Waraka wa Pili wa Mbunge kwa Wananchi wa Jimbo la Ubungo na watanzania

Bigup sana mh. Mnyika na pole kwa majukumu mengi najua unachoka sana kibinadamu ila mungu akutie nguvu na faraja. Naomba kuuliza juu ya daraja la ubungo msewe sijui kama kuna mpango gani labda kwa sasa au baadae.


Asante. Daraja muhimu zaidi la Msewe tulilipigia debe mwaka jana na huu kama sehemu ya kupunguza foleni na hatimaye TANROADS wamelijenga na limeanza kutumika. Tatizo ni maafuriko ya tarehe 20 Disemba yamevunja daraja lingine la mwanzo (sio hili jipya), hili tayari nimeshatembelea na kuona hali halisi wakati tunashughulikia kifo cha Mzee Ibrahim pale darajani. Kazi hii itagharimu kati ya milioni 200 mpaka 300; tayari kupitia kwa Manispaa ya Kinondoni ofisi ya Waziri Mkuu imejulishwa kuingiza kwenye mahitaji ya dharura. Nitaendelea kufuatilia ili serikali iweze kuchukua hatua za mapema. Hata hivyo kwa sasa nawaomba mtumie njia mbadala ya Kimara Bahama mama na kupitia daraja la Msewe jipya mpaka Chuo Kikuu au mnaweza pia kupitia njia ya Golani.

JJ
 
Hongera sana John kwa waraka unaolezea mambo mengi muhimu not only kwa wana Ubungo bali kwa Taifa pia......

Leo nimara ya pili nasoma ripoti/waraka kutoka kwa Waheshimiwa wa Chadema.....i.e. Regia na Mnyika

Notwithstanding kwamba presentation ya Regia inahitaji maboresho.......lakiniilikuwa na mvuto wa aina yake kuisoma

Pamoja na vision uliyonayo....presentation ya waraka wako inahitaji courage kuisoma (in my opinion).......sijui wana-ubungo wangapi watausoma au watapata ujumbe.......nilikuw anapendekeza yafuatayo kwako

  1. weka sehemu/sections kwenye waraka wako zenye kuleta mvuto kwa msomaji kulingana na kazi zako za kibunge (Uhuru na Madiliko ya uchumi, kisiasa, kijamii.......yeah ni nzuri lakini they are too theoretical.....in my opinion)
  2. Tumia vijarida (uweke habari fupi fupi)
  3. Tengeneza video clips na vitu mfano wa public service announcements kupitia redio (sometimes unaweza kuweka short clips kwa wananchi wako kupitia TVs)
  4. Umefanya vitu vingi......onyesha kwa uwazi Jimbo lilikuwa vipi before you and one year under you Vs ahadi zako (usisahau kuelezea challenges though)
So far so good........well done! and keep it up!.........
 
A true leader is recognized from his own action which is the product of his perception. Good start bro keep it up
 
Asante. Daraja muhimu zaidi la Msewe tulilipigia debe mwaka jana na huu kama sehemu ya kupunguza foleni na hatimaye TANROADS wamelijenga na limeanza kutumika. Tatizo ni maafuriko ya tarehe 20 Disemba yamevunja daraja lingine la mwanzo (sio hili jipya), hili tayari nimeshatembelea na kuona hali halisi wakati tunashughulikia kifo cha Mzee Ibrahim pale darajani. Kazi hii itagharimu kati ya milioni 200 mpaka 300; tayari kupitia kwa Manispaa ya Kinondoni ofisi ya Waziri Mkuu imejulishwa kuingiza kwenye mahitaji ya dharura. Nitaendelea kufuatilia ili serikali iweze kuchukua hatua za mapema. Hata hivyo kwa sasa nawaomba mtumie njia mbadala ya Kimara Bahama mama na kupitia daraja la Msewe jipya mpaka Chuo Kikuu au mnaweza pia kupitia njia ya Golani.

JJ

Matengenezo ya daraja lililoharibiwa na maafa nayo yameanza, kesho nitakuwa na ziara ya kufuatilia yanaendeleaje.

JJ
 
Back
Top Bottom