatumikia kwa kadiri nilivyowaomba kupitia uchaguzi ili kuunganisha nguvu za pamoja katika masuala ya kitaifa bungeni lakini pia tukiweka mkazo katika utekelezaji wa ahadi jimboni kwa kuweka kipaumbele kwenye; Akili, Ajira, Miundombinu, Maji, Uwajibikaji, Usalama, Ardhi na Afya (AMUA).

Kimsingi kazi tatu kuu za mbunge ambazo zinatokana na mamlaka ya bunge kwa mujibu wa ibara ya 63 ya katiba ni; Mosi kuwakilisha (representation) wananchi, pili ni kutunga sheria (legislative) na tatu ni kuisimamia serikali (oversight) kuweka mazingira bora ya maendeleo kwa mwananchi mmoja mmoja na nchi kwa ujumla.

Kama sehemu ya uwakilishi na usimamizi mbunge ana wajibu pia wa kuunganisha nguvu ya umma jimboni kuhamasisha maendeleo kupitia mfuko wa maendeleo ya jimbo na wadau wengine.

Mwishoni mwa mwaka tutatoa Jimboni Ubungo taarifa ya kina ya utekelezaji ya kata kwa kata lakini katika waraka huu nitaeleza baadhi katika muktadha wa kutafakari mabadiliko ya nchi yetu kiuchumi, kisiasa na kijamii miaka 50 baada ya Uhuru wa Tanganyika.

Waraka huu ni kwa ajili ya wote wenye kuamini kwamba uhuru wa kweli, si uhuru wa bendera bali ni uhuru dhidi ya umasikini, ujinga, maradhi na ufisadi. Uhuru wa kweli, ni uhuru wenye kuleta maendeleo kisiasa, kijamii na kiuchumi. Uhuru huu ni wenye mabadiliko ya kweli, yenye kuhimili misukosuko ya ukoloni mamboleo; na kujenga taifa lenye kutumia vizuri rasilimali katika kutoa fursa kwa raia wake.

Ili uhuru wetu uweze kuwa wenye matokeo kwenye maisha yetu na ya taifa letu tunahitaji kuungana kufanya mabadiliko ya kweli. Changamoto kubwa ambayo nimeiona ni kwamba kuna udhaifu katika mifumo yetu ya kiserikali kwenye ngazi mbalimbali hali ambayo inakwaza hatua za haraka za kuleta mabadiliko.

Kwa pamoja tunapaswa kuendelea kulitoa taifa letu katika kufilisika kimaadili na kiitikadi na kukubaliana tunu za kitaifa zenye kuwezesha misingi ya uwajibikaji. Uhuru wa kweli wa kisiasa utakuja kwa kuwa na uongozi wenye maono (vision) na maadili (values) na kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika kipindi cha kuanzia sasa na kuendelea kutuwezesha kunufaika na rasilimali zetu: iwe ni vipaji vyetu, kodi zetu au maliasili za nchi yetu.

Binafsi, jambo kubwa ambalo nimelifanya katika kipindi cha mwaka mmoja ni kutimiza majukumu ya kibunge ya uwakilishi, usimamizi na kutunga sheria kwa kuwa na utaratibu wa kufanya mikutano na wananchi, kuwa na ofisi ya mbunge inayohudumia umma na kuwasilisha masuala husika kwa kwa mamlaka mbalimbali bungeni, maofisini, manispaa na kwa njia nyingine mbalimbali. Ni dhamira yangu kuendeleza uwajibikaji tunapokwenda ili kuunganisha nguvu ya umma kila mmoja aweze kutimiza wajibu kwa nafasi yake.

Nihitimishe kwa maneno ya Nyerere kwa taifa siku ya uhuru wa Tanganyika tarehe 9 Disemba 1961 akiwaeleza wananchi kuhusu utendaji kazi wa baraza lake dogo la mawaziri 11 tu: “..mimi na wenzangu ni watumishi wenu ninyi mnaonisikiliza. Tunajua kuwa mnatuamini, nanyi tunawaamini. Na ni ninyi mnaotupa nguvu zetu tunazozihitaji kwa kazi kubwa iliyo mbele yetu…Na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu tutajitahidi kuwatumikieni bila kujitafutia faida zetu wenyewe au fahari ya cheo”. Uhuru na Kazi, Uhuru na Mabadiliko.

