Wana MMU tushirikiane kuboresha Jukwaa letu

Status
Not open for further replies.
Moja ya tofauti kubwa kati ya traditional media na social media ni quality ya content. Kwenye traditional media ni rahisi kuhakiki quality kabla ya ku-publish kwa sababu information ina-flow vertically. Information inapitiswa kwanza kwenye chujuo kuchuja pumba zote kwanza kabla ya kuwa released. Lakini kwenye social media information ina-flow horizontally. Matokeo yake ni kuwa na content ambayo ni high quality, low quality na wakati mwingine abusive content.

Social media ina user generated content. How users generate the content depend on their lives, personal experience, likes, dislikes, how they feel about certain things at a particular time. Pia kadri muda unavyokwenda watu wengi zaidi hasa katika nchi zinazoendelea wana-spend muda mwingi zaidi kwenye social media. Kwa hiyo, kutakuwa na mix ya watu tofauti na ilivyokuwa zamani. Tatizo ni kuwa wengi wao bado hawajui nini waandike au wasiandike kwenye internet na implications za kufanya au kutokufanya hivyo.

Social media ina faida zake nyingi tuu. Lakini pia ina limitations zake hasa kuhusiana na uaminifu wa habari zinazowekwa na maana hasa ya interactions ya watu kwenye social media. Lakini pia social media inaleta demokrasia kwenye internet. Wapo wanaopenda hiyo demokrasia lakini pia wapo ambao wangependa ku-dictate nini kiwe kinaandikwa. Kwenye kitabu kiitwacho "The Cult of the Amateur", Andrew Keen ameikandia social media huku akidai it only helps “the loudest and most opinionated” people to survive. Whether it is true or not I don't know.

Lakini siyo kila kinachoandikwa kwenye social media kinaweza kuleta positive outcomes kama kufundisha, kuelimisha, n.k. Inasemekana kuwa social media inaweza kutumika kama bullying method, ku-maximise sexual satisfaction, sexual propaganda, n.k. Pia tusisahau kuwa JF ni type ya honeycomb framework ya social media ambapo members wanaweza kuamua, pamoja na mambo mengine, kama wanataka kuwa anonymous au ku-reveal their actual identity.

Nadhani, in future itabidi tuwa-treat watu online kama tunavyowa-treat watu mitaani. Kama mtu ni mlevi na hupendi ulevi wake, sidhani kama unaweza kumwambia barmaid au mwenye bar asimwuzie tena bia au ahakikishe anamwuzia soda tuu. Sana sana utamshauri jamaa aache ulevi akikataa it is up to him/her. The same to social media. Kama mtu anaandika utumbo na anaambiwa anachoandika ni utumbo lakini anaendelea kuandika utumbo there is nothing you can do kumzuia kufanya hivyo. Sana sana either utakubali kutokubaliana nae or utamwi-ignore.

In fact, tatizo hili halipo MMU tuu. Lipo pia kwenye majukwaa mengine kama Jukwaa la Siasa. Probably, inabidi tufike mahali tukubali kuwa the way people behave on the internet na hasa hapa JF has changed considerably. Kwa hiyo, it is up to the users wenyewe kuamua kuwa serious kwenye hizo threads, kujihusisha katika threads za majitaka, au ku-igonore kabisa hizo threads. Kuhusiana na utoto ulioingia MMU na kwingineko, inawezekana kweli kuna watoto hapa na hivyo watakachoandika hakitakuwa relevant kwa wakubwa and vice versa.

kwenye red ndicho nilichoazimia kuanzia mwaka huu, na nafikiri si rahisi kumbadilisha mtu na huenda si sahihi sana kwani sina authority na maisha au jinsi mtu anavyopaswa kuishi maisha yake na mwisho nani kasema mtazamo wangu ndio sahihi?
Nimejifunza kuignore nyuzi nyingi sana bila kutia neno (ingawa Eiyer katika uzi wake alisema ni ushetani huo) nikiombwa ushauri nitatoa lakini sioni usahihi wa kuimpose morals zangu kwa watu wengine.
 
Last edited by a moderator:
kwenye red ndicho nilichoazimia kuanzia mwaka huu, na nafikiri si rahisi kumbadilisha mtu na huenda si sahihi sana kwani sina authority na maisha au jinsi mtu anavyopaswa kuishi maisha yake na mwisho nani kasema mtazamo wangu ndio sahihi?
Nimejifunza kuignore nyuzi nyingi sana bila kutia neno (ingawa Eiyer katika uzi wake alisema ni ushetani huo) nikiombwa ushauri nitatoa lakini sioni usahihi wa kuimpose morals zangu kwa watu wengine.

