Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Saloon hizi zina mambo............................!
Jana nilikwenda kunyoa hizi mvi zangu, nilikuta kuna wateja wananyolewa katika saloon hiyo, hivyo ilibidi nikae nje kusubiri huku nikisoma gazeti langu. Pembeni ya hiyo saloon kulikuwa na saloon nyingine ya kike na hapo nje walikaa kina dada wakisukana. Mara akapita kijana mmoja wa pale mtaani ambaye ninafahamiana naye, tulisalimiana kisha akapita na hamsini zake wale kina dada walianza kumjadili……………
"Shoga unamuona yule kaka alivyo mzuri, yaani ana sura nzuri utadhani mwanamke." Alisema dada mmoja kati ya wale kina dada.
"Mwenzangu hayo macho je? Mwanaume ana macho mazuri kama nini, na kifua chake mmekiona? Na huo ndio ugonjwa wangu….." Alidakia mwenzake.
Mwenzao mmoja ambaye alikaa kimya akiwasikiliza alidakia...... "Ni mzuri ndio, lakini kizuri hakikikosi kasoro?"
Wale wenzie wakamuuliza ana kasoro gani?
"Hana kazi mwenzangu..........Yuko mtaani tu na anashinda vijiweni na jioni utamkuta uwanjani anajifanya kocha anafundisha mpira timu ya watoto wa hapa mtaani........... " Alijibu yule dada.
"sasa hiyo ndio kasoro?" Mwenzake mmoja alidadisi........
"Hee, mwanaume asiye na kazi atamtaka nani? Nani atamtaka mwanaume suruale........" Yule dada alijibu kisha wote wakacheka kwa pamoja kwa kebehi................
Duh, mazungumzo yale yalinifanya nitafakari.... Hivi siku hizi mwanaume asiye na kazi huchukuliwa kwamba ana kasoro!
Nilibaki mdomo wazi.