Nawatakia heri ya mwaka mpya wenye upendo, furaha na mafanikio tukiweka mstari wa mbele ukweli, uadilifu, na uwajibikaji katika maisha yetu.

Wenu katika utumishi wa umma,

John Mnyika (Mb)
Jimbo la Ubungo
26/12/2011

Nakubaliana sana na wewe Mh Mbunge wetu,natumai hata sie Kinondoni tungekuwa na mchapa kazi kama wewe,kwa uchungu sana naomba nipate msimamo wako kuhusu watoto wasiokuwa na hatia waliofutiwa majibu na ofisi ya elimu Dar,mwanangu alikuwa shule moja ambayo ni tishio jijini na alikuwa namba moja tangu aingie shule hiyo akiwa darasa la nne,mwanangu pamoja na kuwa juu alikuwa akiamka saa kumi na moja alfajiri kila siku ili awahi kutekeleza majukumu yake shuleni,shule hiyo pia walimu wake walikuwa wakifanya kazi kila siku kwa nguvu sana ili watoto wafaulu,na hii ilihusisha mpaka siku za mapumziko,cha kushangaa,mwanangu ni moja ya watoto ishirini na kitu best waliofutiwa matokeo,naomba kujua pia msimamo wa CHADEMA kwa hili,hawa watoto madhara wanayopewa kisaikolojia na CCM kuwa hautakiwi kusoma sana kwani ukifaulu utakuwa umefundishwa na mwalimu au umeibia?ina maana watu wa elimu walitaka watoto wasipate majibu sawa?kwani mtihani wa darasa la saba siku hizi majibu hayafanani?

Je inawezekana mtu kwenda mahakamani kushtaki ofisi ya elimu kwa hili ili watoto wapewe haki yao na waombwe msamaha kwa upuuzi wa ofisi ya elimu?kuna wakati Lukuvi alikana maneno ya Mr II kwamba Tanzania hakuna haki,lakini kweli haki haipo,na unaisikilizia vizuri unapoguswa moja kwa moja kama hili la mwanangu. Sikatai wale wasio na uwezo na wakafaulu wasichukuliwe hatua,lakini naunga mkono walimu wanaohakikisha watoto wote wapo juu na hakuna anayeachwanyuma kama shulehii iliyo wilaya ya kinondoni.

Nina hasira sana,mwanangu amefanya majaribio ya shule 2 bora za binafsi zenye mitihani migumu kulikohata hiyo yao na alifaulu na atakwenda moja wapo,lakini naona kama ameathirika sana kisaikolojia,anahisi kujiandaa na kufaulu sana ni kosa,huko mbele atafanyeje?

Msaada Mh Mbunge wetu
 
Mnyika toka umechukua Ubunge hatukuoni JF unatisha mdogo wangu sii vizuri kuwasahau wale waliokupa support kubwa ukawa nawe mtu ktk watu ....samahani lakini maana wabunge wengi wa Chadema baada tu ya ushindi wamekimbia JF wanasema ati kijiwe hiki hakifai lakini hawakuyaona zamani..
 
Wakati ukiukumbusha Umma kuhusiana na tumetoka wapi na sasa tuko wapi, INAKUWAJE MHESHIMIWA MBUNGE HUZUNGUMZII SUALA LA KUONGEZEKA GEPU LA WALIONACHO NA WASIONACHO?.

NI VIPI HUZUNGUMZII UNYONYAJI UNAOFANYWA NA WABUNGE KUJILIPA POSHO YA KIKAO KIMOJA SAWA NA MSHAHARA WA MWEZI MZIMA WA MLALAHOI?.

UNA CREDIBILITY GANI YA KUWAELEZA WAPIGA KURA WAKO JUU YA MIIKO YA UONGOZI WAKATI WEWE MBUNGE UNAENDELEA KUCHUKUA POSHO KUBWA AJABU WAKATI NCHI NA JIMBO LAKO NI MASIKINI KUPINDUKIA?- KWA NINI HUWI MFANO WA KUIGWA KWA KUKATAA UNYONYAJI HUU NA KUACHA KUCHUKUA HIZI POSHO, ILI WANANCHI WA UBUNGO WAELEWE UNAPIGANA VITA VYA UMASIKINI KWA MATENDO NA SI MANENO?.
 
adui wa tz ni ufisadi tu mengine yote hutoka humo, ni nani asikilize kilio cha watesekao tz?
 