Kwanza binadamu wote kuna namna tunayopaswa kuishi,suala la nani ana mamlaka ya kuwaelekeza wengine hilo sijui

Hivi kuna mahali nimesema kuwa kuignore bila kutia neno ni ushetani?
Hapa lazima nintakudai ushahidi tafadhali!

Kuna tofauti kati ya kusema ilivyo sahihi na kumimpose morals zako kwa wengine
Hakuna anaeweza kupinga usahihi,usiniulize ni sahihi kwa mujibu wanani kwakuwa sahihi ni sahihi tu na haina mujibu wa yoyote!

Love you!!!!!!!!!!lol!
 
1. Kila tunapo ona Bandiko halifai tutumie Button ya Report Abuse kutoa taarifa mara moja ili itolewe.
2. Tujitahidi kurusha mada za kujenga na sio kubomoa au kumkomoa fulani au kuonyesha madhaifu fulani ya jamii yetu kwa kila atakae weza.
3. Tujitahidi kujadili kwa hoja na kupunguza mizaha na kejeli kwa warusha mada. Kama mada haifai ni kheri kufanya namba moja hapo juu badala ya kuchangia.
4. Kuondoa dharau kwa Mwanamke na Mwanaume pia. Mada za kusanifu Mwanaume ama Mwanamke hazijengi, zinabomoa tu.
5. Tujitahidi kuangalia pande zote za mijadala, isiwe vitu negative tu. Mfano sasa hivi kila inapokuja mada inayohusiana na ndoa huwa ni ya kukatisha tu tamaa, hata wale ambao hawapo kwenye taasisi hiyo hukatishwa tamaa kwa kukuza negatives tu na hali kuna positives pia kwa upande wa ndoa na sio kila ndoa ni majangaa au ina matatizo wapo wenye raha na furaha kwa ndoa zao
6. Masuala ya Ngono, Maumbile ni kheri yakajadiliwe Jukwaa la Wakubwa ambapo kule mjadala utakuwa wa wazi na utapata majibu yote unayoyataka na utajibiwa kwa uwazi bila kificho.

leo mheshimiwa hapa umejipinda sana...................isipokuwa namba 5.0 kama kitu ni hasi hatuwezi kujidanganya na kukichakachua kiwe chanya.........la muhimu tuzingatie ukweli mtupu badala ya kuvikana vilemba vya ukoka...................
 
Mkuu Rutashubanyuma heshima yako mkuu
Ulipotea sana aise karibu tena maana tulikosa mengi sana kutoka kwako
 
Last edited by a moderator:
Wadada wengi humu jamvini mmekuwa na tabia ya kutupa vijembe,kejeli na udhalilishaji kwa wanaume. Mmekuwa na tabia ya ku-generalise tabia ya mwanaume mmoja wa huko mtaani na kutudhalilisha wanaume wote. Sasa,mkae chonjo. Mtakapofanya hivyo,tutajibu mapigo.

Lengo hasa la Jukwaa hili si kukejeliana au kutusiana. Ni kufunzana na kuelekezana mambo mbalimbali ya mahusiano. Ilitokea humu wanaume tulidhalilishwa wazi kabisa.Tulipojibu mapigo,upatanishi ukaombwa haraka.Tabia inajirudia tena.Tutajibu mapigo kiukwelikweli. Yawezekana kila jinsi ina matatizo yake.Lakini tukiyaanika humu hayatatosha. Dawa ni kuheshimiana tu humu tukifunzana bila ya kudhalilishana.

cc Smile Zahra White Madame B lara 1 na wengineo
 
Last edited by a moderator:
Uzi wako uli-generise sana Smile.Acha ubishi

Kama ni suala la kudhalilishwa na kuwa generalized . . . . mbona females tushadhalilishwa sana tena na nyienyie kina baba???? Kuanzia threads za makabila na hata individual experiences watu wanakuja kuzileta jamvini na kuzilebal kwa wanadada/wanawake wote. Tukionesha kutozipenda na kuzikemea . . . ndo kabisa mnaanza oooh ndo walewale na blah blah kibao. Do you think huwa tunafurahia????

Haya ya kwenu yakisemwa ndo mnaona mmekejeliwa. Really???

Sishabikii udhalilishaji kwa jinsia yeyote ile, isipokuwa heshima kwa wote. Na wale ambao mmekuwa na personal issues kwa namna moja ama nyingine ni vyema muwe mnazimalizia hukohuko mjuako nyie. Sio unakuwa na hasira na mtu halafu unakuja kuutapikia umati kwa kumfumbia mtu mmoja tu ulomlenga . . . . THAT'S NO WAY OF GROWN BRAIN.

You can't demand respect if you don't respect yourself. PERIOD!!!
 
