Wanafunzi wengi wanafuja posho wanazolipwa

John W. Mlacha

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
3,504
1,341
Wanafunzi wengi wanafuja posho wanazolipwa
Imeandikwa na Mwalimu Stanislaus Kigosi; Tarehe: 14th July 2011 @ 23:20 Imesomwa na watu: 136; Jumla ya maoni: 0


07_11_kphvp1.jpg

Wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu wakiandamana kudai nyongeza ya posho.

Habari Zaidi:

WANAFUNZI wa vyuo vya juu wamekuwa na madai mengi, mojawapo ikiwa ni kutaka kuongezwa posho.

Nimekuwa nikitafakari kuhusu madai ya wasomi wetu hao, kwamba wanaweza kutafakari vipi juu ya hicho wanachokililia. Sina wivu wala ugomvi na madai yao, lakini napata kigugumizi kuhalalisha madai yao.

Nitatoa ufafanuzi hatua kwa hatua ili tuone ni kwa kiwango gani sasa wasomi wetu, wanakuwa na ubinafsi uliopindukia kiasi hiki. Madai ya wanafunzi wa vyuo vikuu hayajaanza mwaka huu wala si kuwa kizazi hiki cha baada ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere – kumekuwapo madai yasiyo na ukomo.

Nakumbuka kuna siku nilikuwa nikiongea na mmoja wa wanafunzi wa zamani wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), waliosoma nchi ilipotoka kupata Uhuru, ikiwa na mahitaji makubwa sana ya wataalamu wa fani mbalimbali.

Kutokana na uchache wao, wanafunzi walikuwa wakigharamiwa kila kitu na Serikali. Walikuwa wakipata mlo kamili ambao hata katika familia zao ilikuwa ni simulizi ya kusadikika.

Alichoniambia huyu mkongwe ni hiki; “sisi ndio tuliofaidi elimu ya chuo kikuu. Mnaingia chuoni na kukuta kila kitu kipo pale – Serikali imewawekea.” Nadhani huyu mzee alisahau kuwa ni kodi za Watanzania walizokuwa wakizitumbua.

Jambo la kustaajabisha ni kuwa hata katika mlo wao wakikuta eti mkate umekuja bila siagi, basi walifanya mgomo wa kula na kuingia madarasani. Ni kweli waliishi maisha ya raha mustarehe.

Wakati huo huo hakusita kusema ukweli kuwa vitu hivyo kwa mara ya kwanza katika maisha yake alianza kuvitumia akiwa chuo kikuu. Hakuwahi kuvipata mahali pengine popote. Hivyo ukweli ulio hapo ni kuwa wao kama wasomi waliongozwa na choyo na tamaa ya kula na kusaza wakati sehemu kubwa ya Watanzania wakiwa masikini vijijini.

Kuna siku Mwalimu Nyerere, nasimuliwa, aliwahoji wanafunzi wa UDSM baada ya kugoma kuingia madarasani kwa sababu ya kupungua yai moja katika mlo wao: “Je, tuongeze kiwango cha kuwatoza kodi wazazi wenu ili kuweza kupata yai la ziada katika mlo?”

Hapa ndipo inapolala hoja ya kuwa asije akatokea mwanafunzi yeyote wa elimu ya juu akadhani kuwa ni Serikali ndiyo inampa fedha; hiyo ni kodi ambayo wakulima na wafanyakazi wa taifa hili tunakamuliwa ili wanafunzi wasome.

Nikumbushe kuwa mnamo 2008 nchi ilishuhudia mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu, hasa vile vya Serikali, ambao nadhani utaendelea kukaa katika historia ya migomo hapa nchini kwa muda mrefu bila kusahaulika.

Mpaka leo naamini kuwa ule ulikuwa ni mgomo wa haki na wenye kubeba uhalisi wa maisha ya Watanzania wengi. Ulikuwa mgomo ambao wanafunzi walitaka waondolewe mzigo wa ada katika mabega yao na mabega ya wazazi wao.

Wanafunzi hawakudai kupewa fedha ya mfukoni, madai yalikuwa kupata ada kwa asilimia 100. Walitambua kuwa ule ulikuwa ni mkopo na ada inakwenda moja kwa moja chuoni bila kupitia katika mikono ya wanafunzi.

Walikuwa tayari kuendelea kupata fedha ya kujikimu katika kiwango kile kile, lakini walau mzigo wa ada upunguzwe.