Bravo kamanda Mnyika. Nimekukumbuka siku moja ndani ya treni 2005 ulipokuwa unatoka kigoma kwenda dar jinsi ulivyokuwa unahoji uhalali na umuhimu wa shule za kata bila kuwa na maandalizi ya rasilimali watu na fedha. Aisee kama ungeendelea na upadre nchi ingekosa mtu muhimu ktk fani ya siasa. Endelea kukamua mwanangu tutafika tu, hivi vikwazo vya sasa visikuvunje moyo mkuu
 
Hawa ndo viongozi tunaowalilia kila siku katika taifa letu,.its a nice report Mr Mnyika.
Keep it up,.tunategemea mengi zaidi siku zijazo.
 
Mnyika toka umechukua Ubunge hatukuoni JF unatisha mdogo wangu sii vizuri kuwasahau wale waliokupa support kubwa ukawa nawe mtu ktk watu ....samahani lakini maana wabunge wengi wa Chadema baada tu ya ushindi wamekimbia JF wanasema ati kijiwe hiki hakifai lakini hawakuyaona zamani..

Kaka Mkandara,

Hunitendei haki, naonekana JF ingawa si mara kwa mara. Na hali hii ya kutoonekana baadhi ya nyakati haikuanza baada ya kuwa mbunge, naomba urejee tu mijadala yetu ya miaka kadhaa nyuma utabaini kwamba hata kabla ya kuwa mbunge wakati mwingine nilikuwa nakosa wasaa wa kuonekana mara nyingi kutokana na majukumu mengine. Hali hii itaendelea hivi siku zote; tuvumiliane. Tuendelee na utumishi wa umma, mpaka kieleweke

JJ
 
Mnyika toka umechukua Ubunge hatukuoni JF unatisha mdogo wangu sii vizuri kuwasahau wale waliokupa support kubwa ukawa nawe mtu ktk watu ....samahani lakini maana wabunge wengi wa Chadema baada tu ya ushindi wamekimbia JF wanasema ati kijiwe hiki hakifai lakini hawakuyaona zamani..

Mkuu Mkandara! nadhani hii comment ungemuuliza Zitto, kimsingi ndio kahama kabisa kila wakati yupo FB o twitter, Kamanda Mnyika mara kwa mara tunamuona jamvini na hii thread ushahidi lini umeona thread ya Zitto kila kitu anacoment faceBook alivukuwa mnaa...
 
tuna wabunge takribani 360+ tanzania hii, ukiwa na 50 tu wenye upeo kama huu tusingelikuwa tunalala giza totoro, maji shida, na ku sign mikataba usiku wa manane--

SARA / DUA kwa mafisadi kufunga mwaka 2011.

ee mwenezi mungu kwenye rehma tele, tuongoze sisi waja wako tupate kuchagua viongizi bora wenye uzalendo ili waweze kutuongoza vyema kwa haki na usawa kama vile ulivyoagiza wewe kwamba mamlaka na nchi zetu zitambulike na kuheshimwa.

Wapunguzie nguvu zao hao wabunge waroho na wenye njaa kali wanaouza mali za nchi yetu kwa mikataba feki ili kufikia 2012 waweze kuacha tabia yao hiyo wakurudie wewe na pia watutumikie sisi wananchi maskini na wanyonge, waondolee tamaa ya kujifikiria wao wenyewe tu (ubinafsi) kwa posho na vikao bila kufikiria hali ya wananchi wanaowaongoza ilivyo.

Tunapomaliza mwaka huu ee mwenyezi na kukaribisha mpya wa 2012 wajalie wabunge wazalendo tu hekima na afya njema, hasa namuombea mbunge wangu wa Ubungo umpe hekima na afya aendelee kutuongoza kwa haki na upendo kama afanyavyo sasa. Washindwe na walegee wabunge wote wanafiki ambao kila kukicha wanajifanya wanatujali kumbe ni ndumilakuwili, waporaji wakubwa wa mali za umma tena bila aibu, mungu mwenyezi uwatengee adhabu yao ya milele kutokana na makosa yao kama hawatajirekebisha siku ya kupokea mwaka mpya; kwani kila siku wanakuja mbele za madhabahu na miskitini wakijidai wanakuomba kumbe wanafiki watupu. tena wengine wakitoa mamilion ya hela kwa ajiri ya michango ujezi wa nyumba zako baba mwenyezi (makanisa na misikiti) kumbe hela hizo ni za wizi mtupu.

