Wakina Mdee wajipanga kukata rufaa. Je, Spika Tulia ataendelea kuwatambua kama wabunge?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,357
35,832
Baada ya wabunge wa viti maalum wa Chadema kuangushwa mahakamani siku ya leo na kujipanga kukata rufaa kupinga hukumu hiyo, je Spika Tulia ataendelea kuwatambua kama wabunge kwa kigezo kuwa mchakato wa kisheria dhidi yao bado haujakamilika kwa kuwa rufaa wanayojipanga kuikata bado haijasikilizwa?

Kuweka kumbukumbu sawa tu hapa JF, ni kuwa Spika Tulia toka awali aliweka msimamo wa kuwatambua kama wabunge halali, Halima Mdee na wenzake kwa kuwa walikata rufaa kwenye baraza kuu la chama chao kupinga uamuzi wa kuvuliwa uanachama wa CHADEMA uliofanywa na kamati kuu.

Hata baada ya baraza kuu la CHADEMA kubariki uamuzi wa kamati kuu wa kuwavua uanachama wa CHADEMA bado spika Tulia alisema kuwa ataendelea kuwatambua wabunge hao kwa kuwa walimweleza kuwa wanajipanga kupinga uamuzi wa CHADEMA mahakamani.

Sababu kuu ya Spika Tulia anayoitumia ni kuwa, mchakato wa kisheria dhidi ya wabunge hao bado haujakamilika.

Sasa watanzania wanasubiria tena kusikia kauli ya Spika Tulia kuendelea kuwakumbatia wakina Mdee, tofauti na hapo Spika Tulia ataoneka ni mnafiki.
 
Haya Mambo ya kina Halima Mdee yana turudisha nyuma sana ,Kwanza wanatumia pesa za wananchi kinyume na sheria ,pili tunatumia pesa kuendesha hizi kesi na Mwisho viongozi wa nchi hii pamoja na CHADEMA mnatufanya wananchi wajinga Sana .
 
... utashangaa rufaa itasikilizwa na kuamuliwa haraka ambapo watashinda ili kuwahi next Bunge session wakati kesi ya leo imepelekwa kwa mwendo wa kinyonga kutoa nafasi Bunge la bajeti limalize sessions zake kesho nadhani.
 
Baada ya wabunge wa viti maalum wa Chadema kuangushwa mahakamani siku ya leo na kujipanga kukata rufaa kupinga hukumu hiyo, je Spika Tulia ataendelea kuwatambua kama wabunge kwa kigezo kuwa mchakato wa kisheria dhidi yao bado haujakamilika kwa kuwa rufaa wanayojipanga kuikata bado haijasikilizwa?

Kuweka kumbukumbu sawa tu hapa JF, ni kuwa Spika Tulia toka awali aliweka msimamo wa kuwatambua kama wabunge halali, Halima Mdee na wenzake kwa kuwa walikata rufaa kwenye baraza kuu la chama chao kupinga uamuzi wa kuvuliwa uanachama wa CHADEMA uliofanywa na kamati kuu.

Hata baada ya baraza kuu la CHADEMA kubariki uamuzi wa kamati kuu wa kuwavua uanachama wa CHADEMA bado spika Tulia alisema kuwa ataendelea kuwatambua wabunge hao kwa kuwa walimweleza kuwa wanajipanga kupinga uamuzi wa CHADEMA mahakamani.

Sababu kuu ya Spika Tulia anayoitumia ni kuwa, mchakato wa kisheria dhidi ya wabunge hao bado haujakamilika.

Sasa watanzania wanasubiria tena kusikia kauli ya Spika Tulia kuendelea kuwakumbatia wakina Mdee, tofauti na hapo Spika Tulia ataoneka ni mnafiki.

Hahaha atakuwa amefanya kazi yake, tusiingilie kazi za watu Kwa chuki zetu tu
 
😁😁😁
16554546876670.jpg
 
... utashangaa rufaa itasikilizwa na kuamuliwa haraka ambapo watashinda ili kuwahi next Bunge session wakati kesi ya leo imepelekwa kwa mwendo wa kinyonga kutoa nafasi Bunge la bajeti limalize sessions zake kesho nadhani.
Kwa kikao kile Cha ikulu nadhani Mama Samia aliridhia waangushwe mahakamani Ili mazungumzo ya katiba mpya yaendelee. Hakuna namna Mbowe angerudi mezani huku kina Mdee Bado wanadunda tu bungeni
 
Baada ya wabunge wa viti maalum wa Chadema kuangushwa mahakamani siku ya leo na kujipanga kukata rufaa kupinga hukumu hiyo, je Spika Tulia ataendelea kuwatambua kama wabunge kwa kigezo kuwa mchakato wa kisheria dhidi yao bado haujakamilika kwa kuwa rufaa wanayojipanga kuikata bado haijasikilizwa?

Kuweka kumbukumbu sawa tu hapa JF, ni kuwa Spika Tulia toka awali aliweka msimamo wa kuwatambua kama wabunge halali, Halima Mdee na wenzake kwa kuwa walikata rufaa kwenye baraza kuu la chama chao kupinga uamuzi wa kuvuliwa uanachama wa CHADEMA uliofanywa na kamati kuu.

Hata baada ya baraza kuu la CHADEMA kubariki uamuzi wa kamati kuu wa kuwavua uanachama wa CHADEMA bado spika Tulia alisema kuwa ataendelea kuwatambua wabunge hao kwa kuwa walimweleza kuwa wanajipanga kupinga uamuzi wa CHADEMA mahakamani.

Sababu kuu ya Spika Tulia anayoitumia ni kuwa, mchakato wa kisheria dhidi ya wabunge hao bado haujakamilika.

Sasa watanzania wanasubiria tena kusikia kauli ya Spika Tulia kuendelea kuwakumbatia wakina Mdee, tofauti na hapo Spika Tulia ataoneka ni mnafiki.
Everything is possible. It's difficult to speculate. It could go either way depending Maelekezo toka juu yanasemaje. Nafikiri kuna watu CCM wameajiliwa kwa kazi hiyo.... Spin Doctors.
 
Back
Top Bottom