Matokeo yake walifukuzwa vyuoni kama waasi. Nami nilikuwamo. Lakini walau tulirudishwa kwa masharti magumu kiasi, na waliofuata baadaye walikuta walau Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imefanya marekebisho ya kuridhisha kwa kiwango fulani, mabadiliko ni vita.

Lakini tu naomba nitofautiane na madai ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa sasa kutaka kuongezewa fedha ya kujikimu wanapokuwa vyuoni.

Nitapenda kutoa mifano na maelezo ya kina ni kwa nini madai ya wanafunzi wa elimu ya juu, na pengine makundi mengine ya wasomi kutaka kupata sehemu kubwa kuliko watu wengine ambao nao ni raia halali wa taifa hili.

Kwanza ieleweke wazi kuwa wanafunzi wa elimu ya juu kudai kupewa Sh 10,000 kama fedha ya kujikimu kwa siku, maana yake ni kuwa kwa mwezi wanafunzi hawa watakuwa wakijipatia si chini ya Sh 300,000 isiyokuwa na makato yoyote.

Japokuwa hapo kuna madai ya kuwa fedha hiyo ndiyo inayotumika kulipa sehemu ya ada au sehemu ambayo Bodi ya Mikopo inakuwa haijawalipia, vijana wenzangu watambue kuwa fedha hiyo wanayodai ni kubwa mno, hasa tukizingatia kuwa hawazalishi chochote zaidi ya kutumia kilichozalishwa na wengine.

Labda kama hili hawalijui, kuna watu wanalipwa mshahara wa mwezi wa Sh 162,000. Hao ni watumishi wa Serikali wala si wa sekta binafsi. Tukiwa na vigezo kuwa wao wanaishi Dar es Salaam na wamepanga mitaani, hoja hii haina mashiko ya kutosha, kwa sababu kwanza si vyuo vikuu vyote viko Dar es Salaam.

Kuna vyuo viko Iringa, Mbeya, Mwanza na kadhalika. Watu walio katika maeneo hayo nao wakiwa na malalamiko kama ya wenzao wa Dar es Salaam, basi hapo kinachotawala ni uchoyo na hulka ya ubinafsi kwa wanafunzi hawa.

Nikirudi kwa wanafunzi walioko vyuo vya Dar es Salaam, wajaribu kumfikiria mtumishi niliyemtaja anayelipwa mshahara wa Sh 262,000. Anapanga mtaani na ana watoto anaowasomesha.

Hivi kati ya hawa wawili – mwanafunzi wa chuo kikuu na huyu mzazi anayelitumikia taifa ni yupi anastahili kuonewa huruma? Bila kuweka ubinafsi wala uchoyo mbele, kimsingi huyu ambaye tayari ni mzalishaji anatakiwa kuonewa huruma na kupewa kipaumbele ili awe na tija kwa taifa.

Ni kweli kuwa fedha wanayopewa wanafunzi wa elimu ya juu ni kidogo, lakini pia anayopewa huyu mtumishi ni kidogo vilevile. Lakini kitu kimoja wanafunzi wengi wa elimu ya juu wanashindwa kuonesha ni nidhamu ya matumizi katika hiyo fedha kidogo wanayopewa.

Ukitaka kujua kuwa wanafunzi wengi wamekosa nidhamu katika fedha hiyo, tazama kipindi ambacho vyuo vinafunguliwa au kipindi ambacho wanafunzi wamelipwa hiyo fedha ya kujikimu.

Matamasha ya bei mbaya yanakuwa yameandaliwa, na wanafunzi hao hawaoni shida kutoa kwenda kuhudhuria. Nakumbuka nikiwa chuoni, kipindi chuo kinapofunguliwa watu walikuwa na kawaida ya kuandaa matamasha hayo, na kinachotokea watu wanafuja sana fedha kwa anasa na starehe za muda mfupi.

Katika mazingira ya kawaida, hata ukimwambia mtu kuwa fedha haitoshi, atabaki akikutazama na asikuelewe, kwani ameshaona jinsi unavyoifuja fedha hiyo.

Nimalizie kwa kusema kuwa, sasa ni wakati wa wanafunzi na kundi zima la wasomi kukaa na kuwafikiria Watanzania masikini wasiokuwa na uhakika wa mlo japo mmoja kwa siku, ili nao waishi kwa amani na matumaini huku kwa pamoja tukiunganisha nguvu dhidi ya ufisadi.

Mwandishi ni Mwalimu katika Shule ya Sekondari Nyumbu iliyoko Kibaha. Pia ni mwanaharakati wa haki za binadamu na mambo ya vijana katika siasa.


