Matatizo ya Tanzania yaliasisiwa na waliopigania uhuru wa Tanganyika

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,755
Salaam kwenu.

Ni kweli lengo la kupigania Uhuru wa Tanganyika, lilikuwa kuwafanya wananchi ama raia kuwa huru kuchagua aina ya uongozi na viongozi wanaotaka, kujiamulia mambo yao ya Kiuchumi, Kisiasa na Kiutamaduni bila kuingiliwa na kikundi ama mataifa ya nje.

Lakini tujiulize hapa, baada ya uhuru kupatikana. Nini kilitokea?
  1. Je Watanganyika walikuwa huru kufanya shughuli za siasa ama waliamuliwa aina ya siasa ya kuifuata?
  2. Je Watanzania walikuwa huru kuchagua mfumo wa namna nchi itakavyoendeshwa? Au waliundiwa Katiba kwa utashi wa viongozi?
  3. Je Watanganyika walikuwa huru kujiamulia namna ya kuuendesha uchumi wa nchi yao au waliamuliwa namna uchumi utakavyoendeshwa?
  4. Je elimu ya Tanganyika ilikuwa kwa minajili ya kuwanasua watu dhidi ya ujinga?
Leo tunashuhudia chama kilichoasisi uhuru wa Tanzania kikisema wazi kupitia viongozi wake wakuu kwamba, hakitokubali kutoka madarakani hata kama Tanzania nzima wakisema NO!

Tujiulize, je tambo hizo ndizo zilizopelekea kumfukuza mkoloni ili tutengeneze kikundi cha wahuni watakaojimilikisha nchi kama wameiokota jangwani?

Tusipozinduka leo, tutaendelea kusubiri hisani za Rais ambapo ndiye anayeonekana kumiliki kila kitu bila kuhojiwa na yeyote.

I rest my case
 
Salaam kwenu.

Ni kweli lengo la kupigania Uhuru wa Tanganyika, lilikuwa kuwafanya wananchi ama raia kuwa huru kuchagua aina ya uongozi na viongozi wanaotaka, kujiamulia mambo yao ya Kiuchumi, Kisiasa na Kiutamaduni bila kuingiliwa na kikundi ama mataifa ya nje.

Lakini tujiulize hapa, baada ya uhuru kupatikana. Nini kilitokea?
  1. Je Watanganyika walikuwa huru kufanya shughuli za siasa ama waliamuliwa aina ya siasa ya kuifuata?
  2. Je Watanzania walikuwa huru kuchagua mfumo wa namna nchi itakavyoendeshwa? Au waliundiwa Katiba kwa utashi wa viongozi?
  3. Je Watanganyika walikuwa huru kujiamulia namna ya kuuendesha uchumi wa nchi yao au waliamuliwa namna uchumi utakavyoendeshwa?
  4. Je elimu ya Tanganyika ilikuwa kwa minajili ya kuwanasua watu dhidi ya ujinga?
Leo tunashuhudia chama kilichoasisi uhuru wa Tanzania kikisema wazi kupitia viongozi wake wakuu kwamba, hakitokubali kutoka madarakani hata kama Tanzania nzima wakisema NO!

Tujiulize, je tambo hizo ndizo zilizopelekea kumfukuza mkoloni ili tutengeneze kikundi cha wahuni watakaojimilikisha nchi kama wameiokota jangwani?

Tusipozinduka leo, tutaendelea kusubiri hisani za Rais ambapo ndiye anayeonekana kumiliki kila kitu bila kuhojiwa na yeyote.

I rest my case
Shida ilianza na list hii ya hapa ya wana TAA na baadae TANU
1. Master Forojo Ganze
2. Primus Julius Mubanga
3. Shekhe Yahya Hussein
4. Shaibu Kalole
5. Mfaume Goro
 
Baada ya uhuru na hiyo ya Tanganyika ikapotea hadi leo. Kuna haja ya kufungua kesi UN kuwadai waingereza ile nchi waliyoipa uhuru wakabidhi wananchi wa sasa sio wale wahuni
 
Back
Top Bottom