GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Iliichukua TANU chini ya miaka kumi kupata uhuru wa Tanganyika, lakini sasa ni zaidi ya miaka hamsini Tanganyika inapambana kutoka katika shimo lililowekwa na watawala weusi bila mafanikio.
Ingawa Muungano huu bandia uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar unawanufaisha sana Wazanzibar, lakini hata Wazanzibar na wenyewe hawautaki. Inafahamika kuwa viongozi kadhaa wa Zanzibar walijaribu kufurukuta kujitosa kwenye makucha ya watawala wa Muungano lakini hawakufanikiwa. Alianza Abeid Karume, kisha Jumbe na wengine waliofuatia baada yao.
Ingawa kwa asili Watanganyika ni wapole, lakini kutokana na madhila kuzidi, nao walianza kupiga kelele kuitaka Tanganyika yao. Historia inaendelea kuwakumbuka akina Njelu Kassaka waliojitoa muhanga kuidai Tanganyika bila kuuogopa ukali wa Mwl Nyerere. Ingawa azma yao haikutimia, lakini mbegu waliyoipanda ingali ikiendelea kumea mioyoni mwa Watanganyika.
Tokea vuguvugu hilo la Watanganyika lipambe moto miaka ya tisini, ni zaidi ya miaka thelathini sasa na bado watawala wameendelea kuziba masikio.
Alau Wazanzibar wenyewe wana unafuu mkubwa. Wamerudishiwa sehemu kubwa ya mamlaka yao kama nchi pamoja na hongo kemkem inazozipata kutoka kwa watawala wa Tanganyika, stahiki ambazo kimsingi, ni za Tanganyika. Wanafanya hivyo ili kuwanyamazisha Wazanzibar wasiuvunje Muungano batili kati ya Zanzibar na Tanganyika.
Inatafakarisha, kwamba pamoja na kwamba ni Watanganyika ndiyo walioshikilia mpini wa utawala, lakini wao ndiyo wamegeuka mwiba kwa Tanganyika. Udhalimu wao unapita ule wa Mjerumani na Mwingereza. Ukiwalinganisha, utabaini kuwa watawala wa Kizungu walikuwa bora mara mara nyingi sana kuliko hawa wanajitahidi kuididimiza Tanganyika. Wa Kizungu walilenga kuijenga Tanganyika, wa sasa wanajitahidi kuizika japo hawatafanikiwa.
Madhalani, Mwingereza alipodaiwa uhuru wa Tanganyika, hakufanya moyo mgumu. Aliutoa kwa amani.
Lakini Watanganyika kwa miaka mingi sasa, pamoja na kuwasihi watawala wawarudishie Tanganyika yao, ndiyo kwanza wanajitahidi kuziba masikio na macho. Hawataki kusikia wala kuona.
Ndiyo maana najiuliza, watawala wa kikoloni walikuwa na roho nzuri kuliko hawa wanaoitawala Tanganyika kwa sasa?
Ingawa Muungano huu bandia uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar unawanufaisha sana Wazanzibar, lakini hata Wazanzibar na wenyewe hawautaki. Inafahamika kuwa viongozi kadhaa wa Zanzibar walijaribu kufurukuta kujitosa kwenye makucha ya watawala wa Muungano lakini hawakufanikiwa. Alianza Abeid Karume, kisha Jumbe na wengine waliofuatia baada yao.
Ingawa kwa asili Watanganyika ni wapole, lakini kutokana na madhila kuzidi, nao walianza kupiga kelele kuitaka Tanganyika yao. Historia inaendelea kuwakumbuka akina Njelu Kassaka waliojitoa muhanga kuidai Tanganyika bila kuuogopa ukali wa Mwl Nyerere. Ingawa azma yao haikutimia, lakini mbegu waliyoipanda ingali ikiendelea kumea mioyoni mwa Watanganyika.
Tokea vuguvugu hilo la Watanganyika lipambe moto miaka ya tisini, ni zaidi ya miaka thelathini sasa na bado watawala wameendelea kuziba masikio.
Alau Wazanzibar wenyewe wana unafuu mkubwa. Wamerudishiwa sehemu kubwa ya mamlaka yao kama nchi pamoja na hongo kemkem inazozipata kutoka kwa watawala wa Tanganyika, stahiki ambazo kimsingi, ni za Tanganyika. Wanafanya hivyo ili kuwanyamazisha Wazanzibar wasiuvunje Muungano batili kati ya Zanzibar na Tanganyika.
Inatafakarisha, kwamba pamoja na kwamba ni Watanganyika ndiyo walioshikilia mpini wa utawala, lakini wao ndiyo wamegeuka mwiba kwa Tanganyika. Udhalimu wao unapita ule wa Mjerumani na Mwingereza. Ukiwalinganisha, utabaini kuwa watawala wa Kizungu walikuwa bora mara mara nyingi sana kuliko hawa wanajitahidi kuididimiza Tanganyika. Wa Kizungu walilenga kuijenga Tanganyika, wa sasa wanajitahidi kuizika japo hawatafanikiwa.
Madhalani, Mwingereza alipodaiwa uhuru wa Tanganyika, hakufanya moyo mgumu. Aliutoa kwa amani.
Lakini Watanganyika kwa miaka mingi sasa, pamoja na kuwasihi watawala wawarudishie Tanganyika yao, ndiyo kwanza wanajitahidi kuziba masikio na macho. Hawataki kusikia wala kuona.
Ndiyo maana najiuliza, watawala wa kikoloni walikuwa na roho nzuri kuliko hawa wanaoitawala Tanganyika kwa sasa?