w0rM
Member
- May 3, 2011
- 68
- 164
Wanafunzi wa Chuo cha St. Joseph Tawi la Boko linalotoa elimu ya Afya, wamedai kufelishwa na Uongozi wa Chuo hicho na kuambiwa hawawezi kurudi Chuoni hapo na kama wanataka kurudi basi warudie mwaka
Wanadai walifanya mtihani wa UE wakiwa takriban Wanafunzi 200 lakini Wanafunzi waliopitishwa ni 75 ikidhani ni kutokana na chuo hicho kuchukua idadi kubwa ya Wanafunzi kuliko kilivyotakiwa
Kwa kuwa kwa sasa hakuna kwenda Chuoni, Chuo hicho kilifungua makundi ya WhatsApp na kuwaweka wanafunzi, Wanafunzi hao walitakiwa kulipa ada na wasiolipa wanatolewa kwenye makundi hayo ambayo Chuo kilianzisha kikidai ni kwa ajili ya kufundishia
Wanafunzi hao wanadai kuwa Chuo kilichukuwa Wanafunzi wengi ili kupata fedha na sasa baada ya kuwa wamelipa fedha wengi wamefelishwa kilazima.
Wanadai kuna wanafunzi wana Ufaulu wa B nne na C mbili katika masomo ila ameandikiwa amefeli (Discontinuation). Wengi wanashangaa wakidai wana ufaulu mzuri wa 'Assigment 1 na 2' zinazochangia 50% mwenye mtihani wa UE ila wamefeli
Pia, amelalamika kuwa baada ya malalamilo hayo wametumiwa form za kujaza ili kukatia rufaa matokeo yao na kuomba kusahihishiwa upya. Rufaa hiyo ina gharama ya Tsh. 50,000 na mwanafunzi akilipa akifaulu anarudishiwa ila akifeli fedha hairudishwi. Wanafunzi wanadai hiyo ni njia yao ya kupata fedha kwani hakuna mwanafunzi anafaulu
Wanafunzi wanasema kile sio chuo, wanateseka sana, Walimu wanatembea na Wanafunzi na asilimia kuwa ya Wanafunzi waliopitishwa ni wale waliokuwa wakihisiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Walimu. Wameomba ikiwezekana chuo kifungwe na wao wahamishwe
Wanadai walifanya mtihani wa UE wakiwa takriban Wanafunzi 200 lakini Wanafunzi waliopitishwa ni 75 ikidhani ni kutokana na chuo hicho kuchukua idadi kubwa ya Wanafunzi kuliko kilivyotakiwa
Kwa kuwa kwa sasa hakuna kwenda Chuoni, Chuo hicho kilifungua makundi ya WhatsApp na kuwaweka wanafunzi, Wanafunzi hao walitakiwa kulipa ada na wasiolipa wanatolewa kwenye makundi hayo ambayo Chuo kilianzisha kikidai ni kwa ajili ya kufundishia
Wanafunzi hao wanadai kuwa Chuo kilichukuwa Wanafunzi wengi ili kupata fedha na sasa baada ya kuwa wamelipa fedha wengi wamefelishwa kilazima.
Wanadai kuna wanafunzi wana Ufaulu wa B nne na C mbili katika masomo ila ameandikiwa amefeli (Discontinuation). Wengi wanashangaa wakidai wana ufaulu mzuri wa 'Assigment 1 na 2' zinazochangia 50% mwenye mtihani wa UE ila wamefeli
Pia, amelalamika kuwa baada ya malalamilo hayo wametumiwa form za kujaza ili kukatia rufaa matokeo yao na kuomba kusahihishiwa upya. Rufaa hiyo ina gharama ya Tsh. 50,000 na mwanafunzi akilipa akifaulu anarudishiwa ila akifeli fedha hairudishwi. Wanafunzi wanadai hiyo ni njia yao ya kupata fedha kwani hakuna mwanafunzi anafaulu
Wanafunzi wanasema kile sio chuo, wanateseka sana, Walimu wanatembea na Wanafunzi na asilimia kuwa ya Wanafunzi waliopitishwa ni wale waliokuwa wakihisiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Walimu. Wameomba ikiwezekana chuo kifungwe na wao wahamishwe