Simu: +255 754 257 251 au +255 714 801 893, Barua pepe: stanislaussenior@yahoo.com
 
Ni kweli , Nina shemeji yangu yupo muccobs ndo mwaka wa kwanza tulifight hapa Dar akapata mkopo 60% akala km m3 hivi, alikuwa ni mlevi balaa, kwanza zile pesa zilimfanya aswekwe ndani, nasikia alimpiga askari bar wakamsweka rumande! miezi minne mbele yaani wiki mbili zimepiata kaja town dar na GIRLFRIEND wake wote ni wanafunzi hapo chuoni, wanataka kufanya biashara so wanakwenda kariakoo kununua viatu ili wakauze huko Moshi. Nikajiuliza sikupata jibu, lkn hii mikopo wanayopata hawaitumii ipasavyoo kama inavyotakiwa. na dogo bado anatumiwa pesa na wazazi wake. Nahisi miezi minne ijayo atakuwa hana hata shilingi!
 
Ni kweli , Nina shemeji yangu yupo muccobs ndo mwaka wa kwanza tulifight hapa Dar akapata mkopo 60% akala km m3 hivi, alikuwa ni mlevi balaa, kwanza zile pesa zilimfanya aswekwe ndani, nasikia alimpiga askari bar wakamsweka rumande! miezi minne mbele yaani wiki mbili zimepiata kaja town dar na GIRLFRIEND wake wote ni wanafunzi hapo chuoni, wanataka kufanya biashara so wanakwenda kariakoo kununua viatu ili wakauze huko Moshi. Nikajiuliza sikupata jibu, lkn hii mikopo wanayopata hawaitumii ipasavyoo kama inavyotakiwa. na dogo bado anatumiwa pesa na wazazi wake. Nahisi miezi minne ijayo atakuwa hana hata shilingi!
kwa hiyo unataka apunguziwe pesa?
 
kwanza ngoja niweke wazi kabisa kuwa mimi sio mwanafunzi wa elimu ya juu, ila nipingana na mleta mada moja kwa moja, ni kweli kuwa wanafunzi wanadai wapewe shilingi 10,000 kwa siku na ni kweli kiwango hiki ikijulisha kwa mwezi ni 300,000 ambazo mfanyakazi wa kima cha chini hapa nchini hapati. lakni nadhani mwandishi amesahau kufafanua matumizi ya hizo 10,000 kama angeleta pia na matumizi halisi ya wanafunzi hawa kwa siku huko vyuoni kwao tukalinganisha na madai yao ya 10,000 hapo tungeweza kuhukumu vyema kama ni kweli kiwango hiki ni kikubwa sana au la! Kwa ufahamu wangu ni kuwa hizi pesa 10,000 ni kwa ajili ya meal and accomodation allowance na matumizi ya ziada hebu tuangalie mchakato wa matumizi ya hii 10,000 kwa siku kwa huyu mwanafunzi wa elimu ya juu ( mtaalam mtalajiwa anaetakiwa kuyafahamu na kuyaelewa vyema mafundisho darasani, kumbuka ukiwa na njaa huwezi elewa): Chai asubuhi= 1000, Chakula mchana =2500, Chakula usiku=2500, maji kwa siku= 1000, accomodation kwa siku=600 ( hii ni kwa wale wanaokaa hosteli), usafiri kwa siku 1000; jumal ni shilingi 8600. Hapo huyu mwanafunzi bado hajapata mahitaji yake mengine ya lazima kama sabuni, dawa ya meno, hajafua nguo zake, na kwa wanafunzi wa kike ndio zaidi. sasa kwa mazingira haya unawezaje kusema 10,000 ni nyingi sana na wakati huo huo tunataka huyu mwanafunzi azingatie mafundisho yake darasani!
 
duh chakula 2500 sio kweli sijui upo eneo gani kama udom chakula 1000 tu na jion 1000 na asubuhi 1000 na maji 1000 accomodation 500 still hela yabaki, mi naungana na wanaotaka hela iongezwe lakini mi nipo tofauti kidogo na wenzangu mi nashauri pattern za mkopo ziongezwe

kuwe na mkopo wa usafiri mkopo wa vitu vidogovidogo kama kiwi, sabuni, vocha n.k manake vitu hivi huwakost wanafunz watoe hela yao ya meals
 
We mtoa mada unataka 2ishi kama wewe ulivyoishi 2008? Afu we mwenye ndugu mlevi kwa iyo una make cönlusion kwa sample ya m2 mmoja?hamna jipya
 