Kama ni suala la kudhalilishwa na kuwa generalized . . . . mbona females tushadhalilishwa sana tena na nyienyie kina baba???? Kuanzia threads za makabila na hata individual experiences watu wanakuja kuzileta jamvini na kuzilebal kwa wanadada/wanawake wote. Tukionesha kutozipenda na kuzikemea . . . ndo kabisa mnaanza oooh ndo walewale na blah blah kibao. Do you think huwa tunafurahia????

Haya ya kwenu yakisemwa ndo mnaona mmekejeliwa. Really???

Sishabikii udhalilishaji kwa jinsia yeyote ile, isipokuwa heshima kwa wote. Na wale ambao mmekuwa na personal issues kwa namna moja ama nyingine ni vyema muwe mnazimalizia hukohuko mjuako nyie. Sio unakuwa na hasira na mtu halafu unakuja kuutapikia umati kwa kumfumbia mtu mmoja tu ulomlenga . . . . THAT'S NO WAY OF GROWN BRAIN.

You can't demand respect if you don't respect yourself. PERIOD!!!

Its very true
 
Its very true

That's it ma,
Tujiheshimu na tuliheshimu jukwaa letu pia.

Sasa baadhi ya watu wanapoligeuza sehemu ya majibizano yasiyokuwa ya msingi wala ulazima wowote hususani for battle of sexes . . . . inapendeza kweli my dear? Sidhani.
 
That's it ma,
Tujiheshimu na tuliheshimu jukwaa letu pia.

Sasa baadhi ya watu wanapoligeuza sehemu ya majibizano yasiyokuwa ya msingi wala ulazima wowote hususani for battle of sexes . . . . inapendeza kweli my dear? Sidhani.

Haipendezi na inakua tena haisaidii maana at times watu wana kuwa na majibu ya hovyo acha yan inakera sanaa
 
Harafu tusisahau kuwa kwa sasa kuna watoto wengi wanatumia mitandao ya kijamii jf ikiwamo, sasa kuna mambo ambayo wadogo zetu/watoto zetu wakiyajua na kuyafanyia utekelezaji jamii itakuwa siyo haina ustaarabu na tutakuwa tunaibomoa jamii yetu kwa mikono yetu.
 
Harafu tusisahau kuwa kwa sasa kuna watoto wengi wanatumia mitandao ya kijamii jf ikiwamo, sasa kuna mambo ambayo wadogo zetu/watoto zetu wakiyajua na kuyafanyia utekelezaji jamii itakuwa siyo haina ustaarabu na tutakuwa tunaibomoa jamii yetu kwa mikono yetu.

Ni kweli kuhusu maswala ya age sijui tutaweza je controll
kuna watoto wengne vichwa vyao si vyema wanasoma na kuiga wakidhani ni maisha watu wengine wana yaishi
kijana anaona post za #Mzabzab akifikiri watu wanagegenda hovyo at the end inakula kwake
 
Babu Dark City kuna vichwa vya wakati huo vilikuwa vikianzisha thread unajiuliza nichangie nini au nisemeje hapa
Kuna AshaDii na Lizzy na Roulette na akina BAK na EMT na mtu anayeitwa The Boss na The Finest yaani wakianzisha thread unajiuliza mara mbili mbili na bila kuzisahau busara za watu kama Dark City na Asprin na HorsePower na SnowBall na walimu wetu gfsonwin na snowhite jukwaa lilikuwa na raha zake

Asante sana kwa kunimention, ila mimi nilikua mchangiaji zaidi. Kuna watu wawili umewasahau hapo ni MwanajamiiOne na Mbu. hakuna thread yao ilikua inanipita. deep and funny all the same.
Kwa upande mngine there is only so much people can discuss about MMU. zaidi ya hapo zinakua ni case studies tu. Thread hainogi kwa post ya kwanza, inanoka kwa michango ya watu. Hata hivo nawashukuru wanao anzisha threads (wote kwa ujumla) maana JF ni User generated content. Wengi tumeacha kuanzisha mada kwa sababu mbali mbali, basi tusiwalalamikie wale walio chukua muda wao kuanzisha threads na kuwajibu wanao changia. Suala la quality ni lakuangaliwa na wanao changia zaidi.

I would end by saying that the (relative) low quality of threads in MMU reflects our own inability of responding constructively to threads posted by new members.
 
Jipatie
Unlimited Internet
Jipatie
TunnelGuru Voucher @
8,000
/Month; PD Proxy Vouchers @
8,000
/Month
4 More info
: 0688148836
 
Nakosa hata cha ku comment!!
Unafungua thread huku umepanga kichwani cha ku comment kwa kusoma heading tuu, ila ukisoma content unakua kama paka alie mwangiwa maji!!!
Kwa kweli mpaka nachukia, mpaka sometime unaona uvivu wa kufungua jf!!
Tubadilike wapendwa.
Assante sana mleta uziiiiii.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom