Walimu wote kuanza Mgomo Jumatatu Tarehe 01/07/2012

Huu uzi hauna ukweli kiasi fulani,japo mgomo wa walimu upo lakini siyo wa siku tano wala kwa tarehe ambazo mleta mada ametutajia. Hili suala la mgomo wa walimu nimelifuatilia kwa kiasi kikubwa tu na ni kwamba CWT imetangaza mgogoro na serikali tangu tar-8/6 na kwa taratibu za sheria waalimu hawataweza kugoma mpaka kipindi cha siku 30 za mgogoro kipite na kama serikali(mwajiri) atakuwa bado hajatimiza madai ya wafanyakazi(walimu) ndipo mgomo unaweza kutangazwa. kipindi cha mgogoro kati ya serikali na walimu kitaisha tar- 7/7/2012, baada ya hapo ndo mgomo usiokuwa na kikomo na wala siyo wa siku tano na unaweza kuanza tar 8/7 kadiri utakavyo amuliwa mapema na baraza kuu la CWT. Tusipotoshe tafahdal!
 
Na walimu kumbe mtasusia sensa kama shehk ponda! Basi bhana koz hii ni serkal dhaifu basi liwalo na liwe.
 
Ninyi ni wajinga kweli na mtaendelea kudhulumia hadi mtakapo erevuka
Uongozi wa kamati maalum ya kudai haki na maslahi ya walimu kupitia CWT- Chipolopolo; kwa huzuni kabisa tunapenda kuutanfazia Umma kuwa tarehe 01/07/2012 siku ya Jumatatu Walimu wote wa shule za sekondari na shule za Msingi wanakwenda kuanza mgomo wa siku tano kuishinikiza Serikali kuongeza mishahara ya Walimu kuendena na gharama za maisha na inflation. ( Katika mgomo huu walimu wote mnapaswa kushiriki pasipo uoga wowote kwani kwa pamoja tunaweza)

Maombi maalum
1. Tunawaomba wanafunzi wote wa sekondari na msingi wa tuunge mkono kwa siku tano hizo
2. Wazazi wote na wadau wa elimu tunaomba mtuunge mkono katika mgomo wetu ili kuboresha elimu ya watoto wetu
3. Likizo za wanafunzi zitanza kati ya tarehe 7 au 9 Julai hivyo huataathiri mgomo huu
4. Mgomo usio na kikomo kama serikali dhaifu itaendelea kuwa jeuri utafanyika tarehe 16/08/2012 kama ulivyopangwa lakini huu wa tarehe 1/7/2012 ni Pre mgomo kabla shule hazijafungwa na wanafunzi hawajamaliza mitihani na kupata matokeo yao


Walimu tunawajibu wakuitoa ujinga serikali kwa kushiriki mgomo huu pamoja twaweza

Upadate
1.kama Mgomo hautafanikiwa Walimu wote hawatashiriki kutoa na kusahisha mitihani ya nusu muhula ya kwanza
2.Walimu wote kutoshiriki zoezi la sensa ya Watu na Makazi kama wakusanya takwimu
 
Hii serikali Dhaifu sasa imekwisha, muhimu viongoizi wenu muwalinde isije kuwapata yaliyo mpata Dr Ulimboka!
 
hivi chipolopolo unaona waalimu ni watu wa kuwahadaa eti eeh? Ni kweli kabisa kisheria japo shule zimefunga but mwalimu yeyote asiyekuwa na official leave anapaswa kwenda kazini lakini jamani lets be realistic hivi huyu mtu anayekwenda job wakati wanafunzi wakiwa likizo na kusaini daftari la mahudhurio kisha labda kupitia kazi zake ambazo aliziacha kiporo kama ujazaji wa log book na departmental meeting reports ambazo anzifanya at leisure ukimwambia agome itakuwa na tija?

nilifikir kama ni mgomo upangwe wanafunzi wakiwa wamesha resume studies zao na pia hata ikiwezekana wakati wa mtihani ya kitaifa ili serikali ijifunze namna hii na kusema eti wanafunzi hawataathirika ni kama vile kuwaogopa. au labda mnataka wa A-level tu ndio wagome?

najionea kizunguzungu tu na hawa watakuwa ni waalimu wa primary tu siyo bure. kwanza tuvunje cwt may be itatusaidia.
 
Sikuwahi kuona waalimu wakiamua na kutekeleza maazimio yao, so wasitusumbue kwa kutudanganya kila siku kwa maazimio wasioyatekeleza!!!!

 
Nina mashaka na uhalisi na uhakika wa taarifa hii kwa kuwa technically Jumatatu sio tarehe 01/07 bali ni 02/07. Kwa msingi huo ninaipuuzia hoja hii maana hata mtoa taarifa au muitisha mgomo hajakuwa makini kwa suala la msingi kama hilo la siku na tarehe.

NB: Waalimu wakiweza amka, wanaweza tikisa ngome na misingi ya utawala dhaifu, ila kwa hawa walio chini ya CWT ni story ili kusogeza masaa.
 
Mnatakiwa mgome. Fanyeni mgomo usio na kikomo, siyo issue za siku tano hapa. Hivi mnapumbazwa na nini mpaka mnawaogopa haya mafisadi kiasi hiki. Umasikini utawamaliza.
 
walimu tunaomba mgome na mlete impact, mgomo usiwe na kikomo hapo tutawaelewa walimu. walimu achen woga na hakikishen mnadai maslahi yenu kwa vitendo kwa hii serikali dhaifu
 
uongozi wa kamati maalum ya kudai haki na maslahi ya walimu kupitia cwt- chipolopolo; kwa huzuni kabisa tunapenda kuutanfazia umma kuwa tarehe 01/07/2012 siku ya jumatatu walimu wote wa shule za sekondari na shule za msingi wanakwenda kuanza mgomo wa siku tano kuishinikiza serikali kuongeza mishahara ya walimu kuendena na gharama za maisha na inflation. ( katika mgomo huu walimu wote mnapaswa kushiriki pasipo uoga wowote kwani kwa pamoja tunaweza)

maombi maalum
1. Tunawaomba wanafunzi wote wa sekondari na msingi wa tuunge mkono kwa siku tano hizo
2. Wazazi wote na wadau wa elimu tunaomba mtuunge mkono katika mgomo wetu ili kuboresha elimu ya watoto wetu
3. Likizo za wanafunzi zitanza kati ya tarehe 7 au 9 julai hivyo huataathiri mgomo huu
4. Mgomo usio na kikomo kama serikali dhaifu itaendelea kuwa jeuri utafanyika tarehe 16/08/2012 kama ulivyopangwa lakini huu wa tarehe 1/7/2012 ni pre mgomo kabla shule hazijafungwa na wanafunzi hawajamaliza mitihani na kupata matokeo yao


walimu tunawajibu wakuitoa ujinga serikali kwa kushiriki mgomo huu pamoja twaweza

upadate
1.kama mgomo hautafanikiwa walimu wote hawatashiriki kutoa na kusahisha mitihani ya nusu muhula ya kwanza
2.walimu wote kutoshiriki zoezi la sensa ya watu na makazi kama wakusanya takwimu


hivi nyie walimu mbona mnapoteza muda wa kazi kwa kuitishia serikali kila wakati na hii migomo yenu isiyo na faida??? Kama mnaona hiyo kazi haina masilahi si mtafute kazi nyingine???
 
Mleta mada, j3 itakuwa tarehe 2 july na si tarehe 1, edit taarifa hiyo vinginevyo ni *****.
 
Back
Top Bottom