Dk. Kawambwa alisema Tume
maalumu ya kuangalia
matatizo yanayoikabili HESLB
iliyoundwa na Rais Jakaya
Kikwete mwanzoni mwa
mwaka huu, imebaini pia
Tanzania inakopesha kiasi
kikubwa cha mkopo kwa kila
mwanafunzi tofauti na nchi
nyingine.
Alitoa mfano kwamba mwaka
2010/11, Sh bilioni 237
zilitengwa kwa ajili ya
wanafunzi 85,000. “Wastani
wa mkopo kwa mwanafunzi
Tanzania ni Sh milioni 2.8 kwa
mwaka, Ghana ni Sh milioni
0.6 na Kenya ni Sh milioni
1.2,” alisema.
Akimuusia Mwenyekiti wa
Bodi ya Heslb, Profesa Anselm
Lwoga, Waziri alisema,
“Pamoja na jitihada zote hizi,
bado yamekuwapo malalamiko
kutoka kwa wanafunzi kuwa
mikopo haitoshi. Hii ni
changamoto ambayo Bodi yako
inatakiwa iitafutie ufumbuzi”.
Alisema katika ripoti hiyo ya
Tume Maalumu, wadau wengi
wakiwemo wanafunzi, vyuo na
wananchi kwa ujumla
wameonesha kutoridhika na
utendaji kazi wa Bodi kiasi cha
kupendekeza ifanyiwe
mabadiliko.
Alisema yapo mapendekezo
yanayohitaji uamuzi wa
Serikali na mengine yanahitaji
kutekelezwa mara moja na
Wizara yake kupitia Bodi ya
Wakurugenzi.
“Wakati maoni na shutuma
zilizojitokeza zinafanyiwa kazi,
ni matumaini yangu kuwa Bodi
yako itaona umuhimu
unaostahili kwa kuyafanyia
kazi masuala yote ya kero ili
mwisho wa yote muweze
kurudisha imani ya wadau kwa
Bodi ya Mikopo,” alisema
Waziri.
Akielezea changamoto zaidi
ambazo Bodi hiyo ya Mikopo
inabidi izifanyie kazi, Dk.
Kawambwa alisema
urejeshwaji mikopo ni eneo
ambalo Heslb haijafanya vizuri.
Aliishauri iweke mikakati ya
ukusanyaji madeni kutoka kwa
waliokopeshwa ikiwemo
kutoza madeni riba.
Alisema Serikali haiwezi
kuendelea kutenga au
kuongeza bajeti ya mikopo
kadri idadi ya wanafunzi
inavyoongezeka. Alitoa mfano
wa Kenya, kuwa wanakusanya
asilimia 70 ya mikopo
waliyokopesha kipindi
kilichopita wakati Tanzania
inakusanya chini ya asilimia
tatu.
 
Dk.
Kawambwa alisema
urejeshwaji mikopo ni eneo
ambalo Heslb haijafanya vizuri.
Aliishauri iweke mikakati ya
ukusanyaji madeni kutoka kwa
waliokopeshwa ikiwemo
kutoza madeni riba.
Alisema Serikali haiwezi
kuendelea kutenga au
kuongeza bajeti ya mikopo
kadri idadi ya wanafunzi
inavyoongezeka. Alitoa mfano
wa Kenya, kuwa wanakusanya
asilimia 70 ya mikopo
waliyokopesha kipindi
kilichopita wakati Tanzania
inakusanya chini ya asilimia
tatu.
 
Alitoa mfano
wa Kenya, kuwa wanakusanya
asilimia 70 ya mikopo
waliyokopesha kipindi
kilichopita wakati Tanzania
inakusanya chini ya asilimia
tatu.
 
kwa mwezi ni 150,000/=
nalipa pango 50,000/=
chakula 90,000/= yaani each day 3000/=
nabakiza 10000/=
inamaana sijalipia matumizi ya internet, sijatoa photocopy, sijaweka ela ya nauli, sijavaa, sijafua, sijawa entertained, bili ya maji yaningoja, bili yaumeme yagonga hodi, niombe niishi bila kuumwa.
5000/= per day haitoshi hata kidogp.
 
Jamani elf5 ni ndogo sana! Hali ya maisha kwa sasa imepanda mno! 5thousands is nothing 4sure! Just imagine umepata desa la kutoa copy linacost tshs.6,000! Je uache kula,utoe copy,or ule uache kutoa copy,alaf upate supp. Pipo,u beta think deep!
 
Back
Top Bottom