Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,922
- 30,271
MWINYIMBEGU ( MWINYI) DIBIBI si jina geni masikioni mwa watu wa Tanganyika ya kale na hususan wenyeji wa Upwa wa Pwani ya Tanganyika.
Huyu ni Babu yangu ambaye wanamwita kama ni uzao Mkuu ambaye alifanikisha kwa kushinda mapambano ya Uhuru wa Tanganyika katika ardhi ya asili yetu.
Miongoni mwa mambo makubwa ambayo yatabaki katika shajara ya kumbukumbu za Wazalendo wa Tanganyika kwa wakati huo ni mchango wake katika Taifa hili ambalo baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar sasa ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Babu yangu, Mzalendo wa Kiafrika, MWINYIMBEGU DIBIBI ni miongoni mwa watu waliotoa mchango wa hali na mali katika kuanzisha hii leo kinaitwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (rejea tovuti ya chuo kikuu hapo chini)
Si wengi wenye shauku ya kufahamu waliotoa michango kusimamisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, lakini kwa wale wadadisi na wenye kukumbuka wema na hisani, lazima watataka kufahamu Wazalendo kama Babu yangu aliyetoa kiasi cha pesa taslimu na hii ilikuwa Mnamo mwaka 1958 wakati huo vuguvugu la Waafrika kutaka kuondoa Ukoloni na kujitawala wenyewe tutakavyo lilipamba moto.
Ari ya Waafrika wa Tanganyika kutaka kujitawala ilikuwa imemjaa kila mtu, kike, kiume, wa Mjini na Mashamba ilmuradi watu walichoka kutawaliwa na wageni.
Hakuwa babu yangu tu aliyechangia kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, bali kulikuwa na Wazalendo wengine 110 waliotoa mchango wa pesa taslimu.
Mwanafalsafa mmoja, Frederick Douglass aliwahi kusema kwamba " Elimu ni Ukombozi” kwa hakika, Wanamajumui hawa wa Kiafrika kutoka Tanganyika walifahamu ubora wa elimu na umuhimu wake katika kujenga jamii iliyoelimika ambayo wataitumia kama silaha na nyenzo katika kupambana na maisha yanayobadilika kila uchao huku wakikabili changamoto zinazohitokeza.
Kwa kutumia nyenzo ya elimu kama silaha ya kupambana na vikwazo vilivyowekwa na Wakoloni, Waafrika wakielimika katika elimu bora ingewasaidia kufikia malengo na ahadi zao katika kuondoa vizuizi vilivyowekwa na mfumo wa Ukoloni.
Babu yangu ni mmoja wa watu walionithamini sana kiasi cha kunishawishi na kunipa ari ya kipawa changu kutafuta elimu na taaluma ya ujuzi na kuweza kuwasaidia na wengine ambao wanahitaji maarifa na weledi wetu.
Jina lake limeorodheshwa katika tovuti ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akipewa nambari 96.
Kwa hakika kila aliyetenda wema katika mgongo wa dunia anahitaji jazaa njema, nami nachukua fursa hii kuweka kumbukumbu hii ya Babu yangu iwe rejea kwa wale wataopenda kufanya utafiti juu ya historia ya kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mwisho.
Huyu ni Babu yangu ambaye wanamwita kama ni uzao Mkuu ambaye alifanikisha kwa kushinda mapambano ya Uhuru wa Tanganyika katika ardhi ya asili yetu.
Miongoni mwa mambo makubwa ambayo yatabaki katika shajara ya kumbukumbu za Wazalendo wa Tanganyika kwa wakati huo ni mchango wake katika Taifa hili ambalo baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar sasa ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Babu yangu, Mzalendo wa Kiafrika, MWINYIMBEGU DIBIBI ni miongoni mwa watu waliotoa mchango wa hali na mali katika kuanzisha hii leo kinaitwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (rejea tovuti ya chuo kikuu hapo chini)
Si wengi wenye shauku ya kufahamu waliotoa michango kusimamisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, lakini kwa wale wadadisi na wenye kukumbuka wema na hisani, lazima watataka kufahamu Wazalendo kama Babu yangu aliyetoa kiasi cha pesa taslimu na hii ilikuwa Mnamo mwaka 1958 wakati huo vuguvugu la Waafrika kutaka kuondoa Ukoloni na kujitawala wenyewe tutakavyo lilipamba moto.
Ari ya Waafrika wa Tanganyika kutaka kujitawala ilikuwa imemjaa kila mtu, kike, kiume, wa Mjini na Mashamba ilmuradi watu walichoka kutawaliwa na wageni.
Hakuwa babu yangu tu aliyechangia kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, bali kulikuwa na Wazalendo wengine 110 waliotoa mchango wa pesa taslimu.
Mwanafalsafa mmoja, Frederick Douglass aliwahi kusema kwamba " Elimu ni Ukombozi” kwa hakika, Wanamajumui hawa wa Kiafrika kutoka Tanganyika walifahamu ubora wa elimu na umuhimu wake katika kujenga jamii iliyoelimika ambayo wataitumia kama silaha na nyenzo katika kupambana na maisha yanayobadilika kila uchao huku wakikabili changamoto zinazohitokeza.
Kwa kutumia nyenzo ya elimu kama silaha ya kupambana na vikwazo vilivyowekwa na Wakoloni, Waafrika wakielimika katika elimu bora ingewasaidia kufikia malengo na ahadi zao katika kuondoa vizuizi vilivyowekwa na mfumo wa Ukoloni.
Babu yangu ni mmoja wa watu walionithamini sana kiasi cha kunishawishi na kunipa ari ya kipawa changu kutafuta elimu na taaluma ya ujuzi na kuweza kuwasaidia na wengine ambao wanahitaji maarifa na weledi wetu.
Jina lake limeorodheshwa katika tovuti ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akipewa nambari 96.
Kwa hakika kila aliyetenda wema katika mgongo wa dunia anahitaji jazaa njema, nami nachukua fursa hii kuweka kumbukumbu hii ya Babu yangu iwe rejea kwa wale wataopenda kufanya utafiti juu ya historia ya kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mwisho.