eee mwenyezi mungu wewe ni mkuu na unajua yote yanayofanyika nchi kwetu na utaweza kabisa sasa kuchukua hatua maana sisi wanao tulio maskini na mafukara tunateseka sana na hawa jamaa tumewashindwa kwani wana mbinu nyingi mno; hata kwenye sanduku la kura tumewashindwa kabisa kuwaondoa kama ulivyoshuhudia wewe mwezi oct 2010.

Kwa uchungu mkubwa, mimi mwanao kwa niamba ya watanganyika wenzangu tusio na matumaini na thamani tena ya maisha ndani ya nchi yetu hii uliyotujalia wewe kuwa na mali nyingi. mwisho baba nakukabidhi nchi hii mikononi mwa uangalizi wako tunapoenda kuanza mwaka mpya wa 2012. amin.
 
Mkuu Mkandara! nadhani hii comment ungemuuliza Zitto, kimsingi ndio kahama kabisa kila wakati yupo FB o twitter, Kamanda Mnyika mara kwa mara tunamuona jamvini na hii thread ushahidi lini umeona thread ya Zitto kila kitu anacoment faceBook alivukuwa mnaa...

mara ya mwisho Zitto ndani ya JF siyo kipindi kile yuko India?? Ndiyo akililalamikia Tz Daima na Mwanahalisi,na wamiliki wao!
 
Kaka Mkandara,

Hunitendei haki, naonekana JF ingawa si mara kwa mara. Na hali hii ya kutoonekana baadhi ya nyakati haikuanza baada ya kuwa mbunge, naomba urejee tu mijadala yetu ya miaka kadhaa nyuma utabaini kwamba hata kabla ya kuwa mbunge wakati mwingine nilikuwa nakosa wasaa wa kuonekana mara nyingi kutokana na majukumu mengine. Hali hii itaendelea hivi siku zote; tuvumiliane. Tuendelee na utumishi wa umma, mpaka kieleweke

JJ
Haya basi my mistake..lakini pia sintosita kusema niyaonayo na yananikera japokuwa...
Unajua zamani ulikuwa ukija kujibu hoja kufafanua hoja, sera na ilani ya chama pale watu wanapochapia lakini siku hizi naona Chadema haina watetezi hapa janvini mmejikita sana FB tweet na majanvi ya FoS na Wanajamii. Mtanisamehe lakini simuoni Zitto wala Dr. Slaa mara kwa mara wao wakianzisha mada ama kutujuza yatokanayo maana mzigo wa janvi hili wala sio mdogo na wala msiupuuze kama wengine...

Mwaka 2015 wala sii mbali kumbukeni kukiuza chama ni kazi mlochaguliwa ndani ya sekretariet ya chama pamoja na kuwa na majukumu mengine ya Kitaifa hivyo mzigo mkubwa mnao na pengine ili kurahisisha kazi zetu pengine ni wakati muafaka mkaachia ngazi za ndani ya chama washike wenye nafasi...Siasa za leo zinatembea ktk mtandao zaidi hivyo sikatai kulitumikia Taifa lakini pia kumbukeni watu wana uchu wa kuwaulizeni maswala muhimu japokuwa kutakuwa na wale wenye malengo machafu..hapo nyuma nimesoma mtu alouliza maswali mazito na sijaona jibu lolote..
 
Mungu akubariki uwe na afya iliyo bora ili uweze kuendelea na jitahada za kuokoa taifa kutoka kwenye mikono ya maharamia wenye kuhaha nchi nzima kwa lengo la kujaza matumbo yao yasiyo jaa, tena wametengeneza na network yakuwa waingiza watoto wao kwenye system ili waendelee kujaza umasikini kwenye mifuko ya Watz.
 
Bigup sana mh. Mnyika na pole kwa majukumu mengi najua unachoka sana kibinadamu ila mungu akutie nguvu na faraja. Naomba kuuliza juu ya daraja la ubungo msewe sijui kama kuna mpango gani labda kwa sasa au baadae.
 
Back
Top Bottom